Kati ya watangaza nia wote, yupi umeona anafaa?

"Katika hali ya kunishangaza, nilikuwa nabadilishana mawazo na mzungu mmoja raia
wa Ujerumani kwenye N.G.O yake. Katamka maneno yaliyonistaajabisha.
Tumeongea mambo mengi lakini baadae tukaanza kuongelea siasa. Akasema kuna
yule aliekuwa waziri mkuu anaitwa Lowasa, nimeona sasa mnampenda sana. Mimi
nikamjibu inaonekana kuna Watanzania wanampenda awe Rais. Yule Mzungu
akaniuliza, si yule aliejiuzuru kwa sababu ya Corruption?, nikamjibu ndie huyo.
Akasema, wakati ule alionekana amekula Rushwa, sasa anataka kuwa Rais na watu
wanamuunga mkono!, akaongezea kwa kusema how can you easily forget?, how can
you easily change your mind?, yaani mnawezaje kuwa wasahaulifu namna hii,
mnawezaje kubadili fikra zenu haraka hivi juu yake?, hapo mimi nikabaki na
kigugumizi. Akaongeza, au Lowasa amewahi kuwaelezea uhusika wake na hizo
corruption?, mimi nikamjibu hapana. Akasema tena, Or was he cleared by the court?
yaani, je Mahakama iliona hana hatia?, nikamjibu kesi haijawahi kwenda Mahakamani.
Akauliza, then which criteria do you use to support him? Nikamjibu kwakweli sijui wananchi wanatumia kigezo gani.
Yule mzungu akasema, anyway, you are such amazing country, with this style it may
take you so many years to change."

Sent as received.

Pamoja na kwamba ni kastori kakutunga lakini ndio ukweli,how can we easily forget?kama aliachia ngazi kuwalinda maswahiba zake au kulinda chama atashindwa vipi kuwalinda akiwa rais?
Hivi kuwajibika ndio huku?
 
Mtanzania wakati zoezi la kutangaza nia likiwa linafikia ukingoni tunaomba maoni yako kwa kutaja kina tu.

Swali limasema

Kati ya makada wote wa CCM waliojitokeza kutangaza nia ya kuutaka uraisi, ni kada yupi amekuvutia na unakiomba chama cha CCM kimpitishe ili apeperushe bendera ya CCM kugombea uraisi?

Na uko tayari kumpigia kura ya ndiyo?.

Mpaka sasa hakuna mgombea au mtia nia anayefaa. Hawa wote waliotangaza nia ni sehemu ya watawala ambao wamesababisha ufisadi kuongezeka, umaskini kuongezeka, mafukara kuongezeka, matabaka ya wenye nacho na wasio kua nacho kuongezeka, uchumi wa nchi kuporomoka, shillingi kuporomoka na ghrama za maisha kupanda. Kwa ufupi wote waliotangaza nia wanaongelea kushugulikia hizi kero lakini hawaongelei kufumua mfumo huu wa utawala uliosababisha matatizo yote tuliyonayo. Kila mmoja anaejitokeza anaongelea kuondoa umaskini, kukuza uchumi, kuondoa matabaka, kuondoa ufisadi na rushwa, kuboresha huduma za jamii maji, afya, elimu, makazi na kadhalika lakini hawa hawa wanasahau kua ni wao ndio wamekua sehemu ya matatizo haya yote over 50 years za uhuru. Report za CAG ni ufisadi kila mwaka, wengine waliuza nyumba za serikali, wengine wamejiuzulu kwa matuhuma kama escrow and richmond. Tunahitaji mtia nia atakayeongea kufumua mfumo mzima wa utawala na kuchora mstari kwenye baadhi ya masuala kama rushwa na ufisadi. Mtu huyu hawezi hata kidogo kutoka ndani ya ccm kwa sababu ndani ya ccm ukisema kufumua mfumo wa utawala unatafuta shida au uadui, kama unabisha nenda kamuulize mzee Warioba. Kwa maoni yangu ninaamini mtu amabae anaweza kututoa hapa tulipo ni Dr Slaa tu. Hawa wengine ni porojo tu hakuna anaeweza kufumua mfumo hakuna anaeweza kuichukua rasimu ya pili ya katiba ya mzee Warioba na kuisimamia, hakuna ndani ya hawa waliotangaza na ndani ya ccm. Tatizo letu limeanzia kwenye mfumo. Jana katika kipindi cha siasa za siasa Dr RYOBA alimwambia Nape kwamba rushwa inaendelea kuwepo na itaendelea kuwepo mpaka tutakapopata serikali makini itakayosema basi. Mambo yote yamekwama kwa sababu ya mfumo wa utawala uliopo. Kuna mgombea mmoja Sumaye i think kidogo na kwa mbali aligusia kuunda mahakama ya kushugulikia rushwa na ufisadi na kuanzisha chombo maalum cha uchunguzi wa wala rushwa na ufisadi, meaning PCCB wamefeli na DPP hapo alikua anagusa mfumo tata uliopo sasa. Lakni hataweza akiwa ndani ya ccm. Kwa ufupi ni wakati muafaka watanzania tuamuke kuchagua kiongozi atakaefumua mfumo ulichemuka na kufeli kuleta mabadiliko for 50 years. DR SLAA IS MY CHOICE
 
kiukweli walitangaza nia bado hawajakizi haja ya upepo wa siasa kwa sasa,bali mtu pekee atakaye ikomboa ccm ni MAGUFULI TU kama hawataki wafanye tafiti sio kwenye mitandao bali kwenye graund.
 
kulingana na swali la mtoa hoja, mpaka sasa kati ya hotuba zote mtangaza nia pekee ambaye ukiweka ushabiki pembeni na kusikiliza point baada ya point Prof. Muhongo pekee ndo alieongelea maswala yote yanayotatiza nchi kwa facts na kufafanua njia ambazo zinatekelezeka katika kujikwamua.....Pia Tanzania ya leo ambayo imedhamiria katika uchimbaji wa gesi inahitaji mtu kama Muhongo kutupitisha salama kutokana na kujua afanyalo na mafanikio yake yanayotambulika dunia nzima.
 
wote bado, nawashauri ccm wafanye inavyowezekama ROHO YA CCM NI MAGUFULI, sio maoni yangu tu wafanye tafiti kwenye ground.
 
1.Muhongo
2.Magufuli
3.Nchemba
4.Makongoro


Mkuu naunga mkono list yako lkn naomba nikupangie list na waione watengeneze timu moja na kiongozi wao ni,

1, MAGUFULI,
2, NCHEMBA
3, MAKONGOLO
4, MUHONGO,

Kwa timu hiyo chini ya kiongozi wao ni ukombozi wa wabunge wa ccm ambao wako hatarini kupoteza viti vingi
pili ni wachapa kazi na wanakubalika sana kwa watanzania,
 
It is only Prof. Muhongo is who is visionary and thinking Big. We have opportunity to Make Tanzania fly... through a man thinking beyond 10 years...
 
Back
Top Bottom