Kassim Majaliwa: Niambieni ni nchi gani duniani Bunge huonyeshwa kwa saa 8?

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema kuwa hata bunge la Uingereza halionyeshwi ''LIVE " kwa muda mrefu kama ilivyokuwa kwa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambalo lilikuwa likionyeshwa kuanzia saa 3 asubuhi hadi saa 7 mchana, na kuanzia saa 10 jioni hadi saa 2 usiku na kupelekea watu kutokufanya kazi na badala yake kuamka asubuhi kufuatilia bunge kwa muda wa miezi hadi mitatu.

1.jpg
Swali la kujiuliza ni je, kweli wakati wa mchana watu hawaangalii runinga? Kama hawaangalii vile vipindi vinarushwa kwaajili ya nani?
 
Sasa aliwadanganya hao wadanganyika kwamba sababu za kufutwa ni watu hawafanyi kazi, Waziri anasema ni gharama kubwa , mwingine anasema anataka kulia likionyeswa live. very strange in deed. hivi ni kweli watu wenye kazi wanaacha ili kuangalia bunge? Angesema ukweli kuna wasio na kazi na inafaa waangalie bunge lakini wenye kazi huwa hawaachi hadi jioni.
 
Ni muda muafaka kwa wadau wote kusimama na kupaza sauti na kumuambia Magufuli" Hatukukuchagua ili uzuie matangazo Live ya Bunge"
Magufuli hakuchaguliwa bali alisimikwa na kile kikundi cha Uchakachuaji na kamati za Ufundi cha January makamba ndiyo maana kaamua kuwapeleka peleka Watanzania jinsi anavyojisikia
 
Sasa aliwadanganya hao wadanganyika kwamba sababu za kufutwa ni watu hawafanyi kazi, Waziri anasema ni gharama kubwa , mwingine anasema anataka kulia likionyeswa live. very strange in deed. hivi ni kweli watu wenye kazi wanaacha ili kuangalia bunge? Angesema ukweli kuna wasio na kazi na inafaa waangalie bunge lakini wenye kazi huwa hawaachi hadi jioni.
Bunge la Usiku ni baya zaidi maana huonyeshwa usiku wa manane ni Hatari kwa nguvu kazi, watu wakiangalia watasinzia maofisini mchana.
 
Halafu we huwa hujitambuagi fulani hivi. Ni nchi gani kutwa nzima wanaonyesha live bunge kama sio kwenye session muhimu tu!?

Ni nchi gani duniani inayotoa Marahaba wa Madini 97% Kwa wawekezaji na 3% kwa Serikali husika??Kama hakuna basi ujue kila nchi inauhuru wa kuamua kufanya jambo bila kutegemea nchi wafadhili wanafanya nini.Nyingine Kenya wanaonyesha Bunge live kuanzia linapoanza mpaka linaponalizika.

Ni nchi gani viongozi ndiyo wamekuwa wala rushwa kuliko RAIA wake???
 
Hii huku Chadema wanataka waonyeshwe live.
MNAHUJUMU JUHUDI ZA AWAMU ILIOPITA. Hamjajua tu jina la KIKWETE LINAHESHIMIKA SANA NJE pamoja na mapujgufu lakini UWAZ wa habari imemletea sifa sana. Hapa kazi tu kama mna nia ya kweli basi kwa masaa hayo hayo ma4 badala ya kuonyesha asubuhi ONYESHENI JIONI LIVE KIPINDI CHA HOJA. Haya maswali ya kusoma msituletee tutasoma magazetini. Si mnasema kazi kazi ASUBUHI watu kibaruani live ya nini. HUU UJANJA WA SUNGURA HOJA YA KAZI KUYEYUSHA MATAKWA FLANI. A....HOFU YA NINI....
 
Mkuu wa meza alipata na muda wa kupiga simu muda wa kazi kuchangia hoja no actually kupongeza wale vijana wa mawingu kwa jinsi wanavyopendeza
Hata usiku ni Mda wa kazi vilevile, walinzi waache kulinda waangalie bunge? Hosptal waache kutibu wagonjwa waangalie bunge? Mchana na usiku ni mda wa kazi wote, hivyo visingizio vya Majaliwa vimedhihilisha ni kwa jinsi gani amelewa madaraka baada ya kupewa Tenda ya Uagizaji sukari kwa kivuli cha mashirika ya umma.
 
Ndo maana huwa nawashangaa sana wanaomlaumu Nape kuhusu kuzuia bunge live, huo sio uamuzi wa Nape ni
Amri kutoka juu
yeye kapeleka wazo juu likabarikiwa Unafikili aliemueka pale kakosea Jamaa kiunganishi mzuri sana. kwenye nyanja hizo
 
Ni nchi gani duniani inayotoa Marahaba wa Madini 97% Kwa wawekezaji na 3% kwa Serikali husika??Kama hakuna basi ujue kila nchi inauhuru wa kuamua kufanya jambo bila kutegemea nchi wafadhili wanafanya nini.Nyingine Kenya wanaonyesha Bunge live kuanzia linapoanza mpaka linaponalizika.

Ni nchi gani viongozi ndiyo wamekuwa wala rushwa kuliko RAIA wake???
ni Nchi gani vibali vya sukari hutolewa ikulu? Ni nchi gani Bandari imejaza meli za mizigo kwenye foleni baharini kwa visingizio vya Ajabu?
 
Sio lazima tufanane na nchi nyingine,lakini hata ukifananisha ni serious kabisa unafananisha TANZANIA na UINGEREZA?.
 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema kuwa hata bunge la Uingereza halionyeshwi ''LIVE " kwa muda mrefu kama ilivyokuwa kwa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambalo lilikuwa likionyeshwa kuanzia saa 3 asubuhi hadi saa 7 mchana, na kuanzia saa 10 jioni hadi saa 2 usiku na kupelekea watu kutokufanya kazi na badala yake kuamka asubuhi kufuatilia bunge kwa muda wa miezi hadi mitatu.

Kama ni hivyo basi vituo vyote vya Television na Radio vifungwe saa za kazi kwani navyo vitakuwa havina watazamaji kwa kauli hii ya Majaliwa.
 
ni Nchi gani vibali vya sukari hutolewa ikulu? Ni nchi gani Bandari imejaza meli za mizigo kwenye foleni baharini kwa visingizio vya Ajabu?

Hii ni Nchi ya Wagigikoko.Asante kwa maelezo
 
Binafsi nimekata hata tamaa ya kuchangia mawazo hapa JF mapka pale nitakapopata uthibitisho kwamba rais wa zamani wa Kenya aliwahi kusema kuwa "Nyerere anatawala maiti"!
man eat man...man eat nothing society
 
Kazi watafanya saa ngapi sasa? Maana bunge ni miezi 3, hadi June! Akili za machadema za kitoto sana
Big point, Nimeishi marekani miaka zaidi ya mitano sijawahi ona bunge live kama ilivyokua hapa bongo, vyama vingine vimeo kweli kweli nao wameona pakutokea, stupid mind.
Stupid mind ni ipi hapo mkuu sio ile ya kukataa kuonyesha live kuanzia saa 10 jioni maana ndio asilimia kubwa ya wafanyakazi na hata wakulima wanatoka kwenye sehemu zao za kazi shida iko wapi hapo???akili zingine inabidi zishikiliwe hadi zielewe.
 
Hii nchi inahitaji kuchomwa moto tu, vianze viumbe vipya. Kichwa kikubwa kama nyani dume lakini akili hakuna.....masikini sisi tumekosa nini.
 
Hii sababu ya kusema bunge likioneshwa live wananchi hawafanyi kazi ni ya kitoto sana.
Watafute tu sababu nyingine ambazo kidogo zitamfikirisha mtu.
Tunajua hawataki tuangalie bunge kwa sababu zao binafsi,lakini watafute sababu za uongo zenye kufikirisha.
Sio hii ya kutokufanya kazi,haiingii akilini kabisa.

Cha kuchekesha zaidi 'mastermind' wa hili ni Nape!
Ni bora muda wa kuonyeshwa UFUPISHWE ZAIDI.... juzi hatukulala kuangalia bunge usiku wa manane.... Mbunge wenu amepewa nafasi...badala ya kutoa hoja za Msingi akaanzisha HOJA ZA KING KIKI....bunge lote likaamia ku DISCUSS KING KIKI..... ASANTE SANA ZITO KABWE KWA KUJITOFAUTISHA na WAZEE WA KUBADILISHIA GIA ANGANI... kwani umeendelea kuwa na MVUTO KILA UNAPOSIMAMA!
 
Hoja hapa si wao kuonyesha , kama wameamua hivyo wafunge tu bila maneno

Kinachotusumbua wengine ni jinsi wanavyotaka kutafanya mazezeta
Walianza na gharama hoja ikakosa mashiko tena kwa vithibitisho

Wamehamia ktk kufanya kazi, tunawaambia wapige marufuku TV na ving'amuzi vyote

Sasa wanasema mbona Uingereza haifanyi hivyo.

Come on! Mbona hatufanyi kama ya Uingereza mengi tu.

Watoto wanasomea kwenye mibuyu, wapi Uingereza wanfanya hivyo?mbiona hatuigi

Hizi habari nyingine zinatutia shaka na uwezo wa viongozi wetu.

Kudanganya ni jambo baya kimaadili , kiheshima na kiustaraabu.
Waseme tu kuwa hataki, basi ! Siyo kutuletea sababu zisizo na mantiki.

Ukweli unajulikana, CCM na Serikali yake wanahusika na madudu mengi, njia ya kuyaficha ili wananchi waendelee kuimba nyimbo zao za majipu na hapa kazi ni kuzuia kalamu za waandishi, kuziba macho ya wananchi

Miezi michache iliyopita walisema misaada kama ya MCC inadhalilisha.

Jana gazeti moja limeripoti kuwa Uingereza itasaidia miradi ya umeme kama ilivyokuwa MCC. Wamesema hayo mbele ya PM

Leo tunawauliza wale mashabiki wa nyimbo, je msaada wa Uingereza si udhalilishaji tulioukataa? Utaweza kuona wanavyotaka kupelekesha wananchi waimbe nyimbo zao

Ni CCM wale wale waliotufikisha hapa! Utamaduni wa kulaghai na kudanya!~
Ni wale wale, hakuna aliyetoka nje.

Wamelelewa na CCM na wanatabia za CCM wanachokifanya ni yale ya ulezi wa CCM.

12794625_235428676800924_1689569151932962050_n.jpg
 
Hivi tumekuwa watoto kwamba lazima tupangiwe jinsi ya kufanya kazi?
Akili hii ni sawa na akili ya kuwakataza vijana wasicheze Pool wakati hujawatengenezea ajira. Hujajega hata kiwanda kimoja, kazi ni kufukuza watu tu, then unategemea hao vijana wafanye kazi gani...eti wakalime....Hahahahahahaaa....kwa jembe la mkono bila pembejeo? Wapi UFI? wapi viwanda vya Mbolea? Mbegu kwa bei nzuri ziko wapi? na Hayo mashamba yapo wapi?
 
Back
Top Bottom