Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,817
- 11,993
Fuatilia kinachojiri kwenye Sherehe za Uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru, leo Aprili 2, 2024 ambapo Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa ni Mgeni rasmi.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa ametoa wito kwa wananchi kwenda kuhakiki majina yao kabla uchaguzi wa Serikali za Mitaa haujaanza kwani zoezi la kuhakiki wapiga kura kwenye daftari la kudumu tayari umeshaanza.
Amesema kila mtanzania anayo haki ya kuchagua na kuchaguliwa, na wale wanaokusudia kufanya hivyo mwezi wa 10 ni fursa yao.
Kuhusu suala la lishe, Waziri Majaliwa amesema Serikali inapambana na kutokomeza utapiamlo wa aina zote kwa kuimarisha sera, kanuni na miongozo ya kuwezesha watanzania kupata lishe bora.
Kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2022, hali ya lishe nchini bado siyo ya kuridhisha ambapo 30% ya watoto chini ya miaka 5 wanakabiliwa na tatizo la udumavu na 12% wana uzito pungufu na 3% wana ukondefu na mikoa inayoongoza kwa kuwa na kiwango kikubwa cha udumavu na ukondefu wa watoto kwa zaidi ya wastani wa kitaifa ni Iringa, Njombe, Rukwa, Geita, Ruvuma, Kagera, Simiyu, Tabora, Katavi, Manyara, Songwe na Mbeya.
Aidha, 42% ya wanawake wenye umri wa kuzaa wanakabiliwa na changamoto ya upungufu wa damu, pia tatizo la kiribatumbo na uzito uliozidi unataka kuwa janga la taifa.
Akizungumzia suala la Rushwa nchini, Waziri Kassim Majaliwa amesema mbio za mwenge za mwaka huu zitaendelea kusisitiza umuhimu wa kupambana na rushwa na kwa mujibu wa tafiti, Tanzania inafanya vizuri katika kupambana na rushwa.
Hivi karibuni imeibuka aina mpya ya bangi yenye kiasi kikubwa cha kilevi inayofahamika kama 'Cha Arusha' pamoja na 'Skanka'. Aina hii ya bangi yenye sumu nyingi huchanganywa kwenye sigara na wanaoitumia hubadilika kuwa kichaa. Ni wakati mzuri kwa vijana kuacha ili kunusuru maisha yao.
Pia soma:
Bangi ihalalishwe, Sheria zinazotumika kuhusu Bangi. Ziende kudhibiti Ushoga
Kamishna wa Kudhibiti dawa za Kulevya: Bangi ya Tanzania haifai kwenye Masoko ya Kimataifa
Serikali iruhusu kilimo cha bangi na ipunguze masharti ya uingizaji wa fedha nchini ili kukabili uhaba wa dola
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa ametoa wito kwa wananchi kwenda kuhakiki majina yao kabla uchaguzi wa Serikali za Mitaa haujaanza kwani zoezi la kuhakiki wapiga kura kwenye daftari la kudumu tayari umeshaanza.
Amesema kila mtanzania anayo haki ya kuchagua na kuchaguliwa, na wale wanaokusudia kufanya hivyo mwezi wa 10 ni fursa yao.
Kuhusu suala la lishe, Waziri Majaliwa amesema Serikali inapambana na kutokomeza utapiamlo wa aina zote kwa kuimarisha sera, kanuni na miongozo ya kuwezesha watanzania kupata lishe bora.
Kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2022, hali ya lishe nchini bado siyo ya kuridhisha ambapo 30% ya watoto chini ya miaka 5 wanakabiliwa na tatizo la udumavu na 12% wana uzito pungufu na 3% wana ukondefu na mikoa inayoongoza kwa kuwa na kiwango kikubwa cha udumavu na ukondefu wa watoto kwa zaidi ya wastani wa kitaifa ni Iringa, Njombe, Rukwa, Geita, Ruvuma, Kagera, Simiyu, Tabora, Katavi, Manyara, Songwe na Mbeya.
Aidha, 42% ya wanawake wenye umri wa kuzaa wanakabiliwa na changamoto ya upungufu wa damu, pia tatizo la kiribatumbo na uzito uliozidi unataka kuwa janga la taifa.
Akizungumzia suala la Rushwa nchini, Waziri Kassim Majaliwa amesema mbio za mwenge za mwaka huu zitaendelea kusisitiza umuhimu wa kupambana na rushwa na kwa mujibu wa tafiti, Tanzania inafanya vizuri katika kupambana na rushwa.
Hivi karibuni imeibuka aina mpya ya bangi yenye kiasi kikubwa cha kilevi inayofahamika kama 'Cha Arusha' pamoja na 'Skanka'. Aina hii ya bangi yenye sumu nyingi huchanganywa kwenye sigara na wanaoitumia hubadilika kuwa kichaa. Ni wakati mzuri kwa vijana kuacha ili kunusuru maisha yao.
Pia soma:
Bangi ihalalishwe, Sheria zinazotumika kuhusu Bangi. Ziende kudhibiti Ushoga
Kamishna wa Kudhibiti dawa za Kulevya: Bangi ya Tanzania haifai kwenye Masoko ya Kimataifa
Serikali iruhusu kilimo cha bangi na ipunguze masharti ya uingizaji wa fedha nchini ili kukabili uhaba wa dola