Kanuni za Fedha: Jinsi ya kutengeneza pesa na kuendelea kuwa juu!

Makumbele

Member
May 9, 2009
65
390
Naandika thread hii kuwasaidia vijana walio wengi wanaokuwa wakihangaika kusaka the so called 'Utajiri' au kutaka kuwa na pesa na wanajikuta kila mara hawajui zimepotelea wapi.

Kuna threads kadhaa humu JF. Natambua uwepo wa hii thread yenye kanuni 12 Kanuni 12 muhimu za kuzingatia kuhusu pesa - JamiiForums (ambazo ninashauri pia uzisome) na Saikolojia ya fedha na kanuni za mafanikio - JamiiForums pia.

Kilicho hapa chini, ni kwa mujibu wa kitabu "The Rules of Money":

1. Kila mtu anaweza kuwa na fedha anazozitaka, ni suala la yeye kujiweka sawa kwenye kanuni za kutengeneza fedha. Kuwa na pesa ni haki ya kila mmoja bila kujali rangi, kabila, umri, historia ya wazazi wake au utaifa wake. Kila siku inafungua mlango kwako kwa ajili ya kutumia fursa zilizopo ili kuweza kutengeneza pesa unazotaka na hivyo ni muhimu kwako kujifunza mbinu wanazotumia matajiri kutengeneza pesa zaidi na mbinu hizo zipo wazi kwa kila mmoja. Kitu pekee kinachoweza kukukwamisha ni wewe mwenyewe na mtazamo wako juu ya upatikanaji wa fedha. Kanuni hii ndio kanuni kuu ya kutengeneza pesa na kanuni nyingine zinahusu wewe kujijengea misingi ya kuendelea kutengeneza pesa zaidi na ziadi.

2. Kuwa na maana yako ya neno “utajiri”. Katika kanuni hii mwandishi anatushirikisha kuwa utajiri unaanza na wewe kufafanua nini maana ya utajiri kwa mtazamo wako. Nini hasa unataka kupata ili ukishapata vitu hivyo ndo uone kuwa umekuwa tajiri. Hivyo kabla hujaanza safari ya utajiri anza kwa kuadaa orodha ya yale unayoyataka katika maisha yako ya utajiri. Hapa haupaswi kujifunga kwa kutengeneza picha finyu bali unatakiwa kuwa na fikra pana ambazo pengine zinakufanya uziogope kwa sasa.

3. Tengeneza lengo lako. Baada ya kuwa na maana yako ya utajiri ambayo ni sawa na kilele cha safari yako hivyo unapaswa kutengeneza lengo kubwa ambalo litakuwa ni njia ya kuelekea kwenye kilele hicho. Hapa unapaswa kuweka muda ambao unategemea kufikia kilele cha utajiri wako, eleza njia zipi zitatumika kufikia utajiri huo, ainisha changamoto ambazo ambazo unahisi zinaweza kukukwamisha na hatimaye kuwa na mpango wa kupambana na changamoto hizo. Lengo linatakiwa liwe linatekelezeka, lenye uhalisia na linatoka ndani mwako.

4. Lifanye lengo lako kuwa siri. Unapoanza safari ya kuishi lengo kubwa ulilojiwekea ina maana kuwa unaanza maisha mapya ambayo yatakufanya uwe mtu wa tofauti ikilinganishwa na maisha yako ya zamani. Hivyo katika maisha haya mapya wapo wengi ambao hawatafurahia jinsi unavyobadilika kutokana na chuki zao au wivu kwa vile unaelekea kwenye maisha ya tofauti na wao. Kwa hali kama hii, unatakiwa malengo uliyojiwekea yawe siri yako ili usikatishwe tamaa na maneno ya jamii inayokuzunguka.

5. Watu wengi ni wavivu wa kufikia utajiri wao. Hakuna njia nyingine ya kuwa tajiri zaidi ya kufanya kazi kwa bidii. Ni lazima uwe tayari kufanya kazi kwa nguvu zako zote kuhakikisha unafanikisha malengo uliyojiwekea. Hakikisha unaamka asubuhi na kuanza kutekeleza majukumu yako ya kila siku na hata pale unapoenda kulala fanya hivyo ukiwa katika picha kubwa ya lengo kubwa la maisha yako.

Usitegemee kuwa tajiri kwa fedha za kurithi, fedha za bahati nasibu au fedha za kuokota. Watu wengi wanataka utajiri lakini hawapo tayari kujibidisha ili wafikie utajiri huo, hawapo tayari kujifunza, hawapo tayari kufanya kazi, hawapo tayari kutoa sadaka kwa ajili ya kuupata utajiri na mbaya zaidi wengi wana fikra hasi kuwa ili uwe tajiri ni lazima uende kwa wachawi au utajiri ni kwa ajili ya wateule wachache. Utajiri wa kweli hauko hivyo bali ni lazima uandaliwe kwa kutumia misingi na mifumo ambayo inakuhusisha wewe kama mhusika mkuu wa safari hii. Hii ni kutokana na ukweli kwamba matajiri wote wana sifa kubwa ya kufanya kazi za ziada kiasi kwamba kazi wanazofanya kwa siku ni zaidi ya zile tunazofanya kwa mwezi mzima.

6. Jifanyie tathmini ambayo ni ya kweli. Ili uwe tajiri ni lazima ujifanyie upekuzi kwanza. Katika upekuzi huu unatakiwa kufahamu ni tabia zipi ambazo zimekufikisha hapo ulipo na hatimaye weka mikakati ya kukabiliana na tabia ambazo zinakukwamisha. Kaa chini na fikiria ni tabia zipi ambazo ukianza kuzifanya zitapelekea utajiri wako uongezeke na anza mara moja kuzifanyia kazi. Kuwa mkweli kwenye matumizi ya pesa yako, muda, marafiki na manunuzi yako. Kisha jenga tabia ya kutenga kiasi cha fedha kwenye kila shilingi inayoingia mkononi mwako kwa ajili ya uwekezaji wa muda mfupi na muda mrefu.

7. Fahamu imani/kauli zako kuhusu pesa na vyanzo vya kauli hizo. Katika jamii tunazoishi kuna kila kauli juu ya fedha na utajiri kwa ujumla. Wapo wanaoamini kuwa pesa ni chanzo cha maovu yote, utajiri ni kwa wateule tu, matajiri ni watu wabaya, walafi, wachoyo, wachawi kwa maana ya kwamba hauwezi kuwa na fedha na kwa wakati huo huo ukawa msafi wa roho, ni afadhali kuwa maskini na kauli nyinginezo. Je, wewe imani/kauli zako juu ya fedha na utajiri ni zipi? Pata muda wa kutafakari na hatimaye jipe imani/kauli mpya ambazo zitakupeleka kwenye mtazamo mpya juu ya pesa na utajiri.

8. Fahamu kuwa Utajiri ni Mchakato na si zawadi. Katika kutafuta utajiri, ni lazima ujitoe kufanya kazi kwa bidii ili fedha zifuatie kama zawadi kwa bidii na ubunifu katika utendaji kazi wako. Kadri unavyofanyakazi kwa bidii na ubunifu, ndivyo utavyopata pesa zaidi.

9. Andaa sababu zinazokusukuma kuwa tajiri. Hakikisha unaandaa sababu za kwanini unataka kuwa tajiri. Eleza nini utafanyia pesa zako pindi ukiwa na pesa za ndoto yako, chagua ni starehe zipi utakuwa nazo pindi ukiwa tajiri, sehemu zipi utapenda kutembelea, vitega uchumi vipi utapenda kuwa navyo n.k. Hapa unatakiwa kuandaa sababu ambazo zitakufanya uridhike na kufurahia utajiri wako badala ya kuja kuangamizwa na utajiri wako. Pia andaa orodha ya vitu ambavyo hautakuwa tayari kufanya kupitia utajiri wako ili kesho na keshokutwa uongozwe na hiyo kuepuka matumizi mabaya ya fedha zako.

10. Fahamu kuwa Pesa zinatengeneza Pesa. Tumia pesa zako kuhakikisha zinatengeneza pesa nyingine zaidi na zaidi. Ndio maana matajiri wanaendelea kuwa matajiri wakati masikini nao wanaendelea kuwa masikini. Hivyo kwa kutumia kanuni hii unatakiwa kutumia pesa kidogo ulizonazo sasa kwa ajili ya kuzalisha pesa zaidi na zaidi kwani hiyo ndo njia pekee ya kuwa tajiri. Hakikisha unatenga kiasi cha pesa katika pato lako kwa ajili ya kuwekeza ili kiasi hicho ndo kitumike kama mbegu ya kuzalisha pesa nyingine. Kama ilivyo kwa mkulima au mfugaji hawezi kula mbegu au mifugo yake yote na akategemea kuzalisha zaidi shambani au mifugo kuongezeka ndivyo ilivyo kwenye fedha. Uamzi upo mikononi mwako kati ya kuchagua kuwa masikini au kuwa kati ya matajiri.

11. Kokotoa faida kabla ya kuwekeza fedha zako. Utajiri ni hesabu hivyo unatakiwa kabla ya kuwekeza kwenye kitega uchumi chochote kile ni lazima ufanye hesabu za kufahamu faida yako itakuwa kiasi gani hadi pale utakapofanikiwa kurejesha kiasi ulichowekeza. Changanua faida na hasara kwenye kila aina ya uwekezaji unaotaka kufanya. Unapochanganua faida za mradi flani, unatakiwa kukumbuka suala la kodi na gharama nyingine ambazo zitawezesha mradi wako uendelee kukuingizia faida.

12. Kama utachukulia pesa kama suluhisho la matatizo utaiona kama chanzo cha matatizo. Katika safari yako ya utajiri ni lazima ukumbuke kuwa pesa hazitaweza kumaliza matatizo yako yote ya kimahusiano, afya, kijamii, usalama, kiroho na furaha. Hivyo ni muhimu kufahamu fika matatizo yote hayo wewe ndo muhusika mkuu wa kuyatatua na wala sio fedha zako. Fedha haziwezi kukupa furaha ya kudumu, amani, upendo, kupunguza uzito wa mwili wako na mengine mengi na badala yake vitu hivi vinaanzia ndani mwako.

13. Unaweza Kutengeneza Pesa za Kutosha, Unaweza Kuipenda Kazi yako na Unaweza Kupata Usingizi Vizuri. Kwenye jamii kumekuwepo na upotoshaji kuwa ili kuwa tajiri ni lazima kwanza uuze roho yako au uwatoe sadaka ndugu zako, uwe mchoyo, kukosa usingizi na kukosa muda wa kuwajali watu wengine; lakini ukweli ni kwamba utajiri wa kweli ni kinyume kabisa na mitazamo hiyo. Hii ni kutokana na ukweli ambao tumeuona kwenye kanuni ya kwanza kuwa fedha zipo nyingi na za kutosha kwa ajili ya yeyote yule ambaye anajua mbinu halali za kuzitafuta na mbinu hizo zipo wazi kwa kila mmoja. Hivyo wewe ndo mwamuzi wa maisha yako ya utajiri lakini muhimu ni kufahamu kuwa unaweza kuwa tajiri na ukaendelea kupenda kazi yako na kupata usingizi vizuri tu.

14. Usitengeneze Pesa kwa kuwa Mtu Mbaya. Hakikisha unatafuta utajiri kwa njia ambazo ni halali kwani pesa za namna hii ndo zitakupa amani kutoka rohoni mwako tofauti na fedha za wizi, udanganyifu, rushwa, uchawi au kwa kuvunja sheria kwa namna yoyote ile. Ni muhimu zoezi la kutengeneza fedha ulichukulie kama sehemu ya mchezo ambao huwa unaupenda sana na hivyo uendelee kutengeneza fedha kwa kadri upendavyo kupitia mchezo wa fedha. Hii ni kutokana na ukweli kwamba tunahitaji utajiri kwa ajili ya kuendelea kuyaboresha maisha yetu hivyo hatupo tayari kuona utajiri wetu unakuwa chanzo cha kutuweka mbali na wapendwa wetu, kazi zetu, nyumba zetu, hobi zetu na mengine mengi.

15. Fahamu Uhusiano Kati ya Pesa na Furaha. Ni muhimu kufahamu kuwa pesa haiwezi kununua furaha. Wote ni mashahidi kuwa pesa kidogo zinaweza kukufanya uwe na maisha ya huzuni hasa pale mahitaji ya pesa yanapozidi kiasi ulicho nacho. Hata hivyo wapo matajiri wengi ambao wanaishi maisha ya huzuni pamoja na kwamba wana pesa nyingi. Muhimu ni kufahamu kuwa unaweza kuwa masikini/tajiri na ukawa na furaha au ukakosa maisha ya furaha. Hivyo, jambo la muhimu unatakiwa ufahamu kuwa furaha inaanzia ndani mwako pasipo kujali kipato ulicho nacho. Hii ni kutokana na ukweli kwamba sio pesa au vitu unavyomiliki vitakufanya uwe na furaha bali furaha unaitengeneza mwenyewe.

16. Fahamu Tofauti kati ya Bei na Thamani. Sio lazima bei ya kitu iendane na thamani ya kitu hicho. Mfano, ni kawaida sana kukuta chupa moja ya soda katika duka la kawaida inauzwa kwa shilingi 1,000/ lakini soda hiyohiyo ikauzwa kwa shilingi 5,000/ katika hotel kubwa. Kinachotofautisha bei ni mazingira ambayo soda hiyo inatolewa kwa mteja. Somo la kujifunza ni kwamba watu wapo tayari kulipia ongezeko la thamani ya huduma yako kuliko thamani halisi ya huduma husika. Kama unataka kuwa tajiri ni lazima ufahamu somo hili na kulitumia kwa ajili ya kuzalisha faida zaidi kwa ajili ya kuongeza utajiri wako.

17. Fahamu Jinsi Matajiri Wanavyofikiri. Kama unataka kuwa tajiri ni lazima uwe tayari kujifunza maisha ya matajiri jinsi wanavyofikiria, wanvyofanya kazi, wanavyovaa, wanavyotumia pesa zao na maisha yao kwa ujumla. Hii ni kutokana na ukweli kwamba kama unaenda vitani kwa ajili ya ushindi ni lazima utumie muda mwingi kumsoma mpinzani wako ili utakapokuwa kwenye uwanja wa vita asikusumbue. Ndivyo ilivyo kwenye kutengeneza utajiri; ni lazima uwe tayari kufahamu zaidi juu pesa, upate muda wa kuongea na matajiri, kusoma historia zao na kuhakikisha unakuwa na kiu ya kufahamu mbinu wanazotumia kukuza utajiri wao.

18. Usiwe na Wivu na Mafanikio ya Wengine. Wote tunaweka juhudi kila mmoja kwa muda wake na kila mmoja mipango yake hivyo hakuna sababu ya kuwa na wivu kwa mafanikio ya wengine kwani jinsi walivyo ni matokeo ya jitihada na ubunifu katika kazi zao. Jambo la muhimu unaloweza kufanya ni kujifunza kutoka kwao ili kufahamu namna ambavyo wamefanikisha ndoto za maisha yao. Hivyo kila unapopata nafasi ya kukutana na mtu mwenye mafanikio hakikisha unajifunza kitu kipya kutoka kwake. Fanya yale wanayoyafanya matajiri na hatimaye na wewe utakuwa kama wao.

MWISHO:
Kazi kubwa iliyopo mbele yako ni wewe kubadilika na kufanya yale yanayofanywa na matajiri. Kwa maana nyingine kubadilisha tabia zako ili ziendane na tabia za matajiri. Hapa unapaswa kujiuliza maswali kama haya:-
Je, nipo tayari kuanza safari ya utajiri?
Je, nipo tayari kubadilika?
Je, nina nia ya kweli ya kuwa tajiri?
Je, nipo tayari kuvumilia pasipo kukata tamaa?
Je, nina nguvu za kutosha?

Majibu ya maswali haya ni mwanga tosha kuonesha kama upo tayari kuanza safari ya utajiri. Ukifanikiwa katika hatua hii ndipo utagundua kuwa ni vigumu kujidhibiti kuliko ambavyo utadhibiti pesa yako.
 
Mengi umeandika ni ya msingi kufuata ili mtu ufanikiwe kufika walau daraja la kati, ambalo ndio hupaswa kila mtu aishi daraja hilo.
Kwangu utajiri si kipaumbele na sioni umuhimu wa kuwa tajiri.
Mahitaji ya msingi ya mwanadamu yatimilike bila wasi wasi hilo ndio muhimu.
 
Mengi umeandika ni ya msingi kufuata ili mtu ufanikiwe kufika walau daraja la kati, ambalo ndio hupaswa kila mtu aishi daraja hilo.
Kwangu utajiri si kipaumbele na sioni umuhimu wa kuwa tajiri.
Mahitaji ya msingi ya mwanadamu yatimilike bila wasi wasi hilo ndio muhimu.

Unaingia pale kwenye paragraph namba 3 Mkuu, una maana yako halisi ya Maendeleo
 
Naandika thread hii kuwasaidia vijana walio wengi wanaokuwa wakihangaika kusaka the so called 'Utajiri' au kutaka kuwa na pesa na wanajikuta kila mara hawajui zimepotelea wapi.

Kuna threads kadhaa humu JF. Natambua uwepo wa hii thread yenye kanuni 12 Kanuni 12 muhimu za kuzingatia kuhusu pesa - JamiiForums (ambazo ninashauri pia uzisome) na Saikolojia ya fedha na kanuni za mafanikio - JamiiForums pia.

Kilicho hapa chini, ni kwa mujibu wa kitabu "The Rules of Money":

1. Kila mtu anaweza kuwa na fedha anazozitaka, ni suala la yeye kujiweka sawa kwenye kanuni za kutengeneza fedha. Kuwa na pesa ni haki ya kila mmoja bila kujali rangi, kabila, umri, historia ya wazazi wake au utaifa wake. Kila siku inafungua mlango kwako kwa ajili ya kutumia fursa zilizopo ili kuweza kutengeneza pesa unazotaka na hivyo ni muhimu kwako kujifunza mbinu wanazotumia matajiri kutengeneza pesa zaidi na mbinu hizo zipo wazi kwa kila mmoja. Kitu pekee kinachoweza kukukwamisha ni wewe mwenyewe na mtazamo wako juu ya upatikanaji wa fedha. Kanuni hii ndio kanuni kuu ya kutengeneza pesa na kanuni nyingine zinahusu wewe kujijengea misingi ya kuendelea kutengeneza pesa zaidi na ziadi.

2. Kuwa na maana yako ya neno “utajiri”. Katika kanuni hii mwandishi anatushirikisha kuwa utajiri unaanza na wewe kufafanua nini maana ya utajiri kwa mtazamo wako. Nini hasa unataka kupata ili ukishapata vitu hivyo ndo uone kuwa umekuwa tajiri. Hivyo kabla hujaanza safari ya utajiri anza kwa kuadaa orodha ya yale unayoyataka katika maisha yako ya utajiri. Hapa haupaswi kujifunga kwa kutengeneza picha finyu bali unatakiwa kuwa na fikra pana ambazo pengine zinakufanya uziogope kwa sasa.

3. Tengeneza lengo lako. Baada ya kuwa na maana yako ya utajiri ambayo ni sawa na kilele cha safari yako hivyo unapaswa kutengeneza lengo kubwa ambalo litakuwa ni njia ya kuelekea kwenye kilele hicho. Hapa unapaswa kuweka muda ambao unategemea kufikia kilele cha utajiri wako, eleza njia zipi zitatumika kufikia utajiri huo, ainisha changamoto ambazo ambazo unahisi zinaweza kukukwamisha na hatimaye kuwa na mpango wa kupambana na changamoto hizo. Lengo linatakiwa liwe linatekelezeka, lenye uhalisia na linatoka ndani mwako.

4. Lifanye lengo lako kuwa siri. Unapoanza safari ya kuishi lengo kubwa ulilojiwekea ina maana kuwa unaanza maisha mapya ambayo yatakufanya uwe mtu wa tofauti ikilinganishwa na maisha yako ya zamani. Hivyo katika maisha haya mapya wapo wengi ambao hawatafurahia jinsi unavyobadilika kutokana na chuki zao au wivu kwa vile unaelekea kwenye maisha ya tofauti na wao. Kwa hali kama hii, unatakiwa malengo uliyojiwekea yawe siri yako ili usikatishwe tamaa na maneno ya jamii inayokuzunguka.

5. Watu wengi ni wavivu wa kufikia utajiri wao. Hakuna njia nyingine ya kuwa tajiri zaidi ya kufanya kazi kwa bidii. Ni lazima uwe tayari kufanya kazi kwa nguvu zako zote kuhakikisha unafanikisha malengo uliyojiwekea. Hakikisha unaamka asubuhi na kuanza kutekeleza majukumu yako ya kila siku na hata pale unapoenda kulala fanya hivyo ukiwa katika picha kubwa ya lengo kubwa la maisha yako.

Usitegemee kuwa tajiri kwa fedha za kurithi, fedha za bahati nasibu au fedha za kuokota. Watu wengi wanataka utajiri lakini hawapo tayari kujibidisha ili wafikie utajiri huo, hawapo tayari kujifunza, hawapo tayari kufanya kazi, hawapo tayari kutoa sadaka kwa ajili ya kuupata utajiri na mbaya zaidi wengi wana fikra hasi kuwa ili uwe tajiri ni lazima uende kwa wachawi au utajiri ni kwa ajili ya wateule wachache. Utajiri wa kweli hauko hivyo bali ni lazima uandaliwe kwa kutumia misingi na mifumo ambayo inakuhusisha wewe kama mhusika mkuu wa safari hii. Hii ni kutokana na ukweli kwamba matajiri wote wana sifa kubwa ya kufanya kazi za ziada kiasi kwamba kazi wanazofanya kwa siku ni zaidi ya zile tunazofanya kwa mwezi mzima.

6. Jifanyie tathmini ambayo ni ya kweli. Ili uwe tajiri ni lazima ujifanyie upekuzi kwanza. Katika upekuzi huu unatakiwa kufahamu ni tabia zipi ambazo zimekufikisha hapo ulipo na hatimaye weka mikakati ya kukabiliana na tabia ambazo zinakukwamisha. Kaa chini na fikiria ni tabia zipi ambazo ukianza kuzifanya zitapelekea utajiri wako uongezeke na anza mara moja kuzifanyia kazi. Kuwa mkweli kwenye matumizi ya pesa yako, muda, marafiki na manunuzi yako. Kisha jenga tabia ya kutenga kiasi cha fedha kwenye kila shilingi inayoingia mkononi mwako kwa ajili ya uwekezaji wa muda mfupi na muda mrefu.

7. Fahamu imani/kauli zako kuhusu pesa na vyanzo vya kauli hizo. Katika jamii tunazoishi kuna kila kauli juu ya fedha na utajiri kwa ujumla. Wapo wanaoamini kuwa pesa ni chanzo cha maovu yote, utajiri ni kwa wateule tu, matajiri ni watu wabaya, walafi, wachoyo, wachawi kwa maana ya kwamba hauwezi kuwa na fedha na kwa wakati huo huo ukawa msafi wa roho, ni afadhali kuwa maskini na kauli nyinginezo. Je, wewe imani/kauli zako juu ya fedha na utajiri ni zipi? Pata muda wa kutafakari na hatimaye jipe imani/kauli mpya ambazo zitakupeleka kwenye mtazamo mpya juu ya pesa na utajiri.

8. Fahamu kuwa Utajiri ni Mchakato na si zawadi. Katika kutafuta utajiri, ni lazima ujitoe kufanya kazi kwa bidii ili fedha zifuatie kama zawadi kwa bidii na ubunifu katika utendaji kazi wako. Kadri unavyofanyakazi kwa bidii na ubunifu, ndivyo utavyopata pesa zaidi.

9. Andaa sababu zinazokusukuma kuwa tajiri. Hakikisha unaandaa sababu za kwanini unataka kuwa tajiri. Eleza nini utafanyia pesa zako pindi ukiwa na pesa za ndoto yako, chagua ni starehe zipi utakuwa nazo pindi ukiwa tajiri, sehemu zipi utapenda kutembelea, vitega uchumi vipi utapenda kuwa navyo n.k. Hapa unatakiwa kuandaa sababu ambazo zitakufanya uridhike na kufurahia utajiri wako badala ya kuja kuangamizwa na utajiri wako. Pia andaa orodha ya vitu ambavyo hautakuwa tayari kufanya kupitia utajiri wako ili kesho na keshokutwa uongozwe na hiyo kuepuka matumizi mabaya ya fedha zako.

10. Fahamu kuwa Pesa zinatengeneza Pesa. Tumia pesa zako kuhakikisha zinatengeneza pesa nyingine zaidi na zaidi. Ndio maana matajiri wanaendelea kuwa matajiri wakati masikini nao wanaendelea kuwa masikini. Hivyo kwa kutumia kanuni hii unatakiwa kutumia pesa kidogo ulizonazo sasa kwa ajili ya kuzalisha pesa zaidi na zaidi kwani hiyo ndo njia pekee ya kuwa tajiri. Hakikisha unatenga kiasi cha pesa katika pato lako kwa ajili ya kuwekeza ili kiasi hicho ndo kitumike kama mbegu ya kuzalisha pesa nyingine. Kama ilivyo kwa mkulima au mfugaji hawezi kula mbegu au mifugo yake yote na akategemea kuzalisha zaidi shambani au mifugo kuongezeka ndivyo ilivyo kwenye fedha. Uamzi upo mikononi mwako kati ya kuchagua kuwa masikini au kuwa kati ya matajiri.

11. Kokotoa faida kabla ya kuwekeza fedha zako. Utajiri ni hesabu hivyo unatakiwa kabla ya kuwekeza kwenye kitega uchumi chochote kile ni lazima ufanye hesabu za kufahamu faida yako itakuwa kiasi gani hadi pale utakapofanikiwa kurejesha kiasi ulichowekeza. Changanua faida na hasara kwenye kila aina ya uwekezaji unaotaka kufanya. Unapochanganua faida za mradi flani, unatakiwa kukumbuka suala la kodi na gharama nyingine ambazo zitawezesha mradi wako uendelee kukuingizia faida.

12. Kama utachukulia pesa kama suluhisho la matatizo utaiona kama chanzo cha matatizo. Katika safari yako ya utajiri ni lazima ukumbuke kuwa pesa hazitaweza kumaliza matatizo yako yote ya kimahusiano, afya, kijamii, usalama, kiroho na furaha. Hivyo ni muhimu kufahamu fika matatizo yote hayo wewe ndo muhusika mkuu wa kuyatatua na wala sio fedha zako. Fedha haziwezi kukupa furaha ya kudumu, amani, upendo, kupunguza uzito wa mwili wako na mengine mengi na badala yake vitu hivi vinaanzia ndani mwako.

13. Unaweza Kutengeneza Pesa za Kutosha, Unaweza Kuipenda Kazi yako na Unaweza Kupata Usingizi Vizuri. Kwenye jamii kumekuwepo na upotoshaji kuwa ili kuwa tajiri ni lazima kwanza uuze roho yako au uwatoe sadaka ndugu zako, uwe mchoyo, kukosa usingizi na kukosa muda wa kuwajali watu wengine; lakini ukweli ni kwamba utajiri wa kweli ni kinyume kabisa na mitazamo hiyo. Hii ni kutokana na ukweli ambao tumeuona kwenye kanuni ya kwanza kuwa fedha zipo nyingi na za kutosha kwa ajili ya yeyote yule ambaye anajua mbinu halali za kuzitafuta na mbinu hizo zipo wazi kwa kila mmoja. Hivyo wewe ndo mwamuzi wa maisha yako ya utajiri lakini muhimu ni kufahamu kuwa unaweza kuwa tajiri na ukaendelea kupenda kazi yako na kupata usingizi vizuri tu.

14. Usitengeneze Pesa kwa kuwa Mtu Mbaya. Hakikisha unatafuta utajiri kwa njia ambazo ni halali kwani pesa za namna hii ndo zitakupa amani kutoka rohoni mwako tofauti na fedha za wizi, udanganyifu, rushwa, uchawi au kwa kuvunja sheria kwa namna yoyote ile. Ni muhimu zoezi la kutengeneza fedha ulichukulie kama sehemu ya mchezo ambao huwa unaupenda sana na hivyo uendelee kutengeneza fedha kwa kadri upendavyo kupitia mchezo wa fedha. Hii ni kutokana na ukweli kwamba tunahitaji utajiri kwa ajili ya kuendelea kuyaboresha maisha yetu hivyo hatupo tayari kuona utajiri wetu unakuwa chanzo cha kutuweka mbali na wapendwa wetu, kazi zetu, nyumba zetu, hobi zetu na mengine mengi.

15. Fahamu Uhusiano Kati ya Pesa na Furaha. Ni muhimu kufahamu kuwa pesa haiwezi kununua furaha. Wote ni mashahidi kuwa pesa kidogo zinaweza kukufanya uwe na maisha ya huzuni hasa pale mahitaji ya pesa yanapozidi kiasi ulicho nacho. Hata hivyo wapo matajiri wengi ambao wanaishi maisha ya huzuni pamoja na kwamba wana pesa nyingi. Muhimu ni kufahamu kuwa unaweza kuwa masikini/tajiri na ukawa na furaha au ukakosa maisha ya furaha. Hivyo, jambo la muhimu unatakiwa ufahamu kuwa furaha inaanzia ndani mwako pasipo kujali kipato ulicho nacho. Hii ni kutokana na ukweli kwamba sio pesa au vitu unavyomiliki vitakufanya uwe na furaha bali furaha unaitengeneza mwenyewe.

16. Fahamu Tofauti kati ya Bei na Thamani. Sio lazima bei ya kitu iendane na thamani ya kitu hicho. Mfano, ni kawaida sana kukuta chupa moja ya soda katika duka la kawaida inauzwa kwa shilingi 1,000/ lakini soda hiyohiyo ikauzwa kwa shilingi 5,000/ katika hotel kubwa. Kinachotofautisha bei ni mazingira ambayo soda hiyo inatolewa kwa mteja. Somo la kujifunza ni kwamba watu wapo tayari kulipia ongezeko la thamani ya huduma yako kuliko thamani halisi ya huduma husika. Kama unataka kuwa tajiri ni lazima ufahamu somo hili na kulitumia kwa ajili ya kuzalisha faida zaidi kwa ajili ya kuongeza utajiri wako.

17. Fahamu Jinsi Matajiri Wanavyofikiri. Kama unataka kuwa tajiri ni lazima uwe tayari kujifunza maisha ya matajiri jinsi wanavyofikiria, wanvyofanya kazi, wanavyovaa, wanavyotumia pesa zao na maisha yao kwa ujumla. Hii ni kutokana na ukweli kwamba kama unaenda vitani kwa ajili ya ushindi ni lazima utumie muda mwingi kumsoma mpinzani wako ili utakapokuwa kwenye uwanja wa vita asikusumbue. Ndivyo ilivyo kwenye kutengeneza utajiri; ni lazima uwe tayari kufahamu zaidi juu pesa, upate muda wa kuongea na matajiri, kusoma historia zao na kuhakikisha unakuwa na kiu ya kufahamu mbinu wanazotumia kukuza utajiri wao.

18. Usiwe na Wivu na Mafanikio ya Wengine. Wote tunaweka juhudi kila mmoja kwa muda wake na kila mmoja mipango yake hivyo hakuna sababu ya kuwa na wivu kwa mafanikio ya wengine kwani jinsi walivyo ni matokeo ya jitihada na ubunifu katika kazi zao. Jambo la muhimu unaloweza kufanya ni kujifunza kutoka kwao ili kufahamu namna ambavyo wamefanikisha ndoto za maisha yao. Hivyo kila unapopata nafasi ya kukutana na mtu mwenye mafanikio hakikisha unajifunza kitu kipya kutoka kwake. Fanya yale wanayoyafanya matajiri na hatimaye na wewe utakuwa kama wao.

MWISHO:
Kazi kubwa iliyopo mbele yako ni wewe kubadilika na kufanya yale yanayofanywa na matajiri. Kwa maana nyingine kubadilisha tabia zako ili ziendane na tabia za matajiri. Hapa unapaswa kujiuliza maswali kama haya:-
Je, nipo tayari kuanza safari ya utajiri?
Je, nipo tayari kubadilika?
Je, nina nia ya kweli ya kuwa tajiri?
Je, nipo tayari kuvumilia pasipo kukata tamaa?
Je, nina nguvu za kutosha?

Majibu ya maswali haya ni mwanga tosha kuonesha kama upo tayari kuanza safari ya utajiri. Ukifanikiwa katika hatua hii ndipo utagundua kuwa ni vigumu kujidhibiti kuliko ambavyo utadhibiti pesa yako.
God bless you, masomo kama haya hata usome phd huwezi kuyakuta kwenye syllabus
 
Ukitaka kufanikiwa go against the norms!become the blacksheep of the sorrounded pipo!
Simply and well said; kuwa tajiri somehow uwe na roho mbaya + upate wa kumnyonya. Pia matajiri wengi Wana untold stories behind the scene na wanafanya Siri daima. Kufanikiwa na kuwa tajiri hakuna formula.
Ni juhudi+Bahati.
 
Back
Top Bottom