mafinga sio jkt mkuu
kambi active za mafunzo ya jkt kwa sasa ni ...Kanembwa, Bulomborwa (zote Kigoma), Mgambo na Maramba (zote Tanga), Ruvu (Pwani), Msange (Tabora), Rwamkoma(Musoma), pamoja na Mlale(Songea). Hatuwez kusema kambi ipi ina ugumu au urahisi kimafunzo maana hilo suala linategemeana na wakufunzi ambao huwa wanahamishwa vikosi kila leo kwahyo cha msingi ufungue moyo uamini utamaliza depo regardless of kambi utakayopangwa na ujiulize hao waliopita huko wakahitimu wana nini cha ziada ambacho wewe huna?!. Lakini pia kwa upande mwingine wa shilingi kwenye suala la uzalishaji mali kambi ya Mgambo 835KJ wanalima sana wana mashamba ukubwa karibia sawa na umbali wa mbagala-kawe, mlale, msange na kanembwa pia wako vzuri ila cyo kama mgambo, ukitaka kazi wastani nenda maramba au rwamkoma maana viko town, ruvu hapo utalima mpunga mpaka utaomba poo, uwe na adabu maana degree yko unaiacha getini na si ajabu ukiamrishwa kufanya hzo kaz ngumu na katoto tu cha darasa la 7 kalichokuzid cheo so uvumilivu unahitajika
Ulichoongea ni sahihi kiongozi
Yale mashamba ya 835kj mgambo nayafahamu vizuri sana
"Genda genda" "Kwa msanga" ni makubwa kupita maelezo. Jeshi letu linalima si masihara
Na pia muambie huyo mdogo wako "anywe maji mengi"
maji anayonywea nyumbani yatamsaidia vipi kambini??????????
mafinga ipo jkt kijana....na ni majanga sana kwa kokoto,misitu,milima na baridi mpaka mvuke puani na mdom
kwa uelewa wangu mafinga ni kambi ya mafunzo ya tpdf(bakabaka or jeshi kamili)
na si jkt
Ukipitia jkt utaelewa ninachokiongelea hapo