Mimi nimeshangazwa na Wenyeviti wa baadhi ya Kamati za bunge letu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na hasa hawa waliochaguliwa majuzi kuongoza kamati za nishati, miundombinu na kamati ya mambo ya nje, ulinzi na usalama.
Muda mfupi baada ya wakubwa hawa kuteuliwa wamekuwa wanatoa matamko mbalimbali ambayo yanaleta picha kana kwamba wao ni wasemaji wa wizara zilizo chini ya kamati hizo. Wakati mwingine wao wamekuwa kama watendaji wa serikali. Mifano miwili ya haraka ni mwenyekiti wa kamait ya nishati na madini ambaye ame-take advantage ya mgao wa umeme kuwa kama vile yeye ndiye waziri na wakati mwingine MD wa Tanesco. Mfano wa pili ni mwenyekiti wa kamati ya mambo ya nje , ulinzi na usalama ambaye naye ametoa tamko zito kuhusu harakati na hatimaye mapinduzi ya umma yaliyohitimisha utawala wa Mubarak. Mkubwa huyu alitoa tamko ambalo kwa kweli liliibua hisia kwamba huo ndiyo msimamo wa Tanzania bila kujali athari za kidiplomasia na hasa kwa kuzingatia mahusiano yetu na Misri na ukweli kwamba mpaka sasa hivi bado mabaki ya utawala wa Mubarak (kupitia jeshi) yapo madarakani. Ukiachilia mbali unafiki uliojaa katika tamko lake hilo (maana yeye hana tofauti na Mubaraka kwa uchu wa madaraka na kujilimbikizia mali), mimi nafikiri kamati hizi ni vizuri zikaelewa kwamba zenyewe ni watchdog institutions zikitekeleza majukumu ya bunge ambayo ni kuishauri na kuikosoa serikali pale inapobidi. Vinginevyo tutajikuta tukishuhudia watu wakijinyakulia madaraka ya uwaziri wakati hawamo kwenye baraza la mawaziri. Hili ni baya, hasa linapofanywa na kusumkumwa na ajenda ya 2015.
Muda mfupi baada ya wakubwa hawa kuteuliwa wamekuwa wanatoa matamko mbalimbali ambayo yanaleta picha kana kwamba wao ni wasemaji wa wizara zilizo chini ya kamati hizo. Wakati mwingine wao wamekuwa kama watendaji wa serikali. Mifano miwili ya haraka ni mwenyekiti wa kamait ya nishati na madini ambaye ame-take advantage ya mgao wa umeme kuwa kama vile yeye ndiye waziri na wakati mwingine MD wa Tanesco. Mfano wa pili ni mwenyekiti wa kamati ya mambo ya nje , ulinzi na usalama ambaye naye ametoa tamko zito kuhusu harakati na hatimaye mapinduzi ya umma yaliyohitimisha utawala wa Mubarak. Mkubwa huyu alitoa tamko ambalo kwa kweli liliibua hisia kwamba huo ndiyo msimamo wa Tanzania bila kujali athari za kidiplomasia na hasa kwa kuzingatia mahusiano yetu na Misri na ukweli kwamba mpaka sasa hivi bado mabaki ya utawala wa Mubarak (kupitia jeshi) yapo madarakani. Ukiachilia mbali unafiki uliojaa katika tamko lake hilo (maana yeye hana tofauti na Mubaraka kwa uchu wa madaraka na kujilimbikizia mali), mimi nafikiri kamati hizi ni vizuri zikaelewa kwamba zenyewe ni watchdog institutions zikitekeleza majukumu ya bunge ambayo ni kuishauri na kuikosoa serikali pale inapobidi. Vinginevyo tutajikuta tukishuhudia watu wakijinyakulia madaraka ya uwaziri wakati hawamo kwenye baraza la mawaziri. Hili ni baya, hasa linapofanywa na kusumkumwa na ajenda ya 2015.