Kamati ya bunge "yakataa" ardhi ya Tanzania kutumika kwa manufaa ya EAC.

Ngongo

JF-Expert Member
Sep 20, 2008
18,921
31,161
Kamati ya bunge ya mambo ya nje,ulinzi na usalama umeitaka serekali kukataa muundo wowote wa ushirikiano wa Afrika mashariki utakaoruhusu ardhi ya Tanzania kutumika kwa manufaa ya shirikisho.
Kamati ya bunge imeitaka serekali kuwa makini na suala la ardhi kwani ni rasilimali adimu na urithi pekeewa wananchi wa Tanzania.
Kamati ya bunge iliwasilisha rasmi mapendekezo yake kwa waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa mheshimiwa B Membe.
 
Wadau

Kwa hili naomba niipongeze kamati ya Bunge kwa Kazi nzuri iliyoifanya kwani wangeruhusu hardhi yetu itumike kwa manufaaa ya EAC, basi kesho nyake ungeona majiranizutu wa EAC wangevamia kila sehemu ili wapate ardhi. Mfano angalia Kenya wanapigana mpaka leo kwa sababu ya ardhi, the same to Rwanda na Burundi.

Walikuwa wanavizia tukubali ardhi itumike eti kwa manufaa ya EAC. NANI ANATAKA UPUMBAVU HUO. Yaani wanatuona sisi WA TZ ni Mafalaaaaaaaaaaaaa kumbe wao ndio mafalaaaaaaaaaaaa tena wakutupa
 
Kamati ya Bunge wanastahili pongezi kwa hili kwani kumekuwa na tetesi kwamba Wakenya wanataka kutumia mgongo wa Jumuia ya Afrika Mashariki kununua Ardhi ya TZ kwa kuwa wana uwezo kifedha.Tena ni vema kutumia fursa hii kuchunguza Wakenya waliojitwalia Ardhi kinyemela na kuirudisha kwa wananchi.
 
Hakuna mtanzania halisi atakayepingana na kamati ya bunge ya mambo nje,ulinzi na usalama.Tatizo langu mpaka sasa watanzania bado tumeshikilia ardhi tu bila kuangalia mambo mengine muhimu kama free movement nadhani nalo ni hatari sana hasa katika sector ya utalii na usalama wetu.Miaka ya nyuma wakenya waliidanganya dunia kuwa mlima Kilimanjaro uko Kenya sasa kama free movememnt nayo isipoangaliwa vizuri tutarudi kulekule tulikotoka.
Sector ya utalii inatoa mchango mkubwa katika kukuza pato la taifa hakuna asiyejua wenzetu wamepiga hatua kubwa katika sector ya utalii tusipo angalia makampuni makubwa yaliyopo Tanzania yanaweza kutoweka kabisa.
 
Kamati ya bunge ya mambo ya nje,ulinzi na usalama umeitaka serekali kukataa muundo wowote wa ushirikiano wa Afrika mashariki utakaoruhusu ardhi ya Tanzania kutumika kwa manufaa ya shirikisho.
Kamati ya bunge imeitaka serekali kuwa makini na suala la ardhi kwani ni rasilimali adimu na urithi pekeewa wananchi wa Tanzania.
Kamati ya bunge iliwasilisha rasmi mapendekezo yake kwa waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa mheshimiwa B Membe.

Mkuu Ngogo, huu ni msimamo saafi kabisa na ni a true reflection ya maoni ya wa TZ wengi.Ushirikiano ambao jirani yako anainsist kulala nyumbani kwako lazima uwe suspect.
Ushirikiano uanzie katika kuratify tarriffs za kodi,viwango vya bidhaa na huduma nk
Hatimae kuainisha sera za kidemokrasia katika nchi zetu kuzuia migogoro ya kisiasa.
Tusipofanya hivyo tutakaribisha madudu ya nchi nyingine.
 
Hakuna mtanzania halisi atakayepingana na kamati ya bunge ya mambo nje,ulinzi na usalama.Tatizo langu mpaka sasa watanzania bado tumeshikilia ardhi tu bila kuangalia mambo mengine muhimu kama free movement nadhani nalo ni hatari sana hasa katika sector ya utalii na usalama wetu.Miaka ya nyuma wakenya waliidanganya dunia kuwa mlima Kilimanjaro uko Kenya sasa kama free movememnt nayo isipoangaliwa vizuri tutarudi kulekule tulikotoka.
Sector ya utalii inatoa mchango mkubwa katika kukuza pato la taifa hakuna asiyejua wenzetu wamepiga hatua kubwa katika sector ya utalii tusipo angalia makampuni makubwa yaliyopo Tanzania yanaweza kutoweka kabisa.

Mkuu hapo umesema kweli kabisa. Katika miaka ya 80s Kenya Airways ilikuwa inaitwa "The Pride of Kilimanjaro" ...sijui kama wamwbadilisha. Wakati ule ndio watalii walitua Kenya na kulala kwenye mahoteli yao halafu walikuwa wanavushwa kupitia Namanga kwenda kuuona au kuupanda mlima kwa bei "chee".
 
Kichwa cha mada ni kibovu. Kamati ya Bunge haiwezi kukataa "ardhi ya Tanzania kutumika kwa manufaa ya EAC". Mbona tayari ardhi ya Tanzania inatumika vizuri tu kwa manufaa ya EAC? Makao makuu ya EAC yapo kwenye ardhi ya Tanzania, na tungependa watumie ardhi yetu kuweka taasisi za EAC zaidi.

There must be give and take. We must win some and lose some. Ni ajabu kuona nchi yenye makao makuu ya EAC inakuwa mstari wa mbele kupinga mipango ya EAC.

Ukitaka cha mvunguni sharti uiname. Tukitaka umoja sharti tukubali kuuchangia kwa hali na mali.
 
Kichwa cha mada ni kibovu. Kamati ya Bunge haiwezi kukataa "ardhi ya Tanzania kutumika kwa manufaa ya EAC". Mbona tayari ardhi ya Tanzania inatumika vizuri tu kwa manufaa ya EAC? Makao makuu ya EAC yapo kwenye ardhi ya Tanzania, na tungependa watumie ardhi yetu kuweka taasisi za EAC zaidi.

There must be give and take. We must win some and lose some. Ni ajabu kuona nchi yenye makao makuu ya EAC inakuwa mstari wa mbele kupinga mipango ya EAC.

Ukitaka cha mvunguni sharti uiname. Tukitaka umoja sharti tukubali kuuchangia kwa hali na mali.


Excellent A. Mushi.
 
Back
Top Bottom