Kamati Kuu CCM wachukulieni hatua hawa Mawaziri, wanakichafua chama

saidoo25

JF-Expert Member
Jul 4, 2022
602
1,407
Chama cha Mapinduzi (CCM) ni chama kinachoshika dola na kinaundwa kuanzia ngazi ya Shina, Tawi, Kata, Wilaya, Mkoa hadi Taifa lakini jambo la kusikitisha sana licha ya Wanachama wake wawili Mwigulu Nchemba na Januari Makamba kumpa taarifa za uongo Mh Rais wetu ambaye ni Mwenyekiti wa CCM na kusababisha taharuki kubwa kwa watanzania hadi sasa hakuna hatua zozote dhdi yao.


Nilitegemea baada ya Waziri wa Nishati kuthibitika kumdanganya kwa makusudi Mh Rais na Waziri wa Fedha Mwigulu wangeitwa kwenye Kikao cha Kamati Kuu ya CCM iliyoketi leo ili wajieleze walilenga nini kumuandalia taarifa za uongo Mh Rais kuhusu kuhusu Mradi wa Bwawa la Nyerere na kuhusu Tanzania kushuka uchumi wa kati.

Jambo la kushangaza UVCCM ngazi Tawi, Kata, wilaya na mikoa wala Taifa hawajatoa tamko lolote kuhusiana na mawaziri hao, Jumuiya ya Wazazi ngazi ya Tawi, Kata, Wilaya, Mikoa wala Taifa hawajatoa tamko lolote, UWT Tawi, Kata, Wilaya, Mkoa wala Tafa hawajatoa tamko lolote juu ya suala hili

Pia RC Chalamila alisema wako mawaziri wako bize na safari za nje kwenda kutafuta fedha kwa ajili ya Kampeni ya kumtoa Rais Samia 2025 lakini hatujasikia tamko lolote na hatua zozote dhidi ya Mawaziri hao kutoka CCM.
Bila CCM imara Nchi yetu Itayumba- J.K Nyerere
 
Back
Top Bottom