kigogo1ivi
JF-Expert Member
- Jan 15, 2013
- 534
- 323
Mimi yamenitokea pale Buchosa nilipofika Shinyanga katika tafuta tafuta guest nikajikuta nimedondokea pale. Tokea nilipoingia pale ndiyo nikaanza kuona vituko wakina dada zaidi ya kumi wamechukua chumba kimoja na wanapishana kuleta wanaume kibaya zaidi ilipofika usiku wa saa 8 nikiwa nimelala nilianza kugongewa mlango na watu wasiojulikana wakitaka niwafungulie eti wamesahau begi lao chumbani kwangu nilikuwa mbishi ila wakawa wanagonga kwa nguvu ili uvunjike ndiyo nikavuta kitanda na kukiweka mlangoni baada ya kuona mlango umekuwa mgumu wakaondoka.
Kilichonishangaza hata muhudumu hakuwepo, Kulipokucha nikamweleza mmiliki wa hiyo guest yake haina vitu kama ivo lakini watu wengine ndiyo wakaniambia kuwa yeye ndiye hushirikiana na vibaka kuibia wateja wake hasa ukionekana una kitu cha thamani.
Kwahiyo BUCHOSA siyo nyumba yakulala wageni bali ni nyumba ya kulala vibaka.
Kilichonishangaza hata muhudumu hakuwepo, Kulipokucha nikamweleza mmiliki wa hiyo guest yake haina vitu kama ivo lakini watu wengine ndiyo wakaniambia kuwa yeye ndiye hushirikiana na vibaka kuibia wateja wake hasa ukionekana una kitu cha thamani.
Kwahiyo BUCHOSA siyo nyumba yakulala wageni bali ni nyumba ya kulala vibaka.