saidoo25
JF-Expert Member
- Jul 4, 2022
- 602
- 1,407
SUALA la Luhaga Mpina kukatwa jina lake kwenye nafasi ya mgombea wa NEC Mkoa wa Simiyu kwa mwaka huu wa 2022 kuwa amekosa sifa ya kuteuliwa limetuachia maswali mengi hasa sababu 11 zinazodaiwa ndio zimechangia kuondolewa kwenye mchuano huo.
1. Kuhoji bungeni kuhusu madai ya fedha za makinikia Trilioni 360 akitaka kujua nani alisamehe na kama ana mamlaka kisheria kusamehe madai halali ya watanzania ya kiasi cha shilingi Trilioni 5.5 kama ilivyoamuliwa na Mahakama za rufani za Kodi za TRAB na TRAT
2. Kuhoji bungeni juu ya Serikali kushindwa kudai madai halali ya Shilingi Trilioni 1.5 kwa ucheleweshaji wa mradi na CSR kutoka kwa Kampuni ya Arab Contractors ya Misri inayojenga mradi wa kufua umeme wa Bwawa la Julius Nyerere. Lakini pia Serikali kuendelea kutoa taarifa zinazokinzana juu ya ukamilishaji wa mradi huo.
3. Kuhoji bungeni kuhusu kupaa kwa Deni la Taifa kutoka wastani wa kukua kwa asilimia 4 hadi asilimia 13 na kutojulikana zilipo shilingi Trilioni 5 zilizokopwa nje ya bajeti kwa mwaka 2022.
4. Kuhoji bungeni TRA kushindwa kukusanya malimbikizo ya kodi yasiyo na kesi mahakamani kiasi cha shilingi Trilioni 7.5 na ucheleweshaji wa maamuzi ya mapingamizi ya kodi katika mahakama za rufani za kodi kiasi cha shilingi Trilioni 5 bila kuwepo sababu za msingi.
5. Kuhoji bungeni uhalali wa malipo yaliyofanywa na Serikali kwa Kampuni ya Symbion LLC ya shilingi Bilioni 350 nje ya bajeti na bila kuzingatia madai halali ya Serikali ikiwemo kodi na gharama nyinginezo.
6. Kukataa bungeni juu ya uamuzi wa Serikali kujenga Bandari ya Bagamoyo bila kuwepo tathmini ya kina juu ya uwezo wa kiuchumi kugharamia mradi huo
7. Kuhoji bungeni kuhusu Serikali kuingia mikataba mibovu, kushindwa kurejesha ngombe 6,000 za wafugaji walioshinda kesi mahakamani, Serikali kushindwa kudhibiti tembo wanaovamia mashamba na makazi ya wananchi na kusababisha vifo na majeruhi.
8. Kuhoji bungeni kuhusu kupanda kwa bei ya mafuta kwa kisingizio cha vita ya Urusi na Ukraine hali iliyoilazimu Serikali kuweka ruzuku ya shilingi bilioni 100 kila mwezi bila kuwepo unafuu wowote kwa wananchi.
9. Kuhoji bungeni suala la katakata ya umeme na migao ya umeme isiyoisha nchini iliyopelekea kuathiri uchumi na utoaji wa huduma zinazotegemea nishati ya umeme.
10. Kuhoji bungeni kuhusu suala la usimamizi mbovu na kupanda kiholela kwa bei ya mbolea na namna ilivyowaathiri uzalishaji na upatikanaji wa chakula nchini
11. Kuhoji bungeni juu ya kupanda kiholela kwa bei za bidhaa na gharama za maisha hali iliyopelekea mfumko mkubwa wa bei nchini huku Serikali ikishindwa kudhibiti hali hiyo.
KAMA HAYA MAMBO 11 NDIO YAMEMPONZA HADI JINA LAKE KUKATWA BASI TUNA SAFARI NDEFU SANA KAMA TAIFA
1. Kuhoji bungeni kuhusu madai ya fedha za makinikia Trilioni 360 akitaka kujua nani alisamehe na kama ana mamlaka kisheria kusamehe madai halali ya watanzania ya kiasi cha shilingi Trilioni 5.5 kama ilivyoamuliwa na Mahakama za rufani za Kodi za TRAB na TRAT
2. Kuhoji bungeni juu ya Serikali kushindwa kudai madai halali ya Shilingi Trilioni 1.5 kwa ucheleweshaji wa mradi na CSR kutoka kwa Kampuni ya Arab Contractors ya Misri inayojenga mradi wa kufua umeme wa Bwawa la Julius Nyerere. Lakini pia Serikali kuendelea kutoa taarifa zinazokinzana juu ya ukamilishaji wa mradi huo.
3. Kuhoji bungeni kuhusu kupaa kwa Deni la Taifa kutoka wastani wa kukua kwa asilimia 4 hadi asilimia 13 na kutojulikana zilipo shilingi Trilioni 5 zilizokopwa nje ya bajeti kwa mwaka 2022.
4. Kuhoji bungeni TRA kushindwa kukusanya malimbikizo ya kodi yasiyo na kesi mahakamani kiasi cha shilingi Trilioni 7.5 na ucheleweshaji wa maamuzi ya mapingamizi ya kodi katika mahakama za rufani za kodi kiasi cha shilingi Trilioni 5 bila kuwepo sababu za msingi.
5. Kuhoji bungeni uhalali wa malipo yaliyofanywa na Serikali kwa Kampuni ya Symbion LLC ya shilingi Bilioni 350 nje ya bajeti na bila kuzingatia madai halali ya Serikali ikiwemo kodi na gharama nyinginezo.
6. Kukataa bungeni juu ya uamuzi wa Serikali kujenga Bandari ya Bagamoyo bila kuwepo tathmini ya kina juu ya uwezo wa kiuchumi kugharamia mradi huo
7. Kuhoji bungeni kuhusu Serikali kuingia mikataba mibovu, kushindwa kurejesha ngombe 6,000 za wafugaji walioshinda kesi mahakamani, Serikali kushindwa kudhibiti tembo wanaovamia mashamba na makazi ya wananchi na kusababisha vifo na majeruhi.
8. Kuhoji bungeni kuhusu kupanda kwa bei ya mafuta kwa kisingizio cha vita ya Urusi na Ukraine hali iliyoilazimu Serikali kuweka ruzuku ya shilingi bilioni 100 kila mwezi bila kuwepo unafuu wowote kwa wananchi.
9. Kuhoji bungeni suala la katakata ya umeme na migao ya umeme isiyoisha nchini iliyopelekea kuathiri uchumi na utoaji wa huduma zinazotegemea nishati ya umeme.
10. Kuhoji bungeni kuhusu suala la usimamizi mbovu na kupanda kiholela kwa bei ya mbolea na namna ilivyowaathiri uzalishaji na upatikanaji wa chakula nchini
11. Kuhoji bungeni juu ya kupanda kiholela kwa bei za bidhaa na gharama za maisha hali iliyopelekea mfumko mkubwa wa bei nchini huku Serikali ikishindwa kudhibiti hali hiyo.
KAMA HAYA MAMBO 11 NDIO YAMEMPONZA HADI JINA LAKE KUKATWA BASI TUNA SAFARI NDEFU SANA KAMA TAIFA