ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 43,116
- 49,840
Wanamuita Comrede Makonda hapoi Wala haboi.
Atoa miezi 3 Kwa Mchengerwa kuhakikisha Soko na Standi Vinaanza mara Moja.
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimempa miezi mitatu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mohamed Mchengerwa, kuhakikisha wanaanza ujenzi wa stendi ya mabasi na soko la kisasa katika Manispaa ya Bukoba Mjini mkoani Kagera.
Agizo hilo limetolewa leo na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Paul Makonda, wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Mayunga mkoani huko.
Makonda amesema amepokea kero ya ujenzi wa soko lisilokamilika na ameshangazwa Bukoba kukosa stendi ya mabasi ya kisasa.
"Chama kinampa miezi mitatu Waziri Mchengerwa tuone ujenzi wa soko la kisasa na stendi ya mabasi kuanza kujengwa hiki chama sio cha porojo tunatakiwa kutatua kero za wananchi ngoja nimpigie simu Waziri kumjulisha hili,"amesema
Mchengerwa baada ya kupokea simu ya Makonda ambayo wananchi hao walikuwa wakimsikiliza, amesema amepokea maelekezo na tayari, Rais Samia Suluhu Hassan, alishatoa maelekezo kuhusiana na suala hilo na kwa sasa wanaenda kutekeleza kwa kuwa lipo katika ilani ya chama.
Amesema ifikapo Desemba mwaka huu atakuwa ameshafika katika mkoa wa Kagera kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa maagizo aliyopatiwa.
Atoa miezi 3 Kwa Mchengerwa kuhakikisha Soko na Standi Vinaanza mara Moja.
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimempa miezi mitatu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mohamed Mchengerwa, kuhakikisha wanaanza ujenzi wa stendi ya mabasi na soko la kisasa katika Manispaa ya Bukoba Mjini mkoani Kagera.
Agizo hilo limetolewa leo na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Paul Makonda, wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Mayunga mkoani huko.
Makonda amesema amepokea kero ya ujenzi wa soko lisilokamilika na ameshangazwa Bukoba kukosa stendi ya mabasi ya kisasa.
"Chama kinampa miezi mitatu Waziri Mchengerwa tuone ujenzi wa soko la kisasa na stendi ya mabasi kuanza kujengwa hiki chama sio cha porojo tunatakiwa kutatua kero za wananchi ngoja nimpigie simu Waziri kumjulisha hili,"amesema
Mchengerwa baada ya kupokea simu ya Makonda ambayo wananchi hao walikuwa wakimsikiliza, amesema amepokea maelekezo na tayari, Rais Samia Suluhu Hassan, alishatoa maelekezo kuhusiana na suala hilo na kwa sasa wanaenda kutekeleza kwa kuwa lipo katika ilani ya chama.
Amesema ifikapo Desemba mwaka huu atakuwa ameshafika katika mkoa wa Kagera kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa maagizo aliyopatiwa.