Kagera kuna hali ya hatari, kumezuka ugonjwa wa kutokwa damu puani na mdomoni. Watu 5 wafariki dunia 2 wako hospitali. Serikali ichukue hatua haraka

Robot la Matope

JF-Expert Member
Apr 10, 2015
7,091
13,784
Taarifa haijawa rasmi lakini hali iko hivi, huko katika Kata ya Kanyangereko, Wilayani Bukoba Vijijini, kwa marehemu Benjamini.

Wiki 2 zilizopita kijana alifariki, kwa kushikwa na homa kali na kutokwa damu mdomoni na puani, baadae mama mzazi akaumwa ugonjwa huo amefariki jana mchana.

Kijana wa familia hiyo aliembeba mgojwa kumpeleka hospital amefariki jana jioni, na huyu kijana alilazwa majuzi Maruku na alikuwa anatibiwa na kashimun, usiku wa kuamkia leo saa tisa Mama Shangazi wa marehemu naye amefariki na ugonjwa unafanana.

Leo tunaambiwa Kashumun amefariki. Lakini kuna taarifa kwamba nesi mmojawapo aliyemuudumia mgonjwa hospitali ya Mkoa (Government) naye amefariki.

=====

UPDATES;

=====

KAGERA: YADAIWA WATU WANNE WA FAMILIA MOJA WAFARIKI KWA UGONJWA, MMOJA YUPO HOI

Inadaiwa waliopoteza maisha Wanawake ni wawili (Reticia Benjamin na Theonestina Washington) na Wanaume wawili (majina hayajajulikana) huku mwingine mmoja akiwa amelazwa Kituo cha Afya Maruku, chanzo cha ugonjwa bado hakijawekwa wazi

Inadaiwa aliyeanza kufariki ni Mwanaume Machi 1, 2023, siku chache baada ya maziko ndugu watatu waliokuwa wakimuuguza nao wamefariki kwa Machi 15, 2023 kwa dalili za ugonjwa kama za ndugu yao, hali ambayo imezua sintofahamu

Mmoja alifia Hospitali ya Kagondo na wengine wamefia Hospitali ya Serikali Bukoba Mjini, wote wakiwa ni wakazi wa Kata ya Kanyangereko

Inadaiwa miwili ya Wanawake imezikwa Machi 16, 2023 katika Kijiji cha Butayebega wakati mwili wa Mwanaume mmoja ukiwa bado umehifadhiwa hospitali.Taarifa zaidi zitafuata

6D7871D4-E079-43B0-8CC9-5310C994DF7D.jpeg
 
Back
Top Bottom