Kabla ya Tanzania kufungua mipaka kwa wageni, ni lazima kuimarisha mifumo kwanza

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,317
12,617
Nchi zetu za kiafrika ni vigumu watu wake kutembeleana kwa urahisi bila kukutana na vikwazo mipakani/uhamiaji. Hili limetuchelewesha sana kiuchumi.

Sababu kubwa ya kuzuia wageni kuja nyumbani kwako ni ushaghalabagala uliyoko nyumbani kwako. Kama nyumbani kwako ni kuchafu sana, hakujapangiliwa, Kuna watoto wasiokuwa na nidhamu, hakuna chakula wala viti vya kukalia unaweza kusita kukaribisha wageni nyumbani kwako.

Ili Tanzania iweze kukaribisha wageni lazima mifumo yake ya sheria, TRA, kumiliki ardhi, kutambuana, biashara na masoko iwe imara sana, inayosomana na inayotekelezeka.

Bila kufanya hivyo kufungua mipaka litakuwa janga kubwa sana kwa nchi. Unapofungua madirisha upate hewa safi itaingia hewa safi lakini pamoja na vumbi, majani, mbu, panya, papasi na hewa chafu. Hivyo lazima pia uwe na mifumo imara ya kuvitoa ndani visivyohitajika kuingia.

Hatuna sababu za msingi za kuzuia watu kuja kwetu, hasa wale wenye mitaji na ujuzi.
 
Ni kweli kabisa mkuu, tatizo ujuaji wa kijinga huku tukiwa tunaburuza mkia kwa ufukara duniani yaani nchi chache sana tuna afadhali kuliko

Imagine Tz nchi 45 tu Dunia nzima ndio wanaweza kupata visa free
Ya 134 duniani daa.

Yote hayo wanakuambia usalama Wanaotengeneza nuclear na silaha wanaendelea kuwa na passport zenye nguvu duniani. Yangu ni ya 3 duniani kwa nguvu na kila mahali naingia na kupewa visa on arrival.

Sisi Africa nchi zao tu hawawezi kuingia nchini eti mpaka waombe.

Uoga wetu unatufanya tupitwe na kila nchi.

Amkeni Dunia inasonga na imefikia kwenye Artificial intelligence sisi bado tuna jembe la Mkono.
 
Ni kweli kabisa mkuu, tatizo ujuaji wa kijinga huku tukiwa tunaburuza mkia kwa ufukara duniani yaani nchi chache sana tuna afadhali kuliko

Imagine Tz nchi 45 tu Dunia nzima ndio wanaweza kupata visa free
Ya 134 duniani daa.

Yote hayo wanakuambia usalama Wanaotengeneza nuclear na silaha wanaendelea kuwa na passport zenye nguvu duniani. Yangu ni ya 3 duniani kwa nguvu na kila mahali naingia na kupewa visa on arrival.

Sisi Africa nchi zao tu hawawezi kuingia nchini eti mpaka waombe.

Uoga wetu unatufanya tupitwe na kila nchi.

Amkeni Dunia inasonga na imefikia kwenye Artificial intelligence sisi bado tuna jembe la Mkono.
Tuimarishe mambo yetu kisha tuwaalike watu waje TU wafanye biashara, wafanyekazi na waogelee kwenye bahati, mito na maziwa yetu ilimradi wafanyekazi halali na walipe kodi. Alika walimu bora kutoka kokote waje wafundishe watoto wetu badala ya kulinda ajira za walimu wasiokuwa na maarifa, form 4 na UPE kufundisha na kuzaliza vicious cycle. Leta watu wenye mitaji ya kilimo kuja kuzalisha ili vijana wapate ajira huko kwenye mashamba makubwa badala ya kugawia watu ardhi ili walime kwa jembe na kuyageuza kuwa makazi. Yaani ardhi ya kulima inageuzwa kuwa viwanja.
 
Tuimarishe mambo yetu kisha tuwaalike watu waje TU wafanye biashara, wafanyekazi na waogelee kwenye bahati, mito na maziwa yetu ilimradi wafanyekazi halali na walipe kodi. Alika walimu bora kutoka kokote waje wafundishe watoto wetu badala ya kulinda ajira za walimu wasiokuwa na maarifa, form 4 na UPE kufundisha na kuzaliza vicious cycle. Leta watu wenye mitaji ya kilimo kuja kuzalisha ili vijana wapate ajira huko kwenye mashamba makubwa badala ya kugawia watu ardhi ili walime kwa jembe na kuyageuza kuwa makazi. Yaani ardhi ya kulima inageuzwa kuwa viwanja.
Inasikitisha sana mkuu, tutasema ila kutelekeza ni ndoto
Huwa nikiangalia Human zoo huwa najiuliza kwanini wametufanya hivyo wazungu?
Halafu nasema ila bado tuna safari tusiyoifikia
 
Inasikitisha sana mkuu, tutasema ila kutelekeza ni ndoto
Huwa nikiangalia Human zoo huwa najiuliza kwanini wametufanya hivyo wazungu?
Halafu nasema ila bado tuna safari tusiyoifikia
Mama katenga Eka 20 kwa Zambia, afanye hivyohovyo kwa Malawi, Burundi, Uganda, Rwanda na Dr Congo. Hii reli ya sgr ilitakiwa hadi Sasa inatumika kusogeza mizigo ya Rwanda, Burundi, Congo, Uganda, Mwanza kule morogoro na tabora. Hakuna haja ya hizi nchi kuja hadi dar kufuata mizigo Yao wakati hii reli Iko tayari hadi tabora. Nani katuroga?
 
Nchi zetu za kiafrika ni vigumu watu wake kutembeleana kwa urahisi Vila kukutana na vikwazo mipakani/uhamiaji. Hili limetuchelewesha sana kiuchumi.

Sababu kubwa ya kuzuia wageni kuja nyumbani kwako ni ushaghalabagala uliyoko nyumbani kwako. Kama nyumbani kwako ni kuchafu sana, hakujapangiliwa, Kuna watoto wasiokuwa na nidhamu, hakuna chakula wala viti vya kukalia unaweza kusita kukaribisha wageni nyumbani kwako.

Ili Tanzania iweze kukaribisha wageni lazima mifumo yake ya sheria, TRA, kumiliki ardhi, kutambuana, biashara na masoko iwe imara sana, inayosomana na inayotekelezeka.

Bila kufanya hivyo kufungua mipaka litakuwa janga kubwa sana kwa nchi. Unapofungua madirisha upate hewa safi itaingia hewa safi lakini pamoja na vumbi, majani, mbu, panya, papasi na hewa chafu. Hivyo lazima pia uwe na mifumo imara ya kuvitoa visivyohitajika kuingia.
Baeleze baeleze, maana tuna viongozi hawajui madhara ya vitu wanavyohubiri au kutekeleza bila kujua mifumo ya wenzetu ipoje ili ujio wavwageni uinufaishe nchi. Mfano nchi za magharibi ingawa wanakaribisha immigrants lakini mifumo Yao ilivyo mizuri Kiasi kikubwa unachopata kina bakin kwao na kujenga zaidi uchumi wao na miundo mbinu . Unacho kuleta nyumbani ni robo au moja ya tatu ya kipato chako. Lakini wao wakija na mifumo yetu ambayo haikamati mapato mengi ya Kodi ni hasara tupu . Sasa hivi wageni mfano wachina, waturuki nk wengi kuna vipato ambavyo hatuvitozi Kodi hata hawa wapakistani wenye kuuza magari nk
 
Ni kweli kabisa mkuu, tatizo ujuaji wa kijinga huku tukiwa tunaburuza mkia kwa ufukara duniani yaani nchi chache sana tuna afadhali kuliko

Imagine Tz nchi 45 tu Dunia nzima ndio wanaweza kupata visa free
Ya 134 duniani daa.

Yote hayo wanakuambia usalama Wanaotengeneza nuclear na silaha wanaendelea kuwa na passport zenye nguvu duniani. Yangu ni ya 3 duniani kwa nguvu na kila mahali naingia na kupewa visa on arrival.

Sisi Africa nchi zao tu hawawezi kuingia nchini eti mpaka waombe.

Uoga wetu unatufanya tupitwe na kila nchi.

Amkeni Dunia inasonga na imefikia kwenye Artificial intelligence sisi bado tuna jembe la Mkono.
Woga wa kufungua mipaka unaotokana na kukithiri kwa rushwa na mifumo mibovu. Kama utafungua mipaka wakati rushwa kwako Iko juu sana utajikuta ardhi yote inamilikiwa na wageni kiholela, twiga wanapanda ndege na meli mchana kweupe. Lakini Wazungu wanajuwa kuwa kama waafrika watatembeleana na kuuziana kwa urahisi itaua Ile sera Yao ya divide and rule.
 
Woga wa kufungua mipaka unaotokana na kukithiri kwa rushwa na mifumo mibovu. Kama utafungua mipaka wakati rushwa kwako Iko juu sana utajikuta ardhi yote inamilikiwa na wageni kiholela, twiga wanapanda ndege na meli mchana kweupe. Lakini Wazungu wanajuwa kuwa kama waafrika watatembeleana na kuuziana kwa urahisi itaua Ile sera Yao ya divide and rule.
Kidogo nimekuelewa hapo kwenye Rushwa iliyokithiri
Mara nimejikuta nahuzunika kwenye ile vita ya wenyewe kwa wenyewe jirani zetu na kuanza kuingiza silaha kubwa kubwa na na kuteka mabasi na kuvamia maduka

Wakati sisi tulikuwa hatujui silaha nzito kihivyo
Na yote hiyo ni baadhi ya wala rushwa waliruhusu haya
Ila Marehemu aliliona hilo akazuia mauwaji na kuwalaza majambazi wengi na wengine kurudi kwao

Ila nafikiri tungejifunza na mengi kutokana na haya pia kujitahidi kudhibiti wizi na uhujumu uchumi na rushwa
 
Kidogo nimekuelewa hapo kwenye Rushwa iliyokithiri
Mara nimejikuta nahuzunika kwenye ile vita ya wenyewe kwa wenyewe jirani zetu na kuanza kuingiza silaha kubwa kubwa na na kuteka mabasi na kuvamia maduka

Wakati sisi tulikuwa hatujui silaha nzito kihivyo
Na yote hiyo ni baadhi ya wala rushwa waliruhusu haya
Ila Marehemu aliliona hilo akazuia mauwaji na kuwalaza majambazi wengi na wengine kurudi kwao

Ila nafikiri tungejifunza na mengi kutokana na haya pia kujitahidi kudhibiti wizi na uhujumu uchumi na rushwa
Rushwa inaangusha taifa, ndio maana viongozi wa Afrika wanaogopa wageni wengi, uraia pacha na kutbeleana.
 
umeongea la msingi sana, kabla hujaamua lolote linaloweza kuleta shida kwenye maslahi ya watu wako na taifa lako, unapaswa kwanza kuhakikisha mifumo yako ni imara kukabiliana na hilo.
 
Tuimarishe mambo yetu kisha tuwaalike watu waje TU wafanye biashara, wafanyekazi na waogelee kwenye bahati, mito na maziwa yetu ilimradi wafanyekazi halali na walipe kodi. Alika walimu bora kutoka kokote waje wafundishe watoto wetu badala ya kulinda ajira za walimu wasiokuwa na maarifa, form 4 na UPE kufundisha na kuzaliza vicious cycle. Leta watu wenye mitaji ya kilimo kuja kuzalisha ili vijana wapate ajira huko kwenye mashamba makubwa badala ya kugawia watu ardhi ili walime kwa jembe na kuyageuza kuwa makazi. Yaani ardhi ya kulima inageuzwa kuwa viwanja.
Bi kiroboto anaamin kila kitu wageni watatufanyia ,yeye hawezi chochote
 
Unashauri nini kifanyike kama serikali zenyewe zinakubali rushwa kama mfumo wa maisha?
Kama kiwango chetu Cha rushwa Kiko juu bado na mifumo yetu haisomani kutenga Eka 20 kwa wazambia na kuwaongezea muda wa kukaa nchini Kuna madhara kwa taifa. Itakuwa rahisi kumkuta mzambia nanjilinji anafuga bata na ni diwani kama raia TU.
 
Ili Tanzania iweze kukaribisha wageni lazima mifumo yake ya sheria, TRA, kumiliki ardhi, kutambuana, biashara na masoko iwe imara sana, inayosomana na inayotekelezeka.
Jambo muhimu sana kulitazama ni hilo la ardhi, kusipokuwepo umakini kwenye suala la ardhi ipo siku tutakutana na madalali watakaoidanganya serikali kubadili sheria za ardhi na mwisho wa siku yatukute yanayoendelea Israel na Palestina
 
Kama kiwango chetu Cha rushwa Kiko juu bado na mifumo yetu haisomani kutenga Eka 20 kwa wazambia na kuwaongezea muda wa kukaa nchini Kuna madhara kwa taifa. Itakuwa rahisi kumkuta mzambia nanjilinji anafuga bata na ni diwani kama raia TU.
Tuna tatizo kubwa sana na haya yote ni mfumo wetu na malezi toka udogoni
 
Tuimarishe mambo yetu kisha tuwaalike watu waje TU wafanye biashara, wafanyekazi na waogelee kwenye bahati, mito na maziwa yetu ilimradi wafanyekazi halali na walipe kodi. Alika walimu bora kutoka kokote waje wafundishe watoto wetu badala ya kulinda ajira za walimu wasiokuwa na maarifa, form 4 na UPE kufundisha na kuzaliza vicious cycle. Leta watu wenye mitaji ya kilimo kuja kuzalisha ili vijana wapate ajira huko kwenye mashamba makubwa badala ya kugawia watu ardhi ili walime kwa jembe na kuyageuza kuwa makazi. Yaani ardhi ya kulima inageuzwa kuwa viwanja.
Mkuu kwanini serikali isiwakopeshe pesa wakulima wakitanzania ili wananchi wawe matajiri kuliko kuwapa wageni mashamba walime na wananchi waajiriwe kwa mshahara wa laki na nusu, Mali za nchi zikishika na wageni madhara yake wananchi ni kuwa masikini, Waarabu wana pesa kwa sababu ya mafuta na Waarabu wangekuwa na akili kama za Viongozi wa Afrika ya kuwapa visima vya mafuta wageni na wao kungojea kuajiriwa kwa ujira mdogo, hadi leo waarabu wangekuwa masikini na mafuta wanayo, Viongozi wetu wajinga kipindi cha awamu ya Mkapa alikuwa anafukuza wananchi kwenye maeneo yenye madini na kuwapa wazungu, yani sehemu ya wachimbaji wadogo wadogo ana wafukuza na kuwapa wazungu kwa mkataba wa miaka mia, baada ya serikali kuwawezesha wachimbaji wadogo ili wawe matajiri yenyewe ilikuwa inawafukuza na kuwapa wazungu.
 
Baeleze baeleze, maana tuna viongozi hawajui madhara ya vitu wanavyohubiri au kutekeleza bila kujua mifumo ya wenzetu ipoje ili ujio wavwageni uinufaishe nchi. Mfano nchi za magharibi ingawa wanakaribisha immigrants lakini mifumo Yao ilivyo mizuri Kiasi kikubwa unachopata kina bakin kwao na kujenga zaidi uchumi wao na miundo mbinu . Unacho kuleta nyumbani ni robo au moja ya tatu ya kipato chako. Lakini wao wakija na mifumo yetu ambayo haikamati mapato mengi ya Kodi ni hasara tupu . Sasa hivi wageni mfano wachina, waturuki nk wengi kuna vipato ambavyo hatuvitozi Kodi hata hawa wapakistani wenye kuuza magari nk
Mkuu wageni wanaoenda Ulaya na Marekani hawana nguvu ya kiuchumi ya kuwazidi wazawa kwaiyo raia wanaoenda Marekani wanaenda kwaajili ya kutafuta ajira na siyo kuwekeza, Mifumo ya nchi za Ulaya mgeni kutajirika na kumfikia Mo dewj ni ngumu.
 
Mkuu wageni wanaoenda Ulaya na Marekani hawana nguvu ya kiuchumi ya kuwazidi wazawa kwaiyo raia wanaoenda Marekani wanaenda kwaajili ya kutafuta ajira na siyo kuwekeza, Mifumo ya nchi za Ulaya mgeni kutajirika na kumfikia Mo dewj ni ngumu.
Kitu cha msingi ni kumzuia mgeni kukwepa Kodi , akikwepa Kodi hiyo ni utoroshaji wa mtaji
 
Back
Top Bottom