Takribani juma moja tu limebaki kabla ya uchaguzi mkuuTunashuhudia mambo yakizidi kupamba moto kwa kuendelea na kampeni, na gumzo kubwa ni pale Dr Slaa alipofanya mahojiano live na wapiga kura wake pale moven peak, mahojiano ambayo yaalivuta hisia za wengi kwa umahiri mkubwa aliouonyesha Dr Slaa katika kujibu hoja mbali mbali
Kama kawaida maandiko yangu yana angalia zaidi upande wa bara na hasa vyama vya CCM na CHADEMA, hivyo tathimini yangu itaegemea zaidi katika vyama hivi viwili
Nini hasa nguvu za vyama hivi zilipo,wapi ilipo mitaji yao ya kuelekea ktk kushinda uchaguzi mwaka huu kwa maana ya wingi wa kura utakao wapa wabunge wengi na kushinda urais
Kwa kuanza na CCM wanajigamba kushinda uchaguzi huu kwa kuzingatia makundi yafuatayo ambayo kwao wao ndio mtaji mkubwa kwao kulinda rekodi yao ya ushindi kila chaguzi.
WANACHAMA
CCM ianamtaji mkubwa wa wanachama ambao wao kwao CCM ni damu damu, na uzuri wa hawa wanachama takribani wote wamejiandikisha kupiga kura,
Mtandao huu kiukweli ulianza mikakati ya uchaguzi wakati wa uandikishaji wa daftari la wapiga kura kwa kuhakikisha kila mjumbe anasimamia wanachama wa eneo lake kwenda kujiandikisha, na ukaguzi wa nyumba hadi nyumba ukifanyika kuhakikisha wote wamejiandikisha kwanza.na hili linawasaidia sana hasa mijini ambapo watu wengi huwa hawajiandikishi.,
WAZEE NA WANAWAKE
Hili ni kundi lingine ambalo ni mtaji mkubwa kwa CCM
Wazee wengi kwa ujumla wao vichwani mwao bado CCM ni kila kitu, takribani maisha yao yote wamekuwa na CCM tangu TANU hadi leo, CCM ni sehemu ya maisha yao,wengine kwao ni wababaishaji tu
Wanawake wengi Tanzania hawana mwamko wa siasa kabisa, maranyingi wao ni fuata mkumbo (samahani kutumia neno hilo) maranyingi wanapiga kura kwa mazoea na pia wepesi kutishika na kurubuniwa, na kundi hili limeathiriwa sana na mtandao wa CCM kuanzia ngazi ya mjumbe wa shina na vikundi vyao.
VIJIJINI
Kama kuna kundi lenye msimamo, basi ama akika kundi hili lina msimamo, likisema no, ni no. na likisema yes ni yes.
Nikundi ambalo ukilishika basi unahakika na ndio maana hata wapinzani sehemu kubwa waliofanya vizuri ni katika kundi hili.
CCM wamefanikiwa kulishika vilivyo kundi hili kwasababu hawapati habari sahihi,upinzani ni kama uhani kwao, kutofikiwa na wapinzani na ngos kuishia mijini, mfumo wa utawala, kutofautisha chama na watendaji wa serikali, na mwisho wengi wao maisha wanayoishi wanaona kama ndio stahiki yao.
MAJIMBO YASIYO NA WAGOMEA WAPINZANI NA ZANZIBAR
Hata kabla ya uchaguzi tayari kuna majimbo CCM imeshapata ushindi kabla ya uchaguzi kuanzia ngazi ya udiwana na ubunge kwa tanzanaia bara na visiwana ambapo CHADEMA hawajatia kabisa mguu, huu ni mtaji mojawapo CCM wanautegemea ktk kusukuma ushindi wao
Makundi niliyo yataja hapo juu wengi wao ni wale ambao wao wanapiga kura kwa vigezo nilivyo vieleza bila kuangalia maswala ya uzuri wa sera au vitu vingine
Kwa upande wa CHADEMA sitakuwa na mengi sana ya kuandika sababu napata shida kidogo kupata hasa mtajiwao ukowapi, kama nitakuwa sivyo nahakika wadau mtanisawazisha
WASOMI NA WAFANYAKAZI KADA YA CHINI
Hili ni kundi ambalo CHADEMA wamefanikiwa kuli teka vilivyo,
wasomi wengi hasa wa mijini na vyuoni wamekuwa mstari wa mbele kuiunga mkono CHADEMA kutokana na sera zake zenye matumaini kwao na kwa taifa kwa ujumla.
kundi hili linaonekana kuyumbishwa kidogo kutokana na sintofahamu iliyotokea juu ya wanafunzi wa vyuo kuonekana watashindwa kupiga kura
Wafanyakazi wa kada kuanzia kati na chini na wafanyabiashara ndogo ndogo nao ni kundi lingine ambalo linaiunga sana mkono chadema na kuonekana mtaji mkubwa kwa CHADEMA na kundi hili linaonekana sana mijini
AGENDA YA UFISADI NA KASORO ZA CCM
Kimantiki huu ndio mtaji mkuu wa CHADEMA, mtaji ambao hauna kundi specific isipokuwa unatarajiwa kunyakua kura toka ktk makundi tajwa ya CCM ambayo sera kwao sio tija, tija kwao ni kupigia CCM.,
CHADEMA hawana mtandao mkubwa kama CCM wanategemea zaidi agenda hizo ili ziwa bebe kuwa shawishi wapiga kura kupata kura
Na agenda hizo pia zimetokea kuungwa mkono kwa kiasi kikubwa na NGOS mbali mbali na wanaharakati,
Sina nia ya kukatisha tamaa wapinzani,na katika siasa lolote laweza tokea na kila chama kinanafasi ya kushinda lakini kwa kuzingatia nilicho eleza hapo juu naamini hata wewe unapata picha ni chama gani kina nafasi kubwa ya kushinda uchaguzi.
wingi wa watu katika kampeni sio kigezo kabisa cha kushinda kwani kila chaguzi tunaona mambo huwa hivi hivi, mwisho wa siku matokeo wote tuna yajua
Inawezekana kweli kabisa ikawa CCM haifanyi vizuri kiutawala, lakini sio kigezo cha wao kushindwa katika chaguzi na hasa kwa nchi zetu zinazo endelea, mfumo ni tofauti sana na nchi zilizo endelea.
Wito wangu kwa wanamageuzi,wanakazi kubwa sana yakufanya kuleta mageuzi zaidi ya kusimama majukwaani na kuikosoa CCM.
Ukisoma post nyingi utaona ni jinsi gani wana JF wanavyofikiria ushindi kwa upinzani ni rahisi, wao akili yao ipo katika kuibiwa kura tu, wanachoamini wao ukidhibiti wizi wa kura basi umeshinda uchaguzi.
Nahuu ndio ukweli mgumu kuukubali
Mwenye macho haambiwi tazama, let's wait nd see
Pulss
Hivi una wadhifa gani vile katika kile kitengo cha propaganda cha thithiem? Mpigie kura Rais mtarajiwa Dr Slaa na wagombea ubunge wa chadema. Thithiem na kikwete wameshindwa katika utendaji wa kuiongoza nchi na ushahidi upo wa kutosha tu.