sinza pazuri
JF-Expert Member
- Aug 16, 2014
- 2,525
- 7,377
Kazi ya sanaa kama ilivyo taaluma nyingine inahitaji sana discipline.
Na nidhamu ya kazi ni tatizo kubwa sana kwa kaka yetu Juma Nature.
Hatukatai Juma ni legend anaepaswa kupewa heshima, ila amekuwa anazingua sana kwa kutokubali kukua.
Usela wa uswahilini unamharibia sana.
Nature bado anashikwa masikio na mtu aliyewagombanisha na na washikaji zake anaeitwa Rich One huyu mchizi ni wale watu wanaoamini kwenye majungu na fitna ili kusavaivu. Amekuwa akimchafulia sana Nature mambo yake yeye anajua Nature anapenda beer basi akishamtafutia hela ya beer amemmaliza.
Sasa Nature unapopata nafasi ya pili usiitumie vibaya. Wewe unajua kabisa Diamond hawezi na hatokaa hata kufikiria kukulipa laki tano upande juu ya stage.
Nature unajua Diamond anakupambanieni kiasi gani mrudi kwenye game tena bila yeye kupata chochote. Wewe ulishawai mtukana mpaka kwenye nyimbo zako yeye anakulipa kwa kukupa shows mikoa 10 na kusaidia kuwapromotia album mnayoandaa na collabo za wasafi na wasanii wakubwa kawatolea kiroho safi na hapati hata senti 5.
Huyo meneja wako Rich One amewai fanya nini la maana toka utoke kwa Fella?
Haya ameandika alichoandika kwenye akaunti yako, mmepata faida gani? Yeye anataka kukukeep usitoke kwenye mikono yake wewe unapata nini? Beer?
Juma kaka badilika au tafuta kazi nyingine ya kufanya maana unazingua sana, sio leo sio jana achana na ego za nilikuwa mkubwa hata r kelly alikuwa mkubwa ila nyakati zinabadilika tumia akili.