Jukwaa la katiba live!

jogi

JF-Expert Member
Sep 25, 2010
25,558
25,323
Nipo ukumbini, sizuii yeyete anayefuatilia kupitia itv kuongeza alichoona na kusikia.
Deus kibamba ameshafungua kongamano.
 
Prof. Haoni kama ni sawa mchakato wa kuandika katiba unvyoendeshwa kwa maana ya kuminywa haki ya ushiriki huru wa wananchi.
 
Prof. Anachambua tofauti ya shirikisho na muungano, anatolea mfano wa shirikisho la afrika mashariki na muungano wetu wa tanganyika na zanzibar.
 
Prof. Lengo la muungano ilikuwa ni chanzo cha kuunda umoja wa afrika,
kwa maana nchi nyingine zingejiunga baadaye, zambia ilionyesha nia lakini baada ya kuyaona masharti "ambayo ni zanzibar pekee iliyakubali" haikuwa tayari kujiunga, na haikutokea nchi nyingine ya afrika kujiunga.
 
Prof. Mkataba wa muungano ulikuwa na makubaliano 11,
lakini kwa sasa yameongezeka na kufikia 37.
 
Prof. Mabadiliko ya katiba ya zanzibar automaticaly imebadilisha hati ya muungano.
 
Prof. Anachambua tofauti ya shirikisho na muungano, anatolea mfano wa shirikisho la afrika mashariki na muungano wetu wa tanganyika na zanzibar.

Prof ndio nani? Majimarefu au Mwondosya??? Andika jina kamili, mie sina TV wala radio hapa nategemea unipe kitu kamili
 
Prof. Rais wa zanzibar amekuwa mjumbe wa baraza la mawaziri, hakuwa na uchaguzi ispokuwa kukubali akiisoma picha iliyompata aboud jumbe (watu wamecheka kidogo)
 
Prof. Bunge la muungano halina mamlaka juu ya serikali ya zanziba ispokuwa yale tu kwenye mkataba.
 
Prof. Katiba ibara ya 4 inajichanganya juu ya mamlaka ya bunge kwa pande hizi mbili.
 
Prof. Ibara inatoa mamlaka kwa bunge kutunga sheria ambayo inapaswa kuelekeza kuwa hiyo sheria inapaswa kutumika zanzibar tu. Prof. Anashangaa, Kama jambo husika ni la muungano vipi sheria ielekeze jambo kipekee wakati jambo lenyewe lipo kwenye hati ya makubaliano!!!
 
Ubadilishaji ama utibitishaji wa mambo inahitaji theluthi mbili kupitisha jambo husika.
 
Prof. Mahakama kuu ya tz si mahakama ya muungano, na mahakama ya znz ni kitu tofauti kabisa. Sasa ni aje
 
Prof. Msumari wa mwisho kwa jeneza, ilitokea kesi ikasajiliwa znz mahakama ya rufaa, ikaletwa mahakama ya rufaa tanganyika, ikakaliwa, kwa mwendelezo wake hukumu ilikuja toka kuwa zanzibar si nchi, kwa hiyo hapawezi kutokea uhaini huko zanzibar
 
Prof. Ali hassan Mwinyi alipata kusema bungeni kuwa tuna serikali mbili kuelekea moja.
Anamaliza kwa kusema hakuna ugumvi kati ya wananchi wa zanzibar na tanganyika.
 
Back
Top Bottom