Jukwaa la katiba live!

Nimekukubali make vitu vyote muhimu inatoa nipo songea nacheki live huyu mama anasema kuhusu wanawake poa mkuu ww usifumbe macho tupe upptodates nacheki ball kidogo
 
we bwana wewe, Prof ndio nani?????????????????

kafie bafuni huko wewe!! Habari unataka ujeuri wa nini. Sita kutajia huyu profesor kutoka zanzibar mpaka mwisho wa kongamano.
 
Baada ya kufumba macho kwa dakika moja kutafakari juu ya wanawake kufuatia mtoa mada kutuomba kutafakari, muwakilishi wa jinsia sasa analieleza kongamano kuwa wanawake wamekandamizwa na kuonewa na mfumo kutokana na mfumo

my take, naona kama analalamika kwa niaba ya wananwake. Muunganiko na katiba hajauonyesha bado.
 
Mj. Vifo vingi vya akina mama vinatokana na uduni wa elimu, huduma za afya, na umasikini.
 
Wadau huyo Prof aliyemalizia kuchangia ni Prof nani??? Tunabishana hapa! Ni Shivji??
 
He! Kumbe mwanamke mtanzania akiolewa na mwanaume ambaye si Mtanzania mwanamke huyo anapoteza uraia wake? Imenishtua
 
MJ. Wanawake wanamajukumu makubwa sana kwenye jamii, wanawake wanapata maambukizi ya vvu zaidi kuliko wanaume.

UKATILI WA KIJINSIA.
Asilia 44 walioolewa wamefanyiwa ukatili wa kijinsia, 15 wamekumbana na ukatili wa ukeketaji,
chini ya aslimia 15 ndio wanashiriki katika ngazi za kutoa maamuzi katika jamii.
 
JM. Ameunganisha kuwa haki ya umiliki wa uchumi usimbague mwanamke kwenye katiba mpya.
Kuna umuhimu wa katiba kuwa bayana kuhusu muktadha wa utamaduni kuhusu wanawake,
ukitaka kuona watu waliondelea, nenda ukatembelee makaburini.
Tutmie nafasi hii kuhakikisha kuwa tunaondoa sheria zote kandamizi.
 
MJ. Katiba ifafanue wazi kuwa haki ya huduma za kijamii ni lazima kwa wote.

Katiba yetu iwe bayana kuwa ushiriki wa ngazi zote uwe 50 50 kwa jinsia zote.
Ukatili wa kijinsia pawe na zero tolerance.

Mwisho; ni maswala ya kimchakato, tume iwe na uelewa wa kuwaelewa na kuwasaidia kitaalamu ili wanawake watoe maoni yao bila woga.
 
Mmasai. Ardhi iheshimiwe kwa kuzingatia wakaazi na taaluma zao za kiasili ziheshimiwe sana.
Jamii ya wafugaji na ipewe nafasi bungeni, upembuzi yakinifu uwahusishe nao pindi ukifanyika.
 
Diwani mtarajiwa.
Madiwani wana uelewa mdogo angalau kujua baadhi ya mambo vikaoni.
 
Mchangiaji, mkazo kwenye elimu.
Hakubaliana na theluthi mbili kupitisha maamuzi kwenye katiba.
 
Mama kutoka biharamulo.
Analalamikia haki ya mpiga kura.
Viti maalum vinadhalilisha,
kuna rushwa ya mapenzi na ya fedha, ni hatari!
Mchakato wa kuwapata uwe wa kikatiba zaidi.
 
Anaitwa Profesa Abdul Sheriff. Ni mwenyekiti wa Baraza La Katiba Zanzibar.

Asante mkuu kwa kutusaidia, kuna mtu alikuwa anaandika tu Prof Prof hajui kama hata Majimarefu ni Prof. Lakini sio kosa lake huenda alikuwa hamjui vema jina lake.
 
nakubalian a na huyu mama viti maalumu wanatumikia waliowasaidia kupata nafasi hiyo. si tunawaona bungeni, porojo tuu wanatoa na hawajiamini.
 
Asante mkuu kwa kutusaidia, kuna mtu alikuwa anaandika tu Prof Prof hajui kama hata Majimarefu ni Prof. Lakini sio kosa lake huenda alikuwa hamjui vema jina lake.

soma mwanzo wa thread sikuzuia uchangiaji ama uboreshaji.
 
Back
Top Bottom