Gurudumu
JF-Expert Member
- Feb 5, 2008
- 2,349
- 261
Mbunge huyu wa chadema apingana na sera za chadema bungeni. Amesema;
1. Shule za kata ni nzuri kwa sababu kuna vijana wake wamefika chuo kikuu kupitia shule za kata (hajali wamejifunza nini)
2. Amepongeza serikali kwamba imefanya mambo mengi sana kuleta maendeleo ya nchi hii
3. Asema uchaguzi ulikuwa huru na haki
4. Asema wanafunzi wa vyuo vikuu wasijihusishe na siasa, wakati Chadema ina mkakati wa kujiuza vyuo vikuu na wameanzia Makumira
(Maana ya "square peg in a round hole" kwa mujibu wa Oxford Advanced Learner's Dictionary sixth edition ni, "a person who does not feel happy or comfortable in a particular situation, or who is not suitable for it")
1. Shule za kata ni nzuri kwa sababu kuna vijana wake wamefika chuo kikuu kupitia shule za kata (hajali wamejifunza nini)
2. Amepongeza serikali kwamba imefanya mambo mengi sana kuleta maendeleo ya nchi hii
3. Asema uchaguzi ulikuwa huru na haki
4. Asema wanafunzi wa vyuo vikuu wasijihusishe na siasa, wakati Chadema ina mkakati wa kujiuza vyuo vikuu na wameanzia Makumira
(Maana ya "square peg in a round hole" kwa mujibu wa Oxford Advanced Learner's Dictionary sixth edition ni, "a person who does not feel happy or comfortable in a particular situation, or who is not suitable for it")
Mimi ni mwana Rombo na mkereketwa wa maendeleo ya wilaya ya Rombo na taifa zima kwa ujumla hasa katika sekta nyeti ya ELIMU. Mbunge wangu Josephy Selasini kimya kimezidi hatukusikii ukiendesha harakati za maendeleo.
Pengine unaziendeleza ila huweki wazi katika vyombo vya habari maana wengine hatupo jimboni, tupo sehemu mbalimali za Tanzanaia na dunia kwa ujumla. Tuna mawazo mengi sana chanya ambayo tungekushirikisha wewe kama mbunge yangesukuma mbele gurudumu hili la maendeleo. Tupo vijana wasomi wa fani mbalimbali ambao tunaweza kushirikiana na wewe katika kubuni mbinu mbalimbali za kuboresha na kuanzisha miradi mbalimbali ya maendeleo jimboni mwetu. Ushauri wangu ni huu mheshimiwa.
Andaa mkutano wa wana Rombo wote waishio Dar es salaam na sehemu nyingine kwa lengo la kuwaleta watu pamoja ili tuweze kutafakari na kubuni ni kwa namna gani maendeleo ya Rombo yanaweza yakaboreshwa haraka iwezekanavyo.
Mwisho nakutakia maendeleo mazuri katika shughuli zako.