John Pombe Magufuli unatuchefua

Leadership is different from project management. Our crisis partly stems from the fact that we have been electing project managers instead of leaders! And the difference is you need money to successfully manage a project, but you need ideas to be a good leader!

Mwalimu wangu Kitila Mkumbo kwanza nakupa tano. Yani hapa umemaliza kila kitu. Wapuuzi wote ambao wamelewa sifa za Magufuli hawana tena hoja. Alafu hivi kwa nini Mkandala hakupi U-Professor? Au kwa vile anajua wewe ni mwana CDM? Nakupa tano tena my teacher! Baadae!

 
Rafiki yangu Mkumbo,

naona kama kuna ulazima wowote kukuchana kumbe niwe naenda taratibu kidomo kwani nimegundua punde tu kwamba kuna watoto wetu na humu ambao nao hawaishi kutekenya na kiu ya 'Tanzania Tunayoitamani'!

Na kwa uchanganuzi hapo chini ni kwamba hoja imetulia sana. Dr Maghufuli ni Waziri Mkuu zaidi kuliko kuwa Presidential material; lakini mpaka awe anajitokeza hadharani kukemea UFISADI, MAFISADI na kutetea Katiba ya Wananchi.


Leadership is different from project management.

Our crisis partly stems from the fact that we have been electing project managers instead of leaders! And the difference is you need money to successfully manage a project, but you need ideas to be a good leader!
 
Huyu jamaa nilikuwa indifferent sana kwake lakini kadri siku sinavyokwenda nazidi kuamini Urais ni kazi kubwa sana kwake kama ana hiyo ndoto..

nadhani kuna wapambe wake wanataka kumsafishia jina. Wasahau about the project management guy who lacks ideas
 
Kwakweli kwa hali ilivyosasa wengi hatutamani raisi atokee ccm, hapa tulipo ni kwasaabu ya ccm so tunatamani kuona upande mwingine wa uongozi. si Lowasa wala Magufuli tumewachoka wote
 
Mwanzoni tulijua kuwa wewe ni mtu makini kume tumekosea. Nadhani hata wanaokutumikisha wanajua kuwa wewe si makini na ndio maana wanakuwekea spidi gavana na kukuambia uache ubabe. Mwanzoni nilidhani wamekuonea kumbe walikuwa sahihi. Upo kama roboti. Nimegundua hili kutokana na matamshi na kauli zako. Barabara zote nchini unazijua wewe. Vifungu vyote vya sheria umevikariri wewe. Hizo sheria ni kwa ajili ya binadamu lakini wao/sisi sio programmed kama wewe.

Juzi hapa mkizindua barabara pale Dodoma, Pinda alikupiga dongo kuwa Rais alikupeleka uvuvi, na kule unajua idadi ya samaki nchini. Rais akaona bora akurudishe ujenzi. Tatizo lako mkuu unamtumikia kafiri kupitiliza, hadi unampa kero.

Wewe ni mchapakazi sawa, lakini yawezekana huna maadili ya kazi. Hakuna mtanzania anayekuwazia urais. Wanakuwazia uwaziri tu kwa kuwa watanzania wanajua unajua kutumika.

Achana kabisa na siasa zako za maji taka. Sio kila unapotoa neno hadharani usifie chama chako na kuponda upinzani. Kwa taarifa yako, unaowahutubia ni wapinzani. Sasa unapoponda viongozi wao na harakati za upinzani, wanakuchukia kweli. Wanakuoanisha na majina yako.

Tatizo lako mkuu unatupa mawe hovyo kiasi cha kuwatwanga na wazazi wako pia. Nakufananisha na Abunuwasi kukata tawi ulilokalia. Hilo tawi ni wananchi. Mpita njia akikuambia kuwa unafanya kosa kwani utaanguka, unamkejeli. Utakapoanguka utamkimbilia aliyekuambia ukweli kumwomba utabiri zaidi, angalia asijekwambia utakufa lini.

Achana na upinzani kwani ni jeshi kubwa kwa sasa. Una kashfa nyingi tu tunazozifahamu na nyingine zitafahamika. Una kashfa ya kuuza nyumba za serikali. Una kashfa za kumpa kimada wako nyumba ya serikali. Una kashfa ya kunyanyasa staff wako kwa kuletewa majungu na wapambe wako. Una kashfa ya ubabe, n.k, n.k. Fanya kazi, kiongozi kwani huijui kesho. Kazi ya kubwabwaja mwachue nape. Kaajiriwa kwa kazi hiyo. We kazi yako miundombinu. Usiwe kama mzazi anayewapa wanae mahitaji kwa masimango. Wenzako umeshwasikia wanabwabwaja hovyo? Time will tell

Mimi huwa nawa-admire wazazi wa Magufuli,ni vichwa aisee!Jina la Pombe linasadifu kabisa tabia ya huyu robot!
 
Nimesoma maoni ya dr mkumbo. Dr magufuri ni mzuri wa kusimamia mirad na sio mzuri kuongoza.mifano hiko ming ila yeye ni bendera ufuata upepo. Ata magufuri akiaambiwa na kikwete kuwa 1+1=4 magufuri atasimamia uongo huu.atawakasifu wale wanaosema jibu ni 2. Magufuri ni sawa na samwel sita. Magufuri anapashwa awe waziri mkuu na rais awe hard working wa kumuamuru afanye ili na lile.kama anataka urais basi atoke ccm.kura yangu kuipata sio rahisi
 
Urais kwa sasa huchaguliwa kwa kura za wengi na haupewi na mtu, Urais wa kupewa ulikuwa wa Nyerere, yeye ndiye aliepewa kwenye sahani bila kuchaguliwa. Upo hapo ulipo? ni nani alimchaguwa Nyerere kuwa Rais, na yeye akampasia kibaraka wake, MMwinyi na Mkapa. Kikwete kautolea jasho, na kama huyo Magufuli anauwezo na yeye autolee jasho.[/QUOTE]


Kikwete hakuutolea jasho alitumia mabilioni ya pesa zilizochangishwa na kundi lake lililojiita la mtandao wakiwemo Lowassa, Membe na wengineo. Walichangisha pesa hizi kutoka kwa mafisadi mbali mbali hasa wa kidindi akina Jeetu, Manji, etc na kuzitimia kuwahonga tena kwa hongo ya foreign currencies (US Dollars au British pounds) ili wampitishe yeye kama mgombea wa Magamba badala ya Salim ambaye alikuwa ni chaguo la wengi. Mkapa naye kwa sababu anazozijua yeye mwenye na baada ya kuona mgombea aliyemtaka Abdalla Kigoda kupigwa chini akadandia behewa la mtandao na hivyo kusaidia katika kumchafua SAS ili asichaguliwe kama mgombe wa magamba. Kwa hiyo hakuna ukweli wowote kwamba Msanii Kikwete ameutolea jasho Urais bali ukweli ni kwamba alitumia njia za haramu kuingia Ikulu.

 
urais kwa sasa huchaguliwa kwa kura za wengi na haupewi na mtu, urais wa kupewa ulikuwa wa nyerere, yeye ndiye aliepewa kwenye sahani bila kuchaguliwa. Upo hapo ulipo? Ni nani alimchaguwa nyerere kuwa rais, na yeye akampasia kibaraka wake, mmwinyi na mkapa. Kikwete kautolea jasho, na kama huyo magufuli anauwezo na yeye autolee jasho.

kweli kabisa! Nyerere aliachiwa urais na wazungu. No struggles like those found in other african countries, like kenyata with his maumau in kenya.
 
FF mbona unamashambulia sana Nyerere? hii sijui ni post ya ngapi naona una divert mada za watu kuzipeleka kwa nyerere.si umafuate?
--mwinyi na JK ndio wameiharibu nchi
 
toka miaka ya 2000 nani alikuwa hajui kuwa jk atakuja kuwa rais? si ndio kupeana huku na sasa hivi wana mpango wa kumpa lowasa..wape magufuli apige watu bakora nchi inyooke..
 
Wewe ulieandika hii habari unatafuta laana za mwenyezi mungu mjaza neema ndogo ndogo na kubwa nene na fupi nyembamba na ndefu hakika usirudie tena mpwa
huyu kashaalaaanika sijui unatafuta laana gani mpwa
 
WanaJf;
Ni vizuri tutofautishe Mtendaji na Kiongozi. Magufuli ana sifa ya Utendaji lkn siyo Uongozi na ndiyo maana hata maamuzi yake mengine yanasababisha utendaji udorore kwa walio chini yake. Yeye ni mtu wa kupewa kitu cha kukamilisha na si kiongozi wa kuweza kung'amua lipi jema na lipi baya. Rejea hata maamuzi ya kuuza nyumba za Serikali, sawa ni kweli Baraza la Mawaziri lilipitisha hayo maamuzi na yeye kama Waziri husika akawa mtekelezaji. Lkn kama angekuwa mtu ambaye ni Creative angeweza kuona nini yatakuwa madhara ya maamuzi hayo kwa Uchumi wa Tanzania. Magufuli ni sawa na PROJECT MANAGER kama alivyosema Dr. Kitila Mkumbo. Magufuli ana tabia kama za Mbwa wa Mwiindaji ambaye ukienda naye mawindoni, then unamshtua Sungura au Swala kwenye kichaka, then unamruhusu kumfukuza yule mnyama ili amkamate na kukupa kitoweo. Magufuli hata post ya uwaziri Mkuu haumfai, kwani siyo mbunifu. Hawa siyo aina ya viongozi tunaowahitaji kwasasa. Tanzania kwasasa tunahitaji Kiongozi Mbunifu mwenye uwezo wa kund'amua mambo ya msingi na creative kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu. Pia huyo kiongozi awe MZALENDO NA JASIRI na mwenye VISION. Hatuhitaji viongozi aina ya JK ambao hawakuwa/hawana na VISION nyingine tofauti na kutaka tu kuwa RAIS bila kujua kwamba je huo URAIS ATAUFANYIA NINI?
watajeni hao mnaotoa sifa zao kama mwenzenu mleta hoja sio mnazungukazunguka na kusema hafai
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom