Elections 2010 JK: Ridhiwani hahusiki kuondolewa Bashe

Kwa Kifukwe je? Mtoto anajijengea maadui wengi sana na hii itamumbua sana mbele ya safari.Lakini kwa vile anashare DNA na babake hatushangai.
 
MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Taifa, Rais Jakaya Kikwete amesema hana tatizo na wanachama wa chama hicho wanaohamia vyama vingine,lakini wasijaribu kukihujumu.

Aidha amesema,mwanawe Ridhiwani hahusiki katika sakata la kuenguliwa kuwania ubunge Jimbo la Nzega, Hussein Bashe kama ilivyoripotiwa kwenye baadhi ya vyombo vya habari.

Kuhusu Bashe, Mwenyekiti huyo wa CCM Taifa alisema kuenguliwa kwa kijana huyo kulifanywa na Kamati Kuu ambayo ilifanya hivyo kwa manufaa ya chama.

Alisema Kamati Kuu hiyo ilijitahidi kuheshimu uamuzi ya wanachama wake, lakini kutokana na sababu mbalimbali kama uraia na utovu wa maadili ambao ungesababisha chama hicho kuanguka katika jimbo husika, walimteua wanayeona anafaa.

Alisema kuna magazeti yanasema maneno mengi ili wanachama wa chama hicho wachukiane na yakishindwa kuona mema ya chama hicho kwa mwaka mzima.

Hata hivyo, baadhi ya vyombo vya habari vilidai kuenguliwa kwa Bashe aliyeongoza kwa kura zaidi ya 14,000 dhidi ya wagombea wengine wawili, Lucas Selelii na Dk. Hamis Kigwangala, kumetokana na tofauti zake na Ridhiwani ambaye kama Bashe ni Mjumbe wa Baraza Kuu la UVCCM.


Source: Habari Leo

Kuna Habari kuwa Dr. Hamis Kigwangala anafanya kazi au ni Mshauri wa Mama SALMA KKIKWETE kwenye NGO yake ya WAMA. Kwa hiyo kupitia Uhusiano huo ndiyo maana Mkulu alimbeba!!!! Je, kuna mwenye data zaidi atujuze???
 
Kuna Habari kuwa Dr. Hamis Kigwangala anafanya kazi au ni Mshauri wa Mama SALMA KKIKWETE kwenye NGO yake ya WAMA. Kwa hiyo kupitia Uhusiano huo ndiyo maana Mkulu alimbeba!!!! Je, kuna mwenye data zaidi atujuze???

Hii ni kweli kabisa yupo kwenye WAMA!..huenda chapuo imetoka kwa mama na zengwe zaidi kwa Ridhiwan kwenda kwa Bashe..so ukiunganisha ya mama na mtoto basi baba anakuwa hana lakufanya kinyume cha wapendwa wake!
 
leo katika magazeti yamemnukuu muungwana akimtetea mwanae Advocate Ridhwani kuuhusu sakata la Bashe, hii ikiamanisha advocate aliyeaapishwa na mahakama kuu ya TZ anashindwa kuitisha hata press conference na kutoa utetezi wake mwenyewe, mpaka asaidiwe na baba
 
Hata mkisafishana kwa sabuni ya magadi hamtatakata kwa maana huwezi kusafisha kitu chochote na maji taka halafu ujidai eti chombo hicho ni kisafi?!!!! Kweli dictatorship haitaisha Tz?? Yaani wakitaja hilo jimbo la Nzega hawamtaji kabisa mwiba wao Selelii.
 
"like father like son" JK anajikosha tu anajua kabisa kwamba mwanae ni chanzo cha mfarakano UVCCM.Dogo ananibore sana aghaaaaaaaaaaa.
 
kama anahusika jk hawezi kusema kwani jk na ridhiwani wote fitina vinasaba vyao vinafanana wote ni wazandiki wafitini na waongo
 
Hapo naona JK kajisahau kuwa anatakiwa kusimama kama Mwenyekiti wa CCM, Rais wa nchi na Si baba wa Kikwere.
 
Hivi mtu mzima kama Ridhiwani tena Advocate anashendwa kujitetea mwenyewe hadi baba amsemee? Haya si ni mambo ya kisiasa ambayo yanahitaji mtu binafsi kutoa tamko? Poor JK umeanza kuweweseka mara hii kwa kuogopa kivuli cha Bashe
 
Kwa ujumla mimi nalichukulia hilo kuwa ni kundi hatari JK, Ridhiwani, Masha, Rostam, Makamba, Chenge na 'mafisadi' wenzao.

Tuwe makini na hila za mafisadi hao. Tuukomeshe utumwa huu uliokithiri. Hakika wananchi hatujui kuwa tunatumika sana kwa manufaa ya wachache wasio na utu hata wa kuwafikiria kina mama na watoto wanaoteseka vijijini kwa kukosa huduma za lazima, huku viongozi wa CCM wakiendelea kujinufaisha wao, rafiki zao na familia zao. Hii ni dhambi
 
kizuri chajiuza, ifikiapo chama tawala kufikilia kupiga kampeni ya nyumba kwa nyumba/chumba kwa chuimba) hapo kuna shida. nilitegemea sasa baada ya kukaa madarakani kwa kipindi chote hiki basi itakuwa na mema mengi ya kujivunia ambayo yangejiuza menyewe bila kutumia msuli, kwa kuwa imefanya mabaya zaidi kuliko mema hapa pana shughuli pevu ya kuanza ku'derive a complex equeations, with a lot of illogical assumptions!!!' na kuirahisisha na kuanza kutoa shule kwa wananchi waelewe kuwa ufisadi (epa, richmond, meremeta nk) vimeinufaisha nchi, kwani vimehakikisha maisha bora kwa kila mtanzania, ndani ya mfumko wa bei, kuongezeka gharama za umeme na maji yote haya ktk kufidia wizi wa richmond nk, vimewezesha kufanikisha kauri mbiu ya maisha bora kwa kila mtanzania kutimia!!!!!!!!!!!!!!
 
Rais aliulizwa na mtu kama mwanae alihusika ktk kumuengua Bashe, mbona anajishtukia???
 
Back
Top Bottom