Ileje
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 8,797
- 12,239
Rais Kikwete jana akizindua ujenzi wa daraja la Kigamboni aliwataka wapinzani wajifunze utamaduni wa kusifu yale mazuri yaliyofanywa na serikali ya CCM ili nao wakipata madaraka wafanye mara tatu maana ni lazima wataendeleza pale alipoishia yeye.
Naye Waziri wa ujenzi Dr. Magufuli akikubaliana na utabiri huo wa Rais alisema kuwa wanataka uzinduzi ufanywe na Rais Kikwete ili Rais mwingine ajaye asije kujivunia mafanikio hayo awe ametoka CCM au upinzani kwani fedha za ujenzi zimetafutwa na serikali ya awamu ya nne.
Wana JF je tunaweza kubashiri kuwa sasa serikali ya CCM imekubali yaishe? TAFAKARI!
Naye Waziri wa ujenzi Dr. Magufuli akikubaliana na utabiri huo wa Rais alisema kuwa wanataka uzinduzi ufanywe na Rais Kikwete ili Rais mwingine ajaye asije kujivunia mafanikio hayo awe ametoka CCM au upinzani kwani fedha za ujenzi zimetafutwa na serikali ya awamu ya nne.
Wana JF je tunaweza kubashiri kuwa sasa serikali ya CCM imekubali yaishe? TAFAKARI!