Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,468
- 911,174
Mgaya apata mpizani TUCTA
na Datus Boniface
MJUMBE wa Baraza Kuu la Taifa la Chama cha Wafanyakazi nchini (TUCTA), Mussa Mnyeti ametangaza nia ya kuwania nafasi ya Katibu Mkuu ndani ya chama hicho.
Hadi sasa nafasi hiyo inashikiliwa na Nicolas Mgaya, ambapo uchaguzi mkuu ndani ya chama hicho unaratajiwa kufanyika Agosti mwaka huu.
Akizungumza na Tanzania Daima jana jijini Dar es Salaam, Mnyeti alisema nia, uwezo, na sababu anazo za kuwania nafasi hiyo.
Uwezo, nia na sababu ninazo za kuwania na kuwa Katibu Mkuu wa TUCTA, kwa ajili ya maslahi ya wanachama na wafanyakazi wote nchini Tanzania, vijana nawaomba wanikubali katika hili kwa ajili ya malengo hayo yaweza kufanikiwa, alisema.
Alisema sababu zilizomfanya kuwania ni pamoja na kuleta ushirikiano baina ya wafanyakazi na vyama vyao.
Alitaja sababu nyingine ni kupigania haki, maslahi pamoja na usawa wa wafanyakazi wa ngazi zote.
Katika maelezo yake alisema endapo akipata nafasi hiyo atapigania kima cha chini cha mshahara kiwe shilingi 315,000 ili kutimiza pendekezo la TUCTA.
Alisema pia atapunguza kodi za wafanyakazi kutokana na makato mbalimbali yanatofanywa katika mishahara yao.
Aidha aliahidi kuwapigia wafanyakazi kulipwa asilimia saba la pato la taifa.
na Datus Boniface
Hadi sasa nafasi hiyo inashikiliwa na Nicolas Mgaya, ambapo uchaguzi mkuu ndani ya chama hicho unaratajiwa kufanyika Agosti mwaka huu.
Akizungumza na Tanzania Daima jana jijini Dar es Salaam, Mnyeti alisema nia, uwezo, na sababu anazo za kuwania nafasi hiyo.
Uwezo, nia na sababu ninazo za kuwania na kuwa Katibu Mkuu wa TUCTA, kwa ajili ya maslahi ya wanachama na wafanyakazi wote nchini Tanzania, vijana nawaomba wanikubali katika hili kwa ajili ya malengo hayo yaweza kufanikiwa, alisema.
Alisema sababu zilizomfanya kuwania ni pamoja na kuleta ushirikiano baina ya wafanyakazi na vyama vyao.
Alitaja sababu nyingine ni kupigania haki, maslahi pamoja na usawa wa wafanyakazi wa ngazi zote.
Katika maelezo yake alisema endapo akipata nafasi hiyo atapigania kima cha chini cha mshahara kiwe shilingi 315,000 ili kutimiza pendekezo la TUCTA.
Alisema pia atapunguza kodi za wafanyakazi kutokana na makato mbalimbali yanatofanywa katika mishahara yao.
Aidha aliahidi kuwapigia wafanyakazi kulipwa asilimia saba la pato la taifa.