Aqua
JF-Expert Member
- Jul 23, 2012
- 1,658
- 1,229
Mkuu kama ulikuwa hujui au hayo majamaa zenu hayawaambii kila sehemu kuna mtawala wa eneo hilo in physical na spiritual world.Huwezi pita sehemu au kuingia ukiwa umevunja utaratibu wa pale utaingia matatizoni.Mimi sikuzuii kufanya hayo mambo ya astral projection nacho jaribu ni kukushauri,ila kama haumwamini Mungu (Yehova) nifahamamishe nitajua pa kuanzi kukusaidia.Lakini kwa maelezo yangu kama kuna mungu unamwamini huyo si kama ninayemwamini mimi.sasa mkuu, kama hujawahi unauhakika upi na suala la uenyeji? unauhakika upi kama hawa wanaofanya hawaongozwi na mungu? unauhakika upi kama utakutana na roho chafu.
#mwisho ni kwamba kama ikitokea kwako utakuwa na uhakika gani kama utakuwa unaongozwa na mungu?... natumaini utanielezea vizuri ndugu!
Ningependa nijifunze kutoka kwako kama kuna mungu anawaongoza niambie anaitwa nani na taja baadhi ya watumishi wake wa mwazoni kwa maana ya mitume na manabii au majina yoyote.
Uhakika kama ikinitokea nitajua kwani roho iliyomo ndani yangu itanishuhudia kwamba nachofanya kinatokana na Mungu au ni yule adui ambaye tunajua ni baba wa uongo.
Shetani ni mwongo siku zote sasa anatambua mnajifanya wazinduzi ametumia agent wake kuwapa hiyo elimu,sikatai kwamba unaweza kwenda nje ya mwili inawezekana na hata wachawi wanafanya.Na kama ulikuwa hujui wachawi siku zote wanajiona wako juu ya binadamu wa kawaida kwa kuwa wao wanaweza kufanya mambo mengine kama kuruka usiku.Hii AP mnaonjeshwa mkizoea mtafundishwa na mengine.kitu ambacho wanadamu mnashindwa kujua Mungu kuna nguvu ndani yetu imewekwa,wengi waliofanya hii AP mwanzoni wanasema waliingiwa na woga,huo woga unatoka wapi?Walivyozidi kung'anga'nia woga umewatoka.Mungu humwonya mtu kwanza kabla ya kumwadhibu.Mwenye masikio na asikie.
Niko nafuatilia issue ya jicho la tatu,nayo inaonekana uongo kama mtu anaweza kuona kwa jicho la tatu mbona hii ingekuwa ni habari njema kwa vipofu.
Watu wangu wanapotea kwa kukosa maarifa.
Kuna vitu hamvisemi,Rakim mwanzoni alisema with AP huwezi kuchukua vitu sasa anasema ataleta thread ya kuchukua pesa na kuziweka chini ya mtu.Dini zote kuu zinazuia wizi,kuchukua kitu bila ruksa ni wizi sasa kama utaweza chukua pesa zisizo zako huo ni wizi na ni Shiriki kwa lugha ya Quran.
Aidha mnatumiwa hamjijui au mnajua,endeleeni mtazidi kupandishwa vyeo katika huo ufalme kwani mnapeleka roho nyingi za watu .
Mwili ni sehemu ambapo Mungu aliweka nafsi na roho ziishi humo,sasa mnapotoka nje ya mwili hizo nafsi zenu zinakuwa katika mwili upi kama mwili mliopewa na Mungu mnauacha.Fuatilia katika hili kwanza mwili unaokuwa nao ni upi?Mtu anapokufa nafsi aidha inakuwa kuzimu ikisubiria hukumu ya mwisho au Paradiso ikisubilia kwenda mbinguni.
Sasa nafsi zenu zikitoka katika mwili ,zinakuwa wapi?Shetani anauwezo wa kukuonyesha sehemu ikafanana na Manzese au Sinza unayoijua wewe nawe ukadhani umeenda kutembea.
Shetani ana uwezo wa kuvaa sura ya mtu na kutimiza malengo yake,kuwa makini mkuu.Kama AP ingekuwa ni kitu kimegunduliwa basi tungekikuta kwenye elimu zetu na tungefundishwa mnajipa moyo ni elimu ilivyofichwa .