Good Guy
JF-Expert Member
- Oct 24, 2010
- 3,809
- 1,406
Okay, good for you sir!!Good Guy,
Huwa sichoki kuisema hii kauli yangu, wizi wowote ule, kwa kisingizio kuwa sisi au mimi bado yamepitwa na wakati.
Machine yangu personal nimenunua ikiwa na operating system pre-installed, software uchwara ambazo zilikuwa tu za kunivutia na hapo baadae iwe mimi natoa mihela kupata full version. Sikufanya hivyo, bali nilitafuta alternative solutions ambazo ni opensource.
Natumia open-office as an alternative to MS Office. Ila kila mwaka gharama zangu za software ni ndefu tu kwani kazi za watu nazidhamini, nazilipia ndio na wao waendelee kuzi-support na kuzi-develop with new features.
OK Hizi commercial software ni bei mbaya, je ukihamisha fikra kama hizi kwenye mambo mengine itakuwaje? Mimi sina uwezo wa kununua gari, sina nia ya kununua gari, je katika pita pita zangu nikiona gari imeegeshwa niipakue tu, kwani sina uwezo wa kuimiliki. Au kwa sababu software sio physical entity unadhani kuwa huo sio wizi?
Artists wetu, kwenye filamu na pia muziki wanalia, wapo hoi, kwa sababu tunapenda sana, tena sana na kuisifia nyimbo au filamu zao, lakini kununua ola, tunasubiri copy... sasa nani anafaidika?
Kama hatuna uwezo, basi tuujenge uwezo wa kumiliki hivi vitu.