Jinsi ya kupata marafiki na kushawishi watu

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Jan 31, 2021
7,224
12,729
.Kwa sababu hili ni jukwaa la urafiki na mahusiano, basi itakuwa sehemu sahihi kupitia kitabu hiki. How to win friends and influence people

JINSI YA KUPATA MARAFIKI NA KUSHAWISHI WATU



DALE CARNEGIE





Muandishi: Dale Carnegie, 1936.
Mtafsiri: Pictus Publishers ltd
Email: pictuspublishers@gmail.com
©Pictus Publishers ltd2022.
Haki zote zimehifadhiwa. Hakuna sehemu yoyote ya tafsiri hii inayoweza kunakiliwa, kutolewa kivuli, kuhamishwa, kurekodiwa au kutolewa kwa namna yeyote bila ya taarifa ya awali ya kimaandishi ya mtafsiri.

SEHEMU YA KWANZA

KANUNI ZA MSINGI ZA JINSI YA KUSHUGHULIKA NA WATU





KAMA UKITAKA KURINA ASALI USIPIGE TEKE MZINGA

Tarehe 7 mwezi wa tano mwaka 1931 kulikuwa na msako wa aina yake wa mhalifu ambao New York halijawahi kushuhudia. Baada ya msako wa wiki kadhaa, mhalifu aliyejulikana kama Crowley “Bunduki mbili”, muuaji na jambazi wa kutumia silaha ambaye hakutumia wala kuvuta kilevi chochote alikuwa amepatikana. Alikuwa amezingirwa katika makazi ya mpenzi wake katika mtaa wa West End.

Polisi mia moja na hamsini walizingira maficho yake yaliyokuwa kwenye ghorofa ya juu kabisa. Walikuwa wametoboa matundu kwenye paa. Walikuwa wanajaribu kumtoa Crowley “Muua polisi” kwa kutumia gesi ya kutoa machozi. Walitega bunduki katika majengo yanayozunguka. Kwa zaidi ya saa nzima, eneo tulivu la jiji la New York lilirindima kwa milio ya bastola na bunduki za rasharasha. Crowley alijificha nyuma ya sofa na kuwarushia polisi risasi mfululizo. Watu elfu kumi walikuwepo kushuhudia mapambano hayo. Kitu kama kile hakijawahi kutokea katika jiji la New York.

Crowley alipokamatwa, kamishna wa polisi, E. P. Mulrooney alikiri kuwa jambazi Crowley “Bunduki mbili’ ni moja ya wahalifu hatari zaidi kuwahi kutokea katika historia ya jiji la New York. “Huyu haoni taabu kuua,” alisema kamishna.



Lakini Crowley “Bunduki mbili” alikuwa na maoni gani kujihusu? Tunafahamu maoni yake kwa sababu wakati polisi wanarusha risasi kwenye makazi yake, yeye aliandika barua kwa “Yeyote atayejali.” Wakati anaandika barua hiyo, damu kutoka kwenye majeraha yake iliacha alama katika karatasi. Kwenye barua hiyo Crowley alisema: “Katika kifua changu mna moyo uliopondeka lakini wenye rehema, moyo usioweza kumdhuru yeyote.”

Kabla ya tukio hili Crowley alikuwa anafurahia maisha na mpenzi wake katika barabara moja huko Long Island. Ghafla polisi aliwafuata kwenye gari na kusema: “Naomba kuona leseni yako.” Bila kujibu kitu, Crowley alitoa bunduki na kummiminia mvua ya risasi. Polisi yule alipokuwa anakufa, Crowley alitoka ndani ya gari na kuchukua bastola ya polisi na kuumiminia risasi mwili uliokuwa umelala chini, huyo ndiye muuaji aliyesema: “Moyo wangu umepondeka lakini ni wenye rehema, hauwezi kumdhuru yeyote.”

Crowley alihukumiwa kifo kwa kiti cha umeme, alipokuwa anaingia kwenye gereza la wafungwa wanaosubiria kifo alisema, “Je hiki ndicho malipo ya kuua watu? Hapana, haya ni malipo ya mimi kujilinda.”

Lengo la hadithi hii ni kuonyesha kuwa: Crowley “Bunduki mbili” hakuona kama ana kosa lolote.

Je hilo ni jambo lisilo la kawaida kwa wahalifu? Kama unafikiri si la kawaida sikiliza haya:

“Nimetumia miaka yangu kuwapa watu furaha, na kuwasaidia kuwa na maisha mazuri na malipo niliyopata ni uonevu.Kuishi kama digididi.”

Hayo yalikuwa ni maneno ya Alcapone. Muhalifu hatari kabisa Marekani. Kiongozi wa genge la uhalifu hatari kabisa kuwahi kutokea katika jiji la Chicago. Capone hakujilaumu, badala yake alijiona ni mtu anayesaidia jamii. Msaidia jamii asiyeeleweka na asiyethaminiwa inavyostahili.

Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa Dutch Schultz kabla ya kuuwawa na mwanachama wa genge la uhalifu huko Newark. Mtu mmoja alisema katika mahojiano kuwa Dutch Schultz alikuwa ni mtu anayesaidia jamii na aliamini hivyo.

Nimewahi kuzungumza kuhusiana na hili suala na Lewis Lawes ambaye alikuwa ni mkuu wa gereza maarufu huko New York la Sing Sing kwa miaka mingi, alikiri kuwa ni “Wahalifu wachache sana wanajiona kuwa ni watu wabaya. Wanajiona ni watu wa kawaida kama mimi na wewe tu. Wanajiona kuwa wana sababu za msingi za kufanya wanayoyafanya. Wanaweza wakakuambia ni kwanini wanavunja sanduku la pesa, au kwanini ni wepesi kufyatua risasi. Wengi wao hujitahidi kutafuta sababu za uwongo na kweli kutetea uovu wao. Hata wakijaribu kujiaminisha wao wenyewe kuwa hawana hatia. Hupaza sauti wakisema hawakustahili kufungwa.

Iwapo Al Capone, Crowley “Bunduki Mbili,” Dutch Schultz na wanaume na wanawake wengine waliojaa magerezani hawajilaumu kwa chochote, vipi kuhusu watu ambao mimi na wewe tunakutana nao?

Muanzilishi wa maduka ya Wanamaker, John Wanamaker aliwahi kiri hivi: “Nilijifunza miaka thelathini iliyopita kuwa ni ujinga kushutumu. Ninapata ugumu wa kutosha katika kukabiliana na mapungufu yangu, siwezi anza kuhangaika na ukweli kuwa Mungu aliamua kutogawa akili kwa usawa.”

Wanamaker alijifunza jambo hilo mapema sana, lakini mimi imenichukua kufanya makosa kwa theluthi ya karne kabla sijaanza kuelewa kuwa kati ya mia moja, mara tisini na tisa, watu huwa hawajishutumu kwa chochote. Haijalishi ni kibaya kiasi gani. Kushutumu hakusaidii lolote, na zaidi zaidi kunamfanya mtu ajitahidi kujitetea. Shutuma ni hatari kwa sababu zinaharibu heshima ya mtu, inampunguzia kujithamini na huleta chuki.

Mwanasaikolojia maarufu, B. F, Skinner alithibitisha kupitia majaribio aliyoyafanya kuwa, mnyama anayezawadiwa kwa kuwa na tabia njema hujifunza haraka, na hukumbuka vizuri kile alichojifunza kuliko mnyama anayeadhibiwa kwa kuwa na tabia mbaya. Tafiti zilizofuatia zilionyesha kuwa hata kwa binadamu iko hivyo. Kwa kushutumu hatuleti mabadiliko ya kudumu, na mara nyingi tunaishia tu kujenga chuki.

Mwanasaikolojia mwingine maarufu, Hans Selye alisema, “Kama ambavyo tunapenda kukubalika, ndivyo tunavyochukia kushutumiwa.”

Chuki inayoletwa na na shutuma, inaweza athiri ari ya wafanyakazi, washiriki wa familia na marafiki, na bado ikawa haijarekebisha jambo au hali ya mambo iliyosababisha shutuma.

George B Johnston kutoka Enid Oklahoma ni msimamizi wa masuala ya usalama katika kampuni ya uhandisi. Moja ya majukumu yake ni kuhakikisha wafanyakazi wanavaa kofia ngumu kila wanapokuwa kazini.Alisema kuwa, kila alipokuwa anakutana na mfanyakazi ambaye hajavaa kofia ngumu, alikuwa akimwambia kama mtu mwenye mamlaka kuhusu sheria ya kuvaa kofi na kuwa anapaswa aifuate. Matokeo yake ni kuwa walimkubalia kwa shingo upande, na mara tu alipotoka wafanyakazi walivua kofia zao.

Akaamua kutumia mbinu nyingine. Alipokutana tena na wafanyakazi ambao hawajavaa kofia zao, aliwauliza iwapo kofia zinawatinga au haziwatoshi vizuri. Kisha kwa kauli nzuri aliwakumbusha kuwa kofia zimetengenezwa kwa namna itakayowalinda na madhara, na kushauri kuwa zivaliwe mara zote wawapo kazini. Matokeo yake ni kuwa watu wakaongeza uvaaji wa kofia bila kinyongo wala kujihisi vibaya.

Katika historia unaweza kuona mifano mingi ya jinsi ambavyokushutumu kusivyo na faida. Chukulia mfano wa ugomvi wa Theodore Roosevelt na Rais Taft, ugomvi ambao ulikigawa chama cha Republican, ukasababisha Woodrow Wilson kuwa Rais na kubadili historia. Hebu acha tuuchunguze vizuri mfano huo. Punde tu baada ya Theodore Roosevelt kuachia urais mwaka 1908, akaanza kumuunga mkono Taft ambaye alichaguliwa kuwa Rais. Baada ya hapo Theodore Roosevelt akafunga safari kwenda Africa kutalii na kuwinda. Aliporudi aliwaka kwa hasira, akatangaza kutomuunga mkono Taft kwa sababu ya uhafidhina wake, na akajaribu kuingia madarakani kwa muhula wa tatu na akaunda chama kilichoitwa Bull Moose, hilo halikusaidia kitu zaidi ya kukidhoofisha chama cha Republican. Katika uchaguzi uliofuata, William Howard Taft na chama cha Republican walishinda katika majimbo mawili tu, Vermont na Utah. Chama hakijawahi shindwa namna hiyo. Theodore Roosevelt alimlaumu Taft. Lakini je, Rais Taft alijilaumu mwenyewe? Hapana hata kidogo, kwa machozi Taft alisema: “Sioni kama kulikuwa na namna bora ya kufanya mambo zaidi ya nilivyofanya.”

Ni nani wa kulaumiwa? Roosevelt au Taft? Kwa kweli sijui na sijali. Jambo ninalotaka kueleza na kuwa, shutuma zote za Theodore Roosevelt hazikuweza kumuaminisha Taft kuwa alikosea. Badala yake zilimfanya Taft ajitahidi kujitetea hadi kwa machozi akisema: “Sioni kama kulikuwa na namna bora ya kufanya mambo zaidi ya nilivyofanya.”

Au fikiria juu ya kashfa ya Teapot Dome. Kashfa iliyopamba magazeti mwanzoni mwa miaka ya 1920. Ilitingisha nchi. Na katika kumbukumbu za watu leo, jambo kama lile halijawahi kutokea ndani ya Marekani. Kashfa yenyewe ilikuwa namna hii: Waziri wa mambo ya ndani wa Marekani katika baraza la rais Harding, bwana Albert B. Fall alipewa jukumu la kukodisha visima vya mafuta vya serikali huko Elk Hill na Teapot Dome ambavyo viliwekwa kwa ajili ya matumizi ya baadaye ya jeshi la majini. Je Fall aliruhusu mnada kufanyika? Hapana. Alimpatia mkataba huo mnono rafiki yake aliyeitwa Edward L. Doheny. Na Doheny alifanya nini? Alimpatia Fall “mkopo” wa dollar laki moja. Na kwa kutumia madaraka vibaya, Fall akaagiza kikosi cha jeshi la Marekani kuwaondoa wachimbaji wengine wa karibu ambao visima vyao vilikuwa vikinyonya mafuta kutoka ukanda wa Elk Hill. Wachimbaji hawa baada ya kufukuzwa kwa mtutu wa bunduki na singe wakaamua kwenda mahakamani na kufumua kashfa ya Tea Dome. Kashfa yenye harufu mbaya sana kiasi cha kuharibu uongozi wa Rais Harding na kuitia kichefuchefu nchi nzima. Ilisababisha Albert B. Fall kufungwa, na ilitishia kusambaratisha chama cha Republican.

Fall alishutumiwa vikali sana, ni watu wachache sana wamewahi shutumiwa namna ile. Je alitubu? Hata kidogo! Miaka kadhaa baadaye Herbert Hoover alisema hadharani kuwa Rais Harding alikufa sababu ya matatizo ya kiakili yaliyosababishwa na kusalitiwa na rafiki. Mke wa Fall aliposikia jambo hili aliruka kitini, alilia, alijipigapiga na kusema kwa hasira: “Nini! Harding alisalitiwa na Fall? Hapana! mume wangu hajawahi msaliti yeyote. Nyumba iliyojaa dhahabu isingeweza mshawishi mume wangu kutenda ndivyo sivyo. Yeye ndiye aliyesalitiwa na kutolewa kafara.”

Basi hiyo ndiyo hulka ya binadamu, waliofanya makosa hulaumu kila mtu isipokuwa wao wenyewe. Sote tupo namna hiyo. Kwa hiyo, kama kesho tukitaka kumshutumu mtu, acha tuwakumbuke Al Capone, Crowley “Bunduki Mbili” na Albert Fall. Tuelewe kuwa kushutumu ni kama njiwa wa kufugwa. Siku zote hurudi nyumbani. Acha tuelewe kuwa mtu tunayeenda kumshutumu na kumsahihisha labda atajaribu kujitetea, na kutushutumu sisi badala yake: au kama ni mstaarabu kama Taft atasema: “Sioni kama kulikuwa na namna bora ya kufanya mambo zaidi ya nilivyofanya.”

Katika asubuhi ya tarehe 15 mwezi wa nne mwaka 1865 Abraham Lincoln alipokuwa karibu kufa kwenye makazi duni yaliyokuwa ng’ambo ya barabara kutoka ukumbi wa Ford ambako John Wilkes Booth alimpiga risasi. Lincoln akiwa amelala kwa ulalo kitandani kwa sababu mwili wake ulikuwa mrefu sana kutosha kitandani. Mchoro mbovu wa Rosa Bonheur, The Horse fair ukining’inia ukutani mbele ya kitanda na karabai ikitoa mwanga hafifu wa njano.

Lincoln alipokuwa hoi kitandani, waziri wa mambo ya vita , bwana Stanton alisema, “Hapa amelala kiongozi bora kabisa kuwahi kutokea duniani.”

Ni siri gani iliyomfanya Lincoln aweze kuchukuana na watu vizuri? Nimetumia miaka kumi nikisoma maisha ya Abraham Lincoln. Kwa miaka mitatu nilishughulika na kuandika kitabu kiitwacho Usiyoyajua kuhusu Lincoln. Nafikiri nimegusa maisha ya Lincoln kwa undani kadri inavyowezekana. Kwa upekee kabisa, nilijikita kusoma jinsi Lincoln alivyoshughulika na watu. Je alijihusisha na kushutumu? Ndiyo, alipokuwa kijana huko Pigeon creek Valley, Indiana, alijihusisha na sana na kushutumu watu, na siyo kushutumu tu, bali alikuwa akiandika barua na mashairi ya kuwadhihaki watu. Alitupa barua na mashairi hayo barabarani ambako alijua watu watazipata kirahisi. Moja ya barua hiyo ilisababisha kinyongo ambacho kilidumu maisha yote.

Hata baada ya Lincoln kuwa mwanasheria huko Springfield, Illinois, bado alikuwa na tabia ya kuwashambulia wapinzani wake kwa barua alizozichapisha katika magazeti. Lakini mtindo huu haukuwa na mwiho mzuri. Katika majira ya kupukutika ya mwaka 1842 alimshambulia kwa dhihaka mwanasiasa mmoja mkali na mwenye majivuno aliyeitwa James Shields. Alimshambulia kwa barua ya siri iliyochapishwa gazeti la Springfield journal, mji wote ulilipuka kwa vicheko kutokana na barua hiyo. Sababu Shields alikuwa ni mwenye majivuno, akawaka hasira kwa kudharauliwa. Akachunguza na kugundua aliyeandika barua ile, akamuendea Lincoln na kumwambia wapambane ana kwa ana. Lincoln alikuwa hataki kupambana, na alikuwa ni mpinzani wa mapambano kama hayo. Lakini pia haikuwezekana aepuke jambo hilo na kubaki na heshima yake. Aliambiwa achague silaha yake. Kwa sababu alikuwa na mikono mirefu alichagua panga lililotumika na jeshi la wapanda farasi, na akapata mafunzo ya kupigana kwa mapanga kutoka kwa mhitimu wa chuo cha jeshi cha West Point. Siku ya pambano, yeye na Shields wakakutanakwenye mchanga katika mto Mississipi, wakiwa wamejiandaa kupambana hadi kifo. Lakini mwishoni kabla ya pambano, wapambe wao waliingilia kati na kusimamisha pambano.

Hiyo ilikuwa ni hali tete kabisa kwa Lincoln kuwahi kujikuta katika maisha yake binafsi. Lakini alipata somo muhimu sana kuhusiana na kushughulika na watu. Hakuandika tena barua ya dhihaka, wala hakumdhiki yeyote tena. Na kuanzia wakati huo hakumshutumu mtu yeyote.

Wakati wa vita ya wenyewe kwa wenyewe, Lincoln alibadilisha majenerali wake walioongoza mara kwa mara. Na mara zote, majenerali wote—McClellan, Pope, Burnside, Hooker, Meade—Walivurunda vibaya na kumuacha Lincoln akihangaika asijue la kufanya. Nusu ya nchi iliwashutumu vikali majenerali hao kwa uzembe, lakini Lincoln, “Bila ubaya kwa yoyote, na kusaidia wote,” hakutoa shutuma. Moja ya nukuu alizozipenda sana, “Usihukumu nawe hutahukumiwa.”

Na hata mke wake na watu wengine walipowaongelea watu wa kusini kwa ubaya, Lincoln alijibu: “Msiwashutumu, hata sisi tungekuwa katika hali yao tungetenda kama wao.”

Pamoja na hayo, kama kuna mtu alikuwa na haki ya kurusha shutuma basi alikuwa ni Lincoln. Acha tuone mfano mmoja:

Pambano la Gettysburg lilipiganwa katika siku tatu za mwanzo za mwezi wa saba wa mwaka 1863. Katika usiku wa tarehe 4 ya mwezi huo, jenerali Lee, akiwa na jeshi lake lililoshindwa alianza kurudi kusini, mvua kubwa ilikuwa inanyesha. Alipofika kwenye mto Potomac, alikuta umefurika haupitiki, huku jeshi la muungano likiwa nyuma yake. Lee alikuwa amebanwa kwenye kona bila njia ya kutorokea. Lincoln aliona jambo hilo. Ilikuwa ni fursa adhimu ya kuteka jeshi la Lee na kukomesha vita mara moja. Kwa hiyo kwa matumaini makubwa ya ushindi, Lincoln alimuamuru Meade kutoitisha baraza la vita na badala yake amvamie Lee mara moja. Alimtuma mjumbe maalumu na aliyepeleka amri kwa Meade akimtaka avamie jeshi la Lee mara moja.

Lakini Jenerali Meade alifanya nini? Alifanya kinyume kabisa na alichoagizwa. Aliitisha baraza la vita, akikiuka amri ya Lincoln waziwazi. Alisita na kujizungushazungusha. Alituma ujumbe akitoa visingizio kibao. Alikuwa amekataa kutii amri waziwazi. Mwishowe maji yalipungua na Lee akavuka mto Potomac na jeshi lake na kutoroka.

Lincoln alikasirika sana, “Nini maana ya jambo hili?’” alipiga kelele akimwambia Robert, mtoto wake. “Mungu wangu! Nini maana ya jambo hili? Walikuwa wetu kabisa, tulihitaji tu kunyoosha mkono na kuwakamata, lakini hakuna ambacho ningefanya au kusema kulifanya jeshi livamie. Kwa hali aliyokuwa nayo Lee, jenerali yoyote angemshinda. Hata mimi mwenyewe ningekuwepo pale ningemtandika.”

Katika hali hiyo, Lincoln akaketi na kuandika barua kwenda kwa Meade. Na kumbuka kuwa wakati huo Lincoln alikuwa mhafidhina hasa, na alijizuia katika maneno yake. Kwa hiyo barua hii ya mwaka 1863 kutoka kwa Lincoln inaonyesha shutuma kali zaidi alizoweza kutoa.

Mpendwa Jenerali

Siamini kama huelewi hali mbaya aliyokuwa nayo Lee kabla ya kutoroka. Alikuwa kaingia mikononi mwetu. Na kumkamata, pamoja na ushindi tuliopata hivi karibuni, kungemaliza vita. Lakini kwa sababu hilo halikutokea, inaonekana vita hii itaendelea kwa muda mrefu sana. Kama hukuweza kumvamia Lee jumatatu iliyopita, sehemu yenye usalama. Utawezaje kumvamia huko kusini ya mto, sehemu ambayo unaweza kwenda na si zaidi ya theluthi mbili ya jeshi lako? Haiingii akilini kutarajia, na wala sitarajii kama utakuwa na manufaa ya maana. Fursa nzuri ya kufanya hivyo imekwishapita, na hilo jambo limenikoseha amani kabisa.

Unafikiri Meade alifanya nini baada ya kusoma barua hiyo?

Meade hakupata barua hiyo. Lincoln hakuituma. Ilipatikana katika nyaraka zake baada ya kifo chake.

Mimi nadhani-na huku ni kudhani tu- kuwa baada ya kuandika barua ile. Lincoln alitazama nje kupitia dirishani na kujisemea, “Ngoja kwanza, labda sitakiwi kuwa na haraka hivi. Ni rahisi kwa mimi kukaa hapa katika usalama wa ikulu kumuamuru Meade avamie: lakini kama ningekuwepo Gettysburg, na kama ningeona umwagaji wa damu kama alioona Meade wiki iliyopita, na kama masikio yangu yangekuwa yamechomwa na vilio vya majeruhi na wanaokufa, pengine hata mimi nisingekuwa na mshawasha wa kuvamia. Vyovyote vile, yaliyopita si ndwele. Kama nikituma barua hii, itatuliza hisia zangu, lakini itamfanya Meade ajaribu kujitetea. itamfanya anishutumu. Itafanya kuwe na kinyongo kati yetu na na kufanya iwe ngumu kumtumia kama kamanda, na pengine itamfanya ajiuzulu toka jeshini.”

Kama nilivyokwisha sema, Lincoln aliiweka barua hiyo pembeni, alikuwa amekwishajifunza kwa uchungu kuwa shutuma kali na kusuta karibu mara zote huwa na mwisho mbaya.

Theodore Roosevelt aliwahi kusema kuwa alipokuwa anakabiliwa na jambo tata wakati alipokuwa rais, alikuwa akikaa na kuangalia picha kubwa ya Lincoln iliyokuwa imeningi’nizwa juu ya meza ofisini kwake kisha akajiuliza, “Kama Lincoln angekuwa kwenye viatu vyangu angetendaje? Angetatua vipi tatizo hili?”

Wakati ujao tukishawishika kumsuta mtu, tutoe noti ya dola tano kutoka mfukoni na kuangalia picha ya Lincoln kwenye noti hiyo na tujiulize. “Kama tatizo hili lingemkuta Lincoln, angeshughulika nalo namna gani?”

Mark Twain alikuwa ni mtu wa kulipuka hasira mara kwa mara, aliandika barua zenye maneno makali yaliyoweza kubadilisha rangi ya karatasi. Kwa mfano; kuna kipindi alimuandikia mtu aliyemuudhi maneno haya: “Jambo linalokufaa ni kibali cha mazishi yako tu. Sema nami nitahakikisha unakipata.” Wakati mwingine aliandika hivi kwa mhariri baada ya mtu anayehakiki habari kujaribu kurekebisha baadhi ya maneno aliyoandika. Alisema: “Acha hiyo kazi kama nilivyoiandika, na mwambie huyo uliyempa kazi ya kuhakiki abaki na maoni yake katika matope ya ubongo wake uliooza.”

Barua hizi kali zilimfanya Mark Twain ajihisi vizuri. Zilimfanya atoe dukuduku lake, lakini barua hizo hazikuwa na madhara yoyote sababu mke wake alizitoa zisitumwe kwa siri.

Je, unamfahamu mtu yeyote ambaye ungependa kumrekebisha na kumfanya awe bora? Vema! Hilo ni jambo zuri na naliunga mkono. Lakini kwanini usianze na wewe mwenyewe. Kwa mtazamo wa kibinafsi kabisa, hilo ni jambo lenye faida zaidi kuliko kutaka kufanya wengine wawe bora, na pia ni salama zaidi. Mwanafalsafa wa China, Confucius aliwahi kusema: “Usilalamike juu ya theluji iliyo juu ya paa la jirani yako wakati njia ya kuingia ndani kwako ni chafu.”

Nilipokuwa kijana, nilipokuwa najitahidi sana kukubalika na watu niliandika barua ya kipumbavu kwenda kwa bwana Richard Harding Davi, mwandishi ambaye kuna wakati alikuwa mtu mkubwa katika fasihi ya Marekani. Nilikuwa naandaa makala kuhusu waandishi na nilimuomba bwana Davis anieleze kuhusu mbinu za kazi zake. Wiki chache zilizopita nilikuwa nimepokea barua kutoka kwa mtu fulani ambayo mwishoni ilikuwa imeandika, “Maneno ni yangu, lakini barua hii sijaiandika wala kuihariri.” nilistaajabu sana, nilihisi muandishi atakuwa ni mtu mkubwa, na mwenye majukumu mengi sana.

Mimi sikuwa na majukumu yoyote ya kunitinga lakini nilitaka kuonekana wa maana kwa Richard Harding Davis, hivyo mwisho wa barua yangu niliandika: “Maneno ni yangu, lakini barua sijaiandika wala kuihariri.”

Hakujishughulisha na kujibu barua yangu. Badala yake aliirudisha ile niliyoandika chini yake akiwa ameandika: “Tabia yako mbaya inazidiwa ubaya na tabia yako tu.” Ni kweli nilikuwa nimefanya kosa kubwa, na pengine nilistahili kukosolewa. Lakini kwa sababu nami ni binadamu nilichukia hilo. Nilichukia kiasi kwamba nilipopata habari ya kifo cha Richard Harding Davi miaka kumi iliyofuata, kwa aibu nikiri kuwa kitu kilikilichokuwepo kichwani mwangu ni jinsi alivyoniumiza.

Kama mimi na wewe kesho tunataka kutengeneza chuki itakayodumu miongo na miongo mpaka kifo, basi tujihusishe na ukosoaji wenye kuumiza. Haijalishi tunaamini kiasi gani kuwa ukosoaji huo ni muhimu.

Tunaposhughulika na watu inatakiwa tuelewe kuwa hatushughuliki na kiumbe anayeongozwa na mantiki, bali anayeongozwa na hisia, kiumbe aliyeharaka katika kunyanyapaa, anayechochewa na majivuno na kujikweza.

Shutuma kali zilimfanya Thomas Hardy, moja ya waandishi bora kabisa wa fasihi ya kiingereza, kuachana kabisa na kazi ya kundika riwaya. Shutuma zilimfanya Thomas Chatterrton, mshairi wa kiingereza kujiua.

Wakati angali kijana, Benjamin Franklin hakuwa na ujuzi wowote wa maana, lakini baadaye akawa mwanadiplomasia mzuri na mtu mwenye uelewa sana wa jinsi ya kushughulika na watu, hata akafanywa kuwa balozi wa Marekani nchini Ufaransa. Siri ya mafanikio ? Alisema: “Sitamuongelea yoyote kwa ubaya, na nitaongelea mema yote ninayoyafahamu ya watu wote.”

Mpumbavu yoyote anaweza kushutumu, kulaumu na kuhukumu—na wapumbavu wengi hufanya hivyo. Lakini inahitaji uungwana wa hali ya juu kujizuia, kuwa muelewa na mwenye kusamehe.

Caryle aliwahi kusema: “Mtu mkuu huonyesha ukuu wake kwa jinsi anavyowatendea watu wa chini.”

Rubani maarufu na mshiriki wa mara kwa mara wa maonyesho ya anga, Bob Hoover alikuwa anarudi nyumbani kwake huko Los Angeles kutoka katika maonyesho ya anga huko San Diego. Kama habari yake ilivyoandikwa kwenye jarida Flight Operations, ilisemwa alipokuwa kimo cha futi mia tatu angani, injini zote ziliacha kufanya kazi. Kwa utaalamu wake aliweza kuitua ndege lakini iliharibika vibaya, japo hakuna aliyejeruhiwa.

Jambo la kwanza alilofanya Hoover baada ya kutua ni kuchunguza mafuta ya ndege. Kama alivyokuwa amehisi, ndege yake yenye injini ya mapanga, ya zama za vita ya pili ya dunia ilikuwa imewekewa mafuta ya ndege zenye injini ya jet badala ya petrol.

Aliporudi uwanja wa ndege akaomba kuonana na fundi aliyehudumia ndege yake. Fundi mwenyewe alikuwa kijana mdogo tu. Alikuwa amefadhaishwa sana na kosa lake. Machozi yalikuwa yakimtoka Hoover alipokuwa akimfuata. Alikuwa amesababisha uharibifu wa ndege ya gharama sana. Na alikuwa karibu kusababisha vifo vya watu watatu. Unaweza hisi hasira aliyokuwa nayo Hoover. Unaweza kudhania maneno makali ambayo rubani huyu makini na aliyejivuna angetoa juu ya uzembe ule. Lakini Hoover hakumsema fundi huyu wala hata hakumshutumu. Badala yake aliweka mkono wake kwenye bega la fundi yule na kusema, “Kuonyesha kuwa nina hakika hutarudia kufanya hivi tena, nataka kesho uhudumie ndege yangu aina ya F-51.”

Mara nyingi wazazi hushawishika kuwashutumu watoto wao. Labda unategemea niseme, “Wasifanye hivyo.” Hapana hata kidogo. Nitachosema ni kuwa, “Kabla ya kuwashutumu, wasome moja kati ya makala ya maana sana kuwahi kuandikwa na wanahabari wa Marekani, ‘Baba husahau.’ ”

Kwa mara ya kwanza iliandikwa katika gazeti People’s home Journal. Tutaiandika tena hapa kwa ruhusa ya muandishi, kama ilivyofupishwa kwenye jarida la Reader’s Digest.

“Baba husahau’ ni moja ya makala zinazohamsha hisia kwa wasomaji wengi sana kiasi kwamba inachapishwa kila mwaka. Toka ilipochapishwa kwa mara ya kwanza. “Baba husahau” imeandikwa tena na tena, anasema muandishi wake, W. Livingston Larned, “Imeandikwa kwenye mamia ya majarida, vipeperushi na magazeti nchini kote. Pia imeandikwa na kufasiriwa katika lugha nyingi sana. Nimetoa ruhusa kwa maelfu waliotaka waliotaka kuisoma wakiwa kanisani, shuleni au kumbi za mihadhara. Imetangazwa katika vipindi mbalimbali. Na hata vijarida vya vyuo na shule za upili vimeitumia
 
wao kumbe kizuri itabidi nikisome.. nnacho mda kweli cha kingereza lkn
 
Mimi ningeshauri kile kitabu cha how to think and grow rich kifundishwe mashuleni kuliko kile cha pamela na kipini ujinga mtupu bora wafundishe rich dad poor dad mara mia.
Weeee... mdomo koma.

Hadithi zile tamu kuliko unazoongopewa na Babu yako wa hapo Kigilagila.

1. Mandawa na Manenge.

2. Pazi na jogoo.

3. Juma na Uledi.

4. Sikulamba sukari.

5. Pepe huna masikio.

6. Mti utoao siri za Mfalme.

Hapo tushatoka kukimbia mchaka mchaka na ambao hawakuwahi namba adhabu zao ni bakora, kuchimba visiki/changarawe, kufyeka nyasi au kusesa tuta na kutifua.

Baada ya kutoka darasani ni kwenda mapumbani kuruka sarakasi, mtoni kupiga mbizi, kucheza mpira, kutinga kwenye vibanda umiza kuangalia muvi na kurudi home kupewa mkong'oto haswaa hapo bado komborela jioni.

Muda ni ukuta, unatamani urudishe wakati nyuma ufurahie maisha lakini umri ndiyo hivyo tena

Watoto wa kizazi hiki wanacheza mipira kwenye play station na kuendesha magari bila hata kutokwa jasho daaah

Wahenga wezangu msipite hapa bure bila kuongezea hadithi za enzi zetu tuko darasa la 1 - 7...

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
.Kwa sababu hili ni jukwaa la urafiki na mahusiano, basi itakuwa sehemu sahihi kupitia kitabu hiki. How to win friends and influence people

JINSI YA KUPATA MARAFIKI NA KUSHAWISHI WATU



DALE CARNEGIE





Muandishi: Dale Carnegie, 1936.
Mtafsiri: Pictus Publishers ltd
Email: pictuspublishers@gmail.com.
whatsapp 0715278384
©Pictus Publishers ltd2022.
Haki zote zimehifadhiwa. Hakuna sehemu yoyote ya tafsiri hii inayoweza kunakiliwa, kutolewa kivuli, kuhamishwa, kurekodiwa au kutolewa kwa namna yeyote bila ya taarifa ya awali ya kimaandishi ya mtafsiri.

SEHEMU YA KWANZA

KANUNI ZA MSINGI ZA JINSI YA KUSHUGHULIKA NA WATU





KAMA UKITAKA KURINA ASALI USIPIGE TEKE MZINGA

Tarehe 7 mwezi wa tano mwaka 1931 kulikuwa na msako wa aina yake wa mhalifu ambao New York halijawahi kushuhudia. Baada ya msako wa wiki kadhaa, mhalifu aliyejulikana kama Crowley “Bunduki mbili”, muuaji na jambazi wa kutumia silaha ambaye hakutumia wala kuvuta kilevi chochote alikuwa amepatikana. Alikuwa amezingirwa katika makazi ya mpenzi wake katika mtaa wa West End.

Polisi mia moja na hamsini walizingira maficho yake yaliyokuwa kwenye ghorofa ya juu kabisa. Walikuwa wametoboa matundu kwenye paa. Walikuwa wanajaribu kumtoa Crowley “Muua polisi” kwa kutumia gesi ya kutoa machozi. Walitega bunduki katika majengo yanayozunguka. Kwa zaidi ya saa nzima, eneo tulivu la jiji la New York lilirindima kwa milio ya bastola na bunduki za rasharasha. Crowley alijificha nyuma ya sofa na kuwarushia polisi risasi mfululizo. Watu elfu kumi walikuwepo kushuhudia mapambano hayo. Kitu kama kile hakijawahi kutokea katika jiji la New York.

Crowley alipokamatwa, kamishna wa polisi, E. P. Mulrooney alikiri kuwa jambazi Crowley “Bunduki mbili’ ni moja ya wahalifu hatari zaidi kuwahi kutokea katika historia ya jiji la New York. “Huyu haoni taabu kuua,” alisema kamishna.



Lakini Crowley “Bunduki mbili” alikuwa na maoni gani kujihusu? Tunafahamu maoni yake kwa sababu wakati polisi wanarusha risasi kwenye makazi yake, yeye aliandika barua kwa “Yeyote atayejali.” Wakati anaandika barua hiyo, damu kutoka kwenye majeraha yake iliacha alama katika karatasi. Kwenye barua hiyo Crowley alisema: “Katika kifua changu mna moyo uliopondeka lakini wenye rehema, moyo usioweza kumdhuru yeyote.”

Kabla ya tukio hili Crowley alikuwa anafurahia maisha na mpenzi wake katika barabara moja huko Long Island. Ghafla polisi aliwafuata kwenye gari na kusema: “Naomba kuona leseni yako.” Bila kujibu kitu, Crowley alitoa bunduki na kummiminia mvua ya risasi. Polisi yule alipokuwa anakufa, Crowley alitoka ndani ya gari na kuchukua bastola ya polisi na kuumiminia risasi mwili uliokuwa umelala chini, huyo ndiye muuaji aliyesema: “Moyo wangu umepondeka lakini ni wenye rehema, hauwezi kumdhuru yeyote.”

Crowley alihukumiwa kifo kwa kiti cha umeme, alipokuwa anaingia kwenye gereza la wafungwa wanaosubiria kifo alisema, “Je hiki ndicho malipo ya kuua watu? Hapana, haya ni malipo ya mimi kujilinda.”

Lengo la hadithi hii ni kuonyesha kuwa: Crowley “Bunduki mbili” hakuona kama ana kosa lolote.

Je hilo ni jambo lisilo la kawaida kwa wahalifu? Kama unafikiri si la kawaida sikiliza haya:

“Nimetumia miaka yangu kuwapa watu furaha, na kuwasaidia kuwa na maisha mazuri na malipo niliyopata ni uonevu.Kuishi kama digididi.”

Hayo yalikuwa ni maneno ya Alcapone. Muhalifu hatari kabisa Marekani. Kiongozi wa genge la uhalifu hatari kabisa kuwahi kutokea katika jiji la Chicago. Capone hakujilaumu, badala yake alijiona ni mtu anayesaidia jamii. Msaidia jamii asiyeeleweka na asiyethaminiwa inavyostahili.

Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa Dutch Schultz kabla ya kuuwawa na mwanachama wa genge la uhalifu huko Newark. Mtu mmoja alisema katika mahojiano kuwa Dutch Schultz alikuwa ni mtu anayesaidia jamii na aliamini hivyo.

Nimewahi kuzungumza kuhusiana na hili suala na Lewis Lawes ambaye alikuwa ni mkuu wa gereza maarufu huko New York la Sing Sing kwa miaka mingi, alikiri kuwa ni “Wahalifu wachache sana wanajiona kuwa ni watu wabaya. Wanajiona ni watu wa kawaida kama mimi na wewe tu. Wanajiona kuwa wana sababu za msingi za kufanya wanayoyafanya. Wanaweza wakakuambia ni kwanini wanavunja sanduku la pesa, au kwanini ni wepesi kufyatua risasi. Wengi wao hujitahidi kutafuta sababu za uwongo na kweli kutetea uovu wao. Hata wakijaribu kujiaminisha wao wenyewe kuwa hawana hatia. Hupaza sauti wakisema hawakustahili kufungwa.

Iwapo Al Capone, Crowley “Bunduki Mbili,” Dutch Schultz na wanaume na wanawake wengine waliojaa magerezani hawajilaumu kwa chochote, vipi kuhusu watu ambao mimi na wewe tunakutana nao?

Muanzilishi wa maduka ya Wanamaker, John Wanamaker aliwahi kiri hivi: “Nilijifunza miaka thelathini iliyopita kuwa ni ujinga kushutumu. Ninapata ugumu wa kutosha katika kukabiliana na mapungufu yangu, siwezi anza kuhangaika na ukweli kuwa Mungu aliamua kutogawa akili kwa usawa.”

Wanamaker alijifunza jambo hilo mapema sana, lakini mimi imenichukua kufanya makosa kwa theluthi ya karne kabla sijaanza kuelewa kuwa kati ya mia moja, mara tisini na tisa, watu huwa hawajishutumu kwa chochote. Haijalishi ni kibaya kiasi gani. Kushutumu hakusaidii lolote, na zaidi zaidi kunamfanya mtu ajitahidi kujitetea. Shutuma ni hatari kwa sababu zinaharibu heshima ya mtu, inampunguzia kujithamini na huleta chuki.

Mwanasaikolojia maarufu, B. F, Skinner alithibitisha kupitia majaribio aliyoyafanya kuwa, mnyama anayezawadiwa kwa kuwa na tabia njema hujifunza haraka, na hukumbuka vizuri kile alichojifunza kuliko mnyama anayeadhibiwa kwa kuwa na tabia mbaya. Tafiti zilizofuatia zilionyesha kuwa hata kwa binadamu iko hivyo. Kwa kushutumu hatuleti mabadiliko ya kudumu, na mara nyingi tunaishia tu kujenga chuki.

Mwanasaikolojia mwingine maarufu, Hans Selye alisema, “Kama ambavyo tunapenda kukubalika, ndivyo tunavyochukia kushutumiwa.”

Chuki inayoletwa na na shutuma, inaweza athiri ari ya wafanyakazi, washiriki wa familia na marafiki, na bado ikawa haijarekebisha jambo au hali ya mambo iliyosababisha shutuma.

George B Johnston kutoka Enid Oklahoma ni msimamizi wa masuala ya usalama katika kampuni ya uhandisi. Moja ya majukumu yake ni kuhakikisha wafanyakazi wanavaa kofia ngumu kila wanapokuwa kazini.Alisema kuwa, kila alipokuwa anakutana na mfanyakazi ambaye hajavaa kofia ngumu, alikuwa akimwambia kama mtu mwenye mamlaka kuhusu sheria ya kuvaa kofi na kuwa anapaswa aifuate. Matokeo yake ni kuwa walimkubalia kwa shingo upande, na mara tu alipotoka wafanyakazi walivua kofia zao.

Akaamua kutumia mbinu nyingine. Alipokutana tena na wafanyakazi ambao hawajavaa kofia zao, aliwauliza iwapo kofia zinawatinga au haziwatoshi vizuri. Kisha kwa kauli nzuri aliwakumbusha kuwa kofia zimetengenezwa kwa namna itakayowalinda na madhara, na kushauri kuwa zivaliwe mara zote wawapo kazini. Matokeo yake ni kuwa watu wakaongeza uvaaji wa kofia bila kinyongo wala kujihisi vibaya.

Katika historia unaweza kuona mifano mingi ya jinsi ambavyokushutumu kusivyo na faida. Chukulia mfano wa ugomvi wa Theodore Roosevelt na Rais Taft, ugomvi ambao ulikigawa chama cha Republican, ukasababisha Woodrow Wilson kuwa Rais na kubadili historia. Hebu acha tuuchunguze vizuri mfano huo. Punde tu baada ya Theodore Roosevelt kuachia urais mwaka 1908, akaanza kumuunga mkono Taft ambaye alichaguliwa kuwa Rais. Baada ya hapo Theodore Roosevelt akafunga safari kwenda Africa kutalii na kuwinda. Aliporudi aliwaka kwa hasira, akatangaza kutomuunga mkono Taft kwa sababu ya uhafidhina wake, na akajaribu kuingia madarakani kwa muhula wa tatu na akaunda chama kilichoitwa Bull Moose, hilo halikusaidia kitu zaidi ya kukidhoofisha chama cha Republican. Katika uchaguzi uliofuata, William Howard Taft na chama cha Republican walishinda katika majimbo mawili tu, Vermont na Utah. Chama hakijawahi shindwa namna hiyo. Theodore Roosevelt alimlaumu Taft. Lakini je, Rais Taft alijilaumu mwenyewe? Hapana hata kidogo, kwa machozi Taft alisema: “Sioni kama kulikuwa na namna bora ya kufanya mambo zaidi ya nilivyofanya.”

Ni nani wa kulaumiwa? Roosevelt au Taft? Kwa kweli sijui na sijali. Jambo ninalotaka kueleza na kuwa, shutuma zote za Theodore Roosevelt hazikuweza kumuaminisha Taft kuwa alikosea. Badala yake zilimfanya Taft ajitahidi kujitetea hadi kwa machozi akisema: “Sioni kama kulikuwa na namna bora ya kufanya mambo zaidi ya nilivyofanya.”

Au fikiria juu ya kashfa ya Teapot Dome. Kashfa iliyopamba magazeti mwanzoni mwa miaka ya 1920. Ilitingisha nchi. Na katika kumbukumbu za watu leo, jambo kama lile halijawahi kutokea ndani ya Marekani. Kashfa yenyewe ilikuwa namna hii: Waziri wa mambo ya ndani wa Marekani katika baraza la rais Harding, bwana Albert B. Fall alipewa jukumu la kukodisha visima vya mafuta vya serikali huko Elk Hill na Teapot Dome ambavyo viliwekwa kwa ajili ya matumizi ya baadaye ya jeshi la majini. Je Fall aliruhusu mnada kufanyika? Hapana. Alimpatia mkataba huo mnono rafiki yake aliyeitwa Edward L. Doheny. Na Doheny alifanya nini? Alimpatia Fall “mkopo” wa dollar laki moja. Na kwa kutumia madaraka vibaya, Fall akaagiza kikosi cha jeshi la Marekani kuwaondoa wachimbaji wengine wa karibu ambao visima vyao vilikuwa vikinyonya mafuta kutoka ukanda wa Elk Hill. Wachimbaji hawa baada ya kufukuzwa kwa mtutu wa bunduki na singe wakaamua kwenda mahakamani na kufumua kashfa ya Tea Dome. Kashfa yenye harufu mbaya sana kiasi cha kuharibu uongozi wa Rais Harding na kuitia kichefuchefu nchi nzima. Ilisababisha Albert B. Fall kufungwa, na ilitishia kusambaratisha chama cha Republican.

Fall alishutumiwa vikali sana, ni watu wachache sana wamewahi shutumiwa namna ile. Je alitubu? Hata kidogo! Miaka kadhaa baadaye Herbert Hoover alisema hadharani kuwa Rais Harding alikufa sababu ya matatizo ya kiakili yaliyosababishwa na kusalitiwa na rafiki. Mke wa Fall aliposikia jambo hili aliruka kitini, alilia, alijipigapiga na kusema kwa hasira: “Nini! Harding alisalitiwa na Fall? Hapana! mume wangu hajawahi msaliti yeyote. Nyumba iliyojaa dhahabu isingeweza mshawishi mume wangu kutenda ndivyo sivyo. Yeye ndiye aliyesalitiwa na kutolewa kafara.”

Basi hiyo ndiyo hulka ya binadamu, waliofanya makosa hulaumu kila mtu isipokuwa wao wenyewe. Sote tupo namna hiyo. Kwa hiyo, kama kesho tukitaka kumshutumu mtu, acha tuwakumbuke Al Capone, Crowley “Bunduki Mbili” na Albert Fall. Tuelewe kuwa kushutumu ni kama njiwa wa kufugwa. Siku zote hurudi nyumbani. Acha tuelewe kuwa mtu tunayeenda kumshutumu na kumsahihisha labda atajaribu kujitetea, na kutushutumu sisi badala yake: au kama ni mstaarabu kama Taft atasema: “Sioni kama kulikuwa na namna bora ya kufanya mambo zaidi ya nilivyofanya.”

Katika asubuhi ya tarehe 15 mwezi wa nne mwaka 1865 Abraham Lincoln alipokuwa karibu kufa kwenye makazi duni yaliyokuwa ng’ambo ya barabara kutoka ukumbi wa Ford ambako John Wilkes Booth alimpiga risasi. Lincoln akiwa amelala kwa ulalo kitandani kwa sababu mwili wake ulikuwa mrefu sana kutosha kitandani. Mchoro mbovu wa Rosa Bonheur, The Horse fair ukining’inia ukutani mbele ya kitanda na karabai ikitoa mwanga hafifu wa njano.

Lincoln alipokuwa hoi kitandani, waziri wa mambo ya vita , bwana Stanton alisema, “Hapa amelala kiongozi bora kabisa kuwahi kutokea duniani.”

Ni siri gani iliyomfanya Lincoln aweze kuchukuana na watu vizuri? Nimetumia miaka kumi nikisoma maisha ya Abraham Lincoln. Kwa miaka mitatu nilishughulika na kuandika kitabu kiitwacho Usiyoyajua kuhusu Lincoln. Nafikiri nimegusa maisha ya Lincoln kwa undani kadri inavyowezekana. Kwa upekee kabisa, nilijikita kusoma jinsi Lincoln alivyoshughulika na watu. Je alijihusisha na kushutumu? Ndiyo, alipokuwa kijana huko Pigeon creek Valley, Indiana, alijihusisha na sana na kushutumu watu, na siyo kushutumu tu, bali alikuwa akiandika barua na mashairi ya kuwadhihaki watu. Alitupa barua na mashairi hayo barabarani ambako alijua watu watazipata kirahisi. Moja ya barua hiyo ilisababisha kinyongo ambacho kilidumu maisha yote.

Hata baada ya Lincoln kuwa mwanasheria huko Springfield, Illinois, bado alikuwa na tabia ya kuwashambulia wapinzani wake kwa barua alizozichapisha katika magazeti. Lakini mtindo huu haukuwa na mwiho mzuri. Katika majira ya kupukutika ya mwaka 1842 alimshambulia kwa dhihaka mwanasiasa mmoja mkali na mwenye majivuno aliyeitwa James Shields. Alimshambulia kwa barua ya siri iliyochapishwa gazeti la Springfield journal, mji wote ulilipuka kwa vicheko kutokana na barua hiyo. Sababu Shields alikuwa ni mwenye majivuno, akawaka hasira kwa kudharauliwa. Akachunguza na kugundua aliyeandika barua ile, akamuendea Lincoln na kumwambia wapambane ana kwa ana. Lincoln alikuwa hataki kupambana, na alikuwa ni mpinzani wa mapambano kama hayo. Lakini pia haikuwezekana aepuke jambo hilo na kubaki na heshima yake. Aliambiwa achague silaha yake. Kwa sababu alikuwa na mikono mirefu alichagua panga lililotumika na jeshi la wapanda farasi, na akapata mafunzo ya kupigana kwa mapanga kutoka kwa mhitimu wa chuo cha jeshi cha West Point. Siku ya pambano, yeye na Shields wakakutanakwenye mchanga katika mto Mississipi, wakiwa wamejiandaa kupambana hadi kifo. Lakini mwishoni kabla ya pambano, wapambe wao waliingilia kati na kusimamisha pambano.

Hiyo ilikuwa ni hali tete kabisa kwa Lincoln kuwahi kujikuta katika maisha yake binafsi. Lakini alipata somo muhimu sana kuhusiana na kushughulika na watu. Hakuandika tena barua ya dhihaka, wala hakumdhiki yeyote tena. Na kuanzia wakati huo hakumshutumu mtu yeyote.

Wakati wa vita ya wenyewe kwa wenyewe, Lincoln alibadilisha majenerali wake walioongoza mara kwa mara. Na mara zote, majenerali wote—McClellan, Pope, Burnside, Hooker, Meade—Walivurunda vibaya na kumuacha Lincoln akihangaika asijue la kufanya. Nusu ya nchi iliwashutumu vikali majenerali hao kwa uzembe, lakini Lincoln, “Bila ubaya kwa yoyote, na kusaidia wote,” hakutoa shutuma. Moja ya nukuu alizozipenda sana, “Usihukumu nawe hutahukumiwa.”

Na hata mke wake na watu wengine walipowaongelea watu wa kusini kwa ubaya, Lincoln alijibu: “Msiwashutumu, hata sisi tungekuwa katika hali yao tungetenda kama wao.”

Pamoja na hayo, kama kuna mtu alikuwa na haki ya kurusha shutuma basi alikuwa ni Lincoln. Acha tuone mfano mmoja:

Pambano la Gettysburg lilipiganwa katika siku tatu za mwanzo za mwezi wa saba wa mwaka 1863. Katika usiku wa tarehe 4 ya mwezi huo, jenerali Lee, akiwa na jeshi lake lililoshindwa alianza kurudi kusini, mvua kubwa ilikuwa inanyesha. Alipofika kwenye mto Potomac, alikuta umefurika haupitiki, huku jeshi la muungano likiwa nyuma yake. Lee alikuwa amebanwa kwenye kona bila njia ya kutorokea. Lincoln aliona jambo hilo. Ilikuwa ni fursa adhimu ya kuteka jeshi la Lee na kukomesha vita mara moja. Kwa hiyo kwa matumaini makubwa ya ushindi, Lincoln alimuamuru Meade kutoitisha baraza la vita na badala yake amvamie Lee mara moja. Alimtuma mjumbe maalumu na aliyepeleka amri kwa Meade akimtaka avamie jeshi la Lee mara moja.

Lakini Jenerali Meade alifanya nini? Alifanya kinyume kabisa na alichoagizwa. Aliitisha baraza la vita, akikiuka amri ya Lincoln waziwazi. Alisita na kujizungushazungusha. Alituma ujumbe akitoa visingizio kibao. Alikuwa amekataa kutii amri waziwazi. Mwishowe maji yalipungua na Lee akavuka mto Potomac na jeshi lake na kutoroka.

Lincoln alikasirika sana, “Nini maana ya jambo hili?’” alipiga kelele akimwambia Robert, mtoto wake. “Mungu wangu! Nini maana ya jambo hili? Walikuwa wetu kabisa, tulihitaji tu kunyoosha mkono na kuwakamata, lakini hakuna ambacho ningefanya au kusema kulifanya jeshi livamie. Kwa hali aliyokuwa nayo Lee, jenerali yoyote angemshinda. Hata mimi mwenyewe ningekuwepo pale ningemtandika.”

Katika hali hiyo, Lincoln akaketi na kuandika barua kwenda kwa Meade. Na kumbuka kuwa wakati huo Lincoln alikuwa mhafidhina hasa, na alijizuia katika maneno yake. Kwa hiyo barua hii ya mwaka 1863 kutoka kwa Lincoln inaonyesha shutuma kali zaidi alizoweza kutoa.

Mpendwa Jenerali

Siamini kama huelewi hali mbaya aliyokuwa nayo Lee kabla ya kutoroka. Alikuwa kaingia mikononi mwetu. Na kumkamata, pamoja na ushindi tuliopata hivi karibuni, kungemaliza vita. Lakini kwa sababu hilo halikutokea, inaonekana vita hii itaendelea kwa muda mrefu sana. Kama hukuweza kumvamia Lee jumatatu iliyopita, sehemu yenye usalama. Utawezaje kumvamia huko kusini ya mto, sehemu ambayo unaweza kwenda na si zaidi ya theluthi mbili ya jeshi lako? Haiingii akilini kutarajia, na wala sitarajii kama utakuwa na manufaa ya maana. Fursa nzuri ya kufanya hivyo imekwishapita, na hilo jambo limenikoseha amani kabisa.

Unafikiri Meade alifanya nini baada ya kusoma barua hiyo?

Meade hakupata barua hiyo. Lincoln hakuituma. Ilipatikana katika nyaraka zake baada ya kifo chake.

Mimi nadhani-na huku ni kudhani tu- kuwa baada ya kuandika barua ile. Lincoln alitazama nje kupitia dirishani na kujisemea, “Ngoja kwanza, labda sitakiwi kuwa na haraka hivi. Ni rahisi kwa mimi kukaa hapa katika usalama wa ikulu kumuamuru Meade avamie: lakini kama ningekuwepo Gettysburg, na kama ningeona umwagaji wa damu kama alioona Meade wiki iliyopita, na kama masikio yangu yangekuwa yamechomwa na vilio vya majeruhi na wanaokufa, pengine hata mimi nisingekuwa na mshawasha wa kuvamia. Vyovyote vile, yaliyopita si ndwele. Kama nikituma barua hii, itatuliza hisia zangu, lakini itamfanya Meade ajaribu kujitetea. itamfanya anishutumu. Itafanya kuwe na kinyongo kati yetu na na kufanya iwe ngumu kumtumia kama kamanda, na pengine itamfanya ajiuzulu toka jeshini.”

Kama nilivyokwisha sema, Lincoln aliiweka barua hiyo pembeni, alikuwa amekwishajifunza kwa uchungu kuwa shutuma kali na kusuta karibu mara zote huwa na mwisho mbaya.

Theodore Roosevelt aliwahi kusema kuwa alipokuwa anakabiliwa na jambo tata wakati alipokuwa rais, alikuwa akikaa na kuangalia picha kubwa ya Lincoln iliyokuwa imeningi’nizwa juu ya meza ofisini kwake kisha akajiuliza, “Kama Lincoln angekuwa kwenye viatu vyangu angetendaje? Angetatua vipi tatizo hili?”

Wakati ujao tukishawishika kumsuta mtu, tutoe noti ya dola tano kutoka mfukoni na kuangalia picha ya Lincoln kwenye noti hiyo na tujiulize. “Kama tatizo hili lingemkuta Lincoln, angeshughulika nalo namna gani?”

Mark Twain alikuwa ni mtu wa kulipuka hasira mara kwa mara, aliandika barua zenye maneno makali yaliyoweza kubadilisha rangi ya karatasi. Kwa mfano; kuna kipindi alimuandikia mtu aliyemuudhi maneno haya: “Jambo linalokufaa ni kibali cha mazishi yako tu. Sema nami nitahakikisha unakipata.” Wakati mwingine aliandika hivi kwa mhariri baada ya mtu anayehakiki habari kujaribu kurekebisha baadhi ya maneno aliyoandika. Alisema: “Acha hiyo kazi kama nilivyoiandika, na mwambie huyo uliyempa kazi ya kuhakiki abaki na maoni yake katika matope ya ubongo wake uliooza.”

Barua hizi kali zilimfanya Mark Twain ajihisi vizuri. Zilimfanya atoe dukuduku lake, lakini barua hizo hazikuwa na madhara yoyote sababu mke wake alizitoa zisitumwe kwa siri.

Je, unamfahamu mtu yeyote ambaye ungependa kumrekebisha na kumfanya awe bora? Vema! Hilo ni jambo zuri na naliunga mkono. Lakini kwanini usianze na wewe mwenyewe. Kwa mtazamo wa kibinafsi kabisa, hilo ni jambo lenye faida zaidi kuliko kutaka kufanya wengine wawe bora, na pia ni salama zaidi. Mwanafalsafa wa China, Confucius aliwahi kusema: “Usilalamike juu ya theluji iliyo juu ya paa la jirani yako wakati njia ya kuingia ndani kwako ni chafu.”

Nilipokuwa kijana, nilipokuwa najitahidi sana kukubalika na watu niliandika barua ya kipumbavu kwenda kwa bwana Richard Harding Davi, mwandishi ambaye kuna wakati alikuwa mtu mkubwa katika fasihi ya Marekani. Nilikuwa naandaa makala kuhusu waandishi na nilimuomba bwana Davis anieleze kuhusu mbinu za kazi zake. Wiki chache zilizopita nilikuwa nimepokea barua kutoka kwa mtu fulani ambayo mwishoni ilikuwa imeandika, “Maneno ni yangu, lakini barua hii sijaiandika wala kuihariri.” nilistaajabu sana, nilihisi muandishi atakuwa ni mtu mkubwa, na mwenye majukumu mengi sana.

Mimi sikuwa na majukumu yoyote ya kunitinga lakini nilitaka kuonekana wa maana kwa Richard Harding Davis, hivyo mwisho wa barua yangu niliandika: “Maneno ni yangu, lakini barua sijaiandika wala kuihariri.”

Hakujishughulisha na kujibu barua yangu. Badala yake aliirudisha ile niliyoandika chini yake akiwa ameandika: “Tabia yako mbaya inazidiwa ubaya na tabia yako tu.” Ni kweli nilikuwa nimefanya kosa kubwa, na pengine nilistahili kukosolewa. Lakini kwa sababu nami ni binadamu nilichukia hilo. Nilichukia kiasi kwamba nilipopata habari ya kifo cha Richard Harding Davi miaka kumi iliyofuata, kwa aibu nikiri kuwa kitu kilikilichokuwepo kichwani mwangu ni jinsi alivyoniumiza.

Kama mimi na wewe kesho tunataka kutengeneza chuki itakayodumu miongo na miongo mpaka kifo, basi tujihusishe na ukosoaji wenye kuumiza. Haijalishi tunaamini kiasi gani kuwa ukosoaji huo ni muhimu.

Tunaposhughulika na watu inatakiwa tuelewe kuwa hatushughuliki na kiumbe anayeongozwa na mantiki, bali anayeongozwa na hisia, kiumbe aliyeharaka katika kunyanyapaa, anayechochewa na majivuno na kujikweza.

Shutuma kali zilimfanya Thomas Hardy, moja ya waandishi bora kabisa wa fasihi ya kiingereza, kuachana kabisa na kazi ya kundika riwaya. Shutuma zilimfanya Thomas Chatterrton, mshairi wa kiingereza kujiua.

Wakati angali kijana, Benjamin Franklin hakuwa na ujuzi wowote wa maana, lakini baadaye akawa mwanadiplomasia mzuri na mtu mwenye uelewa sana wa jinsi ya kushughulika na watu, hata akafanywa kuwa balozi wa Marekani nchini Ufaransa. Siri ya mafanikio ? Alisema: “Sitamuongelea yoyote kwa ubaya, na nitaongelea mema yote ninayoyafahamu ya watu wote.”

Mpumbavu yoyote anaweza kushutumu, kulaumu na kuhukumu—na wapumbavu wengi hufanya hivyo. Lakini inahitaji uungwana wa hali ya juu kujizuia, kuwa muelewa na mwenye kusamehe.

Caryle aliwahi kusema: “Mtu mkuu huonyesha ukuu wake kwa jinsi anavyowatendea watu wa chini.”

Rubani maarufu na mshiriki wa mara kwa mara wa maonyesho ya anga, Bob Hoover alikuwa anarudi nyumbani kwake huko Los Angeles kutoka katika maonyesho ya anga huko San Diego. Kama habari yake ilivyoandikwa kwenye jarida Flight Operations, ilisemwa alipokuwa kimo cha futi mia tatu angani, injini zote ziliacha kufanya kazi. Kwa utaalamu wake aliweza kuitua ndege lakini iliharibika vibaya, japo hakuna aliyejeruhiwa.

Jambo la kwanza alilofanya Hoover baada ya kutua ni kuchunguza mafuta ya ndege. Kama alivyokuwa amehisi, ndege yake yenye injini ya mapanga, ya zama za vita ya pili ya dunia ilikuwa imewekewa mafuta ya ndege zenye injini ya jet badala ya petrol.

Aliporudi uwanja wa ndege akaomba kuonana na fundi aliyehudumia ndege yake. Fundi mwenyewe alikuwa kijana mdogo tu. Alikuwa amefadhaishwa sana na kosa lake. Machozi yalikuwa yakimtoka Hoover alipokuwa akimfuata. Alikuwa amesababisha uharibifu wa ndege ya gharama sana. Na alikuwa karibu kusababisha vifo vya watu watatu. Unaweza hisi hasira aliyokuwa nayo Hoover. Unaweza kudhania maneno makali ambayo rubani huyu makini na aliyejivuna angetoa juu ya uzembe ule. Lakini Hoover hakumsema fundi huyu wala hata hakumshutumu. Badala yake aliweka mkono wake kwenye bega la fundi yule na kusema, “Kuonyesha kuwa nina hakika hutarudia kufanya hivi tena, nataka kesho uhudumie ndege yangu aina ya F-51.”

Mara nyingi wazazi hushawishika kuwashutumu watoto wao. Labda unategemea niseme, “Wasifanye hivyo.” Hapana hata kidogo. Nitachosema ni kuwa, “Kabla ya kuwashutumu, wasome moja kati ya makala ya maana sana kuwahi kuandikwa na wanahabari wa Marekani, ‘Baba husahau.’ ”

Kwa mara ya kwanza iliandikwa katika gazeti People’s home Journal. Tutaiandika tena hapa kwa ruhusa ya muandishi, kama ilivyofupishwa kwenye jarida la Reader’s Digest.

“Baba husahau’ ni moja ya makala zinazohamsha hisia kwa wasomaji wengi sana kiasi kwamba inachapishwa kila mwaka. Toka ilipochapishwa kwa mara ya kwanza. “Baba husahau” imeandikwa tena na tena, anasema muandishi wake, W. Livingston Larned, “Imeandikwa kwenye mamia ya majarida, vipeperushi na magazeti nchini kote. Pia imeandikwa na kufasiriwa katika lugha nyingi sana. Nimetoa ruhusa kwa maelfu waliotaka waliotaka kuisoma wakiwa kanisani, shuleni au kumbi za mihadhara. Imetangazwa katika vipindi mbalimbali. Na hata vijarida vya vyuo na shule za upili vimeitumia
naomba muendelezo
 
BABA HUSAHAU

W. Livingston Larned

Nisikilize mwana wangu: ninasema haya ukiwa umelala, kiganja kimoja kikiwa shavuni mwako na nywele zako zikiwa zimeng’ang’ania kwenye paji lako la uso. Nimeingia chumbani mwako peke yangu. Dakika chache zilizopita nilikuwa maktaba nikisoma gazeti. Wimbi la hisia likaniingia. Kwa kuhisi hatia, nikaja hapa pembeni ya kitanda chako.

Kuna mambo nilikuwa nikifikiria mwanangu: nimekuwa kauzu kwako. Nimekufokea unapokuwa akijiandaa kwenda shule. Sababu umejifuta tu kijuu juusoni kwa taulo. Nimekufokea kwa kutosafisha viatu vyako. Nimekupigia kelele unapotupa vitu vyako sakafuni.

Wakati wa kifungua kinywa nilikukosoa pia, ulimwaga vitu. Ulimeza chakula kwa sauti. Uliweka viwiko mezani. Ulijaza siagi kwenye mkate. Na ulipokuwa ukienda zako, nami nikielekea kituo cha garimoshi, uligeuka na kunipungia mkono na kusema, “Kwa heri baba!” Nami nilikasirika na kusema, “Simama kwa kunyooka!”

Kisha hayo yakajirudia tena jioni. Nilipokuwa nakuja nilikuona. Umepiga magoti ukicheza gololi. Suruali yako ilikuwa na matundu. Nilikudhalilisha mbele ya rafiki yako kwa kukuongoza kuingia ndani. Suruali ni gharama, kama ni wewe ungekua unanunua, ungekuwa makini nazo! Fikiria mwenyewe mwanagu, eti baba anaongea hayo!

Unakumbuka baadaye nilipokuwa nikisoma kwenye maktaba, jinsi ulivyokuja kwa uoga na macho yako yakionyesha kuna jambo linakutatiza? Nilipoacha kusoma na kukuangalia, nikiwa nimeudhika kwa kukatishwa, ulisita mlangoni. “Unataka nini?” Nilifoka.

Hukusema kitu, kwa hisia kali ulinikimbilia na kunikumbatia shingoni na kunibusu, mikono yako midogo ilinikumbatia kwa nguvu na hisia ambazo Mungu mwenyewe amezifanya zichanue ndani ya moyo wako. Hisia ambazo hata kupuuzwa hakuwezi kuzizima. Kisha ukawa umeondoka, ukipanda sauti ya kupanda kwako ngazi ikisikika.

Punde baada ya hapo gazeti lilinitoka mkononi, hofu kuu ilinijaa. Hii tabia imenifanya kuwa mtu wa aina gani? Tabia ya kutafuta makosa, tabia ya kushutumu—hiyo ndiyo zawadi yangu kwako kwa kuwa mwana wangu. Ni si kwamba sikupendi; ni sababu nilitarajia mambo mengi kutoka kwa kijana. Nilikupima kwa kutumia kipimo cha miaka yangu.

Ukweli ni kuwa kuna mengi ambayo ni mazuri katika tabia yako. Moyo wako japo mdogo, lakini ni mkuu kama machweo ya jua kwenye vilima. Hili lilionyeshwa na tendo lako la kunikimbilia, ukinibusu na kunitakia usiku mwema. Usiku wa leo sijali chochote mwanangu. Nimefika hapa pembeni ya kitanda chako, nimepiga magoti gizani, nikiwa nimejawa na aibu.

Ni ishara ya kujuta na kuomba msamaha; najua hutaelewa mambo haya iwapo nitakuambia ukiwa macho. Lakini kesho nitakuwa baba hasa. Nitakuwa rafiki yako, nitateseka utesekapo na kucheka uchekapo. Nitauma ulimi wangu iwapo maneno ya kukosa subira yatanijia. Nitaendelea kusema kama vile ni sala: “Bado ni mvulana tu—mvulana mdogo.”

Nina wasiwasi kuwa nilikua nikikuchukulia kama mwanaume, lakini ninapokuona sasa, ukiwa umejikunja kitandani kwako, natambua kwamba bado ni mtoto mdogo. Jana tu ulikuwa katika mikono ya mama yako, umelaza kichwa chako begani mwake. Nimetaka mengi, mengi kupita kiasi.

Badala ya kushutumu na kuhukumu watu, acha kwanza tujaribu kuwaelewa. Tuelewe kwanza kwanini wanafanya yale wanayofanya. Hilo ni jambo lenye faida na linavutia kuliko kushutumu; nalo huzaa huruma, kuvumiliana na rehema. “Kujua yote ni kusamehe yote.”

Kama Dr. Johnson alivyowahi kusema: “Mungu mwenyewe hamhukumu mtu mpaka mwisho wa maisha yake.”

Kwanini mimi na wewe tuhukumu wengine?



KANUNI YA 1

Usishutumu, usihukumu wala usilalamike.
 
BABA HUSAHAU

W. Livingston Larned

Nisikilize mwana wangu: ninasema haya ukiwa umelala, kiganja kimoja kikiwa shavuni mwako na nywele zako zikiwa zimeng’ang’ania kwenye paji lako la uso. Nimeingia chumbani mwako peke yangu. Dakika chache zilizopita nilikuwa maktaba nikisoma gazeti. Wimbi la hisia likaniingia. Kwa kuhisi hatia, nikaja hapa pembeni ya kitanda chako.

Kuna mambo nilikuwa nikifikiria mwanangu: nimekuwa kauzu kwako. Nimekufokea unapokuwa akijiandaa kwenda shule. Sababu umejifuta tu kijuu juusoni kwa taulo. Nimekufokea kwa kutosafisha viatu vyako. Nimekupigia kelele unapotupa vitu vyako sakafuni.

Wakati wa kifungua kinywa nilikukosoa pia, ulimwaga vitu. Ulimeza chakula kwa sauti. Uliweka viwiko mezani. Ulijaza siagi kwenye mkate. Na ulipokuwa ukienda zako, nami nikielekea kituo cha garimoshi, uligeuka na kunipungia mkono na kusema, “Kwa heri baba!” Nami nilikasirika na kusema, “Simama kwa kunyooka!”

Kisha hayo yakajirudia tena jioni. Nilipokuwa nakuja nilikuona. Umepiga magoti ukicheza gololi. Suruali yako ilikuwa na matundu. Nilikudhalilisha mbele ya rafiki yako kwa kukuongoza kuingia ndani. Suruali ni gharama, kama ni wewe ungekua unanunua, ungekuwa makini nazo! Fikiria mwenyewe mwanagu, eti baba anaongea hayo!

Unakumbuka baadaye nilipokuwa nikisoma kwenye maktaba, jinsi ulivyokuja kwa uoga na macho yako yakionyesha kuna jambo linakutatiza? Nilipoacha kusoma na kukuangalia, nikiwa nimeudhika kwa kukatishwa, ulisita mlangoni. “Unataka nini?” Nilifoka.

Hukusema kitu, kwa hisia kali ulinikimbilia na kunikumbatia shingoni na kunibusu, mikono yako midogo ilinikumbatia kwa nguvu na hisia ambazo Mungu mwenyewe amezifanya zichanue ndani ya moyo wako. Hisia ambazo hata kupuuzwa hakuwezi kuzizima. Kisha ukawa umeondoka, ukipanda sauti ya kupanda kwako ngazi ikisikika.

Punde baada ya hapo gazeti lilinitoka mkononi, hofu kuu ilinijaa. Hii tabia imenifanya kuwa mtu wa aina gani? Tabia ya kutafuta makosa, tabia ya kushutumu—hiyo ndiyo zawadi yangu kwako kwa kuwa mwana wangu. Ni si kwamba sikupendi; ni sababu nilitarajia mambo mengi kutoka kwa kijana. Nilikupima kwa kutumia kipimo cha miaka yangu.

Ukweli ni kuwa kuna mengi ambayo ni mazuri katika tabia yako. Moyo wako japo mdogo, lakini ni mkuu kama machweo ya jua kwenye vilima. Hili lilionyeshwa na tendo lako la kunikimbilia, ukinibusu na kunitakia usiku mwema. Usiku wa leo sijali chochote mwanangu. Nimefika hapa pembeni ya kitanda chako, nimepiga magoti gizani, nikiwa nimejawa na aibu.

Ni ishara ya kujuta na kuomba msamaha; najua hutaelewa mambo haya iwapo nitakuambia ukiwa macho. Lakini kesho nitakuwa baba hasa. Nitakuwa rafiki yako, nitateseka utesekapo na kucheka uchekapo. Nitauma ulimi wangu iwapo maneno ya kukosa subira yatanijia. Nitaendelea kusema kama vile ni sala: “Bado ni mvulana tu—mvulana mdogo.”

Nina wasiwasi kuwa nilikua nikikuchukulia kama mwanaume, lakini ninapokuona sasa, ukiwa umejikunja kitandani kwako, natambua kwamba bado ni mtoto mdogo. Jana tu ulikuwa katika mikono ya mama yako, umelaza kichwa chako begani mwake. Nimetaka mengi, mengi kupita kiasi.

Badala ya kushutumu na kuhukumu watu, acha kwanza tujaribu kuwaelewa. Tuelewe kwanza kwanini wanafanya yale wanayofanya. Hilo ni jambo lenye faida na linavutia kuliko kushutumu; nalo huzaa huruma, kuvumiliana na rehema. “Kujua yote ni kusamehe yote.”

Kama Dr. Johnson alivyowahi kusema: “Mungu mwenyewe hamhukumu mtu mpaka mwisho wa maisha yake.”

Kwanini mimi na wewe tuhukumu wengine?



KANUNI YA 1

Usishutumu, usihukumu wala usilalamike.
nasubiri muendelezo
 
Back
Top Bottom