trachomatis
JF-Expert Member
- Jun 7, 2011
- 3,758
- 736
Qouted in 2006....
Mimi nina umri wa miaka 34.
Malezi na makuzi yangu yalikuwa ya wazazi ambao kwa sasa wangeitwa "machekibobu". Yaani watu wa kujionyesha kwamba wana fedha,na hawana maisha ya shida..
Nami nilikua na kuishi maisha hayo.Nilikuwa mtu wa kujikweza sana.
Mwaka 2000 nilipata kazikwenye ofisi binafsi maeneo ya Vingunguti..(nilimaliza masomo chuo cha biashara).
Kazi yangu ilikuwa ya kawaida tu,kutumwa hapa na pale,kujaza fomu za hesabu za fedha,na mengine ya aina hiyo.
Nikiwa hapo kazini,nilikutana na msichana mmoja aliyekuwa anafanya kazi kampuni jirani na yetu. Nilikutana naye kwenye mgahawa maeneo hayohayo nilipoenda kupata mlo wa mchana.
Kwa kweli nilimpenda ghafla,lakini naye alionekana kunipenda pia! Tulijikuta tukiwa marafiki baada ya kuwa nimemwanza. Ilikuwa kuna kaugumu kumtongoza kwani alikuwa mzuri sana na alikuwa anamiliki gari aina ya RAV 4 ya milango mitayu. Ila alinikubalia kirahisi hadi nikashangaa.
Katika kujitambulisha,nilijipa ujiko wa ajabu sana! Mimi ni mtu wa Tanga,na baba yangu kidogo anajuana na waziri mmoja mkubwa sana serikalini. Sasa badala ya kusema ukweli kuhusu baba yangu,ambaye kwa maisha yake ya kichekibobu,alikuwa amechalala sana,nilimtaja waziri huyo kama baba.
Yule binti aliamini,na nyumbani kwao,bila shaka alitangaza amepata ampendaye ambaye baba yake ni mtu fulani. Siku hiyo binti alinialika nyumbani kwao kwa ajili ya chakula cha mchana.Ilikuwa Jumapili.
Nilijitahi sana kukodi gari la rafiki yangu kwa Tshs 40,000,ili wajue nina gari.
Unajua kilichotokea?nilipofika nyumbani kwao,nilimkuta mama yake na yule binti. Baba yake alikuwa amefariki zamani. Lakini pia nilimkuta mtu mwingine...! Jaribu kuotea alikuwa nani ................!!!!
Alikuwa ni baba yangu! Nilibabaika sana na kujiuliza maswali mengi bila majibu. Nilipigwa na butwaa kwa muda,na hata baba pia alishikwa na mshangao. Baada ya kumsalimu mama wa binti,nilimsalimu baba,na kumuuuliza,"uko huku?" baba alisema "nashangaa nawe waijua hii familia.
"Mama Lewis tulikuwa naye kazini zamani. Siku nyingi sijamtembelea,leo nimeamua kuja kumuona..."
Yule mama mkwe "mtarajiwa" aliuliza," kwani mnajuana....?"
Baba akajibu,"huyu ni mwanangu wa kwanza.."
Halafu palizuka kimya. Yule mama kwa ajili ya kuua soo,akanikaribisha. Lakini ghafla nilimwona yule binti,alikuwa amebadilika,hakuwa na furaha tena.
Tulikula katika hali ya undavaundava tu. Tulipomaliza kula,sikupoteza muda nikaamua kuaga,kwani nilijua binti na mama yake walikuwa wananisanifu sana. Yaani kutoka mtoto wa mkubwa hadi kuwa mtoto wa mzee aliyecheza na maisha siku za nyuma.
Mbaya zaidi,baba alikuwa amefika pale kuomba msaada! Niliaga na kumwacha baba akiendelea "kupiga virungu" vyake. Nilikuwa na hakika ya kuwa baba aloambiwa yote kwani aliponitembelea jioni kwangu,aliniambia nimejisanifu sana kujifanya mtoto wa waziri.
Je una haja ya kujua kama urafiki na binti uliendelea?
Mimi nina umri wa miaka 34.
Malezi na makuzi yangu yalikuwa ya wazazi ambao kwa sasa wangeitwa "machekibobu". Yaani watu wa kujionyesha kwamba wana fedha,na hawana maisha ya shida..
Nami nilikua na kuishi maisha hayo.Nilikuwa mtu wa kujikweza sana.
Mwaka 2000 nilipata kazikwenye ofisi binafsi maeneo ya Vingunguti..(nilimaliza masomo chuo cha biashara).
Kazi yangu ilikuwa ya kawaida tu,kutumwa hapa na pale,kujaza fomu za hesabu za fedha,na mengine ya aina hiyo.
Nikiwa hapo kazini,nilikutana na msichana mmoja aliyekuwa anafanya kazi kampuni jirani na yetu. Nilikutana naye kwenye mgahawa maeneo hayohayo nilipoenda kupata mlo wa mchana.
Kwa kweli nilimpenda ghafla,lakini naye alionekana kunipenda pia! Tulijikuta tukiwa marafiki baada ya kuwa nimemwanza. Ilikuwa kuna kaugumu kumtongoza kwani alikuwa mzuri sana na alikuwa anamiliki gari aina ya RAV 4 ya milango mitayu. Ila alinikubalia kirahisi hadi nikashangaa.
Katika kujitambulisha,nilijipa ujiko wa ajabu sana! Mimi ni mtu wa Tanga,na baba yangu kidogo anajuana na waziri mmoja mkubwa sana serikalini. Sasa badala ya kusema ukweli kuhusu baba yangu,ambaye kwa maisha yake ya kichekibobu,alikuwa amechalala sana,nilimtaja waziri huyo kama baba.
Yule binti aliamini,na nyumbani kwao,bila shaka alitangaza amepata ampendaye ambaye baba yake ni mtu fulani. Siku hiyo binti alinialika nyumbani kwao kwa ajili ya chakula cha mchana.Ilikuwa Jumapili.
Nilijitahi sana kukodi gari la rafiki yangu kwa Tshs 40,000,ili wajue nina gari.
Unajua kilichotokea?nilipofika nyumbani kwao,nilimkuta mama yake na yule binti. Baba yake alikuwa amefariki zamani. Lakini pia nilimkuta mtu mwingine...! Jaribu kuotea alikuwa nani ................!!!!
Alikuwa ni baba yangu! Nilibabaika sana na kujiuliza maswali mengi bila majibu. Nilipigwa na butwaa kwa muda,na hata baba pia alishikwa na mshangao. Baada ya kumsalimu mama wa binti,nilimsalimu baba,na kumuuuliza,"uko huku?" baba alisema "nashangaa nawe waijua hii familia.
"Mama Lewis tulikuwa naye kazini zamani. Siku nyingi sijamtembelea,leo nimeamua kuja kumuona..."
Yule mama mkwe "mtarajiwa" aliuliza," kwani mnajuana....?"
Baba akajibu,"huyu ni mwanangu wa kwanza.."
Halafu palizuka kimya. Yule mama kwa ajili ya kuua soo,akanikaribisha. Lakini ghafla nilimwona yule binti,alikuwa amebadilika,hakuwa na furaha tena.
Tulikula katika hali ya undavaundava tu. Tulipomaliza kula,sikupoteza muda nikaamua kuaga,kwani nilijua binti na mama yake walikuwa wananisanifu sana. Yaani kutoka mtoto wa mkubwa hadi kuwa mtoto wa mzee aliyecheza na maisha siku za nyuma.
Mbaya zaidi,baba alikuwa amefika pale kuomba msaada! Niliaga na kumwacha baba akiendelea "kupiga virungu" vyake. Nilikuwa na hakika ya kuwa baba aloambiwa yote kwani aliponitembelea jioni kwangu,aliniambia nimejisanifu sana kujifanya mtoto wa waziri.
Je una haja ya kujua kama urafiki na binti uliendelea?