mfianchi
Platinum Member
- Jul 1, 2009
- 11,867
- 8,271
Nimekuta ndio mazungumzo ya Jenerali Ulimwengu kwenye Sibuka FM kipindi cha crossfire ndio yanaishia,kwa hakika Jenerali Ulimwengu kweli ni Jenerali,katika mazungumzo yake kaelezea mengi kati ya hayo ni kuwa watu wanadai eti sasa ni wakati wa Kasi zaidi,Jenerali anauliza hiyo kasi ya kwenda wapi wakati tayari tumepoteza mwelekeo si ingekuwa bora tusimame kwanza tujiulize tunakoenda,pia kuhusu kuhamahama kwenye vyama vya siasa amesema yote hayo yanatokana na vyama kutokuwa na itikadi zaidi ya watu kuangalia mambo ya mshiko ,akazidi kusema afadhali hata klabu za Simba na Yanga ambazo wanachama wao ni waumini wa timu zao kiasi kwamba hakuna mwanachama kutoka kilabu hizo ambaye anaweza kuhama kutoka kilabu kimoja kwenda kingine,loh leo hakika Jenerali katoa darasa murua,nasubiri sehemu ya pili