Jenerali Ulimwengu atoa darasa Sibuka FM,adai Kasi zaidi yanini wakati umepotea

mfianchi

Platinum Member
Jul 1, 2009
11,867
8,271
Nimekuta ndio mazungumzo ya Jenerali Ulimwengu kwenye Sibuka FM kipindi cha crossfire ndio yanaishia,kwa hakika Jenerali Ulimwengu kweli ni Jenerali,katika mazungumzo yake kaelezea mengi kati ya hayo ni kuwa watu wanadai eti sasa ni wakati wa Kasi zaidi,Jenerali anauliza hiyo kasi ya kwenda wapi wakati tayari tumepoteza mwelekeo si ingekuwa bora tusimame kwanza tujiulize tunakoenda,pia kuhusu kuhamahama kwenye vyama vya siasa amesema yote hayo yanatokana na vyama kutokuwa na itikadi zaidi ya watu kuangalia mambo ya mshiko ,akazidi kusema afadhali hata klabu za Simba na Yanga ambazo wanachama wao ni waumini wa timu zao kiasi kwamba hakuna mwanachama kutoka kilabu hizo ambaye anaweza kuhama kutoka kilabu kimoja kwenda kingine,loh leo hakika Jenerali katoa darasa murua,nasubiri sehemu ya pili
 
Nimekuta ndio mazungumzo ya Jenerali Ulimwengu kwenye Sibuka FM kipindi cha crossfire ndio yanaishia,kwa hakika Jenerali Ulimwengu kweli ni Jenerali,katika mazungumzo yake kaelezea mengi kati ya hayo ni kuwa watu wanadai eti sasa ni wakati wa Kasi zaidi,Jenerali anauliza hiyo kasi ya kwenda wapi wakati tayari tumepoteza mwelekeo si ingekuwa bora tusimame kwanza tujiulize tunakoenda,pia kuhusu kuhamahama kwenye vyama vya siasa amesema yote hayo yanatokana na vyama kutokuwa na itikadi zaidi ya watu kuangalia mambo ya mshiko ,akazidi kusema afadhali hata klabu za Simba na Yanga ambazo wanachama wao ni waumini wa timu zao kiasi kwamba hakuna mwanachama kutoka kilabu hizo ambaye anaweza kuhama kutoka kilabu kimoja kwenda kingine,loh leo hakika Jenerali katoa darasa murua,nasubiri sehemu ya pili

Kwenye red: Angetaja pia dini -- ni kama ushabiki wa vyama tu, kwani watu hubadili dini zao.
 
Ni kweli serikali ya Jk imepoteza mwelekeo na kama watataka kasi zaidi katika error waliyo nayo tayari basi Tz kama taifa tutegemee kupata ma-expert hapo baadae kutu opoa ICU ya uchumi, kijamii na kimaadili. Kwa habari ya kuhama vyama, japokuwa kweli kuna cheche za utafutaji wa masilahi binafsi(mshiko) kuliko maslahi ya umma wa wananchi, hatuna budi pia kukubali ukweli huu kwamba siasa ni game of chance(optimistic). Sii dini hii useme kwamba mtu kubadili moja kwenda nyingine atahesabiwa kukufuru. Hata hivyo kuna wanaosema potelea mbali niitwe muasi ikiwa ya kwamba kuasi kwangu kumelenga kumuasi binadamu na wala sio Mungu.
 
Back
Top Bottom