Mkipeleka nchi kizamu hivyo tutaharibu hahaa soon utasikia kaskazini watasema ni zamu yao na wao kuongoza nchi
Nao wa magharibi watibuka na kusema na sisi pia.
Mkitoka humu watakuja kwenye dini nao wakristo watasema ni zamu yao na waislamu watasema ni zamu yao.
Kwenye wakristo kitaubuka wa anaglikan watasema ni zamu mbona mnawapendelea sana wakatoliki.
Cha msingi ni kutafuta mtu makini haijalishi anatoka upande kwa hali ya nchi ya sasa we ned a strong leader kwa kwel na mwenye kufanya maamuz aliye tayar kukubali serikali yake ijifunge mikanda ikate cost zote za kijingA huyo ndo tunamuhitaji
Awe muislamu sijui mkristo sijui mpagan sijui katoka zenji sijui katoka kaskazin kitu kimoja ajue majukumu yake kwamba sisi ndo tuliye mwajili
acha ujanja,tuko kwenye muungano wa nchi mbili,hatuwezi kutawala pekeetu kila siku,lazima tuwe fair,zanzibar ni nchi wala huwezi kufananisha na arusha au mbeya ile ni nchi ndio maana haina mkuu wa mkoa ina rais na bendera,acheni hizo dharau na kejeli kwa wazanzibari ndio na wao kina jussa wanatutukana then tunakasirika...sisi tumeshatoa marais wawili wametuvumilia sasa inatosha,kuhusu material president sijaelewa jamaa alimaanisha nini,lakini wapo kina salim,yupo karume wawili kule mmoja kishakuwa mpaka rais huko atashindwa nini hapa?
Mawazo ya kijinga kabisa kutoka kwa anayejiita great thinker!
Hatutamchagua mtu kwa kuangalia alipotoka. Hatutamchagua mtu kwa kuangalia dini yake. Hatutamchagua mtu kwa kuangalia kabila lake. Ni upuuzi wa ccm kukimbia kivuli chake mambo yakishawawia magumu kwa hoja za kijinga kama hizi. Walipoona uchaguzi uvccm umewakamoto, wakaja na swala la sasa ni zamu ya z'bar. Wakaishia kumweka Masauni ambaye aliishia kufukuzwa kwa kudanganya umri. Ingawa ni makosa kisheria lakini akaachwa na kwenda kugombea ubunge kwao.
Angalia uchaguzi wa spika. Mafisadi walipomkataa Sitta, wakamtanguliza Chenge kuchafua hali ya hewa na kumtuma Makinda kuchukua form. Wakaleta hoja ya "zamu ya mwanamke" na chama kikaona hapo ndio pa kutokea. Angalia bunge lilivyo sasahivi. Upuuzi mtupu!
Sasa wamekuja na hoja ya "sasa ni zamu ya z'bar" kwenye urais baada ya kuona wanasigana na hakuna anayemwamini mwenzake. Wote wanaogopana. Wanaona bora aje wa mbali. Wameanza kuipigia debe hoja yao na kama kawaida wamewatuma vijana kwenye mitandao ya kijamii. Inasikitisha sana kuona na wewe umetumbukia humo!
Amka ndugu yangu. Usiendeshwe na propaganda za magamba. Chama chao kinaelekea kufa. Ni bora ujitoe mapema usije ukazama nao!
Alaska ni sehemu ya Marekani. Haijawahi kutoa rais wa Marekani. Tafakari!
Je Wazanzibar wana material candidate anayefaa kuwa rais wa URT?
Kwahiyo tuchague rais kwa kuwaonea wazanzibari huruma maana wao ni wachache? Sidhani kama hicho ni kigezo kizuri.
Pili, nadhani Watanzania wanao uhuru wa kuhamua kwamba wanamtaka Mzanzibari ama la. Kwa jinsi mnavyojadili, ni kama vile mgombea atakaepitishwa na CCM tayari yeye ni rais! Kama CCM wanataka kuweka Mzanzibari sawa, waweke. Watanzania kama hawamtaki si watachagua mtu kutoka chama kingine?
Leo naona mzee umewaamkia jamaa zetu wa unguja naona umeamua kuja na nyingine kuonyesha msisitizo...basi bwana inatosha,itoshe tu tukubali this time na wao angalau watoe rais then baadae kiti kitarudi tena huku mbona easy tu!