Je, ulifika Third floor(30s) bila kuwa na familia? Hali ilikuwaje?

πŸ˜πŸ˜‚
FB_IMG_17093694342786619.jpg
 
Kuna kitu nahitaji kuwafunza mabinti ambao hawajafika 30.

Ukipata mpenzi ukamuona ana hofu ya Mungu, maisha yake yapo wazi hasa tabia zake, anakupenda kwa dhati, yupo tayari kukutambulisha kwa ndugu zake na kwa familia yake.

Yamkini asiwe na kipato kikubwa sana ila ana uwezo wa kufanya wote mle na mkalala, ISHI HAPO.

Acha tamaa za kutaka uolewe na mwanaume mwenye pesa, anayefanya kazi TRA, bandari, mfanyabiashara mkubwa, mwenye muonekano fulani n.k mwisho mtakuja kuangukia kwa wanaume za watu au kwa wanaume ambao wataishia kukuchezea. Kumbuka sehemu kubwa ya mwanaume mwenye pesa, ngono anachukulia starehe tu, kwahiyo atakuchukua na kukutumia baada ya kukutamani akijua anapiga na kupita zake.

Binti yangu, huyo mwanaume wa mtu unayemuona ana pesa, hazijaja tu hivi hivi, alianza chini kabisa kama huyo kijana ambae kwa sasa wewe unamdharau.

Kama umewahi kumnyanyasa kijana wa watu kisa masikini, yeye sijui hana umbo zuri n.k moyo wake ukaumia, katafute suluhu naye sababu huenda kuna mambo yako yakafunguka.

Mabinti sio kwamba mnakosa watu wa kuwaoa ila tamaa za maisha zimekuwa zikiwatesa wengi, (kumbuka Hawa alidanganywa kwa kutamani pale bustani ya edeni, mwanamke ukiishinda tamaa una sehemu kubwa sana ya kuishi maisha ya furaha duniani). Mnapenda smartphones, kila wiki msuke, utolewe out n.k mnaishi maisha ya udangaji kisa mna uzuri wa sura au mna matako makubwa, kwa bahati mbaya sana, ukishazoea kudanga, mwanaume yeyote atakujua tu, udangaji ni kama ngozi, HAIJIFICHI na hata ukijitahidi, mtu atasikia tu stori zako.

Sasa hivi kijana wa 30, 31, 32 ambapo kwa sehemu kubwa ndo vijana wengi walau kwa sehemu wanaanza kuona mwanga ktk eneo la uchumi hawezi kuwa na mwanamke wa 30, lazima atafute wa 24, 25 au 26 unless awe mpumbavu.

Girls kuweni makini sana na umri, uliowatupa kisa hawana ela, wakipata ela na wao watakuona wewe sio hadhi yao. Tafuta kijana mwezio mtakaopendana, mtie moyo ktk utafutaji, mpende sana na kumpa heshima hata pale ambapo anapungukiwa, mwanaume huyo hatokusahau.
Mkuu umeongea vizuri sana, yamkini binti unahangaika kwasababu kuna kijana honest uliwahi kumnyanyasa kisa hana pesa. Karma is real, vile vile mnavyosemaga machozi ya mwanamke hayaendi bure the same happens with vijana, ni vile tu hua tunalilia ndani ya mioyo yetu. Lkn trust me vijana wengi waaminifu wametendwa na Mungu hua anaingilia kati. Mtafute myajenge, ao omba Mungu akusamehe

Lakini kitu kingine ni nguvu ya maneno yako mwenyewe. Kuna baadhi ya mabinti hupenda kutumia viapo bila kujua madhara yake baadae. Mfano unatongozwa na mtu halafu unamjibu "over my dead body siwezi kua na mtu kama ww" ,
"Siwezi mkubalia labda nikiwa kaburini" na mengine yanayofanana na hayo. Yamkini hukua na maana hio 100% ila as long as ulitamka they will haunt you in a way, na utakuta wakati unahitaji hata mwanaume uliekua unamchukulia poa nae humpati..

Maisha yanakua a series of misery, unakimbilia kwa manabii fake mwisho wa siku unakua dame wa manabii.
 
Habari ya weekend great thinkers?

Maisha yananipa experience tofauti, Sikuwahi kufikiria kama ningefika third floor bila kuwa na familia wala watoto, kuna muda nahisi kupanic nahofia watoto wasije kuniita bibi badala ya mama, au kukosa kabisa sababu ya umri mkubwaπŸ€”

Enzi hizo nilikua nashangaa mtu hasa mdada unafikaje hadi 30s huna familia, aisee kumbe ni kweli now ni mimi mwenyewe.

Mlioanza familia mkiwa 30s je ni kweli au mnaona dalili za watoto wenu kuwaita bibi au babu? Vipi changamoto za uzazi sababu ya umri mkubwa?πŸ˜”

Nipo tayari kwa comments zote.

Happy valentine's day in advance πŸ‘πŸ₯°
No comment
 
Back
Top Bottom