Je,Pete ya ndoa,....?Kwa walio oa na kuolewa.

Siku hizi kuna watu wanaangalia vidoleni tuu,wakikuta pete lazima utongozwe,hii inasababishwa na watu kuchoka usumbufu,wakiwa na imani kuwa wakimfuata mtu aliye kwenye ndoa,hatopata usumbufu wa kufuatiliwa wala mizinga ya kijinga jinga,hapo ni penzi tuu!!

eh! Nimeangalia vibaya au? kuna penzi la kinamna gani apo?
 
Pete ya ndoa haibadilishi tabia ya mtu! Ni kiashiria kwamba huyu mtu ameoa/olewa hasa kwa utamaduni wa kimangaribi...kuna wenzetu ambao nadhani wao kuvaa pete sio lazima....na actually sidhani kama ni lazima kuvaa pete ya ndoa kuthibitisha mapenzi yako kwa mkeo/mumeo


kinachotokea sasa hivi kama walivosema wengine, ni tabia ya baadhi ya watu siku hizi kupenda kuiba na kuendelea kuonekana wako single....hasa akina dada ambao utawakuta wapo mjini, wanamaisha ya juu, usafiri, nyumba nzuri ya kuishi na pesa lakini ukimuuliza kazi gani hasa anafanya huwezi pata jibu..mara afisa uhusiano wa kikampuni uchwara, mara secretary etc....akina dada wa hivi unakuta wanatunzwa na ATM za walio kwenye ndoa....!

Ndo kanakuja kale kautaratibu ketu ka utambulisho,.....kwenye pombe tec.."huyu ni shemeji yenu" hata kama inajulikana ana mke halali wa ndoa.

kwa upande wa wanaume wanaokubali kuwa ATM, sababu ni nyingi na tumeshazijadili sana hapa,

All in all it boils down to an individual, tabia yake ikoje, haiwezi kamwe kubadilishwa kwa kuvaa pete ya ndoa....nikisema hivyo simaanishi watu mkazitupe mmliozivaa!

ZD na Chris mnavishana lini? tupeni progress mi na Mrs hapa tujiandae...
 
Mimi nafikiri pete za ndoa zina umuhimu wake katika kutunza ndoa. Ninaamini kabisa kuwa mnapovalishana pete ni ishara ya kukubali kumilikiana kuwa kila aliyeivaa pete ya mwenzie anakuwa mali ya mwenzie huyo peke yake. Sasa yanayojiri baada ya hapo ni ubazazi tu wa mvaaji.

Si ndio maana zinabarikiwa kwanza huko makanisani au?

By the way naomba mnijuze
Ukiolewa/oa unaruhusiwa kuibadili pete uliyovalishwa siku ya ndoa? meaning kama ulifunga ndoa na pete ya silver unataka kuchange kwenye gold kuna ubaya? Au ulivalishwa mpete mkuubwa unataka kuireplace na ndogo/nyembamba inaruhusiwa au?

kwa nini wataka kuvaa ndogo nyembaba MJ1?...:eek::rolleyes::D
 
All in all it boils down to an individual, tabia yake ikoje, haiwezi kamwe kubadilishwa kwa kuvaa pete ya ndoa....nikisema hivyo simaanishi watu mkazitupe mmliozivaa!

ZD na Chris mnavishana lini? tupeni progress mi na Mrs hapa tujiandae...


Hahaha mpwa bana! Usijali bestman, mtakapokuwa free na mrs wako tustueni. Wapwa wote watakaribishwa kwenye hiyo hafla maalum.
 
ni kweli pete ya ndoa haibadilishi tabia ya mtu
lakini pia siku hizi mabinti wanapenda waume za watu kwa sababu mbili
1;mume wa mtu hasumbui sana na hmbani sana binti;
2;mume wa mtu anaonesha jinsi alivyo na utayari wa kukabili majukumu kwahiyo sio rahisi kulala njaa,sijajua kama na vidume vinapenda wake za watu
 
kwa nini wataka kuvaa ndogo nyembaba MJ1?...:eek::rolleyes::D

Nilijua tu hapa lazima uta'sema'!!

Ni utashi tu wajua sie tunaishi kitaani vibaka wanatukodolea macho sasa mpete mkuuuubwa ukichelewa home usiku inabidi uivue uifutike kama unavyofutika simu ukipanda daladala (ila ole wako ukutwe umeivua lol)
 
Nilijua tu hapa lazima uta'sema'!!

Ni utashi tu wajua sie tunaishi kitaani vibaka wanatukodolea macho sasa mpete mkuuuubwa ukichelewa home usiku inabidi uivue uifutike kama unavyofutika simu ukipanda daladala (ila ole wako ukutwe umeivua lol)

Hahaha! Kuna siku nilii miss place ya kwangu, huo moto wake ilikuwa balaa. Sometimes hizi pete zinaweza kuvunja ndoa. Lol!
 
Chrispin kwa nini uliivua ???

Nilikuwa nahudumia kabustani ka tumigomba. Nikang'atwa na nge kidole kikavimba. Sasa nilipoivua sikumstua wife. Kesho yake asubuhi nilipotimka job si nikasahau kuivaa? Nikarudi mida imeenda kidogo na kaserengeti kamenoga kichwani. Si ndio msala ukazuka.
 
Nilijua tu hapa lazima uta'sema'!!

Ni utashi tu wajua sie tunaishi kitaani vibaka wanatukodolea macho sasa mpete mkuuuubwa ukichelewa home usiku inabidi uivue uifutike kama unavyofutika simu ukipanda daladala (ila ole wako ukutwe umeivua lol)

mmh.....:rolleyes:
 
Nilikuwa nahudumia kabustani ka tumigomba. Nikang'atwa na nge kidole kikavimba. Sasa nilipoivua sikumstua wife. Kesho yake asubuhi nilipotimka job si nikasahau kuivaa? Nikarudi mida imeenda kidogo na kaserengeti kamenoga kichwani. Si ndio msala ukazuka.

pole mwaya hope wife alikuelewa hahahahahahahah
 
pole mwaya hope wife alikuelewa hahahahahahahah

Alinielewa lakini baada ya msala mkubwa. Kilichookoa, kwenye upekuzi wa kuitafuta (tulikubaliana tuitafute hata ikibidi mpaka kukuche) aliipata yeye. Asingeipata nadhani mida hii ningekuwa single.
 
si umemsikia apo juu eti anaogopa 'vibaka' mtaani (sio kitaani)....hivi huwa hawapendi kubeba pochi nzima kuliko kuhangaika na kidole? lol

Hahaha! Bestman umeistukia hiyoe! We kichwa!
 
Alinielewa lakini baada ya msala mkubwa. Kilichookoa, kwenye upekuzi wa kuitafuta (tulikubaliana tuitafute hata ikibidi mpaka kukuche) aliipata yeye. Asingeipata nadhani mida hii ningekuwa single.

huyo ndo saizi yako hakuna kuleta janja ya nyani ....
 
si umemsikia apo juu eti anaogopa 'vibaka' mtaani (sio kitaani)....hivi huwa hawapendi kubeba pochi nzima kuliko kuhangaika na kidole? lol

Unachekesha weye lakini si kosa lako ni tatizo la kuishi matawi

We unadhani wanaridhika hao? utaambiwa vua na hiyo haraka huku ukil avikofi vya ubapa wa panga ah!
 
Nilikuwa nahudumia kabustani ka tumigomba. Nikang'atwa na nge kidole kikavimba. Sasa nilipoivua sikumstua wife. Kesho yake asubuhi nilipotimka job si nikasahau kuivaa? Nikarudi mida imeenda kidogo na kaserengeti kamenoga kichwani. Si ndio msala ukazuka.

Mhhh kwa hiyo ZD atakuwa spare tyre? au ndo mke wa pili?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom