Heart Wood.
JF-Expert Member
- Nov 16, 2014
- 887
- 932
Ukitembea tembea huko mitaani hasa vijijini, utawahurumia sana wananchi wenzetu wanavyoishi kwenye hali duni kabisa kimaisha. Naam, namaanisha uduni wa kukosa huduma za msingi kama vile barabara nzuri, maji safi na salama, elimu bora, matibabu bora, mawasiliano ya uhakika, huduma za nishati n.k.
Natambua kuwa hii nchi yetu bado ni maskini sana ukilinganisha na nchi nyingine zilizoendelea na vilevile kwa kuzingatia viwango vilivyopo vya hali ya maisha ulimwenguni kupitia taasisi za kimataifa kama vile World Bank, IMF n.k. Hata hivyo, nashawishika kusema kuwa waTanzania hawastahili umaskini huu.
Ukiangalia maisha ya anasa wanayoishi viongozi walio wengi, ukatazama na maisha ya watu wa kawaida hasa vijijini, unaweza sema viongozi wetu wanaongoza watu wa nchi nyingine na si hii tuliyonayo hapa Bongo. Ukimleta mgeni atazame viongozi wetu jinsi walivyonona kutokana na utamu wa pesa za wavuja jasho, kisha awatazame na wananchi wa vijijini, atakataa kabisa kuwa hawa viongozi hawatoki kwenye jamii yetu.
Anyway, msingi wa hoja yangu si hali ya umaskini tuliyonayo hapa nyumbani (hali inayotokana na uzembe tu), ila ni namna ambavyo Serikali inashughulika na pesa za umma ambazo huzikusanya au kuzisimamia katika kuboresha maisha ya watu wake.
Ukitizama taarifa za habari, hasahasa ktk ziara za Waziri Mkuu, hutaacha kusikia Waziri Mkuu akilalamika kuhusiana na matumizi ya ovyo na ufujaji wa pesa za umma mahala flani. Tena, nadhani huyu Waziri Mkuu yeye wakati mwingi huwa analalamika lalamika sana na kujaribu kuonesha anachukizwa na mambo ya ovyo yaliyofanyika kuhusiana na ufujaji wa pesa za miradi ya wananchi hasa maskini.
Hata hivyo, huwa anaishia kuagiza kuundwa kwa Tume flani kuchunguza jambo flani na akichukua hatua zaidi basi wahusika huwa wanasimamishwa kupisha uchunguzi na watu wachache sana huwa wanafikishwa mahakamani. Mathalan, watu wanaofikishwa mahakamani, kwa kiasi kikubwa (sio wote), huwa hutupati mrejesho wa hatua za mwisho zilizofanyika.
Kwa kuongezea, kila mwaka utasikia upigaji mkubwa sana kupitia report ya CAG kuhusiana na pesa za nchi hii pendwa yenye umaskini uliopitiliza. Sasa mie huwa najiuliza na kushangaa sana;
i) Ya kwamba, nchi yetu yenye vyombo mahiri kabisa, huwa inashindwa vipi kuzia huu upigaji mpaka kusubiriwa ziara za Waziri Mkuu au kiongozi mwingine wa juu?
ii) Ya kwamba, Serikali yetu sikivu, yenye viongozi mahiri kabisa, imekosa au imeshindwa kabisa kuja na ubunifu wa kuzuia ufujaji wa pesa hizi za umma za watu maskini ktk nchi hii? Ujue nchi yetu si kwamba inakuwa haina pesa za kuboresha huduma za kijamii, isipokuwa, kuna watu wachache tu ndio wanufaika wa hizi pesa huku walio wengi wakiendelea kuwa maskini na fukara.
iii) Ya kwamba, viongozi wetu wanaishia kulalamika tu majukwaani ila wameshindwa kuja na mwarobaini wa tatizo hili? Mbona mambo mengine huwa inaweza kuyafanya kwa ufasaha? Sitaki kuyataja nisije haribu ujumbe wa uzi huu....
Jamani, kwa akili ya kawaida, kama hizi pesa za miradi za wavuja jasho zimekosa mwarobaini wa kuzisimamia vizuri ili kuwasaidia watu maskini hasa vijijini, ni kwa nini sasa Serikali yetu isikiri kuwa tatizo hili limetushinda sisi waAfrika wa hapa nyumbani?
Kwamba tukubali kuwa upigaji ni jadi yetu sisi waAfrika, na kwamba, hata ufanyeje mtu mweusi huwezi kumtenganiusha na tamaa za pesa na ukosefu wa maadili ikiwemo ustaarabu wa kuheshimu mambo yetu wenyewe. Hivyo tuwaite wageni ambao wao watapewa jukumu la kusimamia miradi yote kwa makubaliano maalumu yaliyo ya wazi wakatumia mbinu kama wanavyofanikiwa huko makwao?
Au la,
Kama upigaji imeshindikana kudhibitiwa kwa mfumo huu wa sasa, ni kwanini wasichaguliwe watu wachache tu kitaifa, walio waaminifu sana, kisha wakapewa jukumu la kusimamia miradi yote nchini ambako pesa zake huishia kupigwa na watu wachache huku idadi kubwa ya waTanzania ikibakia kuwa maskini kwa kukosa huduma bora za kijamii?
Ngoja niishie hapa kwa sasa. Jumapili njema iwe nawe msomaji wa ujumbe huu!
Natambua kuwa hii nchi yetu bado ni maskini sana ukilinganisha na nchi nyingine zilizoendelea na vilevile kwa kuzingatia viwango vilivyopo vya hali ya maisha ulimwenguni kupitia taasisi za kimataifa kama vile World Bank, IMF n.k. Hata hivyo, nashawishika kusema kuwa waTanzania hawastahili umaskini huu.
Ukiangalia maisha ya anasa wanayoishi viongozi walio wengi, ukatazama na maisha ya watu wa kawaida hasa vijijini, unaweza sema viongozi wetu wanaongoza watu wa nchi nyingine na si hii tuliyonayo hapa Bongo. Ukimleta mgeni atazame viongozi wetu jinsi walivyonona kutokana na utamu wa pesa za wavuja jasho, kisha awatazame na wananchi wa vijijini, atakataa kabisa kuwa hawa viongozi hawatoki kwenye jamii yetu.
Anyway, msingi wa hoja yangu si hali ya umaskini tuliyonayo hapa nyumbani (hali inayotokana na uzembe tu), ila ni namna ambavyo Serikali inashughulika na pesa za umma ambazo huzikusanya au kuzisimamia katika kuboresha maisha ya watu wake.
Ukitizama taarifa za habari, hasahasa ktk ziara za Waziri Mkuu, hutaacha kusikia Waziri Mkuu akilalamika kuhusiana na matumizi ya ovyo na ufujaji wa pesa za umma mahala flani. Tena, nadhani huyu Waziri Mkuu yeye wakati mwingi huwa analalamika lalamika sana na kujaribu kuonesha anachukizwa na mambo ya ovyo yaliyofanyika kuhusiana na ufujaji wa pesa za miradi ya wananchi hasa maskini.
Hata hivyo, huwa anaishia kuagiza kuundwa kwa Tume flani kuchunguza jambo flani na akichukua hatua zaidi basi wahusika huwa wanasimamishwa kupisha uchunguzi na watu wachache sana huwa wanafikishwa mahakamani. Mathalan, watu wanaofikishwa mahakamani, kwa kiasi kikubwa (sio wote), huwa hutupati mrejesho wa hatua za mwisho zilizofanyika.
Kwa kuongezea, kila mwaka utasikia upigaji mkubwa sana kupitia report ya CAG kuhusiana na pesa za nchi hii pendwa yenye umaskini uliopitiliza. Sasa mie huwa najiuliza na kushangaa sana;
i) Ya kwamba, nchi yetu yenye vyombo mahiri kabisa, huwa inashindwa vipi kuzia huu upigaji mpaka kusubiriwa ziara za Waziri Mkuu au kiongozi mwingine wa juu?
ii) Ya kwamba, Serikali yetu sikivu, yenye viongozi mahiri kabisa, imekosa au imeshindwa kabisa kuja na ubunifu wa kuzuia ufujaji wa pesa hizi za umma za watu maskini ktk nchi hii? Ujue nchi yetu si kwamba inakuwa haina pesa za kuboresha huduma za kijamii, isipokuwa, kuna watu wachache tu ndio wanufaika wa hizi pesa huku walio wengi wakiendelea kuwa maskini na fukara.
iii) Ya kwamba, viongozi wetu wanaishia kulalamika tu majukwaani ila wameshindwa kuja na mwarobaini wa tatizo hili? Mbona mambo mengine huwa inaweza kuyafanya kwa ufasaha? Sitaki kuyataja nisije haribu ujumbe wa uzi huu....
Jamani, kwa akili ya kawaida, kama hizi pesa za miradi za wavuja jasho zimekosa mwarobaini wa kuzisimamia vizuri ili kuwasaidia watu maskini hasa vijijini, ni kwa nini sasa Serikali yetu isikiri kuwa tatizo hili limetushinda sisi waAfrika wa hapa nyumbani?
Kwamba tukubali kuwa upigaji ni jadi yetu sisi waAfrika, na kwamba, hata ufanyeje mtu mweusi huwezi kumtenganiusha na tamaa za pesa na ukosefu wa maadili ikiwemo ustaarabu wa kuheshimu mambo yetu wenyewe. Hivyo tuwaite wageni ambao wao watapewa jukumu la kusimamia miradi yote kwa makubaliano maalumu yaliyo ya wazi wakatumia mbinu kama wanavyofanikiwa huko makwao?
Au la,
Kama upigaji imeshindikana kudhibitiwa kwa mfumo huu wa sasa, ni kwanini wasichaguliwe watu wachache tu kitaifa, walio waaminifu sana, kisha wakapewa jukumu la kusimamia miradi yote nchini ambako pesa zake huishia kupigwa na watu wachache huku idadi kubwa ya waTanzania ikibakia kuwa maskini kwa kukosa huduma bora za kijamii?
Ngoja niishie hapa kwa sasa. Jumapili njema iwe nawe msomaji wa ujumbe huu!