Fafanua acha kujichekesha wakati mtu anahitaji msaada.Hapo gharama zake ni Kama kununua PASSO😂😂😂😂TANZANIA NI TANGANYIKA ILIYOIMEZA ZANZIBAR.
Sahau kulitumia hilo gari kwa usajiri wa Zanzibar huku bara lazima ukifika utaambiwa kubadili ila chaajabu mtanzania akienda na gari kutoka bara anatumia tu vizuri kule Zanzibar bila shida ndio
Hizi gari ambazo ziko hapa Dar zenye namba za Zanzibar inakuwaje?
Sahau kulitumia hilo gari kwa usajiri wa Zanzibar huku bara lazima ukifika utaambiwa kubadili ila chaajabu mtanzania akienda na gari kutoka bara anatumia tu vizuri kule Zanzibar bila shida ndio
Vibali vinapatikana vipi?
Inawezekana lakini utaratibu wake umekua mgumu kifogo siku za hivi karibuni.
Naomba nitoe maelezo kidogo, Zanzibar ni tofauti na Bara, ukiwa Zanzibar unaweza kulipia ushuru 30%, 40% au 50% na ukachukua gari yako bandarini ukaendelea na maisha, hivyo magari mengi yanadaiwa ushuru.
Bara ni nadra kama sio haiwezekani kuitoa gari bandarini bila kukamilisha malipo ya ushuru.
Hapo ndio changamoto inapoanzia, awali ilikua unaandika barua kuomba kutumia gari yako bara kwa miezi mitatu na ilikua unapewa kibali, ikaonekana wajanja wanatumia huo mwanya kupeleka magari bara wanafanya manuva, gari haiurudi, inapigwa juu kwa juu huko huko na kubadilishwa usajili.
Sasa hivi utaambiwa uache dhamana sawa na kiasi cha kodi inayodaiwa gari husika. Sasa kwa huo usumbufu si bora umalizie kodi iliyobaki ili hata ukivuka nalo hakuna mlolongo mrefu?
Ikiwa gari yako imelipiwa ushuru asilimia zote, haidaiwi, unaandika tu barua TRA/ ZRB kisha utamalizana na Agent na usafirishaji ambazo gharama zitategemea na ukubwa wa gari.
Nafikiri umepata mwanga kidogo mkuu.
Nimepiga simu tra bara kuulizia, na wao wameniambia, niende ZRB watanipa kibali then nakuja na gari Dar kwa miez mitatu