Elections 2010 Je; Mtanzania Limeshikishwa Adabu na CHADEMA?

Ila ipo kazi bado watanzania wengi kuelimika . . .

Asubuhi nilikuwa naongea na sister wangu moja na jirani yake, bado wanaamini CHADEMA ni watu wa vurugu na watavuruga amani. Nilipowadodosa hawana hoja ila tu wao wanaona bora CCM pamoja na kuwa wanajua nini Slaa kafanya.

Bado CHADEMA wanayo kazi ngumu ya kuwashawishi watu kama hawa waelewe.

Hii inawezekana kutokea kwa sababu hata wewe mwenyewe lugha uliyotumia kwenye heading yako ni kuonesha chadema kama cha vurugu.
 
kuhusu chadema kununua muda wa hewani, je wenye TV watakubali, maanake wote kama ccm vile
 
kuhusu chadema kununua muda wa hewani, je wenye TV watakubali, maanake wote kama ccm vile

So far, hawakubali.

Kuna sehemu nimesoma invisible kaandika kuwa Chanel 10 walikataa kuwauzia chadema air time kwa ajili ya uzinduzi wa kampeni.
 
Ila ipo kazi bado watanzania wengi kuelimika . . .

Asubuhi nilikuwa naongea na sister wangu moja na jirani yake, bado wanaamini CHADEMA ni watu wa vurugu na watavuruga amani. Nilipowadodosa hawana hoja ila tu wao wanaona bora CCM pamoja na kuwa wanajua nini Slaa kafanya.

Bado CHADEMA wanayo kazi ngumu ya kuwashawishi watu kama hawa waelewe.

mi nusu nimzibue makofi sister wangu eti anasema CHADEMA ikishinda tutalazimishwa kuvaa yale magwanda ya kaki..nimetamani kumzaba makofi
 
So far, hawakubali.

Kuna sehemu nimesoma invisible kaandika kuwa Chanel 10 walikataa kuwauzia chadema air time kwa ajili ya uzinduzi wa kampeni.

Inavyoelekea CHADEMA hawakujiandaa ipasavyo kwa upande wa utumiaji wa vyombo vya habari kwa kuanzisha vyombo vyao binafsi vya TV, Radio na magazeti ili visaidie katika kusaidia shughuli za kampeni zao. Halikadhalika, hawakujishushughulisha vya kutosha kuwahamasisha wana CHADEMA katika mitaa wanakosihi kuwania uongozi wa matawi katika ngazi za shina ili kuwashinda wajumbe wa nyumba kumi wa CCM.

Ili kuweza kuua nguvu ya wajumbe wa nyumba kumi kumi kwenya mashina/mitaa ilipaswa wanachama wa CHADEMA kwenye mitaa hiyo waukatae mfumo huo wa CCM na kutaka mfumo mbadala ambao unatoa fursa kwa vyama vyote kushiriki katika kugombania na kushinda nafasi za ujumbe wa shina.

Hata hivyo, kinachoweza kufanyika sasa ni wanachama wa CHADEMA mmoja mmoja kuongeza nguvu katika kuwashawishi wananchi wasio wanachama wa chama chochote kile na hata wale wa vyama vingine wanaotaka mabadiliko wampe Dr. Slaa na wawape wagombea wa CHADEMA kura zao. CCM walitoa rai kwamba kila mwanachama mmoja wa CCM atafute wananchi wengine watatu kuiwezesha CCM ipate ushindi wa kishindo. Mnyika na kundi lake na wao wafanye kazi ya ziada ya kuwahamasisha wana CHADEMA ili mwanachama mmoja mmoja apate watu 3 hadi 5 watakao kumuunga mkono katika kumpigia kura mgombea wa CHADEMA.

Penye nia hapakosi njia na hakuna lisilowezekana - Mwalimu alisema: It can be done, Play your part!!

Ushauri mwingine wa bure: CHADEMA wanayo ruksa ya kulitumia jina na busara na msimamo wa Baba wa Taifa katika uongozi wa nchi kwa sababu kama tunavyomwita ni Baba wa Taifa zima na si wa CCM pekee! Wapo baadhi ya viongozi wanaolinyanyapaa jina la Baba wa Taifa kwa sababu zao binafsi! Jina la Mwalimu litumike zaidi kwenye kampeni vijijini ambako wananchi wengi bado wanamkumbuka kwa namna alivyojali wananchi aliokuwa akiwaongoza.
 
Mimi nashauri CHADEMA kama wakiweza, wawe wananunua strategic Airtime katika TV na Redio ambazo Watanzania wengi wanasikiliza. Vipindi hivi viambatane na Muziki ambavyo Watanzania wengi wanapenda.

Kupitia vipindi hivi Sera za CHADEMA na Elimu ya kutosha itolewe ili wengi waweze kushawishika.

Magazeti pia yatumike kila siku kuelezea sera kwa lugha nyepesi na hata ya picha au cartoon bila kuleta hadithi nyingi. watanzania wengi si wasomaji. Zitengenezwe DVD zilizoambatana na Muziki safi na zigawiwe kwa wingi huku vijarida vidogo vinavyoonyesha vipaumbele kwa lugha nyepesi vikigawiwa.
mkuu niliwahi kutoa ushauri wa bure mwaka juzi kuwa itumike njia ya kusambaza elimu kwa umma ili CHADEMA wanapoingia ktk mchakato wa kampeni wasiwe wageni masikioni mwa watanzania wengi. Bado naamini tulioelimika kuhusu uhalisia wa mambo ni wachache mno. hatari iliyoko wapigakura wengi hawajui hata kama WAMEDANGANYIKA vya kutosha.

Nipo tayari kujitolea muda wangu kusaidia kupanga mipango ya namna ya kuwafikia waliowengi na kuwapa elimu sahihi ya nini thamani yao na wajibu wao dhidi ya hali tuliyonayo sasa.
 
Wamepondwa sana na raia na wengi walikuwa wameanza kutolisoma ndo maana wanajaribu kujirudi!
 
Mimi nashauri CHADEMA kama wakiweza, wawe wananunua strategic Airtime katika TV na Redio ambazo Watanzania wengi wanasikiliza. Vipindi hivi viambatane na Muziki ambavyo Watanzania wengi wanapenda.

Kupitia vipindi hivi Sera za CHADEMA na Elimu ya kutosha itolewe ili wengi waweze kushawishika.

Magazeti pia yatumike kila siku kuelezea sera kwa lugha nyepesi na hata ya picha au cartoon bila kuleta hadithi nyingi. watanzania wengi si wasomaji. Zitengenezwe DVD zilizoambatana na Muziki safi na zigawiwe kwa wingi huku vijarida vidogo vinavyoonyesha vipaumbele kwa lugha nyepesi vikigawiwa.


ITV, TEN na Star TV wameikatalia katakata CHADEMA kutumia station zao.
 
Back
Top Bottom