Je, Marekani ina uwezo wa kupigana na Houthi kuilinda Israel?

Webabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
7,305
11,165
Wengine wanaweza kusema swali hilo ni kichekesho, lakini hali ilivyo sasa ni swali linalokwenda na wakati na kutaka kupatiwa jibu lake.

Tangu wanamgambo wa Houthi waanze kuingia kwenye mapambano kuwasaidia wenzao wa Gaza, Marekani imekuwa ikikasirika sana na hata kuwahi kusema Yemen ni rogue nation inayopasa kushughulikiwa.

Wanamgambo wa Houthi ambao ndio wanaoitawala Yemen hawajaonekana kutishika na maneno hayo ya Marekani kwani hapo juzi walizitia mchakamchaka meli 4 zenye mahusiano na Israel ikiwemo meli ya kivita ya Marekani yenyewe. Meli hiyo ya USS corney ilirushiwa kombora na droni na haijajulikana kwa uhakika madhara iliyopata.

Katika hali hiyo jee Marekani ina uwezo wa kuingia vitani na wanamgambo hao ili iwaondoe madarakani na kuihakikishia usalama wake Israel.

Hali za kisiasa duniani na uwezo wa kijeshi na kiuchumi wa Marekani jee unaipa nguvu nchi hiyo kupigana na Houthi na kuishinda na mwishowe kuweka kiongozi kibaraka watakayemchagua?

Ikumbukwe kuwa Houthi ni watawala wa taifa dhaifu sana lakini wamekalia eneo muhimu sana kiuchumi wa dunia na mienendo ya kijeshi. Kupambana nao mpaka kuwashinda moja kwa moja kunaweza kukamaliza nguvu zote za mtu huyo atakayejaribu kuingia vitani nao
 
Kama ilivyo kwa Iran haiwezi kupigani na Israel moja kwa moja , ndivyo itakavyokuwa kwa USA 🇺🇲 kamwe haiwezi peleka jeshi lake kupambana na Houth bali itatengeneza vikundi vidogo vidogo vitakavyokuwa vinapambana kwa niaba yake.
 
Kama ilivyo kwa Iran haiwezi kupigani na Israel moja kwa moja , ndivyo itakavyokuwa kwa USA kamwe haiwezi peleka jeshi lake kupambana na Houth bali itatengeneza vikundi vidogo vidogo vitakavyokuwa vinapambana kwa niaba yake.
Nahuu ndio ukweli
Tena hasa kwanyakati hizi zasasa kisiasa kiuchumi na kijeshi zilivyo us hawezi ama hana uwezo kuingiza boot kwa ground katika laifa lolote lile
Kwanza atakosa sapota kwa mashost zake maana kwahali ya kiuchumi ilivyo us itamfata nani pale NATO au EU aende akampe kampani maana wote hali kwao tete kama sio kisiasa basi kijeshi nakama sio kijeshi basi kiuchumi
Naikitokea ndio us akavamia basi hii nafasi yawazi kabisa kuzidi kuangamia kwake itakayotumiwa na iran ☫ na Russia kumpelekesha us
Us mwenyewe nna imani anajua kama kwasasa kama kuna mtu anaetafutwa aingie mkenge ni yeye sidhanii kama wanaweza wakauingia huo mkenge
Mtoa mada hongera kwako hii mada nzuri sana
 
Wajaze na mafuta ila hamas haitakaa iondoke ghaza
Yaani israhell wamekua muflis namna hii wakat waliyatwanga mataifa yote ya kiarabu kwa siku sita
Pua israhell
Subiri hamas wajifie kwa mafuriko humo kwenye mashimo
 
Wajaze na mafuta ila hamas haitakaa iondoke ghaza
Yaani israhell wamekua muflis namna hii wakat waliyatwanga mataifa yote ya kiarabu kwa siku sita
Pua israhell
Jionee moto wanaopelekewa hamas!
 
Nahuu ndio ukweli
Tena hasa kwanyakati hizi zasasa kisiasa kiuchumi na kijeshi zilivyo us hawezi ama hana uwezo kuingiza boot kwa ground katika laifa lolote lile
Kwanza atakosa sapota kwa mashost zake maana kwahali ya kiuchumi ilivyo us itamfata nani pale NATO au EU aende akampe kampani maana wote hali kwao tete kama sio kisiasa basi kijeshi nakama sio kijeshi basi kiuchumi
Naikitokea ndio us akavamia basi hii nafasi yawazi kabisa kuzidi kuangamia kwake itakayotumiwa na iran ☫ na Russia kumpelekesha us
Us mwenyewe nna imani anajua kama kwasasa kama kuna mtu anaetafutwa aingie mkenge ni yeye sidhanii kama wanaweza wakauingia huo mkenge
Mtoa mada hongera kwako hii mada nzuri sana

Ni kweli hakuna muungano utakaokubali kujitoa muhanga kwa ajili ya USA 🇺🇲 tena, mara kwa mara kila nchi inapojaribu kuisaidia USA moja kwa moja hiyo nchi inajikuta inapoteza mwelekeo pande zote..FRANCE , BRITAIN 🇬🇧, GERMAN 🇩🇪 zote hizo ni nchi zilizokuwa na nguvu na ushawishi nyanja zote lakini baada tu ya kufungamana na USA wote wamepoteza mvuto na ule ushawishi wao kidunia.

Hapo mashariki ya kati alikuwa amejifunga kwa Saudi 🇸🇦 , Jordan 🇯🇴, Bahrain 🇧🇭 n.k ili tu kuzuia ushawishi wa Iran 🇮🇷 anayeonekana tishio kwa Israeli 🇮🇱 mshirika wake wa kudumu .

Mambo yamebadilika sasa na dunia inaelekea uelekeo sahihi na ni suala la muda tu Ira
n na Saudi 🇸🇦 watakuwa kitu kimoja na kuweka tofauti zao za kimadhehebu, jambo ambalo litakuwa pigo kubwa kwa USA na Israel na vizazi vyao vyote.
 
Kama ilivyo kwa Iran haiwezi kupigani na Israel moja kwa moja , ndivyo itakavyokuwa kwa USA 🇺🇲 kamwe haiwezi peleka jeshi lake kupambana na Houth bali itatengeneza vikundi vidogo vidogo vitakavyokuwa vinapambana kwa niaba yake.
Tumesema dunia imebadilika.VIkundi vya fitina kama Alshabaab,bokoharm na Iss havina nafasi tena .
Watu maeneo mengi wametoka ujinga.
Israel nayo ilijaribu sana kufanya hivyo ndani ya Gaza na wakashindwa.Watu wake waliwahiwa kabla hawajaanza kazi isipokuwa wachache sana.
 
Ni kweli hakuna muungano utakaokubali kujitoa muhanga kwa ajili ya USA 🇺🇲 tena, mara kwa mara kila nchi inapojaribu kuisaidia USA moja kwa moja hiyo nchi inajikuta inapoteza mwelekeo pande zote..FRANCE , BRITAIN 🇬🇧, GERMAN 🇩🇪 zote hizo ni nchi zilizokuwa na nguvu na ushawishi nyanja zote lakini baada tu ya kufungamana na USA wote wamepoteza mvuto na ule ushawishi wao kidunia.

Hapo mashariki ya kati alikuwa amejifunga kwa Saudi 🇸🇦 , Jordan 🇯🇴, Bahrain 🇧🇭 n.k ili tu kuzuia ushawishi wa Iran 🇮🇷 anayeonekana tishio kwa Israeli 🇮🇱 mshirika wake wa kudumu .

Mambo yamebadilika sasa na dunia inaelekea uelekeo sahihi na ni suala la muda tu Ira
n na Saudi 🇸🇦 watakuwa kitu kimoja na kuweka tofauti zao za kimadhehebu, jambo ambalo litakuwa pigo kubwa kwa USA na Israel na vizazi vyao vyote.
Saudia huwa anapata akili kidogo kidogo halafu wazimu unamrudia.Hata hivyo mambo yanavyokwenda atakaa sawa.
Mwenzake Bahrain amejuliza maswali mengi kuhusu mkataba wa Abraham alioingia na Israel.
Saudia haikudhaniwa kuwa angekaa meza moja na Iran au kwamba angesema mafuta yake si lazima yanunuliwe kwa dola za kimarekani.Na amefanya hivyo.
 
Back
Top Bottom