Kiswahili ni Kibantu au Kiarabu?

Baada ya ufafanuzi uliopewa hapo juu ndio umepata hitimisho kuwa kiswahili ni CHOTARA?.
Mkuu kiswahili ni KIBANTU full stop.
Kwanini kibantu? lugha zote duniani zina asili yake na asili ya kiswahili ni kibantu kwa maana ya kuwa iliasili utamkwaji aka rithm au kwa maana nyingine pronaunciation yake ni ya kibantu licha ya kukopa maneno lukuki kutoka katika kiarabu.
Moja ya sifa ya lugha ni namna unavyotamka maneno pronaunciation, ndio maana mengi ya hayo maneno ya kiarabu hayatamkwi exactly kama waarabu wenyewe wanavyo yatamka na kuyaandika.
Kibantu si kabila ila inamaana ujumla wa makabila yaliyozaliwa katika asili moja yanayo share baadhi ya maneno na utamkwaji na hii inafanya kiswahili kuwa kibantu.
Najua kwanini katika wote waliotoa michango umemkubali zaidi ZOMBA ni kwasababu unaelekea kuipeleka hoja hii ktk udini, ionekane atutaki kusema ni kiarabu kwakuwa kiarabu kina uislam ndani yake(which is not true) naamini ndugu yangu umepitia madrassa unaweza kulinganisha maneno mliyojifunza huko kimatamshi yapo sawa na yaliyotoholewa kuwa kiswahili? mfano sahil na mswahili, ni wazi utamkwaji upo tofauti yaliyotoholewa yanatamkwa ktk tone ya kibantu.
Mwisho mkuu zomba inferiority complex ndio inayo kusumbua wewe na wenzio mnaodhani watu wapo kupinga uislam tu, hapana watu wapo bize kujenga mahospitali, mashule, mavyuo mabenki nk ili watu kama ninyi mpate huduma huko serikali iliposhindwa na si kukomalia kiswahili ni kiarabu, haiwasaidii

Naomba pitia hiyo risala yako utazame ni maneno mangapi humo unaweza kusema ya asili ya kiarabu na mangapi yana asili ya ubantu.

Point yako ya lafdhi, haina mantiki kwa sababu hiki kiswahili chenyewe lafdhi tofauti hutumika kulinganisha na sehemu kitumiwacho. Mfano, kiswahili ni lugha mama ya waswahili (watu wa pwani ya Afrika Mashariki), lakini hubadilika lafdhi mji mpaka mji wa pwani hiyo hiyo. Kwa hiyo huwezi kusema kuwa lafdhi ndio inakifanya kiswahili kuwa Kibantu. Kiswahili ni maneno ya lugha nyingi lakini kiarabu ndio chenye maneno asilimia kubwa katika kiswahili kuliko lugha nyingine yeyote. Kama unabisha kwa hilo tuanze kuhisabu maneno ya kiswahili.

Pia napenda ujuwe kuwa kiswahili kilijulikana kama lugha ya waIslam, kwani hao waswahili wenye asili ya kiswahili wengi wao 99% ni waIslam.
 
safiii na nikwel ila kama unarud kwa PAULSS na nimefurah kuona umerekebisha panapo watatiza wajio na vchwa vgumu kuelewa senkyu senkyu sanaaa
 
safiii na nikwel ila kama unarud kwa PAULSS na nimefurah kuona umerekebisha panapo watatiza wajio na vchwa vgumu kuelewa senkyu senkyu sanaaa

6¦6
6¦6MUREFU na ZOMBA inabidi "nikubaliane" na nyinyi kuwa kiswahili si kibantu bali ni "kiarabu" na ni lugha ya "waislam" na ndio maana "wakristo" wanafanya juu chini kufuta maneno ya "kiislam" yaani kiarabu katika msamiati wa kiislam yaani kiarabu aka kiswahili.6¦6Mmeridhika?
 
acha ujinga wewe, wewe ni m2 mzma haiwezekan wewe uongee ujinga kama huo m2 mzma wewe na umesoma wewe sawa kuwa na akil PAULSS haiwezekan useme ki2 kama hcho 2mia akil kwanza sawa kijana
 
?6¦6
?6¦6MUREFU na ZOMBA inabidi "nikubaliane" na nyinyi kuwa kiswahili si kibantu bali ni "kiarabu" na ni lugha ya "waislam" na ndio maana "wakristo" wanafanya juu chini kufuta maneno ya "kiislam" yaani kiarabu katika msamiati wa kiislam yaani kiarabu aka kiswahili.?6¦6Mmeridhika?
Una uelewa mpana sana, zaidi ya unavyostahiki kwa hili.
 
Disko kaingia MMasai
kama unataka kufaulu mtihani basi sema iswahili ni kibantu ila kama unataka kujua kiukweli basi lugha hii ni krioli ya kibantu na kiarabu....ninavyofahamu mimi ni kuwa katika Afrika yote hakuna lugha iso na kabila ....je nani kabila lake mswahili ? najua kuna waswahili ambao wengine wana makabila wazaramo,mijikenda nk. na wengine waoyajua makabila yao kama kule zenji, lakini hawa ndio waswahili ila hakuna kabia la kiswahili hii kwa maoni yangu ni kuwa hii lugha haikuwepo hapo kale ila baada ya mchanganyiko wa hawa watu wa mrima(watu wa mwambao) na waasia na makbila mengine ndipo ikazaliwa hii lugha.inategemea lafdhi ya mtu kwani kuna wengine hutamka maneno yenye asili ya kiarabu kama kiarabu na wengine hawatamki hivyo....pia inategemea ni kama mswahili wa kuzaliwa ama wa kusoma hii lugha,kuna tofauti kubwa baina ya lafdhi ya watu hawa.
kiswahili kina lahaja nyingi sana 20 ?? wenye ujuzi nifahamisheni kutokea kaskazi ni kibarawa,kibajuni (kiamu-kilamu,kigunya) ,kimvita nk
jambo linalonishangaza mimi ni kuwa hawa wanofanya kazi ya taasisi mbalimbali za kiswahili za afrika mashariki wengi wao sio waswahili wa asili kwani wao wamesoma, je kwa nini watafute maneno ya kiswahili katika lugha nyengine wakati jambo la kwanza inabidi neno litafutwe katika lahaja na kama likikosekana basi ndipo litafutwe kwengine...........
nilisikia mtu 1 wa mombasa akilalamika kuwa mwanawe kafeli kiswahili kwa kuwa msainishaji hakuwa mweledi katika lugha,akatoa mfano 1 ukiambiwa mbuzi kwa mswahili atafahamu kuwa ni aidha ya kukunia nazi ama yule mnyama ,sasa kwa mtu alietoka nakuru ambako hakuna minazi aaelewaje kitu hichi ?
ni mawazo tu
 
Asilimia kuubwa ya maneno ya kiswahili yanatokana na Kiarabu, hakuna lugha duniani inaitwa kibantu, kibantu ni mchanganyiko wa lugha nyingi za watu wenye asili ya kibantu. Watu wenye asili ya kibantu hupatikana kusini mwa sahara. Wale wa Afrika wengine wasio wabantu, ambao na hapa kwetu wapo wengi tu, kama vile wamasai, waIraqw, waRangi, wa Zanaki, waJaluo na kadhalika, utakuta wana asili za kiarabu kwenye lugha zao. Ikumbwe pia uArabu ni lugha na si utaifa. Kuna mataifa mengi katika Afrika yanayoongea kiarabu na wao hujiita wa Arabu, si kwa uTaifa bali kwa lugha.

Ukichukuwa Kiarabu na lugha ambazo si za kibantu lakini za kiafrika zilizongiza maneno yake kwenye kiswahili utakuta kuwa maneno ya lugha za kibantu si mengi sana katika kiswahili, hayawezi fika asilimia 40%, asilimia chache zingine zinatokana na lugha za nchi ambazo zilikuwa na muingiliano mkubwa wa kibiashara na utawala katika pwani ya afrika mashariki, kama vile Kireno, Kijerumani, Kiingereza, Kihindi, Kichina.

Duniani, kila mawasiliano yanavyozidi ndio lugha huchukuwa maneno kila muingiliano wa mataifa unapozidi, ni lugha chache sana zinazojitolesheza na maneno yake yeneyewe, na hizi ni lugha za zamani na huitwa kugha tajiri, utajiri wa kuwa na maneno mengi.

Kiswahili kimebahatika kuwa na maneno mengi ya Kiarabu (Kiarabu ni Lugha tajiri) na nadhani ni hivi ppunde tu na chenyewe kitakuwa moja ya lugha tajiri.

Kwa sasa, kuna hujuma za wazi za kukitowa kishahili kutoka uasili wa kiarabu kwa sababu tu uarabu unahusishwa na uIslaam. Kilanjia zinafanyika kubuni maneno mapaya ambayo hayana hata msamiati wala lafdhi za kiswahili, ili mradi tu, kitoke kwenye asili yake ya asili.

Baraza la kiswahili limeingiliwa na watu wasio na asili ya lugha ya kiswahili. Wenye asili ya lugha ya kiswahili ni watu wa pwani ya Afrika Mashariki na wanaoongea kiswahili kama lugha mama.

Hta neno ki- swahili lenyewe linatokana na kiarabu "sahil", pwani, "sawahil" watu wa pwani.

Swadakta swadakta maneno sawia kabisa pasi na shaka.

ndio maana watu wa Pwani ya Afrika mashariki ndio wazungumzaji wa kuu wa kiswahili.
 
Kiswahili ni lugha ya Kibantu yenye misamiati mingi ya Kiarabu inayozungumzwa katika eneo kubwa la Afrika ya Mashariki.
Lugha hii ina utajiri mkubwa wa misamiati, misemo, mithali, mashairi, mafumbo, vitendawili na nyimbo. Kiswahili hutumika mashuleni na kuna vitabu vingi vilivyotungwa kwa kutumia lugha hii, vikiwa vya hadithi, hekaya au riwaya.

Historia ya lugha

Lugha ilianza takriban miaka 800-1000 iliyopita katika mazingira ya vituo vya biashara vya pwani ambako wafanya biashara kutoka Uarabuni, Uajemi na Uhindi walikutana na wenyeji Waafrika. Lugha kuu ya kimataifa ya biashara hii ilikuwa Kiarabu. Inaonekana ya kwamba lugha mpya ilijitokeza wakati wenyeji wa pwani waliokuwa wasemaji wa lugha za Kibantu walipopokea maneno mengi hasa ya Kiarabu katika mawasilaino yao. Kwa hiyo msingi wa Kiswahili ni sarufi na msamiati wa Kibantu pamoja na maneno mengi ya Kiarabu. Imekadiriwa ya kwamba theluthi moja ya maneno ya Kiswahili yana asili ya Kiarabu.
Kando na Kiarabu kuna pia athira ya lugha mbalimbali kama Kiajemi, Kihindi na Kireno. Wakati wa karne ya Ishirini maneno mengi yalipokelewa kutoka Kiingereza.
Kwa karne nyingi iliandikwa kwa herufi za Kiarabu (سواحلي sawaHili au لغة سواحيلية lugha sawaHiliya). Sarufi ya kwanza pamoja na Kamusi iliandikwa mnamo 1848 na Dr. Ludwig Krapf hukoRabai Mpya / Mombasa.
Kiswahili kilikuwa na lahaja nyingi kutokana na lugha mbalimbali za Kibantu zilizochangia mle. Tangu karne ya 19 lugha ilianza kuenea barani kwa njia ya biashara. Wakati wa ukoloni wa Uingereza lugha ilisanifishwa kwenye msingi wa lahaja ya Unguja.

Wasemaji


Hakuna uhakika kuhusu idadi za wasemaji wa lugha; idadi zinazotajwa zinatofautiana. Wasemaji wa lugha ya kwanza wako labda kati ya milioni 7 hadi 10, na wasemaji wa lugha ya pilizaidi ya milioni sabini. Idadi ya wasemaji wa lugha ya kwanza inakua, kwa sababu lugha inaenea katika maeneo ambapo lugha nyingine zilikuwa lugha kuu, na hasa katika miji yaTanzania imekuwepo lugha kuu, badala ya lugha za kikabila.
Kati ya nchi ambapo Kiswahili kinatumika ni Tanzania, Kenya, Uganda, Kongo-Kinshasa, Rwanda, Burundi, Msumbiji, Somalia na visiwa vya Bahari Hindi kama Visiwa vya Ngazija(Komoro).


Lugha rasmi

Kiswahili kimekuwa lugha rasmi katika nchi zifuatazo:

  • Tanzania: Lugha ya taifa; ni lugha ya shule za msingi, lugha ya utawala serikalini na mahakamani; inatumika kote nchini, kanisani, kwenye misikiti, redioni, runinga na idadi kubwa ya magazeti.

  • Kenya: ni lugha ya taifa lakini Kiingereza ni lugha rasmi ya Kiutawala; Kiswahili ni lugha ya kwanza ya
  • mawasiliano kati ya wanachi wakikutana nje ya eneo penye kabila moja tu; ni lugha inayofundishwa lakini si lugha ya kufundisha mashuleni; ni lugha inayotumika na polisi na jeshi, ni lugha ya kuhutubia wanachi mjini na kitaifa; sehemu za ibada makanisani inatumia Kiswahili; kuna gazeti moja tu la Kiswahili; sehemu
  • za programu redioni na kwenye runinga ni kwa Kiswahili. Lugha inachanganywa mara nyingi na Kiingereza na lugha za maeneo au kikabila. Hata hivyo baada ya rasimu ya katiba mpya kupitishwa mnamo tarehe 4, Agosti 2010, Kiswahili sasa kitakuwa lugha rasmi, sawa na Kingereza.
  • Uganda: imetangazwa kuwa lugha ya kitaifa tangu 2005; iliwahi kuwa lugha ya kitaifa wakati wa utawala wa Idi Amin; wakati wa ukoloni ilifundishwa mashuleni ikaelekea kuwa lugha rasmi pamoja na Kiingereza
  • lakini matumizi haya yalipingwa hasa na Waganda hivyo Waingereza waliacha mipango haya. Ni lugha ya polisi na jeshi hali ambayo imeleta ugumu kwa lugha kukubalika na wanachi wengi kutokana na historia ya utawala wa kijeshi Uganda; watu wengi bado hukumbuka hasa matusi ya wanajeshi waliowatesa wakisema Kiswahili. Lakini kuna maeneo ya Uganda ambako Kiswahili kinatumika na watu wengi kama lugha ya sokoni na barabarani. Wona UBC, WBS tv.

  • Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo: Kiswahili ni kati ya lugha nne za kitaifa, pia lugha ya jeshi katika mashariki ya nchi. Kiswahili kimefika na misafara ya biashara ya watumwana pembe za ndovu kutoka Zanzibar na pwani la Tanganyika. Imeenea zaidi kati ya mchanganyiko wa wafanyakazi kwenye migodi ya Shaba.

Lugha ya kwanza, lugha ya pili



Kiasili Kiswahili kilikuwa lugha ya kwanza tu ya wakazi wa miji ya Waswahili kwenye pwani, katika sehemu za pwani pia kijijini. Baada ya kuenea kimekuwa lugha ya watu wengi mjini hasa Tanzania lakini pia Kenya.
Kimeenea zaidi kama lugha ya mawasiliano na biashara pale ambako watu wa makabila mbalimbali

wanakutana. Pamoja na nchi zinazotajwa hapo juu Kiswahili kinatumika katika Kaskazini ya Msumbiji, Kusini kabisa ya Somalia, Mashariki ya Burundi. Maeneo ya mpaka wa Tanzania kuna pia wasemaji kadhaa huko Malawi na Zambia.

Tanzania na Kenya zilipokea wakimbizi wengi waliojifunza Kiswahili lakini hakuna uhakika kama bado kinatumika wakirudi Rwanda, Sudan au Somalia.


Kimataifa.


Lugha hii leo imekuwa na umuhimu mkubwa duniani kwa jumla, na hasa Africa, kwa sababu ya kuenea kwake nchi mbali mbali, na kukusanya kwake watu wa makabila na nchi kadha wa kadha wakaweza kufahamiana kwa lugha moja, hasa ilivyokuwa ni lugha mojawapo katika lugha kubwa za Africa ambazo zinachukuwa mahala pa lugha za kigeni na Wakoloni, kamaKiarabu, Kiurdu, Kihebrania, Kireno na kadhalika.
Leo, imekuwa inatumiwa katika kusambaza habari katika vituo mbali mbali ulimwenguni kama vile Sauti ya Amerika, BBC, Deutsche Welle, Monte Carlo, na nchi nyenginezo za Uchinana Urusi na Irani na kwengineko. Aidha, imekuwa ni mojawapo ya lugha muhimu zinazofundishwa katika vyuo vikuu nchini Marekani, Uingereza, Ulaya, Urusi, Uchina, na barani Afrika.

Maendeleo ya Kiswahili

Lugha ina maendeleo: inaweza kukua, kukwama au kufa. Athira nyingi hutokea bila mpangilio pale ambako wasemaji wanapokea maneno mapya, wanaacha kutumia maneno mengine au hubadilisha kawaida ya matamshi au sarufi. Haya yote hutokea pia katika uwanja wa Kiswahili.
Kuna mzaha unaosimuliwa hasa Tanzania: Kiswahili kilizaliwa Unguja, kilikua Tanzania Bara, kikafa Kenya na kuzikwa Uganda. Hali halisi Kiswahili kina maendeleo yake katika nchi hizo zote labda zaidi Kongo. Lakini itategemea pia juhudi za serikali kama umoja wa lugha utatunzwa kwa sababu kuna athari nyingi kutoka lugha za kila eneo zinazoingia katika ukuzi wa Kiswahili kwa namna zinazotofauitiana.

Taasisi zinazokuza Kiswahili


Kuna taasisi zinazolenga kukuza na kuimarisha Kiswahili kama vile Taasisi ya Taaluma za Kiswahili (TATAKI) kwenye Chuo Kikuu cha Dar es Salaam pamoja na idara za Kiswahili katika vyuo vikuu vingine vya Kenya na pia Uganda.
Nchini Tanzania kuna Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) na Baraza la Kiswahili Zanzibar (BAKIZA) ilhali nchini Kenya kuna Chama cha Kiswahili cha Taifa (CHAKITA). BAKITA na CHAKITA pamoja na wawakilishi kutoka Uganda wanaandaa kuundwa kwa Baraza la Kiswahili la Afrika Mashariki (BAKAMA).
Uchunguzi wa Kiswahili huendelea pia katika idara za vyuo vikuu vingi duniani, kwa mfano katika Institute National des Langues et Civilisations Orientales, mjini Paris, Ufaransa. Matumizi yake ni kwa njia ya lahaja za Kingwana.

Kamusi za Kiswahili

Makala kuu ya: Kamusi za Kiswahili
Kati ya shughuli muhimu ni kazi ya kukuza msamiati wa Kiswahili yaani kutafuta maneno mapya au kupanusha matumizi ya maneno yaliyopo ili kutaja mambo ya maisha ya kisasa yaliyobadilika. Kutunga kwa kamusi za Kiswahili hupanusha elimu hiyo.






 
Kiswahili ni Kiswahili (Full stop), sio Kiarabu wala Kibantu.
Wale wanaodai kuwa Kiswahili ni Kiarabu kwa sababu kina maneno mengi ya Kiarabu, hawana hoja kwa sababu maneno ya Kiswahili hayatamkwi kama Kiarabu. Pia wanaodai hivyo, sababu yao ni kuwa hakuna kabila la Waswahili. Ni kweli haliko, lakini kuna Australia, Marekani na Newzeland kwa mfano, ambazo lugha yao ya Taifa ni Kiingereza lakini wao si Waingereza. Kwa ufupi, si lazima kuwe na kabila ndio ipatikae lugha.

Hatuwezi kusema Kiswahili ni Kiarabu kwa sababu hakitamkwi kama Kiarabu kinavyotamkwa. Hata yale baadhi ya maneno yaliyoingizwa katika Kiswahili kama maneno ya dini (Salat, alfajir, maghrib, al-asir, Ramadhan, kufur, diin, na kadhalika), tutaona kuwa maneno (mengi) ya Kiarabu yanaishia na konsonanti. Kinyume chake, MANENO YOTE ya Kiswahili yanaishia na vokali.

Kwa sababu hiyo hapo juu, na kuhusu asili ya Kiswahili, tunaweza kusema na kuthibitisha kuwa Kiswahili kina asili ya Kibantu wala sio Kiarabu kwa sababu MANENO YOTE katika lugha zenye asili ya Kibantu yanaishia na vokali.

Ni mawazo na ufahamu wangu, niko tayari kufahamishwa hata kukosolewa kwa hoja.
 
Huo uswahili wenyewe usingekuwepo pasi na Kiarabu. Hilo neno "swahili" ni kiarabu.
 
Mimi ni muIslam na kama uIslam wangu unakufanya unione mdini basi hayo ni maono yako.

Nani asiejuwa kuwa uIslam unahusishwa na uArabu ingawa wa Arabu ni asilimia chache sana kati ya Waislaam wa duniani.

Kiswahili kina maneno mengi mazuri lakini utakuta hayatumiki na yanabuniwa mengine mapya ambayo hayana asili ya uswahili. Lugha si kubuni maneno tu, hayo maneno yanayobuniwa yafanane na lafdhi za kiswahili ili kukipa raha yake ya asili kiswahili chetu kitamu.
nakubaliana na wewe 100% na ni kwamba uchumi wetu kuwa mdogo umekifanya kiswahili kuwa ni lugha inayoingiziwa maneno yasiyo na maana..ilitakiwa kiswahili kiongezewe maneno mengi ya kibantu lakini yenye maana ya bidhaa zetu ili watu wanaotumia kiswahili waendelee kukijua kupitia local products,sasa hivi hali ilivyo baada ya miaka kadhaa ijayo kiswahili kitakoma kufika songea,kigoma,unyakyusa n.k kwa vile mahitaji yao ya kila siku hayahusishi kiswahili na watu wa pwani kwa sababu hawana bidhaa wanazidi kuki-arabisha..when you move far from Dar unakuta watu wote hawajui kiswahili kwa vile it doesn't connect with the products they use!!!!!!kwa ujumla watu wenye dhamana ya kuendeleza kiswahili waanze ku-connect maneno ya kibantu ambayo yanaweza kuzoeleka kwa wabantu wote yenye maana kwenye maisha yao ya kila siku..
 
Ila naomba mniseidie lugha ya kiswahili ni muunganikano wa makabila magapi mpaka kutengeneza kiswahil
 
Kiswahili si muunganiko wa lugha wala makabila. Ni lugha ambayo asili yake nikatika familia ya lugha za Kibantu. Unaposema lugha ni ya Kibantu au Kiarabu unaangalia muundo wake. Je, maneno yake yanaundwa vipi? Je sentensi zake zinaundwa vipi? Je, virai vyake vinaumbwa vipi? Je, maneno yake ya msingi (common core vocabulary) inatoka wapi? Sasa, kukipambanua Kiswahili na Kiarabu (na kwa hakika lugha zote za Kisemitiki), angalia ngeli za Kiswahili (lugha mchanganyiko haitunzi mfumbo wa ngeli tangamano vile); angalia upatanisho wa kisarufi (lugha mchanganyiko haitunzi mfumo kama huo, itaufanya uwe rahisi zaidi); angalia hata jinsi vitenzi vinavyoundwa. Vya Kiarabu vinatokana na mizizi ya konsonanti tatu ktb, drs, nk. Mizizi ya Kiswahili ni kama -pig-, -som-, nk. Utaambisha kwenye Kiarabu kwa kuchomeka sauti mbalimbali, na ktk Kiswahili utaongeza viambishi mbele na nyuma. Kwa upande wa msamiati. Kiswahili hivi leo kina maneno mengi sana kutoka Kiingereza. Basi je tuseme Kiswahili kinatokana na Kiingereza? Kila lugha huchukua maneno kutoka lugha nyingine. Kuchukua maneno kutoka lugha nyingine hakubadilishi nasaba ya lugha. Kiswahili kimekopa maneno ya kiutamaduni kama vile yanayohusu elimu na dini kutoka Kiarabu. Lkn hakikuchukua mfumo wa Kiarabu. Watu hasa huangalia Kiswahili ili kufahamu muundo wa lugha za Kibantu. Ingelikuwa ni lugha mchanganyiko jambo hilo lisingewezekana.
 
Kiswahili ni lugha ya Kibantu yenye misamiati mingi ya Kiarabu inayozungumzwa katika eneo kubwa la Afrika ya Mashariki.
Lugha hii ina utajiri mkubwa wa misamiati, misemo, mithali, mashairi, mafumbo, vitendawili na nyimbo. Kiswahili hutumika mashuleni na kuna vitabu vingi vilivyotungwa kwa kutumia lugha hii, vikiwa vya hadithi, hekaya au riwaya.

Historia ya lugha

Lugha ilianza takriban miaka 800-1000 iliyopita katika mazingira ya vituo vya biashara vya pwani ambako wafanya biashara kutoka Uarabuni, Uajemi na Uhindi walikutana na wenyeji Waafrika. Lugha kuu ya kimataifa ya biashara hii ilikuwa Kiarabu. Inaonekana ya kwamba lugha mpya ilijitokeza wakati wenyeji wa pwani waliokuwa wasemaji wa lugha za Kibantu walipopokea maneno mengi hasa ya Kiarabu katika mawasilaino yao. Kwa hiyo msingi wa Kiswahili ni sarufi na msamiati wa Kibantu pamoja na maneno mengi ya Kiarabu. Imekadiriwa ya kwamba theluthi moja ya maneno ya Kiswahili yana asili ya Kiarabu.
Kando na Kiarabu kuna pia athira ya lugha mbalimbali kama Kiajemi, Kihindi na Kireno. Wakati wa karne ya Ishirini maneno mengi yalipokelewa kutoka Kiingereza.
Kwa karne nyingi iliandikwa kwa herufi za Kiarabu (سواحلي sawaHili au لغة سواحيلية lugha sawaHiliya). Sarufi ya kwanza pamoja na Kamusi iliandikwa mnamo 1848 na Dr. Ludwig Krapf hukoRabai Mpya / Mombasa.
Kiswahili kilikuwa na lahaja nyingi kutokana na lugha mbalimbali za Kibantu zilizochangia mle. Tangu karne ya 19 lugha ilianza kuenea barani kwa njia ya biashara. Wakati wa ukoloni wa Uingereza lugha ilisanifishwa kwenye msingi wa lahaja ya Unguja.

Wasemaji


Hakuna uhakika kuhusu idadi za wasemaji wa lugha; idadi zinazotajwa zinatofautiana. Wasemaji wa lugha ya kwanza wako labda kati ya milioni 7 hadi 10, na wasemaji wa lugha ya pilizaidi ya milioni sabini. Idadi ya wasemaji wa lugha ya kwanza inakua, kwa sababu lugha inaenea katika maeneo ambapo lugha nyingine zilikuwa lugha kuu, na hasa katika miji yaTanzania imekuwepo lugha kuu, badala ya lugha za kikabila.
Kati ya nchi ambapo Kiswahili kinatumika ni Tanzania, Kenya, Uganda, Kongo-Kinshasa, Rwanda, Burundi, Msumbiji, Somalia na visiwa vya Bahari Hindi kama Visiwa vya Ngazija(Komoro).


Lugha rasmi

Kiswahili kimekuwa lugha rasmi katika nchi zifuatazo:

  • Tanzania: Lugha ya taifa; ni lugha ya shule za msingi, lugha ya utawala serikalini na mahakamani; inatumika kote nchini, kanisani, kwenye misikiti, redioni, runinga na idadi kubwa ya magazeti.

  • Kenya: ni lugha ya taifa lakini Kiingereza ni lugha rasmi ya Kiutawala; Kiswahili ni lugha ya kwanza ya
  • mawasiliano kati ya wanachi wakikutana nje ya eneo penye kabila moja tu; ni lugha inayofundishwa lakini si lugha ya kufundisha mashuleni; ni lugha inayotumika na polisi na jeshi, ni lugha ya kuhutubia wanachi mjini na kitaifa; sehemu za ibada makanisani inatumia Kiswahili; kuna gazeti moja tu la Kiswahili; sehemu
  • za programu redioni na kwenye runinga ni kwa Kiswahili. Lugha inachanganywa mara nyingi na Kiingereza na lugha za maeneo au kikabila. Hata hivyo baada ya rasimu ya katiba mpya kupitishwa mnamo tarehe 4, Agosti 2010, Kiswahili sasa kitakuwa lugha rasmi, sawa na Kingereza.
  • Uganda: imetangazwa kuwa lugha ya kitaifa tangu 2005; iliwahi kuwa lugha ya kitaifa wakati wa utawala wa Idi Amin; wakati wa ukoloni ilifundishwa mashuleni ikaelekea kuwa lugha rasmi pamoja na Kiingereza
  • lakini matumizi haya yalipingwa hasa na Waganda hivyo Waingereza waliacha mipango haya. Ni lugha ya polisi na jeshi hali ambayo imeleta ugumu kwa lugha kukubalika na wanachi wengi kutokana na historia ya utawala wa kijeshi Uganda; watu wengi bado hukumbuka hasa matusi ya wanajeshi waliowatesa wakisema Kiswahili. Lakini kuna maeneo ya Uganda ambako Kiswahili kinatumika na watu wengi kama lugha ya sokoni na barabarani. Wona UBC, WBS tv.

  • Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo: Kiswahili ni kati ya lugha nne za kitaifa, pia lugha ya jeshi katika mashariki ya nchi. Kiswahili kimefika na misafara ya biashara ya watumwana pembe za ndovu kutoka Zanzibar na pwani la Tanganyika. Imeenea zaidi kati ya mchanganyiko wa wafanyakazi kwenye migodi ya Shaba.

Lugha ya kwanza, lugha ya pili



Kiasili Kiswahili kilikuwa lugha ya kwanza tu ya wakazi wa miji ya Waswahili kwenye pwani, katika sehemu za pwani pia kijijini. Baada ya kuenea kimekuwa lugha ya watu wengi mjini hasa Tanzania lakini pia Kenya.
Kimeenea zaidi kama lugha ya mawasiliano na biashara pale ambako watu wa makabila mbalimbali

wanakutana. Pamoja na nchi zinazotajwa hapo juu Kiswahili kinatumika katika Kaskazini ya Msumbiji, Kusini kabisa ya Somalia, Mashariki ya Burundi. Maeneo ya mpaka wa Tanzania kuna pia wasemaji kadhaa huko Malawi na Zambia.

Tanzania na Kenya zilipokea wakimbizi wengi waliojifunza Kiswahili lakini hakuna uhakika kama bado kinatumika wakirudi Rwanda, Sudan au Somalia.


Kimataifa.


Lugha hii leo imekuwa na umuhimu mkubwa duniani kwa jumla, na hasa Africa, kwa sababu ya kuenea kwake nchi mbali mbali, na kukusanya kwake watu wa makabila na nchi kadha wa kadha wakaweza kufahamiana kwa lugha moja, hasa ilivyokuwa ni lugha mojawapo katika lugha kubwa za Africa ambazo zinachukuwa mahala pa lugha za kigeni na Wakoloni, kamaKiarabu, Kiurdu, Kihebrania, Kireno na kadhalika.
Leo, imekuwa inatumiwa katika kusambaza habari katika vituo mbali mbali ulimwenguni kama vile Sauti ya Amerika, BBC, Deutsche Welle, Monte Carlo, na nchi nyenginezo za Uchinana Urusi na Irani na kwengineko. Aidha, imekuwa ni mojawapo ya lugha muhimu zinazofundishwa katika vyuo vikuu nchini Marekani, Uingereza, Ulaya, Urusi, Uchina, na barani Afrika.

Maendeleo ya Kiswahili

Lugha ina maendeleo: inaweza kukua, kukwama au kufa. Athira nyingi hutokea bila mpangilio pale ambako wasemaji wanapokea maneno mapya, wanaacha kutumia maneno mengine au hubadilisha kawaida ya matamshi au sarufi. Haya yote hutokea pia katika uwanja wa Kiswahili.
Kuna mzaha unaosimuliwa hasa Tanzania: Kiswahili kilizaliwa Unguja, kilikua Tanzania Bara, kikafa Kenya na kuzikwa Uganda. Hali halisi Kiswahili kina maendeleo yake katika nchi hizo zote labda zaidi Kongo. Lakini itategemea pia juhudi za serikali kama umoja wa lugha utatunzwa kwa sababu kuna athari nyingi kutoka lugha za kila eneo zinazoingia katika ukuzi wa Kiswahili kwa namna zinazotofauitiana.

Taasisi zinazokuza Kiswahili


Kuna taasisi zinazolenga kukuza na kuimarisha Kiswahili kama vile Taasisi ya Taaluma za Kiswahili (TATAKI) kwenye Chuo Kikuu cha Dar es Salaam pamoja na idara za Kiswahili katika vyuo vikuu vingine vya Kenya na pia Uganda.
Nchini Tanzania kuna Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) na Baraza la Kiswahili Zanzibar (BAKIZA) ilhali nchini Kenya kuna Chama cha Kiswahili cha Taifa (CHAKITA). BAKITA na CHAKITA pamoja na wawakilishi kutoka Uganda wanaandaa kuundwa kwa Baraza la Kiswahili la Afrika Mashariki (BAKAMA).
Uchunguzi wa Kiswahili huendelea pia katika idara za vyuo vikuu vingi duniani, kwa mfano katika Institute National des Langues et Civilisations Orientales, mjini Paris, Ufaransa. Matumizi yake ni kwa njia ya lahaja za Kingwana.

Kamusi za Kiswahili

Makala kuu ya: Kamusi za Kiswahili
Kati ya shughuli muhimu ni kazi ya kukuza msamiati wa Kiswahili yaani kutafuta maneno mapya au kupanusha matumizi ya maneno yaliyopo ili kutaja mambo ya maisha ya kisasa yaliyobadilika. Kutunga kwa kamusi za Kiswahili hupanusha elimu hiyo.







Aisee leo nimmepata somo ambalo nilikuwa nalitafuta miaka mingi sana.
Asante sana mkubwa kwa somo zuri.
 
Katika utangulizi wa kitabu kinachoitwa A Handbook of the Swahili
Language, Askofu Steere alijadali suala la tahajia au hati za maandishi ya
Kiswahili, kwa undani. Karibu maandishi yote ya Kiswahili kabla ya
wakati wake yalikuwa yameandikwa kwa hati za Kiarabu. Mengi kati ya
maandishi hayo yalikuwa ni tenzi na mashairi ya kidini na mambo ya
kawaida yaliyoandikwa kwa lahaja ya kishairi ya Kaskazini ambayo
Steere alishuku iwapo ilieleweka na watu wengi. Ingawa Kiswahili cha
wakati wake kilikuwa kikitumiwa katika kuandikiana barua, Steere
anasema kwamba barua kama hizo zilianzia na salamu kwa Kiarabu na
pia maneno na vifungu vya maneno ya Kiarabu vilikuwa vikichanganywa
na Kiswahili.
 
Katika utangulizi wa kitabu kinachoitwa A Handbook of the Swahili
Language, Askofu Steere alijadali suala la tahajia au hati za maandishi ya
Kiswahili, kwa undani. Karibu maandishi yote ya Kiswahili kabla ya
wakati wake yalikuwa yameandikwa kwa hati za Kiarabu. Mengi kati ya
maandishi hayo yalikuwa ni tenzi na mashairi ya kidini na mambo ya
kawaida yaliyoandikwa kwa lahaja ya kishairi ya Kaskazini ambayo
Steere alishuku iwapo ilieleweka na watu wengi. Ingawa Kiswahili cha
wakati wake kilikuwa kikitumiwa katika kuandikiana barua, Steere
anasema kwamba barua kama hizo zilianzia na salamu kwa Kiarabu na
pia maneno na vifungu vya maneno ya Kiarabu vilikuwa vikichanganywa
na Kiswahili.
 
ni kwamba wasomi wengi
wa Kiswahili waliokuja baada ya Krapf na Steere waliamua kutumia hati
za Kirumi walizokuwa wamezizoea badala ya hati za Kiarabu zilizokuwa
zikitumika kuandika Kiswahili.
 
ni kwamba wasomi wengi
wa Kiswahili waliokuja baada ya Krapf na Steere waliamua kutumia hati
za Kirumi walizokuwa wamezizoea badala ya hati za Kiarabu zilizokuwa
zikitumika kuandika Kiswahili.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom