Kiswahili ni Kibantu au Kiarabu?

Dhehebu la UMCA lilichapisha vitabu kufuatia mtindo uliotumiwa
katika kuchapisha vitabu vya Steere. Misheni wa Kizungu walifanana na
waanzilishi wa uchunguzi wa Kiswahili kwa kuwa ilikuwa rahisi kwao
kutumia hati za Kirumi badala ya zile za Kiarabu. Mkutano wa Dar es
Salaam wa 1925 uliamua kutozitumia hati za Kiarabu pamoja na
konsonanti za Kiarabu kama vile kh. 18* Uamuzi huu wa l925 uliwakasirisha
wengi wakiwa ni pamoja na gazeti la Mombasa, Al-Islah, kama ilivyo-
jadiliwa kwa kireru katika sehemu ifuatayo.

Profesa Carl Meinhof alipohudhuria mkutano wa Mombasa wa 1928,
waliohudhuria walikuwa na nafasi ya kushauriana naye kuhusu othografia
ya Kiswahili. Meinhof alikubaliana na nyingi kati ya tahajia iliyopendeke-
zwa kwa kuwa ilikuwa rahisi bila kutatanisha, isipokuwa katika herufi ch
na ng'. Meinhof alipendekeza c itumiwe badala ya ch. Badala ya kutumia
alama tatu za maandishi (ng') kusimamia sauti moja, alipendekeza
kutumiwa kwa n yenye mkia itumiwe kama ilivyo katika maandishi ya
kifonetiki.

Lakini mashauri haya ya Meinhof hayakukubaliwa. Wasomi wa
Kiswahili wakati huo walijiona kuwa sahihi, na kwamba mapendekezo ya
Meinhof yalifaa tu katika maandishi ya kifonetiki katika isimu lakini
hayakufaa othografia ya kawaida ya Kiswahili.
 
Dhehebu la UMCA lilichapisha vitabu kufuatia mtindo uliotumiwa
katika kuchapisha vitabu vya Steere. Misheni wa Kizungu walifanana na
waanzilishi wa uchunguzi wa Kiswahili kwa kuwa ilikuwa rahisi kwao
kutumia hati za Kirumi badala ya zile za Kiarabu. Mkutano wa Dar es
Salaam wa 1925 uliamua kutozitumia hati za Kiarabu pamoja na
konsonanti za Kiarabu kama vile kh. 18* Uamuzi huu wa l925 uliwakasirisha
wengi wakiwa ni pamoja na gazeti la Mombasa, Al-Islah, kama ilivyo-
jadiliwa kwa kireru katika sehemu ifuatayo.

Profesa Carl Meinhof alipohudhuria mkutano wa Mombasa wa 1928,
waliohudhuria walikuwa na nafasi ya kushauriana naye kuhusu othografia
ya Kiswahili. Meinhof alikubaliana na nyingi kati ya tahajia iliyopendeke-
zwa kwa kuwa ilikuwa rahisi bila kutatanisha, isipokuwa katika herufi ch
na ng'. Meinhof alipendekeza c itumiwe badala ya ch. Badala ya kutumia
alama tatu za maandishi (ng') kusimamia sauti moja, alipendekeza
kutumiwa kwa n yenye mkia itumiwe kama ilivyo katika maandishi ya
kifonetiki.

Lakini mashauri haya ya Meinhof hayakukubaliwa. Wasomi wa
Kiswahili wakati huo walijiona kuwa sahihi, na kwamba mapendekezo ya
Meinhof yalifaa tu katika maandishi ya kifonetiki katika isimu lakini
hayakufaa othografia ya kawaida ya Kiswahili.
 
Othografia ya Kiswahili sanifu haikukosa malalamiko. Kulikuwa na
upinzani na kutoelewana hata kati ya misheni. Kasisi Roehl katika makala
yake "Hali ya lugha katika Afrika Mashariki" (Africa Vol.3, Na.2, 1930),
anaeleza masikitiko yake kwamba Idara ya Elimu huko Dar-es-Salaam
ilikuwa imeanzisha othografia kinyume cha mapendekezo ya wataalamu
wa isimu wa misheni. Roehl analalamika kwamba, kati ya makosa
mengine, othografia inazipa nafasi za kipekee sauti za Kiarabu na
kulazimisha zitumike babala ya kuwapa wazungumzaji wa Kiswahili
uhuru wa kuzitamka kutegemea vile wanavyotamka sauti za lugha yao na
kuziandika sauti hizo vile wanavyozitamka. Roehl 19* anaeleza kwamba
othografia ya Kiswahili yatakikana iwe ya Kiswahili wala si ya Kiarabu au
ya Kiingereza.

Kasisi Roehl anaeleza zaidi kwamba katika kuunda othografia ambayo
inafaa Kiswahili zaidi, isiwe ni Tanganyika pekee ambayo inatoa uamuzi.
Anapendekeza Kenya, Uganda na Congo (Zaire) zihusike ili kuunda
othografia sanifu kwa watu wote wanaotumia Kiswahili. Kama tunavyojua
sasa upungufu mkubwa uliofanywa na nchi za Afrika Mashariki katika
kusanifisha Kiswahili ulikuwa ni kushindwa kushirikisha Zaire katika
shughuli za Kamati ya Kiswahili ya Afrika Mashariki kama alivyo-
pendekeza Kasisi Roehl. Upungufu huo, licha ya jitihada za Ronald
Snoxall, unaeleza kuwepo kwa tofauti kadha kati ya Kiswahili cha Zaire
na Kiswahili sanifu.

Kama inavyofahamika na kuelezwa wazi na wasomi kama vile John
Williamson katika uchambuzi wake wa Kingwana cha maandishi (I.L.C.

---
19* Roehl hakutaja sauti za Kiarabu alizokuwa akimaanisha. Yawezekana alimaanisha sauti
kama vile dh katika fedheha dhulumu na adhibu au gh katika ghadhabu gharika na lugha
ambazo hazipatikani kwingine ila katika maneno yaliyoazimwa kutoka Kiarabu.
 
Jaribio la pili alilofanya Snoxall lilikuwa ni kuwaalika Wabelgiji wawili
kutoka Kongo (Zaire) kuhudhuria mkutano wa Kamati ya Kiswahili ya
Afrika Mashariki mjini Nairobi. Wabelgiji hao waliitikia mwaliko lakini
walishangaa kuona kwamba kamati ya Kiswahili ya Afrika Mashariki
ilikuwa na wajumbe Waafrika. Wabelgiji hawakufikiria kwamba wajumbe
wa Kiafrika kama vile Shaaban Robert wangeweza kuwa wataalam wa
lugha yao. Kwa hivyo Wabelgiji hawakutaka kujiunga na Kamati ya
Kiswahili ya Afrika Mashariki. Hawakuona kama ingekuwa vizuri
kufanya hivyo.

Ingawaje, Kamati ya Kiswahili ya Afrika Mashariki, iliweza kuwajulisha
watawala wa Kongo ya Ubelgiji kwamba tofauti kati ya Kingwana na
Kiswahili sanifu ilikuwa ni matamshi yasiyofuata kanuni za safuri.
 
Canon G. W. Broomfield alijibu makala ya Kasisi Roehl kwa haraka
alipoiandika makala yake "Kukifanya Kiswahili kiwe cha Kibantu"
(Africa Vol.4 Na. 1,1931). Broomfield anaanza kwa kumfahamisha Roehl
kwamba othografia ambayo Roehl anaizungumzia ilifanywa na kamati
mjini Dar es Salaam mwezi Oktoba 1925. Kwa hivyo, anaeleza kwamba
othografia hiyo haikubuniwa na Idara ya Elimu kama alivyodai Roehl.
Anasema kwamba Tanganyika pamoja na Zanzibar zilihudhuria na
kwamba Kenya haikuhudhuria kutokana na kutoelewana hata ingawa
ilikuwa imealikwa.
 
Anaendelea kueleza kwamba othografia iliyoidhinishwa ni ile ambayo
ilikuwa ikitumiwa kwa miaka mingi na UMCA isipokuwa kutokutumiwa
kwa kh. Maneno ambayo hapo awali yalikuwa yakiandikwa kwa kutumia
konsonanti mbili zikifuatana kama vile hatta, milla na marra ingebidi
yatumie konsonanti moja: hata, mila na mara. Kutumiwa kwa kh katika
maneno kama vile khabari, khatia na khalisi, ilibidi yatumie h pekee:
habari, hatia na halisi.

Katika makala hiyo Broomfield anataja pia kwamba mmishonari
mmoja alipinga othografia hiyo katika mkutano wa Dar es Salaamu wa
1925, lakini wanachama watano waliiunga mkono. Maelezo haya yana-
onyesha kwamba ni watu wachache sana waliohusika katika kuamua
suala la othografia. Yawezekana kwamba kanisa la Roehl, misheni ya
Lutheran, haikualikwa kutoa maoni yao au kuhudhuria mkutano huo
wa 1925.
 
Kuhusu msamiati wa Kiarabu katika Kiswahili ambao unasababisha

33

kuwepo na konsonanti za Kiarabu katika othografia ya Kiswahili,
Broomfield anaeleza kwamba maneno yenye asili ya Kiarabu ni maneno
ya Kiswahili. Anadai kwamba maneno yenye asili ya Kiarabu ni maneno
ya Kiswahili hivi kwamba Kiswahili hakijawahi kuwepo bila ya maneno ya
Kiarabu na kwamba hakiwezi kuyaondoa.
 
Pittway anaeleza kwamba kwa kuwa usanifishaji unahusu lahaja tofauti
kusiwe na lahaja yoyote muhimu itakayopuuzwa. Anasema kwamba
maneno ambayo si ya Kiunguja, semi, na miundo ya kisarufi, yastahili
kukubaliwa kutumiwa sambamba na Kiswahili sanifu ili kutajirisha lugha.
Kwa maoni yake, kukubaliwa kwa matumizi hayo ya kilahaja kutasaidia
kufanya Kiswahili kipendwe sana na watu.

Pittway anaendelea kupendekeza kwamba mw inayotangulia u igeuzwe
kuwa mu. Anaeleza kwamba ni kawaida mu kugeuka kuwa mw inapo-
tangulia a,i,e na o, lakini kifonetiki si jambo la kawaida kwa mu kugeuka
kuwa mw inapotangulia u. Pittway alitaka mabadiliko hayo kwa sababu
dhehebu lake la C.M.S. Iililokuwa limeamua kusanifisha Biblia na Kitabu
cha Maombi lilihitaji muongozo. Alisema kwamba mabadiliko hayo
yalikuwa muhimu kwa sababu matumizi ya mu na mw katika vitabu
vilivyopitishwa na Kamati ya Kiswahili ya Afrika Mashariki yaelekea
hayakufuata kanuni yoyote.

Kama ilivyotarajiwa, makala ya Pittway iliyoandikwa mara tu baada ya
kuchapishwa kwa kamusi za Kiingereza-Kiswahili na Kiswahili-Kiingereza,
ilipingwa mara moja. Katika jarida, Bulletin Na. 14 la 1948, Ronald
Snoxall anatahadharisha dhidi ya othografia inayokwenda kinyume cha
kamusi sanifu iliyoichukua kamati miaka mingi kutayarisha. Kwa hivyo
pendekezo la Pittway halipaswi kukubaliwa kuvuruga othografia iliyo-
kubaliwa. Snoxall anapendekeza othografia iliyotumika katika kamusi
ikubaliwe vile ilivyo.
 
2.3 Maoni kuhusu usanifishaji

Kumbukumbu iliyojulikana kwa jina "Kiswahili cha Kisasa", I.L.C.
Bulletin Na. 7 1934, iliandikwa na afisa wa Idara ya Elimu nchini Kenya.
Kumbukumbu hiyo ilipelekewa katibu wa Kamati ya Kiswahili ya Afrika
Mashariki na Mkurugenzi wa Elimu ili ijadiliwe katika mkutano wa
Kamati. Mwandishi ambaye hakutaja jina lake alitahadharisha Kamati
kwamba Kiswahili walichokuwa wakishughulikia kilikuwa kikiendelea
kuwa lugha ngeni kwa Waswahili wenyewe kwa kutengenezewa kanuni
mpya na wageni. Sehemu moja ya kumbukumbu hiyo ilisema hivi:-

"Tumesanifisha Kiswahili, na katika shughuli za kufanya hivyo
yaonekana Kiswahili kimekuwa lugha mpya. Bila shaka sote tunakiri
kwamba kama lugha zingine Kiswahili kitaendelea na kitapanuka

35

katika nyanja za muundo, semi na msamiati kwa kuathiriwa na
ustaarabu wa walowezi. Lakini maendeleo hayo yafaa yatokane na
mawazo ya Waswahili; haifai kuwalazimisha kuyapokea. Lakini
hivyo ndivyo ilivyo; tuko katika harakati za kuwafunza Waswahili
Iugha yao kupitia vitabuni, vingi ambavyo si vya Kiswahili kimuundo
au kimawazo, na ambavyo lugha yake inafanana kidogo sana na
lugha inayozungumzwa. Labda tuna haraka sana kuhepa ukweli
kwamba Waswahili wenyewe wana uwezo wa kurekebisha lugha yao
kufaa mahitaji ya siku hizi na kwamba tayari wanafanya hivyo kwa
haraka ya kustaajabisha. Hivi ndivyo hali ilivyo huko Mombasa na
inaweza kudhihirishwa na wachunguzi wengi. Jambo muhimu sana
ni kwamba jitihada zetu hizi za kupata mwana haramu huyu,
Kiswahili cha Kiingereza, zina matokeo ya kututenganisha na jamii
tunaojaribu kuelimisha. Au tukieleza kwa maneno mengi, tunafikiria
kwa Kiingereza hadi wao wanafikiria kwa Kiswahili na hatuwezi
kuziba pengo hili." (I.L.C. Bulletin Na. 7 1934: 4).
 
Baada ya ufafanuzi uliopewa hapo juu ndio umepata hitimisho kuwa kiswahili ni CHOTARA?.
Mkuu kiswahili ni KIBANTU full stop.
Kwanini kibantu? lugha zote duniani zina asili yake na asili ya kiswahili ni kibantu kwa maana ya kuwa iliasili utamkwaji aka rithm au kwa maana nyingine pronaunciation yake ni ya kibantu licha ya kukopa maneno lukuki kutoka katika kiarabu.
Moja ya sifa ya lugha ni namna unavyotamka maneno pronaunciation, ndio maana mengi ya hayo maneno ya kiarabu hayatamkwi exactly kama waarabu wenyewe wanavyo yatamka na kuyaandika.
Kibantu si kabila ila inamaana ujumla wa makabila yaliyozaliwa katika asili moja yanayo share baadhi ya maneno na utamkwaji na hii inafanya kiswahili kuwa kibantu.
Najua kwanini katika wote waliotoa michango umemkubali zaidi ZOMBA ni kwasababu unaelekea kuipeleka hoja hii ktk udini, ionekane atutaki kusema ni kiarabu kwakuwa kiarabu kina uislam ndani yake(which is not true) naamini ndugu yangu umepitia madrassa unaweza kulinganisha maneno mliyojifunza huko kimatamshi yapo sawa na yaliyotoholewa kuwa kiswahili? mfano sahil na mswahili, ni wazi utamkwaji upo tofauti yaliyotoholewa yanatamkwa ktk tone ya kibantu.
Mwisho mkuu zomba inferiority complex ndio inayo kusumbua wewe na wenzio mnaodhani watu wapo kupinga uislam tu, hapana watu wapo bize kujenga mahospitali, mashule, mavyuo mabenki nk ili watu kama ninyi mpate huduma huko serikali iliposhindwa na si kukomalia kiswahili ni kiarabu, haiwasaidii
Achana Naye Boya huyo!
 
Anaendelea kusema kwamba
wale wanaoitetea hii lugha mpya wanasema kwamba ndiyo ya pekee
inayoweza kueleweka na makabila yasiyokuwa ya Waswahili.
 
Ili kuthibitisha kwamba Waswahili walipinga mtindo huu mpya wa
Kiswahili na othografia yake, mwandishi wa "Kiswahili cha Kisasa"
aliambatisha makala kutoka gazeti la 'Al-lslah' la Mombasa. Makala hiyo
ilikuwa ya Juni 20, 1932 ambayo mwandishi aliishambulia othografia
mpya ya Kiswhili. Othografia iliyokubaliwa kama tulivyoeleza haikuwa
na baadhi ya herufi kama vile kh inayopatikana tu katika maneno
yaliyoazimwa kutoka kwa Kiarabu. Othografia iliyokubaliwa ingekuwa
na h badala ya kh na hii ni mojawapo ya sababu zilizomfanya mwandishi
wa makala ya Al-lslah alalamike. Makala hiyo inasema hivi:

"Ni madhara makubwa tupatayo kwa Kiswahili hiki kilichoharibiwa
ni Wazungu. Kiswahili ni lugha ya watu wa Pwani, nacho hakiwi safi
ella kitanganyikapo na Kiarabu. Tangu kufika Wazungu, wame-
kigeuza na kukiharibu kwa wapendavyo wao; wamepunguza baadhi

36

ya harufu ambazo ni lazima ziwemo katika baadhi ya maneno, na
pengine hubadilika maana kwa kukosekana harufu hizo. Wameitungia
vitabu vya nahau, na pengine hao watungao vitabu hivyo ni
Wazungu wageni hawajui sana lugha hii, na ambao wavitowa
makosa ni Wazungu wa bara, wasiojuwa Kiswahili. Na wakiambiwa
ni mtu wa Pwani kuwa ni makosa, hawakubali ella kile kile chao ..."
(I.L.C. Bulletin Na. 7, 1934: 8).
 
kila hoja kati ya kiswahili no kibantu au kiarabu inategemea na hoja zilizojengwa na mtetezi wa mtu husika. kwa ufupi tu lugha inasifa ya kuzaliwa ,kukua na hata kufa km kilatini basi hizo zote no vyanzo vya lugha. lakini kibantu kina ushahidi wa kiisimu na kihistoria
 
Mwandishi wa "Kiswahili cha Kisasa" anaendelea kutilia nguvu mambo
aliyoyataja kwa kusema kwamba baadhi ya vitabu vilivyochapishwa hivi
karibuni vilikuwa tafsiri ya neno kwa neno ya vitabu vya Kiingereza.
Anasema kwamba matumizi ya kanuni za sarufi yalikuwa yakihimishwa
sana jambo ambalo lilifanya vitabu vilivyochapishwa kuwa sahihi kisarufi,
lakini vilikuwa mbali sana na Kiswahili halisi kwa kuwa sarufi peke yake
haiundi lugha. Anataja upungufu mkubwa wa Kiswahili "kipya". Upungu-
fu huo ni, tafsiri ya neno kwa neno, kuzingatia matumizi ya kanuni za
sarufi bila ya kujali methali na semi pamoja na kutojali tabia ya kishairi ya
Kiswahili. Mwishowe anatoa mifano ya sentensi ambazo zina upungufu
kutokana na vitabu vilivyoandikwa kwa Kiswahili sanifu vilivyokuwa
vikitumika shuleni wakati huo.

Katika jarida hilo hilo la Kamati ya Kiswahili ya Afrika Mashariki,
kufuatia makala hiyo ya "Kiswahili cha Kisasa" kuna jibu lake lililo-
andikwa na Kasisi Canon Broomfield mwandishi wa kitabu kijulikanacho
kama Sarufi ya Kiswahili, ambaye kwa wakati huo alikuwa mhariri
kutoka Zanzibar. Canon Broomfield alikuwa ameombwa na katibu wa
Kamati kumjibu mwandishi wa "Kiswahili cha Kisasa" kwa manufaa ya
wasomaji wa jarida.

Katika jibu lake Canon Broomfield anaonelea kwamba mwandishi wa
"Kiswahili cha Kisasa" ametia chumvi suala la kugeuka kwa Kiswahili
kuwa lugha mpya. Anasema kwamba marekebisho yaliyokuwa yakitokea
yalikuwa hayana budi kuwepo kwa kuwa lahaja moja ndiyo ilichaguliwa
kuwa msingi wa kusanifisha Kiswahili. Kwa hiyo marekebisho yalifanywa
ili kusaidia kutumiwa kwa lahaja hiyo kama lugha ya mawasiliano kote.
Usanifishaji ulihitaji kusomesha Kiswahili hicho ambacho chaonekana
kuwa kipwa. Anaeleza zaidi kwamba Kiswahili sanifu chaonekana kuwa
lugha mpya zaidi katika lahaja zinazotofautiana sana na Kiunguja,
ambacho ndicho msingi wa usanifishaji.

Kuhusu athari za Kiingereza katika Kiswahili, Broomfield anaeleza
kwamba hilo ni jambo lisiloweza kuepukika kwa sababu lugha mbili
zinapotumika katika eneo moja hazina budi kuathiriana na haziwezi
kubaki kuwa safi, pia matokeo ya kuazima huenda yakatajirisha lugha

37
 
dah! Mpka sasa bado cjaelewa kiswahl ni nini mana naona mnanizungusha kama 2livyokuwa 2nazungushana mana cjaelewa kiswahl ni nini labda kama ikiwezekana itakuwa vzur ukinipa hstoria ya kiswahili
Kiswahili sio kibantu wala kiarabu, Kiswahili ni Kiswahili tu
 
Yaonekana wazi kwamba hatimaye Zanzibar italazimika kutumia
vitabu vya shule vilivyoandikwa kwa lugha yao iliyochafuliwa. Hili
ni jambo la kusikitisha hata ingawa yaonekana haliepukiki. Hii ni
gharama kubwa ya kulipa dhidi ya usanifishaji wa Kiswahili. Watu
wa Zanzibar wanaojiona kwamba wanakitumia Kiswahili safi
wanachukizwa na kutumiwa kwa Kiswahili cha bara ambacho kwao
wanakiona kwamba ni lugha iliyoharibiwa. Kuhakikisha kwamba
shule zetu zinatumia Kiswahili sanifu kutakuwa kazi ngumu isiyo-
pendeza na itachukua muda kabla matumizi ya bara hayajakuba-
lika." 21*
 
Jambo muhimu lililosababisha masikitiko ni kule kutumika shuleni
kwa vitabu vilivyotafsiriwa vibaya vikiwa na ithibati ya Kamati ya
Kiswahili ya Afrika Mashariki. Matumizi ya semi na miundo ya Kiingereza
katika vitabu hivyo vilivyotafsiriwa neno kwa neno hayakukanushwa na
Broomfield kama nilivyotaja. Baadhi ya wanakamati pia waliyapigia
makelele matumizi hayo.

Alipokuwa akiandika kuhusu siku hizo za mwanzo wa usanifishaji wa
Kiswahili, Snoxall anatukumbusha kwamba kulikuwa na vitabu vichache
sana na kwamba kamati ilitegemea sana tafsiri za Kiingereza zilizokuwa
zikitafsiriwa na wanakamati wenyewe. Vitabu vya waandishi kama vile
Rivers-Smith, Mkurugenzi wa Elimu Tanganyika, vilifaa sana. Snoxall
anasema kwamba baadhi ya tafsiri hizo zilikuwa za neno kwa neno na
anashangaa iwapo wanafunzi walizielewa. (Snoxall 1982: 3) 22
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom