Je, Fatma Karume amechakachua kiwanja cha Kanisa Znz? Karume stands by daughter...

Shadow

JF-Expert Member
May 19, 2008
2,897
671
Karume stands by daughter in land row Send to a friend Sunday, 02 January 2011 09:11 digg

By Salma Said, Zanzibar

The retired Zanzibar President, Amani Abeid Karume has defended her daughter’s claim that she is the rightful owner of a plot in dispute near a graveyard between her and the Anglican Church in the Isles.

Dr. Karume’s defence of her daughter, Fatma, came a day after worshipers of the Anglican Church stormed the plot at Mfuuni, Mbweni area on Friday and demolished structures being erected there for a building under construction. While Fatma was reported to be the legal owner of the plot, the Anglican Church claimed it was part of the church area since before nationalization, and the land was earmarked for cemetery expansion.

Addressing a press conference with his daughter at his side at his home yesterday, ex-President Karume said his daughter has the title deed for the land issued by the government after she complied with all land allocation requirements, and that she is entitled to build a house there as she wish.

He added that he was the one who took the initiative to protect and maintain the cemetery area from invasion after the Anglican Church leadership and worshipers neglected it for a long time.

According to the ex-President, he and his family played a big role to defend the Anglican properties, including hiring security guards to avoid vandalism, as the owners did not take proper care of the area, and the doors of the church building were left open for a long time.

“The cemeteries that you see there have been under the care of our family for 20 years now…it is me personally and my family members that are taking care of them, and sometimes we hire labourers to weed out grass and clean the entire cemetery,” Karume told reporters.

He expressed his disappointment over the utterances made by the Anglican Church leaders, saying they were over-carried by emotion in instructing the worshipers to invade the disputed piece of land instead of telling them the truth.

Fatma also expressed her dismay over the church’s claims, and alleged that heaps of soil thrown at the cemetery was the work of a Chinese firm authorized by the same church leaders to do so. The firm is construction a hotel nearby, according to Ms. Karume.

Friday invasion of the controversial plot by the Anglican worshipers was preceded by special prayers presided over by Canon Mathew Mhagama who alleged that crosses at the cemetery were being pulled out by land grabbers, and equated the acts with blasphemy

Source: Karume stands by daughter in land row


Church-Karume daughter plot saga takes fresh twist




By Mwinyi Sadallah



2nd January 2011


email.png

Email



printer.png

Print



comment_bubble.png

Comments








KarumeDaughter(1).jpg

Former Zanzibar President, Amani Abeid Karume, flanked by his daughter Fatma, briefing journalists on a dispute between his daughter and the Anglican Church.


A dispute in which Fatma, daughter of the immediate former Zanzibar President Amani Abeid Karume, is contesting ownership of a piece of land on the main island, Unguja, took a dramatic turn yesterday, when the father visited the site.
Fatma commissioned construction works on the plot recently, but it has transpired that she doesn’t have official building permits. The Church, on its part, claims that it is the long-time, rightful owner of the piece of land.
A high-level meeting was held yesterday to resolve the dispute but it didn’t yield the anticipated outcome.
Those in attendance included Second Vice President Ambassador Seif Ali Iddi, leaders from Zanzibar Municipal Council, land department and a delegation of five people from the Zanzibar Diocese of Anglican church led by retired bishop John Ramadhani.
Information that leaked from the tripartite meeting stated that officials from Zanzibar urban authorities found themselves in a tough time after they were required to explain whether or not they issued building permits on the disputed plot.
“As far as we are concerned we have not issued any building permit and this matter is strange to us,” an official was heard as saying while quoting officials from Zanzibar urban municipality.
Secretary of the Zanzibar Diocese of Anglican Nuhu Salanya confirmed that the meeting was held, in the wake of a police ban on a planned demonstration by Church worshippers to protest against what they described as an invasion of their property. Salanya, however, declined to disclose what was discussed at the meeting.
Recently, Zanzibar’s Minister for Lands Ali Juma Shamhuna nullified 20 title deeds of various government officials who owned plots in Mombasa area in Zanzibar urban, including the plot that was owned by CCM Deputy Secretary General Saleh Ramadhan Feruz.



SOURCE: GUARDIAN ON SUNDAY
 
Karume ametia aibu Zanzibar

picture-11.jpg

Na Jabir Idrissa - Imechapwa 05 January 2011


Kalamu ya Jabir
NILIPOSIKIA Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Idi anaapa kwamba serikali mpya haitakubali ufisadi wa ardhi vyovyote vile, nilijua safari ngumu imeanza.

Ni safari ngumu na sina shaka italazimu Balozi Seif mwenyewe, Rais aliyemteua, Dk. Ali Mohamed Shein na waziri anayehusika na usimamizi wa raslimali ya ardhi, Ali Juma Shamhuna, wafunge mikanda.

Bali itakuwa safari ngumu kwa jumla maana ni lazima baraza zima la mawaziri liamue kwani watalaumiwa na wale watakaoguswa na “operesheni futa ufisadi wa ardhi.”

Niliposikia baadaye kuwa baadhi ya viongozi waandamizi wa serikali na Chama Cha Mapinduzi (CCM) wametakiwa kusalimisha hati za kumiliki ardhi kifisadi, nikajua kweli hakuna kisichowezekana.

Kufikia leo, taarifa zisizokanushika zinasema serikali imeshafuta zaidi ya hati 20 za kumiliki viwanja kwenye maeneo ambayo kwa asili yake ni ya wazi – ambazo ilizitoa huko nyuma.

Raslimali ya ardhi imekuwa matatizoni sana katika kipindi cha miaka 20 sasa kote Unguja na Pemba. Kumekuwa na malalamiko mengi ya makundi na watu binafsi kudai wameporwa ardhi.

Lakini katika kipindi cha miaka 10 kilichoishia Oktoba mwaka jana, malalamiko hayo yalizidi. Uporaji ulisikika kila mahali na viongozi wa juu wakitajwa kuhusika.

Tukio la wazi likahusisha vigogo waliovamia shamba la mzee Abdalla Shariff wa Shakani, nje ya mjini Zanzibar. Na licha ya mzee huyo kushinda kesi hadi mahakama ya rufani, hajarudishiwa ardhi aliyoporwa.

Mawaziri, makatibu wakuu na wabunge walihusishwa. Ni wao walifanikiwa kutumia madaraka kushawishi serikali ikatae haki na mpaka leo mwenye haki, Mzee Shariff, akifungwa mdomo.

Mara kadhaa polisi wa kutuliza ghasia walipelekwa kukaza hukumu lakini walirudi bila ya kutekeleza walichotakiwa; na sababu ikawa, “Pale kuna watu wamebeba mawe na bakora wametuzuia.”

Aibu ilioje, polisi kuzuiwa kufanya kazi halali na wanawake na watoto wadogo waliobeba bakora!

Tukio lililotokea wiki iliyopita linathibitisha ukubwa wa tatizo la ufisadi wa ardhi Zanzibar. Kule kuhusisha viongozi wa ngazi za juu wa utawala kumeshtua.

Katikati ya mgogoro wa ardhi ya Kanisa la Anglikana unaohusisha eneo la asili la kanisa hilo kijijini Mbweni Mfuuni, nje ya mji, ni familia ya Mzee Abeid Amani Karume, kiongozi mtukuka aliyeuawa kwa risasi 7 Aprili 1972.

Mkuu wa familia sasa ni Amani Abeid Karume, rais mstaafu wa Zanzibar aliyeongoza kwa miaka kumi serikali ya awamu ya sita – 2000/2010.

Bila ya kutarajia, mstaafu Karume amembeba mwanawe wa kike, Fatma Amani Abeid Karume, akisema anamiliki kihalali kiwanja kilichopo eneo la Kanisa, Mbweni Mfuuni.

Anasema Fatma anazo nyaraka halali. Kupitia picha za televisheni nikashuhudia Karume akiinua nyaraka na kuzionyesha kwa waandishi “mahsusi” walioitwa na familia hiyo ili kupaisha sauti yao.

Sikuwepo. Kwa bahati mbaya pia, waandishi ninaowaamini kikazi hawakuitwa. Sijapata simu ya Fatma, wala ya rais mstaafu Karume.

Ningeuliza, “Bibi Fatma umepata lini hati ya kumiliki kiwanja hapa?” Ningetaka kunukuu kumbukumbu za hati hiyo ikiwemo tarehe iliyotolewa, nani aliidhinisha na ilitolewa kwa maombi gani?

Vyanzo vyangu vinanieleza kumbe Fatma amepata hati mwaka 2009 – mwaka juzi. Hati ilitolewa baada ya shinikizo nyingi na maofisa wa Idara ya Ardhi na Usajili walikimbizana kila mmoja akiogopa kujiingiza. Wanasema ulikuwa “mtego mbaya.”

Ni kama vile siku walipotakiwa kupima eneo la Kibweni, mita chache kutoka nyumba ya mkereketwa mkuu wa CCM, mfanyabiashara Mohamed Raza Dharamsi na pembeni mwa Ikulu ndogo ya Kibweni. Walitakiwa kupima kwa nguvu.

Lakini kiwanja kinachobishaniwa Mbweni ni cha Kanisa la Anglikana, lenye eneo kubwa tangu karne ya 18. Tukumbuke Waanglikana ndio wakristo wa kwanza kuhamia Zanzibar. Walinunua maeneo Unguja na Pemba; hili la Mbweni ni eneo mojawapo.

Kwa sababu za kibinafsi zaidi kuliko haki, hawajapewa hatimiliki licha ya kuhangaikia kwa muda mrefu hasa baada ya kuona hatari ya wajanja kutwaa maeneo yao.

Mpaka leo wanalalamika hawajalipwa fidia kwa serikali kuchukua eneo lao Madungu, Chake Chake, Pemba palipojengwa Posta wala yalipo Makao Makuu ya Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba - Wete.

Hawajatimiziwa ahadi ya wizara inayohusika na raslimali ya ardhi kuwa itatoa hati hizo. Wizara ilishindwa kutoa hati mpaka uporaji umefanyika.

Anaposimama baba hadharani kutetea mwana eti “anamiliki kihalali kiwanja” katika eneo la Kanisa, wakati eneo la mzee Karume – ambalo lenyewe lilitokana na kumegwa eneo la Kanisa – limo ndani ya ukuta uliojengwa kwa fedha nyingi, inasikitisha.

Ukweli ni kwamba kiwanja anachodai Fatma ni chake kipo nje ya ukuta wa eneo kubwa la familia yao. Wala Kanisa halina mgogoro wowote na anayeitwa mwekezaji wa hoteli pembeni na karibu na ufukwe.

Kama Fatma hana nyaraka za kuuziwa kiwanja na Kanisa, aseme amepataje uhalali huo. Isije ikawa alipata katika ule mtindo wa chukua chako mapema ulioshamiri kipindi cha miaka 20 nyuma.

Wakubwa na rafiki zao “walichukua, wakaweka waa” kwa kila walichokitaka, siyo utawala tu wakati wa uchaguzi. Nani mwenye ubavu wa kulalamika wakati ule? Yalimkuta kijana wa Kipilipilini Chwaka alipolalamika kuporwa ardhi ya kurithi na kutumiwa kujengea kituo cha petroli cha Gapco, alionyeshwa moto.

Amefunguliwa kesi ya jinai na jamhuri, na mwandishi aliyemsaidia kuchapisha malalamiko yake, Mwinyi Sadallah, akajumuishwa. Eti wachochezi. Hatimaye mpaka leo ukiingia mwaka wa tatu ushahidi tu haujamalizika.

Haya ni matukio yanayokera maana yanadhoofisha utawala bora katika nchi yenye watu wastaarabu.

Sasa hii inayomhusu rais mstaafu Karume ni kashfa nzito. Inaashiria mwanzo wa kufumuka mambo mengi kwa sababu ipo kesi mahakamani inamhusu mjomba wa Fatma, Mansour Yusuf Himid.

Mansour alikuwa waziri kwa miaka kumi ya utawala wa Amani Karume. Sasa ni Waziri wa Kilimo na Maliasili. Ni mmoja wa walioshindwa kesi na Mzee Shariff kule Shakani.

Anatajwa katika kesi nyingine iliyopo Mahakama ya Ardhi akidaiwa kutwaa ardhi visivyo. Uamuzi wa kesi hii ukitolewa, ukweli utajulikana.

Mtoto wa rais mstaafu Karume anatajwa kumiliki kwa hila eneo kubwa la ardhi kijijini Muyuni, Wilaya ya Kusini Unguja, ambako wenyeji wakitumia kwa shughuli za kilimo.

Walilalamika lakini walinyamazishwa kwa mbinu za kidola. Wamenyamaza sawa, lakini hawajaridhika maana wangali wanadai ni haki yao, hawakushirikishwa na wamezuiwa kutumia eneo la asili kwa shughuli zao.

Nahisi itakuwa shida. Mkoa wa Kusini na Kaskazini Unguja kuna malalamiko kwa familia hii kuhusu ardhi. Kuna malalamiko kisiwani Pemba kuhusu hayohayo. Mtandao wa WikiLeaks umeyaona. Mimi si mtabiri, lakini naona mengi yatafumuka.

Gazeti toleo lenye makala hii
0
Average:
 
Back
Top Bottom