TBOSS
JF-Expert Member
- Feb 13, 2017
- 252
- 376
Tukiwa kwenye harakati za kumuuguza mke wangu mpendwa,Mama alikuwa msaada mkubwa kwangu na kwa mke wangu,siku hiyo nimetoka hospitali kumuona mke wangu,nafika nyumbani nikaambiwa mama ananiita kwake,nikaenda na kumkuta ana huzuni sana,akaniuliza tu mgonjwa anaendeleaje?nikamwambia anaendelea vizuri sana,akaniambia "moyo wangu unaniuma sana nimeshindwa kwenda kumuona,miguu yangu haifanyi kazi kabisa,ila naamini tu Mungu ATANIKUTANISHA naye siku moja" niliondooka kwake saa tano usiku,tukaagana,akaenda kulala na mimi nikaenda kwangu,siyo mbali sana! Usiku wa kama saa nane nikapigiwa simu na mtu aliyekuwa hospitali alipokuwa amelazwa mke wangu!akaniambia hali ya mke wangu imekuwa mbaya ghafla,hivyo kama nitaweza niende asubuhi,hospitali yenyewe ilikuwa mkoa mwingine, nikakosa amani kabisa! Kufika saa kumi hivi usiku nikapigiwa simu tena! Roho ikapasuka paah!! Kuicheki ni mdogo wangu anayeishi na mama,nikapokea,akawa analia huku akiniambia "njoo nyumbani haraka" nikatoka mbio,nikafika na kumkuta mdogo wangu nje ana haha na kulia,nika muuliza kuna nini?akanikumbatia huku akilia na kuniambia niingie ndani,nikaingia mbio,nikaenda haraka chumbani kwa mama! Nikamkuta amelala huku anakoroma kwa sauti ya chini kabisa nikajaribu kkumwamsha kwa kumtikisa! Hakujibu,wala hakuamka,Akaondoka hivyo!! Tukaandaa mazishi na kumzika hapo hapo nyumbani huku mke wangu akiwa bado hospitali na akiwa na hali mbaya,siku tumezika mmke wangu ni kama alipata nafuu ghafla na kuongea na dokta aniambie nimpe mama simu aongee naye,nikamwambia mama ametoka kidoogo,akasisitiza sana,maana siku mama yangu anazikwa mimi nilienda hospitali asubuhi na mke wangu akawa anaongea kwa tabu akinilaumu kwa kumnyima kuongea na mama,akasema kuna kitu anataka amwambie mama ili mmama aniambie mimi,akasema "mimi nakufa,ila kuna jambo nataka nimwambie mama kwa ajili yako, basi tukamzika mama!! Mke wangu hakujua kuwa mama amefariki hadi siku moja alipoambiwa na mgonjwa mwingine aliyefika hospitalini akkitokea huku tunakoishi siku hiyo mke wangu alilia sana,akaniita,nikaenda,akalalamika kwa nini Mungu amemchukua Mama aliyekuwa mzima na mwenye aliyempenda sana na kumuacha yeye akiteseka kitandani kwa miaka!! Nimekuwa na wakati mgumu toka hapo ndugu zangu! Wiki mbili baada ya kumzika mama mke wangu mpenzi naye akafariki!! Lile neno alillotaka kumwambia mama aliniambia mimi mwishoni,nikamzika nyumbani pembeni ya mama aliyependa na waliopendana sana!! Mimi bado nipo kwenye msiba mzito!! Ni wiki tatu tu zimepita tangu nimzike mke wangu,mke wangu aliugua saratani ya ziwa(breast cancer) naandika huku machozi yananimwagika.
Pole sana, samahani mlifanikiwa kupata watoto !?