Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,064
- 22,757
NEC imeingilia uhuru wa Bunge-Slaa
Wednesday, 19 August 2009
Na Waandishi wetu - Majira.
UAMUZI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa kuwakata makali wabunge wake kwa lengo la kupunguza mashambulizi dhidi ya Serikali, umetafsiriwa kuwa ni uvunjaji sheria za nchi na ni kosa la jinai kwani ni kuingilia wajibu wa Bunge.
Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Wilbrod Slaa, alipozungumza na waandishi wa habari makao makuu ya chama hicho, Dar es Salaam jana.
Alisema; "Ibara ya 100 ya Katiba inaeleza kuwa uhuru wa Bunge hauwezi kuingiliwa na chombo chochote, wanapowazuia wabunge asiongelee suala fulani wanaingilia uhuru wa Bunge."
Kauli hiyo ya Dkt. Slaa imekuja siku moja tangu Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM ikiwa imeunda kamati ndogo ya watu watatu kuchunguza kiini cha mashambulizi ya wabunge dhidi ya Serikali, itakayoongozwa na Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi, ikiwajumusiha Makamu wa Mwenyekiti wa CCM, Bw. Pius Msekwa na Mjumbe wa Kamati Kuu, Bw. Abdulrahman Kinana.
Akizungumzia tishio lililokuwa likimkabili Spika wa Bunge, Bw. Samuel Sitta, kiasi cha kufikia hatua wajumbe NEC kutaka anyang'anywe kadi ya CCM kwa madai ya kushindwa kusaidia chama chake bungeni, Dkt. Slaa alijibu;
"Acha Sitta ashughulikiwe mimi sina huruma na hilo, akitaka kuwa huru asijadiliwe kwenye vikao vya chama basi ajiengue kwenye ujumbe wa NEC...Katiba ya nchi haimtaki awe mjumbe wa NEC na CC (Kamati Kuu) ya CCM."
Alisema walishamtaka aache kuhudhuria vikao vya Kamati ya Uongozi ya CCM inayotokana na wabunge, lakini alishindwa kufanya hivyo.
Alidai wabunge wamekuwa wakimpelekea hoja zao ili zijadiliwe na Bunge, lakini anazipeleka kwenye Kamati ya Uongozi ya Wabunge wa CCM na kujadiliwa kwanza.
Alitolea mfano hoja aliyotaka kuwasilisha bungeni ya watuhumuwa wa ufisadi aliowataja katika mkutano wa Mwembe Yanga kuwa ilikwamishwa na Kamati ya Wabunge wa CCM baada ya kupelekwa huko na Spika pamoja na watu wa Usalama.
"Kama anataka kushughulikia ufisadi basi ajitose, aache kushughulikia vita hiyo nusu nusu," alisema na kuongeza kuwa kama asingekuwa ndani ya CCM Bunge lingemlinda.
Alisema kwa sasa CCM inajivunia kipengele kimoja kilichopo kwenye kanuni za Bunge kinachoeleza kuwa kamati za vyama zinatambuliwa ndani ya bunge.
Akizungumzia suala hilo, Mwanasheria wa CHADEMA na wakili wa kujitegemea, Bw. Tindu Lissu, alisema ofisi ya Spika inatakiwa kulindwa vinginevyo chombo hicho muhimu kitakuwa kinatelekezwa.
Kuhusu uamuzi wa NEC kuwakata makali wabunge wa CCM, Bw. Lissu alisema; "Kilichofanyika ni uvunjaji wa sheria."
Aliongeza kuwa uhuru wa mawazo na majadiliano ndani ya Bunge hautakiwi kuhojiwa na chombo chochote kile hata kama ni mahakama.
Bw. Lissu alisema wajibu wa Bunge ni kutunga sheria na kuidhibiti Serikali, ndiyo maana lina mamlaka ya kumuondoa Rais, Waziri Mkuu au Waziri yeyote kwenye wadhifa wake, endapo halitaridhika na utendaji kazi wake.
Alisema ili Bunge liweze kutekeleza wajibu huo, linahitaji uhuru na kama utaondolewa basi Tanzania itakuwa imerudi kwenye mfumo ule unaofanana na wa chama kimoja.
"Tuna wajibu kama wananchi kutetea hadhi ya Bunge, tukiruhusu wabunge watishwe basi hatutakuwa na Bunge lenye uwezo wa kudhibiti Serikali,"alisema Bw. Lissu. Alisema sheria ya Bunge ya mwaka 1998 imeweka kinga na madaraka ya Bunge.
Akinukuu sheria hiyo, Bw. Lissu alisema; "Sheria inasema mtu atakayefanya vitendo ambavyo vinapunguza madaraka ya bunge atakuwa ametenda kosa la jinai."
"NEC ya CCM imetenda kosa la jinai kama kuna mtu wa kwenda kuwafungulia RB kwa Manumba (Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jina DCI Robert Manumba) afanye hivyo lakini na yeye hawezi kutusaidia kwa kuwa na yeye ni CCM.
Alisema kwa mwelekeo wa sasa Bunge litaanza kufanyakazi kwa namna ambayo CCM inataka. Aliongeza kuwa kwa mwenendo wa aina hiyo mijadala kama ya Richmond, Buzwagi na EPA isingeweza kuibuliwa ndani ya Bunge.
Akizungumzia sakata la mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira, Bw. Lissu alisema Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Bw. Benjamin Mkapa, hawezi kusafishwa tuhuma hizo na vikao vya NEC na CC kwa kuwa alijimilikisha mgodi huo mali ya umma akiwa rais, hivyo alikiuka sheria ya maadili ya viongozi.
"Hilo ni kosa la jinai na mahala pake ni mahakamani na siyo kujadiliwa na NEC au CCM," alisema na kuongeza;
. "Kutwaa mali ya umma siyo sehemu ya mamlaka ya rais...ni kwa nini alichukua mali ya umma na kuifanya ya kwake?"Alihoji Bw. Lissu.
Alisema Bw. Mkapa ameshindwa kufikishwa mahakamani kwa kuwa wale wanaosimamia sheria nao wanatakiwa kufikishwa mahakamani.
Akieleza kuhusu hilo, Dkt. Slaa hawataacha kupiga kelele kulalamikia kitendo cha Bw. Mkapa kujimilikisha mgodi wa Kiwira. "Hatutakaa kimya, tutazuiwa kumuongelea ndani ya Bunge ,lakini mahakama ya mwanasiasa siyo bungeni ni kwa wananchi," alisema.
Aliongeza kuwa; "Ukiona chama kinawazuia wabunge wasizungumzia kitu chochote basi hicho kinakaribia kufa," alisema.
Alielezea mshangao wake kuhusiana na Serikali kutaka kuchukua mgodi wa Kiwira na kuwarejea wamiliki wake akiwemo Bw. Mkapa fedha zao.
Alisema Serikali inaendelea na mchakati huo wakati haijulikani waliokuwa wafanyakazi wa mgodi huo fedha zao kiasi cha dola milioni saba wanazodai kama malimbikizo ya NSSF watazipataje.
Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF) Profesa Ibrahim Lipumba, alidai kuwa NEC imedhihirisha kuwa CCM ni chama cha mafisadi na wale wote wanaopambana na vita hiyo ni bora wakang'atuka ili kuwamaliza mafisadi hao.
Akizungumza na gazeti hili, Prof. Lipumba alikwenda mbali zaidi na kudai kuwa Rais Jakaya Kikwete hawezi kupambana na mafisadi waliomo ndani ya chama hicho kwani ndio waliounda kundi la wanamtandao lililomweka madarakani na kuwa lina nguvu ndani ya chama hicho.
Profesa Lipumba alisema kuwa kama kweli Spika Sitta na wabunge wengine wanataka kupambana kidete na ufisadi lazima watoke CCM kwani inaonekana kete za mafisadi wa CCM ni kali.
Wednesday, 19 August 2009
Na Waandishi wetu - Majira.
UAMUZI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa kuwakata makali wabunge wake kwa lengo la kupunguza mashambulizi dhidi ya Serikali, umetafsiriwa kuwa ni uvunjaji sheria za nchi na ni kosa la jinai kwani ni kuingilia wajibu wa Bunge.
Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Wilbrod Slaa, alipozungumza na waandishi wa habari makao makuu ya chama hicho, Dar es Salaam jana.
Alisema; "Ibara ya 100 ya Katiba inaeleza kuwa uhuru wa Bunge hauwezi kuingiliwa na chombo chochote, wanapowazuia wabunge asiongelee suala fulani wanaingilia uhuru wa Bunge."
Kauli hiyo ya Dkt. Slaa imekuja siku moja tangu Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM ikiwa imeunda kamati ndogo ya watu watatu kuchunguza kiini cha mashambulizi ya wabunge dhidi ya Serikali, itakayoongozwa na Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi, ikiwajumusiha Makamu wa Mwenyekiti wa CCM, Bw. Pius Msekwa na Mjumbe wa Kamati Kuu, Bw. Abdulrahman Kinana.
Akizungumzia tishio lililokuwa likimkabili Spika wa Bunge, Bw. Samuel Sitta, kiasi cha kufikia hatua wajumbe NEC kutaka anyang'anywe kadi ya CCM kwa madai ya kushindwa kusaidia chama chake bungeni, Dkt. Slaa alijibu;
"Acha Sitta ashughulikiwe mimi sina huruma na hilo, akitaka kuwa huru asijadiliwe kwenye vikao vya chama basi ajiengue kwenye ujumbe wa NEC...Katiba ya nchi haimtaki awe mjumbe wa NEC na CC (Kamati Kuu) ya CCM."
Alisema walishamtaka aache kuhudhuria vikao vya Kamati ya Uongozi ya CCM inayotokana na wabunge, lakini alishindwa kufanya hivyo.
Alidai wabunge wamekuwa wakimpelekea hoja zao ili zijadiliwe na Bunge, lakini anazipeleka kwenye Kamati ya Uongozi ya Wabunge wa CCM na kujadiliwa kwanza.
Alitolea mfano hoja aliyotaka kuwasilisha bungeni ya watuhumuwa wa ufisadi aliowataja katika mkutano wa Mwembe Yanga kuwa ilikwamishwa na Kamati ya Wabunge wa CCM baada ya kupelekwa huko na Spika pamoja na watu wa Usalama.
"Kama anataka kushughulikia ufisadi basi ajitose, aache kushughulikia vita hiyo nusu nusu," alisema na kuongeza kuwa kama asingekuwa ndani ya CCM Bunge lingemlinda.
Alisema kwa sasa CCM inajivunia kipengele kimoja kilichopo kwenye kanuni za Bunge kinachoeleza kuwa kamati za vyama zinatambuliwa ndani ya bunge.
Akizungumzia suala hilo, Mwanasheria wa CHADEMA na wakili wa kujitegemea, Bw. Tindu Lissu, alisema ofisi ya Spika inatakiwa kulindwa vinginevyo chombo hicho muhimu kitakuwa kinatelekezwa.
Kuhusu uamuzi wa NEC kuwakata makali wabunge wa CCM, Bw. Lissu alisema; "Kilichofanyika ni uvunjaji wa sheria."
Aliongeza kuwa uhuru wa mawazo na majadiliano ndani ya Bunge hautakiwi kuhojiwa na chombo chochote kile hata kama ni mahakama.
Bw. Lissu alisema wajibu wa Bunge ni kutunga sheria na kuidhibiti Serikali, ndiyo maana lina mamlaka ya kumuondoa Rais, Waziri Mkuu au Waziri yeyote kwenye wadhifa wake, endapo halitaridhika na utendaji kazi wake.
Alisema ili Bunge liweze kutekeleza wajibu huo, linahitaji uhuru na kama utaondolewa basi Tanzania itakuwa imerudi kwenye mfumo ule unaofanana na wa chama kimoja.
"Tuna wajibu kama wananchi kutetea hadhi ya Bunge, tukiruhusu wabunge watishwe basi hatutakuwa na Bunge lenye uwezo wa kudhibiti Serikali,"alisema Bw. Lissu. Alisema sheria ya Bunge ya mwaka 1998 imeweka kinga na madaraka ya Bunge.
Akinukuu sheria hiyo, Bw. Lissu alisema; "Sheria inasema mtu atakayefanya vitendo ambavyo vinapunguza madaraka ya bunge atakuwa ametenda kosa la jinai."
"NEC ya CCM imetenda kosa la jinai kama kuna mtu wa kwenda kuwafungulia RB kwa Manumba (Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jina DCI Robert Manumba) afanye hivyo lakini na yeye hawezi kutusaidia kwa kuwa na yeye ni CCM.
Alisema kwa mwelekeo wa sasa Bunge litaanza kufanyakazi kwa namna ambayo CCM inataka. Aliongeza kuwa kwa mwenendo wa aina hiyo mijadala kama ya Richmond, Buzwagi na EPA isingeweza kuibuliwa ndani ya Bunge.
Akizungumzia sakata la mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira, Bw. Lissu alisema Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Bw. Benjamin Mkapa, hawezi kusafishwa tuhuma hizo na vikao vya NEC na CC kwa kuwa alijimilikisha mgodi huo mali ya umma akiwa rais, hivyo alikiuka sheria ya maadili ya viongozi.
"Hilo ni kosa la jinai na mahala pake ni mahakamani na siyo kujadiliwa na NEC au CCM," alisema na kuongeza;
. "Kutwaa mali ya umma siyo sehemu ya mamlaka ya rais...ni kwa nini alichukua mali ya umma na kuifanya ya kwake?"Alihoji Bw. Lissu.
Alisema Bw. Mkapa ameshindwa kufikishwa mahakamani kwa kuwa wale wanaosimamia sheria nao wanatakiwa kufikishwa mahakamani.
Akieleza kuhusu hilo, Dkt. Slaa hawataacha kupiga kelele kulalamikia kitendo cha Bw. Mkapa kujimilikisha mgodi wa Kiwira. "Hatutakaa kimya, tutazuiwa kumuongelea ndani ya Bunge ,lakini mahakama ya mwanasiasa siyo bungeni ni kwa wananchi," alisema.
Aliongeza kuwa; "Ukiona chama kinawazuia wabunge wasizungumzia kitu chochote basi hicho kinakaribia kufa," alisema.
Alielezea mshangao wake kuhusiana na Serikali kutaka kuchukua mgodi wa Kiwira na kuwarejea wamiliki wake akiwemo Bw. Mkapa fedha zao.
Alisema Serikali inaendelea na mchakati huo wakati haijulikani waliokuwa wafanyakazi wa mgodi huo fedha zao kiasi cha dola milioni saba wanazodai kama malimbikizo ya NSSF watazipataje.
Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF) Profesa Ibrahim Lipumba, alidai kuwa NEC imedhihirisha kuwa CCM ni chama cha mafisadi na wale wote wanaopambana na vita hiyo ni bora wakang'atuka ili kuwamaliza mafisadi hao.
Akizungumza na gazeti hili, Prof. Lipumba alikwenda mbali zaidi na kudai kuwa Rais Jakaya Kikwete hawezi kupambana na mafisadi waliomo ndani ya chama hicho kwani ndio waliounda kundi la wanamtandao lililomweka madarakani na kuwa lina nguvu ndani ya chama hicho.
Profesa Lipumba alisema kuwa kama kweli Spika Sitta na wabunge wengine wanataka kupambana kidete na ufisadi lazima watoke CCM kwani inaonekana kete za mafisadi wa CCM ni kali.