Je, CCM Itatawala Milele Au?

Status
Not open for further replies.
absolutely! kwa sababu hatujaathirika moja kwa moja na hayo yote unayoyasema. Sasa hivi tunaishi kwa misingi kuwa endapo mimi na familia yangu tumepata chakula cha jioni, na watoto waemeenda shule na tuna nguo na mahali pa kulala hayo mengine mimi sijali. Hatukasirishwi na kuona mwingine anahangaika na mahitaji yake ya kila siku.

Wakati mwalimu aliongoza kwa sera ya "kabla wachache hawajishi katika anasa, wengi wapate mahitaji yao muhimu" leo hii kina Kikwete wanahakikisha "wachache wanazidi kuishi katika anasa huku wengi wakiahidiwa mahitaji yao muhimu". Matokeo yake, leo hii tunategemea wageni kutuchimbia visima; tunatarajia watu binafsi kuendesha shule za msingi na sekondari, n.k

Watu wakikataa kuridhika na wakatamani makubwa zaidi, mazuri zaidi na mema zaidi kwa sababu wanastahili wataona umuhimu wa cha kufanya. Lakini tukipewa kanga na tsheti huku tunaburudishwa na wimbo wa "nambari wani eeh" tunaridhika na kufurahia kuwa na sisi tumepata vikofia vya chama!

Mkjj umesema kitu kikubwa sana hapo. Nimeliona hili kwa marafiki wengi sana ambao ukiongelea matatizo yanayotokana na uongozi mbovu nchini mweru wanakuwa hawakuelewi kabisa na kutaka kukuonyesha kwamba hujui unaongea nini basi watakwambia "Wewe unaishi nje hali hapa nyumbani si mbaya kiasi hicho usiyaamini sana yote unayoyasikia au kusoma kwenye magazeti." Wengi wa hawa ni wale ambao wameridhika na maisha yao wana mishahara minono wanaweza kuafford shule za kulipia wana magari wengine zaidi mawili. Mimi huwaambia kwamba mficha ugonjwa maradhi yatamuumbua kwa maana kwamba ncghi yetu ina matatizo makubwa sana na Watanzania wengi wamekata tamaa ya maisha kutokana na utendaji mbovu wa Vuongozi wa juu ndani ya Serikali ambao wameweka mbele maslahi yao au ya CCM na kuwasahau kabisa mabilioni ya Watanzania ambao wanaishi maisha ya dhiki ya kutisha, siku ambayo hawa waliokata tamaa ya maisha wakisema sasa basi liwalo na liwe hata hao ambao wana maisha mazuri basi maisha yao yatakuwa hatarini na watajuta kwa nini walifumbia macho uongozi mbovu kwa miaka mingi nchini kwetu.
 
absolutely! kwa sababu hatujaathirika moja kwa moja na hayo yote unayoyasema. Sasa hivi tunaishi kwa misingi kuwa endapo mimi na familia yangu tumepata chakula cha jioni, na watoto waemeenda shule na tuna nguo na mahali pa kulala hayo mengine mimi sijali. Hatukasirishwi na kuona mwingine anahangaika na mahitaji yake ya kila siku.

Wakati mwalimu aliongoza kwa sera ya "kabla wachache hawajishi katika anasa, wengi wapate mahitaji yao muhimu" leo hii kina Kikwete wanahakikisha "wachache wanazidi kuishi katika anasa huku wengi wakiahidiwa mahitaji yao muhimu". Matokeo yake, leo hii tunategemea wageni kutuchimbia visima; tunatarajia watu binafsi kuendesha shule za msingi na sekondari, n.k

Watu wakikataa kuridhika na wakatamani makubwa zaidi, mazuri zaidi na mema zaidi kwa sababu wanastahili wataona umuhimu wa cha kufanya. Lakini tukipewa kanga na tsheti huku tunaburudishwa na wimbo wa "nambari wani eeh" tunaridhika na kufurahia kuwa na sisi tumepata vikofia vya chama!

Mzee Mwanakijiji pamoja na majibu yako mazuri lakini bado nikuulize:Hivi Tanzania kuna middle class?Asilimia ngapi vile?Na masikini kwa kiwango cha chini ya dola moja kwa siku ni asilimia ngapi vile?
Kwa mtazamo wangu naona wengi ndiyo wanaathirika moja kwa moja na huu ubinafsi wa kina Chenge na Ndulu manake masikini ndiyo wengi na siyo vijijini tu hata mijini kama Dar Es Salaam ambayo mara nyingi ndiyo inatumika kama kioo cha Tanzania bado kuna watu wanaishi maisha ya dhiki sana.Sasa tatizo letu nini mpaka tukaridhika kiasi hiki hata Tanesco wanapandisha bei ya umeme kisa kuilipa Richmond lakini tunaishia kulalamika tu na tusichukue hatua yoyote?Kuridhika gani huku tunajua viongozi wetu wanapoteza mabilioni ya shilingi kujiagizia magari ya kifahari,wanalipana posho nzitonzito kwenye vikao visivyo na tija wakati sisi hatujui jioni tutakula nini au lini dawa zitakuwepo kwenye zahanati zetu ya kata?Kwavile hatujui haki zetu au?Yaani pamoja na utandawazi wote huu,utitiri wote huu wa habari na mawasiliano?Hao wazee waliokuwa wanagoma kuburuzwa na Nyerere wangepata bahati kama tuliyokuwa nayo sisi,hii nchi ingenyooka haraka sana.Mkuu mimi naona hatujaridhika.Tuna donge zito sana katika mioyo yetu isipokuwa tunaogopa kulitoa na kuliweka katika vitendo.Tunataka mabadiliko isipokuwa bado tuna uoga katika kuchukua hatua na ndiyo maana tunaishia kunung'unika chinichini.
 
Mzee Mwanakijiji pamoja na majibu yako mazuri lakini bado nikuulize:Hivi Tanzania kuna middle class?Asilimia ngapi vile?Na masikini kwa kiwango cha chini ya dola moja kwa siku ni asilimia ngapi vile?

Tanzania hatujajenga middle class; we have created a lower class and an upper class.. Mtu anataka atoke kwenye lower class kwenda kwenye upper class; hakuna anayetaka kuwa kwenye middle class. Mtu akipata tufweza kidogo anataka ajenge nyumba aikodishe kwa wazungu au watu wengine; anunue gari na jingine la biashara; n.k n.k Aliyeko juu hafikirii hata kidogo kurudi hapa chini kwa hiyo atafanya kila analoweza kubakia huko juu.

Sasa utaona kimsingi ufisadi ni mapambano kati ya wale walio chini wanaotaka kwenda juu na wale waliojuu wasiokuwa tayari kuvutwa chini. Daraja la kati is simply a temporary state of affairs. Ni daraja la mpito.

Kwa mtazamo wangu naona wengi ndiyo wanaathirika moja kwa moja na huu ubinafsi wa kina Chenge na Ndulu manake masikini ndiyo wengi na siyo vijijini tu hata mijini kama Dar Es Salaam ambayo mara nyingi ndiyo inatumika kama kioo cha Tanzania bado kuna watu wanaishi maisha ya dhiki sana.

Hilii ni kweli lakini mtu wa kawaida haoni matatizo yake kuwa yanahusiana na ufisadi. Watawala hawataki mwananchi wa kawaida asikie uchungu wa ufisadi au uongozi mbovu hivyo anakuwa kama yule mbwa ambaye wezi wanapokuja kuiba wanakuja na mfuko wa nyama nyama. Hawampi zote kwa mkupuo; wanampa kwa vipande kila akitaka kunguruma anarushiwa mfupa! Anaridhisha njaa yake na hamu yake lakini wakati huo huo anaachilia watu wanaiba. Tungepata nafasi ya kumuuliza imekuwaje atatuonesha nyamanyama na mifupa!

Sasa tatizo letu nini mpaka tukaridhika kiasi hiki hata Tanesco wanapandisha bei ya umeme kisa kuilipa Richmond lakini tunaishia kulalamika tu na tusichukue hatua yoyote?Kuridhika gani huku tunajua viongozi wetu wanapoteza mabilioni ya shilingi kujiagizia magari ya kifahari,wanalipana posho nzitonzito kwenye vikao visivyo na tija wakati sisi hatujui jioni tutakula nini au lini dawa zitakuwepo kwenye zahanati zetu ya kata?Kwavile hatujui haki zetu au?Yaani pamoja na utandawazi wote huu,utitiri wote huu wa habari na mawasiliano?Hao wazee waliokuwa wanagoma kuburuzwa na Nyerere wangepata bahati kama tuliyokuwa nayo sisi,hii nchi ingenyooka haraka sana.Mkuu mimi naona hatujaridhika.Tuna donge zito sana katika mioyo yetu isipokuwa tunaogopa kulitoa na kuliweka katika vitendo.Tunataka mabadiliko isipokuwa bado tuna uoga katika kuchukua hatua na ndiyo maana tunaishia kunung'unika chinichini.

kuna ganzi ambayo tunapigwa kila siku tusisikie maumivu; inaitwa misaada ya kigeni. Ni misaada ya kigeni ndiyo inaficha athari hasa ya ufisadi kwani fedha za kodi zinazoibwa na kukombwa na watendaji wafadhili hufanya haraka kuziba pengo hilo na mwananchi wa kawaida hawezi kuona uchungu wa kuzikosa kwani kwake anachotaka anapata!
 
Sasa tatizo letu nini mpaka tukaridhika kiasi hiki hata Tanesco wanapandisha bei ya umeme kisa kuilipa Richmond lakini tunaishia kulalamika tu na tusichukue hatua yoyote?Kuridhika gani huku tunajua viongozi wetu wanapoteza mabilioni ya shilingi kujiagizia magari ya kifahari,wanalipana posho nzitonzito kwenye vikao visivyo na tija wakati sisi hatujui jioni tutakula nini au lini dawa zitakuwepo kwenye zahanati zetu ya kata?Kwavile hatujui haki zetu au?Yaani pamoja na utandawazi wote huu,utitiri wote huu wa habari na mawasiliano?Hao wazee waliokuwa wanagoma kuburuzwa na Nyerere wangepata bahati kama tuliyokuwa nayo sisi,hii nchi ingenyooka haraka sana.Mkuu mimi naona hatujaridhika.Tuna donge zito sana katika mioyo yetu isipokuwa tunaogopa kulitoa na kuliweka katika vitendo.Tunataka mabadiliko isipokuwa bado tuna uoga katika kuchukua hatua na ndiyo maana tunaishia kunung'unika chinichini.

Ahsante sana Mama. Kuhusu woga ni kweli Watanzania ni waoga. Nakumbuka Slaa alipoanza kuongelea mafisadi ndani ya Serikali na kuamua kuwataja hadharani wengi walimtisha sana kwamba watamfungulia mashtaka hivyo awaombe radhi kwa kuwaharibia reputations zao lakini ukweli ulipodhihiri hakuna hata mmoja aliyemfungulia mashtaka Dr Slaa. Pia nakumbuka kwamba Dr Slaa alipoanza kutwaambia Watanzania kuhusiana na ufisadi mkubwa uliofanywa na EPA, Kikwete alitamka hadharani nadhani ilikuwa kwenye sherehe za mei mosi kwamba hawa CHADEMA wanataka umwagaji wa damu utokee nchini kwa kusema mambo ambayo ni ya uwongo kabisa kuhusu wizi mkubwa pale BoT. Sasa kama Slaa angeogopa na kuamua kunyamaza basi Watanzania tusingejua kabisa wizi mkubwa wa shilingi bilioni 133. Mimi inaniuma sana kuona madudu yote yaliyofanywa tangu 2005 CCM inarudoi tena madarakani kilaini na itazoa tena asilimia kubwa ya viti vya bunge pamoja na kuwa hakuna lolote lile walilolifanya tangu 2005 hadi hii leo.

Ahadi zao zote hakuna hata moja waliyotimiza, Mafisadi wote wa EPA, Rada, Kiwira n.k bado wanapeta bila wasiwasi, vyama vya upinzani ndiyo hivyo tena wengine toka upinzani akina Mrema na Cheyo wameamua kumpigia debe Kikwete sasa sijui kwanini wanaendelea kujiita ni wapinza!? CHADEMA ndiyo hao wanavurugana na hali ya nchi ikizidi kudidimia ahhhhh! inasikitisha sana nchi yetu jamani :(
 
Mkjj umesema kitu kikubwa sana hapo. Nimeliona hili kwa marafiki wengi sana ambao ukiongelea matatizo yanayotokana na uongozi mbovu nchini mweru wanakuwa hawakuelewi kabisa na kutaka kukuonyesha kwamba hujui unaongea nini basi watakwambia "Wewe unaishi nje hali hapa nyumbani si mbaya kiasi hicho usiyaamini sana yote unayoyasikia au kusoma kwenye magazeti." Wengi wa hawa ni wale ambao wameridhika na maisha yao wana mishahara minono wanaweza kuafford shule za kulipia wana magari wengine zaidi mawili. Mimi huwaambia kwamba mficha ugonjwa maradhi yatamuumbua kwa maana kwamba ncghi yetu ina matatizo makubwa sana na Watanzania wengi wamekata tamaa ya maisha kutokana na utendaji mbovu wa Vuongozi wa juu ndani ya Serikali ambao wameweka mbele maslahi yao au ya CCM na kuwasahau kabisa mabilioni ya Watanzania ambao wanaishi maisha ya dhiki ya kutisha, siku ambayo hawa waliokata tamaa ya maisha wakisema sasa basi liwalo na liwe hata hao ambao wana maisha mazuri basi maisha yao yatakuwa hatarini na watajuta kwa nini walifumbia macho uongozi mbovu kwa miaka mingi nchini kwetu.

- Mkuu Bubu, tafadhali sana ndugu yangu naomba uwe na amani ya bwana inayozidi zote duniani, in our generation hiyo haitakuja kutokea ndio maana ninasema we are in for milele na hawa watawala,

- Wanasayansi wanatuambia kwamba miaka 35 ndiyo sasa life expectancy kwetu, sasa kwa wale tunaozidi hiyo tuna bahati sana, meaning kwamba milele inakuja very soon, Ndugu yangu Bubu hebu niambie ni nchi gani duniani unayoifahamu yenye wananchi kama sisi Tanzania?

- Please name me one country, just one please ambapo kiongozi aliyeliingiza taifa kwenye hasara ya kulipa Dola za US $154, 000 kwa siku kwa miaka miwili kwa ajili ya umeme ambao haupo anavyoweza bado kuitikisa political system ya lile taifa na hata kutaka kugombea urais na hata kutaka kumng'oa Spika wa lile taifa kazi yake, please just name me one country! phew!

- Bubu ni sisi tu mazee na sasa ndio we are going down the road ya milele! I am sorry, lakini hii ni fact bro we are damned no matter what or how you look at it!

Respect.


FMEs!
 

Leo hii nilikuwa naongea na bwana mdogo wangu na tukawa tunajadili juu ya hii kitu.

CHADEMA inabidi wanunue projectors na kwenye kampeni zao, wawe wanaongea kidogo na kuonyesha picha kama hizi ili hao wananchi waone tofauti. Sina uhahika kama itasaidia ila nafikiri picha wakati mwingine inaweza kuongea zaidi ya Zitto na DR, Slaa wakihutubia siku nzima.
 
2009 Maybach 62 S Sedan




maybach_62_s_sedan_2010



Pricing Information: Pricing Definitions


MSRP $456,500
]

Price Tag: $ 456,500



Price Tag?: $ 15.00

- Sasa look my friend: $ 456, 500 - $ 15.00 = $ 456, 485 Yes I said it!

- Mungu Aibariki Tanzania!

Respect.


FMEs!
 




Price?

- Mungu Aibariki Tanzania!

Respect.


FMEs!


Duh...vipaumbele vipaumbele...yaani haya ndiyo mambo yanayotufanya waafrika wote tuitwe manyani kwenye nchi za watu.Haya ndiyo yanayotufanya tuonekane hatuna akili,yanayofanya Afrika yote chini ya sahara ionekane ni masikini,haina lolote zaidi ya Ukimwi,nyumba za tope,Utapiamlo,mitala...
Kingine nadhani na Nyerere naye ametuharibu sana na siasa yake ya Ujamaa.Tumebaki kuwa watu wa huruma huruma na slow sana to take solid stances.Ndiyo maana Wakenya wanasema tuna inferiority complex!
 
Mkuu naona umekula maji ya bendera mtatawala milele maana wadanganyika wamesha lewa na maji ya bendera ya kijani.
 
Wakuu:

Halafu picha ya juu walioshika mabango ya sita na kikwete utaona wengi waliojitokeza ni vijana ambao huko juu nimetoa hoja kwamba hao ndio nguvu ya mabadiliko.
 
Wakuu:

Halafu picha ya juu walioshika mabango ya sita na kikwete utaona wengi waliojitokeza ni vijana ambao huko juu nimetoa hoja kwamba hao ndio nguvu ya mabadiliko.

Hao wakipewa kofia ya buku 2 na flana ya buku jero wanauza uhuru wao
 
Hao wakipewa kofia ya buku 2 na flana ya buku jero wanauza uhuru wao

Mkuu,

It's so sad.System inatumia bakora ya umaskini kuendelea kuwadhulumu raia wake

Pia,still baraza huru la vijana lina-play sehemu kubwa sana ya ukombozi pamoja na kuleta mwamko wa mabadiliko.Elimu ya uraia nayo ni shida.

Elimu ya uraia ingetolewa basi mtu angweza pewa tshirt na pilau but kisirisiri still akampigia kura mtu wa chaguo lake
 
- Mkuu wangu hata mimi I am lost kama wewe if you will, I mean ninaona jinsi Health Care bill ilivyokwama tena over the most popular ever president wa US, na hii inafanywa na the minority party, sasa swali langu ni kwamba sisi tunashindwa nini?

- Look kina Raila Odinga sasa hivi, hawa ni nini they are doing right mpaka wanasikilizwa na watawala wao ambacho sisi tunashindwa?

Respect.

FMEs!

Mkuu tupeane pole, maana kwa kweli haya majambo yanauma. Nafikiri jambo moja ambalo hatujafanikiwa kulifanya ni kuhusisha ubovu wa uongozi tulio nao na shida ambazo wananchi wanazipata. Kila nipitapo vijijini nikiongea na wananchi unawaona wanavyosononeka, lakini ukiwauliza mnafikiri tufanyeje hatuongei lugha moja kama hii hapa JF. Hawaoni kabisa kama mazira yaliyopo yamesababishwa au yanasabishwa na uongozi na serikali tuliyo nayo kwa kiasi kikubwa na hawaoni kama hii serikali ndiyo inapaswa kuwa kinara wa kuyatatua. Ndio kusema wanapoenda kupiga kura hawaendi kuchagua mtu wa kutatua matatizo yao na ya taifa; wanaangalia vigezo vingine--mostly the most visible party and we all know which party this is. Na kama kuna sehemu watawala wamefanikiwa ni hapa-'keep them in dark for ever strategy'. Na hapa ndipo walipoanzia akina Raila. Leo hii wakenya wapo clear na kipi cha serikali na kipi cha mwananchi, na wanajua wanapokwama wapi wajilaumu wao na wapi waijabishe serikali yao.

Leo hii watanzania, tena wasomi kabisa, hata kazi za bunge hatuzijui--kama umefuatilia mjadala wa wanabidii. Utachoka!!
 
Hata Ian Smith aliapa kwamba Rhodesia itaendelea kupeta, Je tangu aliposema maneno yale ya kejeli ilichukua muda gani? Chama Cha Majambazi waendelee kujihadaa lakini I gurantee you the light is near than many people think.
 
Mkuu tupeane pole, maana kwa kweli haya majambo yanauma. Nafikiri jambo moja ambalo hatujafanikiwa kulifanya ni kuhusisha ubovu wa uongozi tulio nao na shida ambazo wananchi wanazipata. Kila nipitapo vijijini nikiongea na wananchi unawaona wanavyosononeka, lakini ukiwauliza mnafikiri tufanyeje hatuongei lugha moja kama hii hapa JF. Hawaoni kabisa kama mazira yaliyopo yamesababishwa au yanasabishwa na uongozi na serikali tuliyo nayo kwa kiasi kikubwa na hawaoni kama hii serikali ndiyo inapaswa kuwa kinara wa kuyatatua. Ndio kusema wanapoenda kupiga kura hawaendi kuchagua mtu wa kutatua matatizo yao na ya taifa; wanaangalia vigezo vingine--mostly the most visible party and we all know which party this is. Na kama kuna sehemu watawala wamefanikiwa ni hapa-'keep them in dark for ever strategy'. Na hapa ndipo walipoanzia akina Raila. Leo hii wakenya wapo clear na kipi cha serikali na kipi cha mwananchi, na wanajua wanapokwama wapi wajilaumu wao na wapi waijabishe serikali yao.

Leo hii watanzania, tena wasomi kabisa, hata kazi za bunge hatuzijui--kama umefuatilia mjadala wa wanabidii. Utachoka!!

- Mkuu Kitila, ahsante sana mkuu, kwa kukubali ukweli badala ya kulaumu wengine!

Respect.


FMEs!
 








CCM london
Shoto ni katibu siasa na uenezi Bw. M Katega akiwakabidhi katiba ya chama cha Mapinduzi viongozi wa tawi la South London Mwenyekiti Bw. Kassim Hassan na katikati mjumbe wa tawi hilo Bw. Seth Mdendemi
katibu siasa na uenezi Bw. M Katega akiwakabidhi katiba ya chama cha Mapinduzi viongozi wa tawi la East london Katibu wa tawi Bi Mariamu Mungula na Mjumbe Bw. Iddy Mwanga

kushoto Bw. Frank Mukiza, Kassim Hassan, Mariamu Mungula, M Katega, Seth Mdendeni na aliyekaa ni Pashency Linus
kutoka shoto ni Neema Kumba, mwandishi wa Tanzaniaone UK Bw. Ally Muhdin na Katibu wa tawi la East London Bi. Mariamu Mungula

Chama cha Mapinduzi CCM jana jumamosi ya tarehe 27 mwezi wa pili mwaka 2010 kilifungua mashina mawili na kuchagua viongozi wa kuongoza mashina hayo jijini London Uingereza. Mashina hayo yalifunguliwa na katibu siasa na uenezi Bw. Katega. Mashina yaliyofunguliwa ni sina la South London na Shina la East London.

- CCM inazidi kujitandaza mpaka majuu jamani! sasa hawa sio wananchi wa vijijini ndio maana ninasema sometimes huwa ninawaza sana kwamba hapa JF huenda hatuwakilishi mawazo ya wananchi wengi wa Tanzania, au?

Respect.


FMEs!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom