Je, CCM Itatawala Milele Au?

Status
Not open for further replies.
Mkuu tupeane pole, maana kwa kweli haya majambo yanauma. Nafikiri jambo moja ambalo hatujafanikiwa kulifanya ni kuhusisha ubovu wa uongozi tulio nao na shida ambazo wananchi wanazipata. Kila nipitapo vijijini nikiongea na wananchi unawaona wanavyosononeka, lakini ukiwauliza mnafikiri tufanyeje hatuongei lugha moja kama hii hapa JF. Hawaoni kabisa kama mazira yaliyopo yamesababishwa au yanasabishwa na uongozi na serikali tuliyo nayo kwa kiasi kikubwa na hawaoni kama hii serikali ndiyo inapaswa kuwa kinara wa kuyatatua. Ndio kusema wanapoenda kupiga kura hawaendi kuchagua mtu wa kutatua matatizo yao na ya taifa; wanaangalia vigezo vingine--mostly the most visible party and we all know which party this is. Na kama kuna sehemu watawala wamefanikiwa ni hapa-'keep them in dark for ever strategy'. Na hapa ndipo walipoanzia akina Raila. Leo hii wakenya wapo clear na kipi cha serikali na kipi cha mwananchi, na wanajua wanapokwama wapi wajilaumu wao na wapi waijabishe serikali yao.

Leo hii watanzania, tena wasomi kabisa, hata kazi za bunge hatuzijui--kama umefuatilia mjadala wa wanabidii. Utachoka!!

Mkuu Kitila tuanze na elimu ya uraia huko basi manake ndiyo tatizo.I mean tusisubiri mwezi ujao uchaguzi ndiyo tuanze kujitokeza kwa wananchi na kuwaambia kuwa umasikini wao unasababishwa na CCM.Hawawezi wakakuelewa,watajua umeenda kutafuta kura(read kula)tu!Na ndipo balaa inaanza hapo kwa vile walishazoea kupewa elfu mbili ili 'watoe kula' basi lazima na wewe wakuulize vipi unazo hizo 2000?Kama huna anza kuhesabu maumivu!!
Kuna sehemu nyingine Mkuu siyo siri wananchi wamechoka na wabunge wa CCM,isipokuwa hakuna potential alternatives,inafikia wanaona heri wachague yule yule wa CCM.Kuna mkulu mmoja wa NCCR nakumbuka 2005 nilishiriki kampeni yake kwenye jimbo ninakotoka.Sisi vijana tulimsaidia sana tena bila ya kulipwa hata senti tano.Na kizuri ilikuwa yule mgombea wa CCM aliyekuwa kipenzi pale na alishinda kwenye kura za maoni,jina lake likaja kuondolewa.CCM wakaja kutuletea Mbunge yuleyule ambaye tulikuwa hatumtaki.Lakini mkulu wa NCCR pamoja na hii golden chance aligalagazwa sana na yule babu wa CCM.
Sababu kubwa hakujiandaa.Maandalizi yake yalikuwa finyu sana na alichelewa kuonyesha nia yake ya kugombea.
 
Na wewe ngoja ujibiwe kwa namba.
1.Mifano yako ya akina Mkwawa haijatulia. Inaonekana ni kati ya wale watu wanaoamini kuwa kusoma ndio kuwa na akili. Hiyo futa kabisa kichwani mwako. Ni ukweli usiopingika kuwa wapiga kura wengi hawana akili. Huwezi mtu ukawa na akili timamu ukapewa kanga au kofia ukatoa kura yako. Huko ni kukosa akili. Pilau ya siku moja kama unaakili timamu haina thamani ya kura. Hao machifu uliowataja wangekuwa na akili kama za wapiga kura wengi wasingepambama. Walikuwepo wasiokuwa na akili kama Mangngo wa Msovero. Shanga tu zilitosha kutoa nchi ndio kama hao wapigakura walio wengi.
2. Hata kama hajatokea kama Mrema demage ilishafanyika na hapo ndio tunarudi wa kwa wapiga kura kuwa ni mbumbumbu wasiotumia vichwa vyao kufikiri vinginevyo wangeelewa kuwa hizo ni propaganda tu.
3. unaelewa utaratibu wa kubadilisha Katiba wewe? Bunge! Nani anashikilia Bunge? Ebu tueleze CUF wemefika pazuri wapi? Halafu kwani CUF kama ndio wataalam kwani Bara hawapo?
4. Kama unajua kuwa ukosefu wa uzalendo ndio jibu sasa inakuwaje unalalamikia vyama vya upinzani?
5. Watagombana kwa sababu ya sera? Mbona CCm mwenyekiti wao alisema sera hazitekelezeki na wengine wakasema zinatekelezeka bado walikaa pamoja? Haya maswala ya sera ni mismiati tu ya wanasiasa. Sera ni moja tu, Usitawi wa jamii ya Watanzania
6. Eti uchaguzi hauna mizengwe! ptuh! Temea mate chini na uache kututukana hapa. Tuanzie mwaka 1995 hivi kwa nini Dar uchaguzi ulirudiwa? Huko Zanzibar ni lini CCm ilishinda? Wabunge wangapi waliondoshwa kwenye ubunge baada ya matokeo kutenguliwa? Sasa kama hivyo vyote si mizengwe kwako mizengwe ni ipi?

Nakuunga mkono kwa pointi yako ilichaandika ni fact tupu. Kuhusu hoja hii CCM haitatawala milele hilo halina ubishi.
 
Mkuu tupeane pole, maana kwa kweli haya majambo yanauma. Nafikiri jambo moja ambalo hatujafanikiwa kulifanya ni kuhusisha ubovu wa uongozi tulio nao na shida ambazo wananchi wanazipata. Kila nipitapo vijijini nikiongea na wananchi unawaona wanavyosononeka, lakini ukiwauliza mnafikiri tufanyeje hatuongei lugha moja kama hii hapa JF. Hawaoni kabisa kama mazira yaliyopo yamesababishwa au yanasabishwa na uongozi na serikali tuliyo nayo kwa kiasi kikubwa na hawaoni kama hii serikali ndiyo inapaswa kuwa kinara wa kuyatatua. Ndio kusema wanapoenda kupiga kura hawaendi kuchagua mtu wa kutatua matatizo yao na ya taifa; wanaangalia vigezo vingine--mostly the most visible party and we all know which party this is. Na kama kuna sehemu watawala wamefanikiwa ni hapa-'keep them in dark for ever strategy'. Na hapa ndipo walipoanzia akina Raila. Leo hii wakenya wapo clear na kipi cha serikali na kipi cha mwananchi, na wanajua wanapokwama wapi wajilaumu wao na wapi waijabishe serikali yao.

Leo hii watanzania, tena wasomi kabisa, hata kazi za bunge hatuzijui--kama umefuatilia mjadala wa wanabidii. Utachoka!!


kabla ya lawama zoe kwa serikali tujiulize tumeifanyia nini nchi ama serikali na si kuuliza serikali imefanya nini
 
is it because we are so kind and good hearted citizen kwa hiyo issue za magomvi kama Kenya hatuziwezi, hivyo hatutaweza kuwapata akina Odinga?
Kote huko tunazunguka tu; tatizo ni hili hapo juu kwetu sisi wa-TZ. Hakuna miujiza wala nini CCM hawaweezi kuachia utamu wa nchi hii kirahisi. La sivyo tutangoja mabadiliko mpaka milele yetu itakapofika.
 
kabla ya lawama zoe kwa serikali tujiulize tumeifanyia nini nchi ama serikali na si kuuliza serikali imefanya nini

- Mkuu wangu tupo pamoja hapo na ndio hasa msingi wa hoja yangu, tunafanya nini serious cha kuwahistusha watawala kwamba tunakerwa na uongozi wao mbovu?

- Na je ni kweli tunawawakilisha wananchi wengi wa Tanzania na vilio vyetu au? Na ni nini we are not going right?

Respect.


FMEs!
 
- Wakuu wote JF heshima mbele sana, nimekuwa nikisumbuliwa sana na swali moja tunalalamika sana kuhusu matatizo ya uongozi wa CCM kwa taifa letu. Ni miaka 47 sasa CCM imetutawala Tanzania, nikiangalia historia inaonekana wenzetu yaani wazee wa zamani pamoja na uchache wao kielimu na tools, sio siri kwamba walikuwa wanatoa upinzani mzito sana kwa TANU/CCM kuliko sisi vijana wa sasa.

- Inaonekana kama wenzetu hawakuwa na maneno mengi sana, ila walikuwa na vitendo vizito sana na siku zote walikuwa wakiilaza macho serikali na CCM, tizama kina Anangisye, Mwabulambo, Kambona, Bibi Titi, Kassanga Ntumbo, wazee kama kina Chipaka, Magee, Lugangira yaani huyu pamoja na kumfunga jela alitoroka anyways, Nyirenda na wengineo, I mean mbona inaonekana kama they were more effective kuliko sisi wenye akili sana katika kuipigisha magoti serikali na TANU/CCM? Kila walipomaliza kufanya vitu vyao kuna mabadiliko flani yalikuwa yakifanyika kuitikia vilio vyao kuhusu taifa, infact ni wao ndio walishinikiza Sokoine kupewa power na ile vurugu ya mafisadi, sasa nini kimetokea sasa tena ukitilia maanani kwamba sisi tuna tools nyingi in our hands zaidi ya walizokuwa nazo wao! Hebu soma historia yetu utasikia kila wakati kulikuwa na tafrani somehow somewhere!

- Tuna vyama vingi vya siasa, tuna uhuru wa kuongea na kuandika, I mean wale hawakuwa na yote haya lakini they were more effective na vitendo vyao bubu kuliko sisi, WHY? Hebu tuambiane nini challenge ya maana iliyowahi kufanyika against CCM na serikali yake toka tuingie vyama vingi Mwaka 1995 to this date katika kuwafahamisha kwamba wananchi tumechoka na ***** mwingi wanaoufanya mpaka kuwashitua ili watusikilize kama wale wenzetu wa zamani?

- I mean I could be wrong vile vile, lakini this is what I see, we are just not effective enough or convincing to watawala, WHY? Halafu kumbuka kwamba milele ni pale tu mwisho wa maisha yako unapofika na sio anything esle!

Respect.


FMEs!


Mkuu Field Marshall ES aka W. J. Malecela, Le Mutuz.

Ni kwa sababu tuna watu vigeugeu kama wewe, waganga njaa.

Unasemaje kuhusu utapeli uliofanya wakati ule?
 
Last edited by a moderator:
Hivi unakumbuka 1995 kwanini matokeo ya uchauguzi mkuu mkoa wa Dar es Salaam yote yalifutwa?! Hiyo haikuwa shock kwa CCM?!

Hivi unajua 1995 Nyerere alipoiambia ZEC ibadilishe matokeo ya kura za urais wa ZNZ in favour of Dr. Salmin Amour, Bado unasema tu CCM haijawahi kutikishwa na upinzani?.

Hivi unakumbuka 2010 Akina Lut General Abdulahaman Shimbo walivyowatisdhiwa wananchi kwa sababu ya UOGA wa CCM. Bado unakumbuka uchakachuaji wa kura wa Dr. Kikwete 2010?!. Kama hakuogopa kwanini alichakachua matokeo ya kura. Najua ulikuwa US hebu ulizia majimbo ambayo CDM ilitangaza mshindi hali ilikuwaje? Kama sio uoga wa CCM ni nini?

Nakwambia hakuna katika uhai wa CCM/TANU ambapo imetishwa/inatishika kama sasa. Wako madarakani tu kwasababu ya TUME ya UCHAGUZI na vyombo vya dola period.
 
Katika kile kinachoonekana hakuna chama mbadala kinachoweza kuenzi amani iliyopo tz,watz wameamua sasa ccm kiwe chama chao cha maisha,Hili limetokana na vyama vya upinzani nchini kukumbwa na kashfa nzito ambazo zinatishia mustakabali wa taifa hili changa kama ufuatavyo;CHADEMA--Kuna ukabila wa kufa mtu,kama wewe si mchaga hauthaminiwi chamani kama ilivyo kwa zitto,CUF-nyumbani kw waisilamu waliowengi;TLP-ukabila pia ukipingana na mrema tu out!; NCCR-MAGEUZI-ukabila pia,pingana na mbatia uone,muulize classmate wangu kafulila atakwambia;TLP-wasukuma wa kinyantuzu wamejaa,pingana na cheyo uone cha moto! Kwa mambo haya yasiyowapendeza watz hakuna mbadala wa ccm japokuwa watz wamachoka kuongozwa na ccm,wakimbilie wapi sasa?2010 watz walikuwa hawajashtuka subirieni 2015 chadema haifurukuti tena! Ukabila na udini waanza kuitafuna tz hata kwenyeb ajira!
 
…politically..(MTANZANIA).!!! ……watch … you're …. Steps….!!!!! …are …you …moving …back… or …..Forward…..watch your steps….!!!!
 


…
KI..UHALISIA ..(MTANZANIA) .!!! ……watch … you're …. Steps….!!!!! …are …you …moving …back… or …..Forward…..watch your steps….!!!!
 
Katika kile kinachoonekana hakuna chama mbadala kinachoweza kuenzi amani iliyopo tz,watz wameamua sasa ccm kiwe chama chao cha maisha,Hili limetokana na vyama vya upinzani nchini kukumbwa na kashfa nzito ambazo zinatishia mustakabali wa taifa hili changa kama ufuatavyo;CHADEMA--Kuna ukabila wa kufa mtu,kama wewe si mchaga hauthaminiwi chamani kama ilivyo kwa zitto,CUF-nyumbani kw waisilamu waliowengi;TLP-ukabila pia ukipingana na mrema tu out!; NCCR-MAGEUZI-ukabila pia,pingana na mbatia uone,muulize classmate wangu kafulila atakwambia;TLP-wasukuma wa kinyantuzu wamejaa,pingana na cheyo uone cha moto! Kwa mambo haya yasiyowapendeza watz hakuna mbadala wa ccm japokuwa watz wamachoka kuongozwa na ccm,wakimbilie wapi sasa?2010 watz walikuwa hawajashtuka subirieni 2015 chadema haifurukuti tena! Ukabila na udini waanza kuitafuna tz hata kwenyeb ajira!

Mheshimiwa sana wa Nambari one, leo nimepata nafasi tena ya kuwa hapa jamvini. Sasa mkuu, anzisha thread nyingine basi ili tuchangie.!
 
hujui maana ya milele?wewe ngoromiko na kilaza mkubwa kweli! Wasiliana na mwalimu wako wa darasa la tatu akufundishe ndipo uingie jf tena,umewahi sana

Sidhani kama kuna shida katika kuuliza, na kama ungekuwa na jibu dhahiri usingetumia lugha hiyo! Au ungekuwa mtu wa kujiheshimu usingeandika ulichokiandika hapo juu kama una jibu la swali. As a great thinker learn

Pili, Hata kama ningekuwa ni "kilaza" je nisingekuwa na stahili ya kujuzwa?Au ni nani anayekuwa "kilaza zaidi" aliyeuliza akihitaji kupata ufahamu(common ground) au aliyekimbia swali kwa kejeli na matusi?!

Tatu, as a great thinker you should learn to know/understand the motive of every question posed to you! Dont think every question has cheap answer as the question might seem!So having said that, jibu swali au skip it kama hujui/huwezi/ au kama unaona halina relevance!
 
Katika kile kinachoonekana hakuna chama mbadala kinachoweza kuenzi amani iliyopo tz,watz wameamua sasa ccm kiwe chama chao cha maisha,Hili limetokana na vyama vya upinzani nchini kukumbwa na kashfa nzito ambazo zinatishia mustakabali wa taifa hili changa kama ufuatavyo;CHADEMA--Kuna ukabila wa kufa mtu,kama wewe si mchaga hauthaminiwi chamani kama ilivyo kwa zitto,CUF-nyumbani kw waisilamu waliowengi;TLP-ukabila pia ukipingana na mrema tu out!; NCCR-MAGEUZI-ukabila pia,pingana na mbatia uone,muulize classmate wangu kafulila atakwambia;TLP-wasukuma wa kinyantuzu wamejaa,pingana na cheyo uone cha moto! Kwa mambo haya yasiyowapendeza watz hakuna mbadala wa ccm japokuwa watz wamachoka kuongozwa na ccm,wakimbilie wapi sasa?2010 watz walikuwa hawajashtuka subirieni 2015 chadema haifurukuti tena! Ukabila na udini waanza kuitafuna tz hata kwenyeb ajira!

We sijui tukuite vuvuzela la CCM au zezeta
 
Katika kile kinachoonekana hakuna chama mbadala kinachoweza kuenzi amani iliyopo tz,watz wameamua sasa ccm kiwe chama chao cha maisha,Hili limetokana na vyama vya upinzani nchini kukumbwa na kashfa nzito ambazo zinatishia mustakabali wa taifa hili changa kama ufuatavyo;CHADEMA--Kuna ukabila wa kufa mtu,kama wewe si mchaga hauthaminiwi chamani kama ilivyo kwa zitto,CUF-nyumbani kw waisilamu waliowengi;TLP-ukabila pia ukipingana na mrema tu out!; NCCR-MAGEUZI-ukabila pia,pingana na mbatia uone,muulize classmate wangu kafulila atakwambia;TLP-wasukuma wa kinyantuzu wamejaa,pingana na cheyo uone cha moto! Kwa mambo haya yasiyowapendeza watz hakuna mbadala wa ccm japokuwa watz wamachoka kuongozwa na ccm,wakimbilie wapi sasa?2010 watz walikuwa hawajashtuka subirieni 2015 chadema haifurukuti tena! Ukabila na udini waanza kuitafuna tz hata kwenyeb ajira!
kamuzu Banda pamoja na kuitawala Malawi kwa mkono wa chuma hata kufikia kujiita rais wa maisha alikuja kuondolewa kwa sanduku la kura,chama cha KANU pamoja na kuwa mojawapo wa vyama vikongwe barani Afrika kilifutika katika ramani ya siasa kupitia sanduku la kura vivyo hivyo chama cha Rais Kaunda wa Zambia,Rais Obote wa Uganda n.k. na hili linaweza kutokea kwa CCM.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom