Nianze kwa kumtakia kila la kheri katika majukumu yake si mapya bali mapya katika kuwatumikia moja kwa moja wananchi wa Bumbuli.
Sisi hapa Bumbuli tulikuwa tunammiss sana na ilikuwa wakati fulani shida kumpata mbunge wetu.
Lakini kuondoka kwake katika Uwaziri ambao baadhi yetu tulishasemaga ipo siku ataukosa kwa ujinga wake, kunatupa muda wa kutafakari zaidi.
January ni miongoni mwa watoto wa wastaafu katika uongozi wa nchi hii ambaye ni bahati mbaya wanasadifu kile Mwalimu Nyerere alichopigania sana wanawe wasijiingize katika siasa.
Ukiacha Makongoro ambaye amepambana sana na hajafanikiwa sana, Mwalimu Nyerere alifahamu madhara ya kisaikolojia kwa watoto wa kiongozi kuingia katika siasa. Aliwaepusha sana wanawe.
Somo la January na watu aina ya Nape Nnauye libaki milele kwenye mbao za madarasa ya sayansi za siasa kwamba watoto wa viongozi, si wote, wengi hujawa na kasumba, na sio wao tu, hata baadhi ya wazazi wao, kuona kwamba wao wanahatimiliki fulani na uongozi na siasa za nchi.
Hakika mzazi usipokuwa na busara kama alivyoonesha Mzee Makamba kwa kumuongoza hovyo mwanae, mwisho huwa wa aibu.
Nasema January na Nape mwisho wao unatufundisha jambo kwa sababu wote hata walipokuwa ndani ya Serikali ulikuwa unawaona kabisa ni kama vile bado hawaridhiki na walipokuwa.Unajiuliza walikuwa wanataka nini zaidi na kwa nini?
Walikuwa na viburi vya aina mbili; wakati Nape alikuwa na kiburi cha usoni, Januari alijawa na kiburi cha rohoni.
Ndio maana, waraka wa "wazazi" wao ambao sasa umebainika wao nao walishiriki kuuandaa na kugawa hela kwa wahariri usambae, ni kielelezo tu cha kibri chao na ukweli kwamba walikiwa wakifanya mikakati mingi ya pembeni katika siasa zao kuliko kutekeleza majukumu yao ya umma.
Nafahamu wapo viongozi, watoto wao wameingia katika siasa na wana utulivu, lakini somo la Makamba na Nape ni kubwa na tulitafakari. Msichukulie poa.
Siwahukumu lakini nyuso na roho zao zikisadikishwa na matendo yao vinaonesha kiburi cha "mchango wa wazee" wao kila mara kiliongoza siasa zao.
Kila mara January alikuwa akijinasibu na "Mzee Makamba aliniambia..."
Nape naye alikuwa mtu wa "Mapambano yangu katika kuisaidia CCM hayakuanza leo...Mzee wangu Nnauye alimaliza nguvu zake zote kwa ajili ya Chama hiki."
Niseme tu hawa madogo walikosea sana, ukiacha majina ya viongozi wanaojulikana kisiasa, wapo watanzania wengi waliofanya mengi iwe katika kuzuia ukoloni, kupambana na ukoloni, kupigania uhuru au kuijenga Tanzania mpya.
Hawa ni wengi na pengine wapo, kwa utaalamu na hata damu yao, waliodhurika zaidi kuliko Wazee Makamba na Nnauye.
Hakuna mwenye hatimiliki ya Tanzania zaidi ya mwingine, kila Mtanzania anasehemu yake. Tujifunze kwa hawa vijana wawili.
Kwa heri January Makamba katika Uwaziri, karibu katika ubunge.
Jamal Shehoza, Soni, Lushoto.
Sisi hapa Bumbuli tulikuwa tunammiss sana na ilikuwa wakati fulani shida kumpata mbunge wetu.
Lakini kuondoka kwake katika Uwaziri ambao baadhi yetu tulishasemaga ipo siku ataukosa kwa ujinga wake, kunatupa muda wa kutafakari zaidi.
January ni miongoni mwa watoto wa wastaafu katika uongozi wa nchi hii ambaye ni bahati mbaya wanasadifu kile Mwalimu Nyerere alichopigania sana wanawe wasijiingize katika siasa.
Ukiacha Makongoro ambaye amepambana sana na hajafanikiwa sana, Mwalimu Nyerere alifahamu madhara ya kisaikolojia kwa watoto wa kiongozi kuingia katika siasa. Aliwaepusha sana wanawe.
Somo la January na watu aina ya Nape Nnauye libaki milele kwenye mbao za madarasa ya sayansi za siasa kwamba watoto wa viongozi, si wote, wengi hujawa na kasumba, na sio wao tu, hata baadhi ya wazazi wao, kuona kwamba wao wanahatimiliki fulani na uongozi na siasa za nchi.
Hakika mzazi usipokuwa na busara kama alivyoonesha Mzee Makamba kwa kumuongoza hovyo mwanae, mwisho huwa wa aibu.
Nasema January na Nape mwisho wao unatufundisha jambo kwa sababu wote hata walipokuwa ndani ya Serikali ulikuwa unawaona kabisa ni kama vile bado hawaridhiki na walipokuwa.Unajiuliza walikuwa wanataka nini zaidi na kwa nini?
Walikuwa na viburi vya aina mbili; wakati Nape alikuwa na kiburi cha usoni, Januari alijawa na kiburi cha rohoni.
Ndio maana, waraka wa "wazazi" wao ambao sasa umebainika wao nao walishiriki kuuandaa na kugawa hela kwa wahariri usambae, ni kielelezo tu cha kibri chao na ukweli kwamba walikiwa wakifanya mikakati mingi ya pembeni katika siasa zao kuliko kutekeleza majukumu yao ya umma.
Nafahamu wapo viongozi, watoto wao wameingia katika siasa na wana utulivu, lakini somo la Makamba na Nape ni kubwa na tulitafakari. Msichukulie poa.
Siwahukumu lakini nyuso na roho zao zikisadikishwa na matendo yao vinaonesha kiburi cha "mchango wa wazee" wao kila mara kiliongoza siasa zao.
Kila mara January alikuwa akijinasibu na "Mzee Makamba aliniambia..."
Nape naye alikuwa mtu wa "Mapambano yangu katika kuisaidia CCM hayakuanza leo...Mzee wangu Nnauye alimaliza nguvu zake zote kwa ajili ya Chama hiki."
Niseme tu hawa madogo walikosea sana, ukiacha majina ya viongozi wanaojulikana kisiasa, wapo watanzania wengi waliofanya mengi iwe katika kuzuia ukoloni, kupambana na ukoloni, kupigania uhuru au kuijenga Tanzania mpya.
Hawa ni wengi na pengine wapo, kwa utaalamu na hata damu yao, waliodhurika zaidi kuliko Wazee Makamba na Nnauye.
Hakuna mwenye hatimiliki ya Tanzania zaidi ya mwingine, kila Mtanzania anasehemu yake. Tujifunze kwa hawa vijana wawili.
Kwa heri January Makamba katika Uwaziri, karibu katika ubunge.
Jamal Shehoza, Soni, Lushoto.