Jamani huyu msichana mie simuelewi. Naombeni ushauri

Joel360

JF-Expert Member
Sep 21, 2013
981
631
Habari za saa hizi wana jukwaa.

Kwanza nikiri kabisa, nimekuwa single kwa mda mrefu na hii ni kutokana na kukataliwa na waschana wengi niliokuwa nikiwatongoza. Baada ya hapo nikaamua kupotezea mchongo wa mahusiano so sikutaka kujihusisha kimahusiano na msichana yeyote.

Sasa juzi hapa kazini kwetu alikuja msichana fulani kufanya field ambapo wakati anaanza field mie nilikuwa likizo hivyo nilikuja kurudi kazini nikakuta kashakuwa mwenyeji na kashazoeana na watu hapa kazini.

Mara ya kwanza hatukuzoeana sana nae, hivyo zaidi ya salamu tulikuwa hatuzungumzi kitu ila ni mtu fulani muongeaji sana (yaani sana) kwahiyo alikuwa ananiongelesha mambo madogo madogo kama 'Joel mida ya kuondoka imefika, vipi bado upo?' sasa katika kuzungumza mambo madogo kama hayo akawa ameanza kunizoea hivyo akaanza kuniletea utani wa hapa na pale.

Sasa kuna kipindi pale kazini kulikuwa na tukio maalumu kwahiyo wafanyakazi walikuwa wanakuja wachache tena vijana tu, wale wengine walikuwa wanaenda huko kwenye hilo tukio. Kwa nafasi hiyo ya watu kuwa wachache akawa ananiletea utani flani hivi ambao ulianza kunistua na kuamsha hisia zangu.

Alikuwa ananiita na kuanza 'Joel, daah nimekumiss sana' akinambia hivo namchunia mara 'Joel, kwani mi huwezi kunioa? Nna kasoro gani?' au wakati mwingine anasema: 'Joel, I love you' au anaweza sema 'Joel, nakosa usingizi kwa ajili yako', sasa mie nilikuwa nachukulia utani ila nikaanza kuhisi labda anamaanisha ila anashindwa kusema siliasi.

Kingine kuna rafiki yake pale kazini aliwahi kumtuma aje aniambie kuwa ananitaka ila huyo rafiki ake utani mwingi so alinambia kiutani utani. Sasa sijui alikuwa siliasi kumtuma huyo rafiki yake au la?

Basi nikaanza mchakato wa kumfukuzia ili nimpate, shida ikaanzia hapo, nikimwita niongee nae faragha anakataa anasema 'njoo wewe' wakati anajua kuwa anapokaa yeye pale kazini wanakaa kibao so siwezi kuongea nae faragha. Nikimwita wakati wa kutoka anasema nna haraka nataka niondoke. Nikaona isiwe tabu ngoja nimuombe namba ili weekend niombe appointment sasa ikawa kila nikiomba appointment anakataa mara 'oooh nna kazi nyingi' basi jumamosi flani nikaamua nimpigie simu nimtongoze, nikamtongoza anakanambia namtania then simu akakata simu. Kesho jumapili nikampigia simu hakupokea nikamtumia sms hakujibu nikampigia tena mara kibao hakupokea. Nikaamua nimpotezee, Jumatatu anafika, akaanza tena shobo zake 'Joeeel, nimekumisi' nikamlia bati(nikamchunia).

Nilipoona anashobo sana na nimekula bati nikahisi labda anataka ila hataki kutongozwa kwenye simu, nikaaza kumwita tena faragha akawa anazingua. Akazingua hivyovyo mpaka umefika mda wa field kuisha akaondoka.

Sasa baada ya kuondoka nilimpigia simu akapokea mara moja tu ila akanambia hatuwezi kuongea yuko bize nikamwambia ntakupigia kesho. Kesho imefika hapokei simu wala hajibu sms mpaka leo hii.

Kiukweli ni mzuri sana tu, halafu mweupeee, chotara flani hivi la kiarabu, hiyo shepu ndo usiseme kwahiyo na mi nampenda. Ila sasa mpaka sa hivi hapokei simu wala hajibu text sasa wakuu hebu nishaurini nifanye nini ili apokee simu yangu maana mie nshaoza kwake Dah!

Natamani apokee simu niongee nae nimuombe date ila ndo hivyo hapokei, text ndo hajibu kabisaaa nimetuma karibia kumi. Sasa mie sitaki kumwacha naombeni mnishauri cha kufanya ili nimpate.

Ananiumiza sana kichwa aiseee, leo kutwa nzima namuwaza yeye.

Mnisamehe kama nimewakwaza kwa kuandika maneno mengi.

Nashkuru kwa ambao mtanishauri vizuri bila kunitukana au kunidhihaki.
 
atakuwa anapenda drama za mapenzi ya kukimbizana kama wahindi, kwahiyo kama huwezi drama jiandae kuumia zaidi ila kama na wewe ni mzuri kwenye drama basi waweza endelea.
 
Ushamkosa huyo umeanza vibaya jipange upya au nipe hela na details zake muhimu nikusaidie mkuu siku 7 tu mtoto anakua wako.
 
Mapenzi ya kutafuta hivyo huwa hayàdumu hata, achana nae ama la uamuzi wa mwisho ni wako
 
Huyo ni mjuzi wa kuwasha moto aone ni upi utachukua muda kuzima. Jiulize, Je, weye ndo handsome kuliko wote pale ofisini?? Kwa nini hakuna mwingine aluye thubutu kujimwaga ka weye??
Kaka, alikuamsha mdadi akakuacha ukijiminyaminya tu. Huyo bado hajafikia wakati wa hayo mapenzi. Aweza kuwa ana malengo ya mbaali usimpoteze njiani.
Wewe una malengo gani?? Yeye anayo malengo. Msichana mwenye malengo huwa ana focus mbele zaidi ya pua yake tu. Mwache atulie. Kama anakumind hata kwa kope za macho tu, wewe tulia jifanye huna shida na yeye. Akiona kimya atakutafuta. Siku akikupigia usifanye haraka kumjibu. Mwambie nipo bize nipigie baadaye.
 
Back
Top Bottom