Jaji mstaafu Mark Bomani naye atoa mpya..

Akumbushwe tena kuwa kifungu cha katiba namba 41 kinataka raisi awe amechaguliwa na kushinda uchaguzi kwa kupata kura nyingi zaidi ya nusu ya kura zilizopigwa (kulingana na version ya kiingereza ya hiyo katiba). Tuna ushahidi wa kutosha kuwa Kikwete hakupata idadi hiyo ya kura kwa hiyo hakuchaguliwa kwa mujibu wa katiba, hivyo yeye siyo rais halali wa jamhuri ya Tanzania.

Uchaguzi wa Rais hauna uhusiano wowote na uchaguzi wa wabunge ingawa wote wanachaguliwa siku moja. Uchaguzi wa wabunge unatawaliwa na vifungu vya katiba namba 77 hadi 79 wakati uchaguzi wa raisi unatawaliwa na kifungu 41. Kwa hiyo tunaweza kuwatambua wabunge bila kumtambua rais na kusiwe na tatizo lolote.

Kumbe uwezo wa Bomani katika kutafsiri sheria ni sifuri kweli kweli, inatia shaka sana kwenye umakini wa mashauri aliyoamua wakati wakiwa jaji; inawezekana ndiyo maana tuna majaji wanashindwa kuamua kesi za muhimu kama ile ya mgombea huru kwa sababu uwezo wao wa kuchambua sheria ni kama ulivyo wa JAJI bomani. Nina wasi wasi wanazidiwa hata na walimu wa ngumbaru kabisa watu hawa.


Asante......clearly put!
 
AGE...Calculate half life ya Brain yake then nipe jibu kama umekuta kitu.......Obvious EMPTY SET
 
Asante Kichuguu kwa tafsiri nzuri.

Bomani kasemea kule MTANZANIA! Fullstop! Ulitegemea nini kiandikwe na Mtanzania? Tena yawezekana kabisa wamemnukuu vibaya! Wanoko sana wale, sikuwahi kuwasoma hata mara moja wakisemea vizuri Chadema! Bila shaka ni kwa sababu ya RA.
 
Huyu si ni miongoni mwa members wa Board of directors wa SBL? Atakuwa anatetea maslahi tu!
 
Kulingana na sheria zilizopo hapa nchini kuna tofauti kubwa kati ya uchaguzi wa rais na wabunge. Kwani mtu yeyote hasiporidhika na matokeo ya uchaguzi wa mbunge anaruhusiwa kupinga uchaguzi huo mahakamani, lakini inapokuja kwa suala la rais, fursa hiyo haipo. hali hiyo inayoondoa uwezekano wa uchaguzi wa rais kupingwa mahakamani ndiyo inayofungua mlango wa kutomtambua rais aliyetokana na uchaguzi ambao kuna sababu ya mtu kuamini kwamba uliendeshwa ndivyo sivyo.
 
Makumbuka uchaguzi wa 1995 huyu jaji nae alichukua form eti agombee urais kwa tiketi ya CCM! Hakujua mpaka mwalimu J.K. alipomuumbua kwa kumwuliza kasikia wapi majaji wakijiingiza kwamye siasa!!
 
wanasheria jukumu lao ni kutoa tafsiri ya sheria, maoni yao kama watu binafsi wapaswa wayatoe pale tu wanapodhihirisha utashi wao kwa jamii unaelekea pande zipi. Wasiingilie maoni ya watu wenye hekima zinazo kubalika na umma wa watanzania, wataaibishwa!
 
Hawa wazee ndani ya recycle bin ya system bado wana ndoto za mtindo wa kale (analogy), na ndio huu wanaoutumia kuchakachua kura katika kipindi hiki chenye vijana mahiri wa ki-digitali (digital). Katika zamani hizi za technology na wataalam wa IT, ni aibu kwa hawa babu wa ccm kufikiri na kutenda vile wanavyotenda. Ni vema wakae tu pembeni wawaachie vijana kazi wao wachukue nafafi ya kutoa ushauri pale inapobidi kufanya hivyo. Dr Slaa ana mantic na realistic katika madai yake na yeyote anaetaka kujadili ni lazima awe specific na sio kuleta bla bla za ku-politize issues's
 
Do not take him seriously HE IS A SPENT FORCE NEVER TO RECKONED WITH AGAIN!!! Kwisha kazi huyo
 
The guy has a point. Kama mnasema uchaguzi haukuwa wa huru na haki. Mbona mnamkubali Mdee, Mnyika halafu mnamkataa Kikwete? au ni masuala ya ruzuku?

I think CCM should replace Chiligati and put somebody who can effectively call your bluffs na hoja zenu za upande mmoja. Its Chadema's way or no way.
 
The guy has a point. Kama mnasema uchaguzi haukuwa wa huru na haki. Mbona mnamkubali Mdee, Mnyika halafu mnamkataa Kikwete? au ni masuala ya ruzuku?

I think CCM should replace Chiligati and put somebody who can effectively call your bluffs na hoja zenu za upande mmoja. Its Chadema's way or no way.

Mkuu Mimi Si Mwanasheria lakini haihitifaji hata Diploma Kujua kwamba, Dk. Slaa alikuwa Mgombea wa Urais na anawajibika kama Slaa kukubali Matokeo au Kuyakataa kwa yeye kuweka Signature yake, Vile vile kwa Wabunge ni wao indivudualy wanaokataa au kukubali matokeo ya Ubunge

Ukindoa kwamba Uchaguzi wa Ubunge na Urais vinafanyika Siku moja lakini ukweli ni kwamba kila mmoja unatawaliwa na kifungu tofauti katika Katiba kama Alivyoanisha Mkuu Kichuguu.

kwa Hiyo kusema kwamba Dr. Slaa alipaswa vile vile kuyapinga Matokeo ya Ubunge wakati Hakuwa anagombea Ubunge ni Ufinyu tu wa Kutumia just Common Sense katika kuchambua mambo na kutokana na Habari yenyewe kuwa kwenye Gazeti la Mtanzania wala siondoi Uwezekano wa Kuwa Jamaa wa Mtanzania wamemchakachua Bomani

After all Utakubali vipi Matokeo katika Uchaguzi wa Kihuni kabisa kama huu, ona Mpaka sasa NEC bado wanarekebisha Statistics za matokeo baada ya Kusikia kwamba Dr. Slaa anajiandaa kuja na Ushahidi utakaowavua Nguo akina Makame na Kiravu
 
hawa wazee wanatakiwa wapumzike kwanza..lol..bado wanabisha nini?
leo matokeo ya Ubunge jimbo la Vunjo yamerudiwa kuhesabiwa na kuonekana kulikuwa na makosa makubwa tu,je mnataka muambiwe nini zaidi kuwa matokeo yaliibwa??mwenye macho haambiwi tazama,kazi kwenu...
Ushindi wa Mrema Vunjo waongezeka kwa asilimia 4 Send to a friend Tuesday, 16 November 2010 22:22
Daniel Mjema,Moshi
UTATA katika ujumlishaji matokeo ya kura umezidi kuongezeka baada ya matokeo ya uchaguzi wa ubunge wa Jimbo la Vunjo yaliyotangazwa na Tume ya Uchaguzi (NEC) kutofautiana na yaliyotangazwa awali na msimamizi wa uchaguzi.
Kutangazwa kwa matokeo mapya ya jimbo hilo kumefanyika katioka kipindi ambacho Chadema imeamua kutotambua matokeo ya uchaguzi wa rais kwa madai kuwa kulikuwa na ukiukwaji mkubwa wa sheria na taratibu na wizi wa wazi uliolenga kukibeba chama tawala.
Katika kudhihirisha uzito wa tuhuma zake, Chadema ilitoa mfano wa matokeo ya urais ya majimbo ya Hai, Geita na Segerea na baada ya Nec kupitia upya ilikiri kuwa kulikuwa na makosa katika Jimbo la Geita.
Huku hali ikiwa haijatulia, Nec imetangaza matokeo mapya ya Jimbo la Vunjo yanayoonyesha kuwa mgombea wa TLP, Augustine Mrema alipata ushindi wa asilimia 54 na si 50 kama ilivyotangazwa awali.
Kadhalika katika matokeo hayo mapya ambayo Mwananchi inayo nakala yake, kura za mgombea wa CCM, Chrispin Meela zimeshuka kutoka 23,870 hadi 17,498, tofauti ambayo ni sawa na asilimia 39.
Katika matokeo yaliyotangazwa na msimamizi wa uchaguzi Moshi Vijijini, Annah Mwahalende mbele ya wagombea hao, Mrema alikuwa amepata kura 30,810 tofauti
lakini matokeo ya awali yanaonyesha alipata kura 29,047.
Kwa matokeo hayo mapya, Mrema alishinda kwa asilimia 54 huku Meela wa CCM akiibuka wa pili kwa kupata asilimia 32 na si 39. John Mrema wa Chadema alipata asilimia 12 na si 10, huku David Lyimo wa NLD akipata asilimia 2 badala ya 1.
Kwa mujibu wa matokeo hayo mapya, Mrema wa Chadema alipata kura 6,558 na si kura 6,316 zilizotangazwa mwanzo huku Lyimo wa NLD akiwa amepata kura 811 tofauti na kura 118 zilizokuwa zimetangazwa awali.
Hata hivyo kumekuwepo na mabadiliko katika idadi halisi ya wapigakura kutoka 55,013 iliyotangazwa awali hadi kufikia 55,102 ya sasa huku idadi ya kura halali sasa ikiwa ni 53,914 tofauti na kura halali 53,705 zilizotangazwa awali.
Kutokana na hali hiyo, Mrema ameiomba Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kuchunguza mazingira ya mabadiliko hayo ya kura, akisema kuwa anahisi kulikuwepo na njama za kuchakachua matokeo ambazo ziligonga mwamba.
“Nasikia kuna tajiri mmoja alikuja pale ule usiku akiwa na Sh100 milioni akitaka atangazwe mshindi anayemtaka, lakini nguvu ya umma ilishinda kutokana na watu kupaza sauti wakisema kama noma na iwe noma hawatakubali,” alidai Mrema.
Mrema alihoji kama karatasi ya matokeo mapya inaonyesha yalikuwa tayari saa 11:45 jioni, ilikuwaje yatangazwe usiku saa 4:00 na bado yakatangazwa matokeo ambayo hayakuwa sahihi na badala yake kurekebishwa kimyakimya.
Mbunge huyo, ambaye pia ni mwenyekiti wa TLP, alisema kutokana na mazingira hayo ana shaka kuwa hata idadi ya madiwani wa kambi ya upinzani walioshinda ikawa tofauti na akataka kura pia zimlishwe upya.
Hata hivyo, msimamizi wa uchaguzi wa Moshi Vijijini, Mwahalende aliliambia Mwananchi jana kuwa hapakuwepo na uchakachuaji wowote wa kura bali kilichosababisha tofauti hizo ni makosa katika kujumlisha matokeo hayo.
“Tulitumia calculator (mashine ya kuhesabia) kutokana na presha ya wananchi kwa kuwa walikuwa hawajui mfumo mpya tuliokuwa tukiutumia kwa hiyo baada ya kutangaza tuliendelea kuingiza kwenye mfumo ndio ulitupa matokeo sahihi,” alisema.
Msimamizi huyo alisisitiza kuwa matokeo hayo hayana tofauti kwa kuwa mshindi amebakia kuwa yule yule. Katika uchaguzi huo, Chadema ilipata madiwani wawili huku CCM ikipata madiwani sita na TLP madiwani saba.,

Mwananchi.
 
The guy has a point. Kama mnasema uchaguzi haukuwa wa huru na haki. Mbona mnamkubali Mdee, Mnyika halafu mnamkataa Kikwete? au ni masuala ya ruzuku?

I think CCM should replace Chiligati and put somebody who can effectively call your bluffs na hoja zenu za upande mmoja. Its Chadema's way or no way.

Perhaps in the absence of uchakachuaji and voters-register fiddling all these won't be necessary. The rightful candidate would have been in place and the chief party whips wouldn't have to go through or put up with this bedlam!!
 
Katika gazeti la leo la Mtanzania limetuhabarisha ya kuwa Jaji Mstaafu Mark Bomani amehoji kuhusu Dr. Slaa kukataa kuyatambua matokeo ya kura ya Uraisi huku akiyatambua yale ya wabunge na madiwani...............

Tukumbuke kwanza Jaji huyu amekuwa akinufaika na teuzi nyingi mbalimbali za CCM na ndiyo maana anaona kuna uhaja wa kujitokeza kutetea wale wanaompa ulaji wa kudumu......Hivyo ana masilahi mazito ya ubia na serikali kadha wa kadha za CCM ikiwemo hii ya JK inayotuhumiwa kuiba kura za raia wanyonge na kujisimika madarakani isivyo halali na kinyume cha sheria................................

Maoni yangu ni kuwa Jaji Mstaafu Mark Bomani tumpuuze kwa sababu hajajikitisha kujibu hoja ya msingi ya Dr. Slaa ambayo ni matokeo ya kura yaliyotangazwa na NEC yanatofautiana kabisa na yale ambayo yalitangazwa vituoni..........Hivi NEC matokeo waliyoyatangaza waliyatoa wapi?.........au waliyatoa kibindoni tu?....Hii ni hoja ya msingi kabisa ambapo tungelimtegemea kiongozi wa siku nyingi kama Jaji Mstaafu Bomani kuijibu badala ya kurukia kuwa mbabaishaji tu kwa kuishambulia taswira ya haiba ya Dr. Slaa na kuhoji uwezo wake kama kiongozi..........................

Kushindwa kwa jaji huyu kujibu hoja za kimsingi tajwa kunanithibitishia ya kuwa hoja za Dr. Slaa ni za kweli tupu na hazina majibu zaidi ya JK kukiri kuwa yeye siyo Raisi halali aliyechaguliwa na watanzania kulingana na mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania............

Ama kwa hakika Jaji Mstaafu Mark Bomani ametoa mpya hii ya kujidhalilisha machoni mwa jamii......

Tutakuwa tunamuonea, huyu mzee aliwahi ulizwa na Mwalam JK 1995 kuwa amewahi sikia duniani jaji ni Rais, akatoa jina lake. Sasa kama anashindwa kujua vitu rahisi ataweza mawali magunu ya Dr Slaaaaa?
 
Mkuu Mimi Si Mwanasheria lakini haihitifaji hata Diploma Kujua kwamba, Dk. Slaa alikuwa Mgombea wa Urais na anawajibika kama Slaa kukubali Matokeo au Kuyakataa kwa yeye kuweka Signature yake, Vile vile kwa Wabunge ni wao indivudualy wanaokataa au kukubali matokeo ya Ubunge

Ukindoa kwamba Uchaguzi wa Ubunge na Urais vinafanyika Siku moja lakini ukweli ni kwamba kila mmoja unatawaliwa na kifungu tofauti katika Katiba kama Alivyoanisha Mkuu Kichuguu.

kwa Hiyo kusema kwamba Dr. Slaa alipaswa vile vile kuyapinga Matokeo ya Ubunge wakati Hakuwa anagombea Ubunge ni Ufinyu tu wa Kutumia just Common Sense katika kuchambua mambo na kutokana na Habari yenyewe kuwa kwenye Gazeti la Mtanzania wala siondoi Uwezekano wa Kuwa Jamaa wa Mtanzania wamemchakachua Bomani

After all Utakubali vipi Matokeo katika Uchaguzi wa Kihuni kabisa kama huu, ona Mpaka sasa NEC bado wanarekebisha Statistics za matokeo baada ya Kusikia kwamba Dr. Slaa anajiandaa kuja na Ushahidi utakaowavua Nguo akina Makame na Kiravu

Ni kweli hatuhitaji Diploma kuchanganua haya mambo. Kuna mambo mawili 1)Mpaka hivi sasa, Chadema hawajatupa vielelezo vyovyote ambavyo vinaidhinisha kwamba yeye alipata kura nyingi kuliko Jakaya. 2)Allah katuumba binadamu kuwa wasahaulifu, lakini Chadema hawakufanya kampeni nchi nzima, na kuna majimbo mengi hawakuweka hata mgombea. Sasa wakati kura hazikutosha, badala ya kuangalia mmefanya wapi makosa mjirekebishe, nyie mnayakataa matokeo. 3)NEC ndio mratibu wa mchanganuo wote wa upigaji kura, ubunge, udiwani, na uraisi. Kama msingi wenu wa malalamiko ni NEC walichakachua kura, mbona ni kwenye uraisi peke yake na majimbo ambayo hamkushinda? Ni suala la msimamo tu, kwamba kura zimechakachuliwa, hatumtambui Raisi, Mbunge, na Madiwani wote. Huo ndio uwe msimamo wenu. Mimi naamini NEC wana makosa yao, lakini Dk. Slaa hakupata kura za kutosha hata kama tungepiga kura na mashine. Ili Chadema muweze kusonga mbele, jifunzeni makosa yenu na mujipange kwa chaguzi zijazo. Kampeni yenu haikuwa "text book" kampeni, mumefanya makosa mengi tu ya kiufundi.
 
... Mimi naamini NEC wana makosa yao, lakini Dk. Slaa hakupata kura za kutosha hata kama tungepiga kura na mashine. Ili Chadema muweze kusonga mbele, jifunzeni makosa yenu na mujipange kwa chaguzi zijazo. Kampeni yenu haikuwa "text book" kampeni, mumefanya makosa mengi tu ya kiufundi.

Kwa vile NEC ni chombo tunachokitegemea katika chaguzi, kwanini wananchi wasiyajue kwa marefu na mapana hayo makosa unayoyasema na kuyakubali kuwa yapo ndani ya NEC ambayo yanaweza kabisa kuwa ndicho chanzo kikubwa cha malalamiko ya Chadema? Badala yake unashinikiza tu Chadema wakubali kuwa kuna makosa ndani ya NEC lakini wakubali na kwenda kujipanga upya? Utajipangaje upya hali hujui kwa undani kile kilichosababisha failure yako mwanzoni??!! Would this be acceptable to you if were to be the other way around?!
 
Back
Top Bottom