Israel fingerprints all over 9/11 attacks: US lawmaker

Kama kazi walifanya Mossad basi wamarekani hawawezi hata siku moja kujua ilifanyika vipi maana jamaa ni wazee wa kazi haswa
 
Habari hii haina ukweli hata kidogo.
1) huyu Bwana Duke si mbunge wa Marekani. Ni mbaguzi rangi aliyekuwa kiongozi wa Ku Klux Klan (shirika katika Marekani inayohubiri chuki dhidi ya watu weusi na wayahudi; leo wako wachache lakini walikuwa muhimu sana huko!)

2) Kwa kipindi kifupi alikuwa mbunge wa jimbo la Lousiana (mnamo 1989/90, kwa njia ya by-election).


3) akiwa mbaguzi rangi anayechukia wayahudi si ajabu ya kwamba anatangaza takataka yoyote kuhusu nchi ya Israeli. Si ajabu ya kwamba shirika la Kiislamu inatangaza haya (ingawa inasikitisha!)

4) akiwa mbaguzi rangi anayedharau watu weusi ni kichekesho ya kwamba takataka zake zinasambazwa hapa JF!

Jamani kwa nini tunaletewa hapa takataka tupu??? Je mtu anayeleta hapa kopi-paste hawezi kuchungulia mwenyewe kma kuna ukweli wowote katika site anapoona habari?????

Kuhusu Bwana Duke soma: David Duke - Wikipedia, the free encyclopedia
Kama hujui Ku Klux Klan: Ku Klux Klan - Wikipedia, the free encyclopedia


Mkuu bora umeliona hilo. Kwanza heshima kuweka mambo sawa.

Ni aibu kwa baadhi ya watoa hoja kupost bila kufanya utafiti wa kina.

-Mambo ya septemba 11 yapo wazi, akina mohamedi ata na wenzie

-Audio communiction za watekaji

-Mawasiliano ya baadhi ya abilia waliokuwa wanapambana na watekaji ndani ya ndege kwa familia zao

-Maelezo ya kusambalatika kwa majengo kitaalamu baada ya chuma kupata moto yalitolewa vizuri na wamalekani nk.


mtu hawezi kuubadili ukweli kuwa uwongo na hii inaendelea kulifedhehesha jukwaa letu, tunaelekea wapi mimi sijui.
 
kwa yale majengo am sure kuna kitu kiliwekwa ndani mi nahisi ilipangwa toka zamani sana I guess waliweka explosives kwni haiwezekani jengo lishuke chini kama box palikuwa na explosives nadhani

You are right mkuu kuna documentary ilishawahi kuwekwa humu JF inaonyesha kila kitu kulikuwa na explosives offcourse zile ndege zisingeweza kuyaangusha yale majengo kirahisi vile
 
Ukiangalia kawaida hahaha. Pale mchezo ulichezwa

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom