Habari hii haina ukweli hata kidogo.
1) huyu Bwana Duke si mbunge wa Marekani. Ni mbaguzi rangi aliyekuwa kiongozi wa Ku Klux Klan (shirika katika Marekani inayohubiri chuki dhidi ya watu weusi na wayahudi; leo wako wachache lakini walikuwa muhimu sana huko!)
2) Kwa kipindi kifupi alikuwa mbunge wa jimbo la Lousiana (mnamo 1989/90, kwa njia ya by-election).
3) akiwa mbaguzi rangi anayechukia wayahudi si ajabu ya kwamba anatangaza takataka yoyote kuhusu nchi ya Israeli. Si ajabu ya kwamba shirika la Kiislamu inatangaza haya (ingawa inasikitisha!)
4) akiwa mbaguzi rangi anayedharau watu weusi ni kichekesho ya kwamba takataka zake zinasambazwa hapa JF!
Jamani kwa nini tunaletewa hapa takataka tupu??? Je mtu anayeleta hapa kopi-paste hawezi kuchungulia mwenyewe kma kuna ukweli wowote katika site anapoona habari?????
Kuhusu Bwana Duke soma: David Duke - Wikipedia, the free encyclopedia
Kama hujui Ku Klux Klan: Ku Klux Klan - Wikipedia, the free encyclopedia
kwa yale majengo am sure kuna kitu kiliwekwa ndani mi nahisi ilipangwa toka zamani sana I guess waliweka explosives kwni haiwezekani jengo lishuke chini kama box palikuwa na explosives nadhani