Israel ni strategic ally wa Marekani pale Mashariki ya Kati, hivyo Marekani kuingilia kati kuisaidia Israel ni win-win strategically. Inachokifanya Marekani kwa ajili ya Israel kinaisaidia Marekani pia katika nyanja za kiintelijensia, kijeshi, kiuchumi na geopolitically kwa ujumla.

Kwahiyo, sio kwamba Israel isingeweza kujihami dhidi ya Iran ama adui mwingine bila ya usaidizi wa Marekani, bali ni beneficial zaidi kwa Marekani kuisaidia Israel kama namna bora zaidi ya kulinda maslahi yake ya msingi pale Mashariki ya Kati.
Kifupi,nchi ya Israel ni military base ya marekani, uingereza na ufaransa kwa ajili ya kuidhibiti mashariki ya kati
 
99% ya makombora yameshushwa. Hakuna tofauti na makombora ya Iraq ya scard.
Ulikuwepo? Umeyashuhudia?!
-Israel imedhalilishwa na HAMAS
-Huko bahari nyekundu,kinachofanyika,kinaeleweka
-Cha kujifunza: hatutakiwi kuwa mashabiki sana wa media,kwa sababu duniani humu, kila vita vinapopiganwa,wenye masrahi hawawezi kuongea ukweli.

-Israel ilidai inaenda kumaliza kazi. Nini kinajadiliwa sasa hivi?
-Ukraine ilidai hakika mambo yako sawa na wanaenda kuimaliza Urusi.
Ikaingizwa NATO kisirisiri, imebaki wazi Russia inapigana na NATO kwa mwamvuli wa Ukraine.
Na Irani,mpaka wanakiri kambi ya jeshi la anga imepigwa, lazima kuna makubwa yaliyojitokeza. Tungesubiri basi waliopo maeneo yaliyopigwa,ndo tungekadilia hiyo 99%.
 
Hivi ujui Isreal ana nuclear mbona mnaleta ushambiki kwenye vita wanasema na Iran pia ana nuclear Tuombe Mungu hawa jamaa wakae mezani yaishe Nuclear haina mbabe
Acha wazitumie mkuu. Si ndo zilichoundiwa? Sisi tuziojua hili wala lile,ambao leo hii ndo mashabiki,tutakufa nao tu. Maana hata huko wanakorushiana, kuna wasio na hatia wanaishia.
 
Huenda ni wewe mleta uzi ndiye ambaye uko gizani na ulidhani Iran inatania.

Kama Israel ingedhani Iran inatania basi isingetangaza hadharani kuweka mifumo yake ya ulinzi katika utayari dhidi ya hali ya tahadhari. Matokeo yake, Israel isingeweza kukabiliana na mashambulizi kama ambavyo imefanya mpaka sasa na kwa ufanisi mkubwa.
Ufanisi gani?
Asilimia kubwa ya mashambulizi yamezuiwa na Marekani , Uingereza, na Ufaransa yaani nchi nne zimeungana kuzuia mashambulizi lakini bado baadhi ya makombora yakapenya.
Hiyo Israel huwa mnaikuza hali ya kuwa bila ya Marekani ni takataka fulani.
 
kwa vile umejenga hoja kama mtu timamu( maana humu wachambuzi wasio na mihemko wamekuwa adimu), unadhan nani atakuwa mhanga zaid wa hali hii
Hapo wahanga ni Israeli, Iran na eneo lote la mashariki ya kati.

Ndo maana Iran wamesema sasa case closed wamejibu kilichofanywa na Israeli tarehe 1 April.

Na pia Iran wametoa onyo kwamba Israeli wasifanye makosa kujibu mashambulizi haya.

Marekani na Uingereza wao ni kama waangalizi na wapigania kuwepo deescalation.
 
Hata Iran amepeleka rasharasha tu amesema Isreal ikijibu tu basi atapeleka full dose wainywe vizuri.

Isreal hana ubavu wa kupigana uso kwa uso na Iran huwa anategemea support ya mabwawa zake USA na UK.
Japo hatuombei, ila sidhani kama Marekani mwenyewe anaweza kujiingiza kichwa kichwa. Nae ana mahesabu. Kwani Ukraine amesaidia nini? Kumbuka, Iran nae si wa kuchezea chezea hivo,sema tu nguvu ya media ndo inamshusha kana kwamba hajiwezi. Katika ukanda huo,nani anakubali USA itumie anga au ardhi yake?
Kumbuka,kuna dogo nae sehemu furani anawashwa. Tutaangamia wengine,labda hatutojua mwisho wake,lakini,kama pamoja na umoja wao,kuna yaliyopita na kutua, hata wao lazima wafikilie mara mbili. Na haiwezi kutokea,mtu akaanza vita na siraha kali. Hivyo,tutegemee labda wakati mwingine wababe wakionyesha ubabe wao. Hamas na Hezbollah walionesha mafanikio. Iweje Iran leo ndo iferi?
 
Ufanisi gani?
Asilimia kubwa ya mashambulizi yamezuiwa na Marekani , Uingereza, na Ufaransa yaani nchi nne zimeungana kuzuia mashambulizi lakini bado baadhi ya makombora yakapenya.
Hiyo Israel huwa mnaikuza hali ya kuwa bila ya Marekani ni takataka fulani.
Hayo yaliyopenya yameleta madhara gani ukilinganisha ni kile kilichofanywa na Israel pale ubalozini Damascus?
 
Ujasiri wa Iran umeifanya Israel inywee kiaina tofauti na wengi tulivyotaraji kuwa ikipigwa kweli na Iran itarusha mvua ya makombora Tehran papo kwa papo.
Kitisho cha vita vikubwa zaidi kiko wazi baada ya Iran kuiambia Marekani ikae mbali katika vita vyake na Israel.
Baada ya mashambulio ya jana mpaka kwenye kambi za jeshi za Tel Aviv,Iran imesema mpaka hapo imefunga ukurasa wake wa mwanzo wa vita.Inasubiri iwapo Israel itajibu na wao waendeleze ukurasa mwengine mpana zaidi
Waisrael kwenye ubalozi wa Iran Syria waliua watu 8 akiwepo kiongozi mkubwa sana wa Jeshi la Iran

Hayo makombora ya Iran yameua wanajeshi au raia wangapi huko Tel Aviv?
 
Waisrael kwenye ubalozi wa Iran Syria waliua watu 8 akiwepo kiongozi mkubwa sana wa Jeshi la Iran

Hayo makombora ya Iran yameua wanajeshi au raia wangapi huko Tel Aviv?
Iran haija shambulia kwa ajili ya kuuwa watu bali ilikuwa ni kwa ajili ya kupiga base ya kijeshi.
Hapo ndo uone tofauti kati majeshi yanayo fanya kazi kwa weledi na yale yanao fanya kazi kama wahuni na wavuta bangi.
 
Hayo yaliyopenya yameleta madhara gani ukilinganisha ni kile kilichofanywa na Israel pale ubalozini Damascus?
We jamaa uelewa wako mdogo sana....Jamani wemgine someni tu comments za wajuvi wa mambo ili mpanue maoblangata yenu... Kwausichofahamu Israel na Syria ni km Namanga TZ na Namanga KE... Ata kwa mguu unafika....Pili Diplomatic premises (ubalozi) hua haushambuliwi lile ni jengo tu halina threat yoyote sasa Israel kushambulia Jengo nayo nimafanikio kwako kweli?? Ebu jaribu kupitia military blogs za kimataifa ujifunze kitu.... Israel analindwa kwa gharama kubwa sana na US...bila US/UK/France na Jordan leo ingekua ni kilio kikubwa kwa Israel.... Jiulize Iran imeishambulia Israel lakini US president na baraza lake la usalama wamekaa kujadili as if US ndo kashambuliwa....
 
Waisrael kwenye ubalozi wa Iran Syria waliua watu 8 akiwepo kiongozi mkubwa sana wa Jeshi la Iran

Hayo makombora ya Iran yameua wanajeshi au raia wangapi huko Tel Aviv?
Target ya Iran haikua kwenye majumba ya watu km balozi....Target ilikua military na air bases... Sasa ubalozi nikama nyumba ya babako tu apo ulipo... Ata kibaka yoyote anaweza itaget na kuua familia nzima.... JF ni uwanja wa great thinkers na sio watoto km wewe
 
We Ali wazi,
Shughuli ya huko ni nzito kuliko unavyoota ukila daku.
Anga Iran tayari wanaume wako pale,baharini tayari kumezingirwa.
Hivi we ngumbaru unadhani vita ya Iran ni kama kupiga Hamas au Houthi.
Hao ni nzi tu.
Ye kalianzisha na vidrone vyake.
Inteligensia inapiga kazi wazayuni wanajipanga huko watavunjavunja kila kitu.
Mda utaongea
 
Iran haija shambulia kwa ajili ya kuuwa watu bali ilikuwa ni kwa ajili ya kupiga base ya kijeshi.
Hapo ndo uone tofauti kati majeshi yanayo fanya kazi kwa weledi na yale yanao fanya kazi kama wahuni na wavuta bangi.
So wameharibu Military base ya Israel?
 
Target ya Iran haikua kwenye majumba ya watu km balozi....Target ilikua military na air bases... Sasa ubalozi nikama nyumba ya babako tu apo ulipo... Ata kibaka yoyote anaweza itaget na kuua familia nzima.... JF ni uwanja wa great thinkers na sio watoto km wewe
Sawa mama, Impact ya shambulio la Iran kwenye Military base ya Israel ni ipi?
 
Back
Top Bottom