Magazetini
JF-Expert Member
- Aug 16, 2014
- 588
- 1,698
KAMPUNI ya kufua umeme IPTL/PAP sasa imezidi kufahamika kuwa haina kesi au mgogoro wowote mahakamani baina yake na Shirika la Umeme Tanzania(TANESCO), imefahamika.
Hali hiyo imekuja wakati kukiwepo na habari katika mitandao na baadhi ya vyombo vya habari(isipokuwa gazeti hili) kuwa IPTL/PAP haikustahili kulipwa malipo ya ESCROW kwa kuwa kuna kesi mahakamani.
Taarifa zaidi zinaeleza kesi hiyo inadaiwa imefunguliwa na TANESCO kuhusiana na ukubwa wa gharama za uendeshaji ‘Capacity charge' unaofanywa na Kampuni ya IPTL.
Hata hivyo, taarifa zaidi kuhusiana na suala hilo, zinasema kwamba kesi hiyo ilishatolewa hukumu yake tangu 2001, ambapo Mahakama ya Kimataifa ya usuluhishi wa kibiashara ICSID iliagiza IPTL ishushe gharama zake kutoka dola milioni 4.2 hadi dola milioni 2.6 kwa mwezi.
Taarifa zilisema baada ya kumalizika kwa kesi hiyo, ndipo kukazuka mgogoro mwingine wa kimaslahi baina ya waliokuwa wabia wa IPTL, ambao ni Kampuni ya VIP na Mechmar ya nchini Malaysia uliopelekea VIP kuomba kampuni ifilisiwe na isilipwe hata thumni na TANESCO.
Kutokana na maombi hayo ya kampuni ya VIP, Mahakama Kuu iliamriwa kufunguliwa kwa akaunti maalumu itakayokuwa inatunza fedha zinazolipwa na TANESCO kwa ajili ya huduma ya umeme inayotumia.
Katibu na Mwanasheria wa Kampuni ya IPTL, PAP, Joseph Makandege alisema hawana kesi na TANESCO na anashangazwa na taarifa zinazotolewa.
"Si kweli kwamba ESCROW akaunti ilifunguliwa kutokana na maombi ya TANESCO kuhusiana na mgogoro wa capacity charge, Kesi ya TANESCO iliisha 2001, na akaunti ya ESCROW ilifunguliwa kwa hukumu ya 2006,''alisema.
Aliongeza; "VIP ndio waliomba kufunguliwa kwa ESCROW, hivyo kusema kwamba TANESCO na IPTL kuna kesi ni upotoshaji unaopaswa kukemewa,''.
Makandege, alisema kesi iliokuwepo kwa sasa ni ya mgogoro wa umiliki kati PAP/IPTL na benki ya Standard Chartered ya Hongkong inayodai kununua deni la Kampuni ya Mechmar ya Malaysia.
"Kesi kati ya Standard Chartered na IPTL/PAP haihusiani na TANESCO na wawaache TANESCO watimize wajibu wao na sisi tuyatimiza wajibu wetu kwa Watanzania na tutapambana mahakamani,''alisema Makandege kwa kujiamini.
Hivyo, alisema wanaolalamika kwamba PAP/IPTL imelipwa kwa makosa wao ndio wanafanya makosa ya kupotosha ukweli wa suala hilo au labda waeleze kwamba Standard Chartered ni Shirika la Umma.
CHANZO: Majira