Ipo siku yaja kwa huyu mwenezi msipomfunda CCM na Rais Samia mtavuna mabua

Duh! Kwa hiyo,wafanyakazi serikalini wabembelezwe kufanya kazi zao? Wakijisikia walale,mwisho wa mwezi walipwe.
Kwa nini wafanye kazi kwa woga? Wakitimiza wajibu wao,nani atawafatilia kuwawajibisha!?
Kwani makonda ndiye mkuu wa divisheni/idara zote za serikali? Huko wanakofanya kazi hawo watumishi wa umma hakuna wakuu wao wanaowaongoza kutimiza majukumu yao au unataka kusema nini mkuu?
 
Hili nililisema tangu zamani kwamba Makonda ni timu Sukuma Gang na kwamba baada ya kupenya kuingia uongozini, ataanza mchakato wa kumuangusha mama kupitia chawa wengi wa kundi hili waliomo serikalini. Ikifika 2025 tayari kundi hili litakuwa limeota mizizi ya kutosha. Halitaweza kurudishwa nyuma wala kutishwa kwa vyovyote vile na timu ya mama.

Sasa ni wakati muafaka timu ya mama imshughulikie mapema kiongozi huyu wa Sukuma Gang kabla hajaleta madhara kwa chama, serikali na kundi la mama. Wasipoziba ufa mapema, watakuja kujenga ukuta.

Hakuna tatizo kwa wanaCCM wenye uwezo kujitokeza kugombea na Mama Samia 2025. Mama hakugombea kile kiti. Alikipata kwa bahati nzuri tu. Sasa anatakiwa apitie mchakato wa kugombea urais kwenye nchi yenye watu milioni 61, lakini haina uwezo wa kukusanya kodi na kuendesha nchi kwa pesa za ndani zaidi ya kutegemea misaada inayokuja na masharti ama ya ushoga, ugaidi, na itikadi zisizofaa kwenye nchi hii kwa usalama wa wananchi wote kwa na vizazi vijavyo.

Hatutaki kumpa mtu yeyote nchi kwa bahati. Mtu asimame aseme nini maono yake kwa Watanzania wote. Mtu atuambie nini kinachosababisha umaskini wa kitaifa wakati kuna wachache waliopo kwenye madaraka wanaogelea kwenye mali kutokana na madili ya kuhujumu nchi. Atapambana vipi na wahujumu uchumi kwa kutumia katiba iliyopo endapo hana mpango wa kuleta katiba mpya? Je, katiba iliyopo ataitumia vipi kupambana na ufisadi wakati taasisi zote hazina meno ya kuwang'ata na kuwakemea wateule ambao ndio wafujaji wa mali za umma?

Wagombee wengi kutoka makundi mbalimbali watuambie kwa nini kodi zinaongezeka kwa kasi na mikopo kila siku, lakini matumizi na starehe kwa watawala yanakwenda juu na wao hawajali? Nini watafanya kwa kutumia katiba hii ya kidikteta bila kutawala kwa misingi ya kuwafukuza na kuwakemea wezi?

Atuambie ni kwa nini alisema katiba ni kijitabu tu kisicho na nguvu wakati ndicho kinachompa nguvu na kuyafanya majeshi yenye nguvu kumtii kwa misingi ya kijitabu hicho hicho?

Aliyepo muda wake unaisha 2025 kwa msingi wa uteuzi wake ndani ya Chama 2015 hadi 2025. Wajitokeze wengine wagombee kushindanisha serikali na maono. Historia ya dunia inaonyesha kuwa dunia inaleta mabadiliko kutokana na maono ya mtu mmoja na sio chama, wala wanachama, wala makundi ya watu.

Musa, Yesu, na Muhammad ni mtu mmoja aliyeibadili dunia kwa maono yake na misingi aliyoiamini. Kwa sasa, aliyepo yupo pale kwa sababu ya umakamu wa rais 2015-2025.
 
Mama yenu mwenyewe kampigia simu Makonda LIVE mkutanoni huko Moshi juzi tu na kusema anamuunga mkono kwenye huo ufuatiliaji wa utekelezaji wa ILANI ya chama na kusikiliza kero za wananchi.

Ndiyo maana hutokaa umsikie tena Nchimbi wala Kinana akipiga vijembe anachokifanya Konda,hapo tayari kaamua kiutu uzima.

Actually,hiki anachokifanya Konda ndiyo watz wengi wanakitaka, uwajibikaji nchi hii kwa sasa ni sifuri huko maofisini.
 
Mkiongozwa na chuki Makonda atawanyoosha kwelikweli...

Tatizo ninaloliona hapa kuna watu walitamani kumpamgia raisi, nani ashirikiane naye na nani amwache...

Kitu unachopaswa kujua nyinyi mungekuwa na uwezo wa kumsaidia raisi, angewateua nyinyi badala ya huyo munayemchukia ...

Kutokuteuliwa ninyi ni ishara kwamba hamuna uwezo wowote wa kumsaidia raisi na hamkubaliki kwa wananchi...
Rais anahitaji msaada gani?! Huyo Makonda sasa anatoa msaada gani Kwa Rais?
 
Kwani makonda ndiye mkuu wa divisheni/idara zote za serikali? Huko wanakofanya kazi hawo watumishi wa umma hakuna wakuu wao wanaowaongoza kutimiza majukumu yao au unataka kusema nini mkuu?
1. Mimi nimeongelea aliesema woga wa wafanyakazi kuwajibishwa.
2. Nadhani kila kitengo kina mkubwa wa kuwajibishwa, na pia nadhani kuna njia sahihi ya kuwajibishwa kisheria.

Labda kwao hawanaga wakubwa! Pengine hata kwa umri wake na anaowaajibisha, alitakiwa apunguze kasi.
Ila sasa, kama katumwa, afanyeje?
 
Mleta mada kuna wimbo wa Bob Marley unaitwa "Who cap fit, let them wear it."

Kwenye huu wimbo kuna maneno yanasema

"Who Jah/God bless, you can't curse him".

Makonda ana kila dalili za kuwa mtu aliyebarikiwa sana sana.

Makonda amepitia majaribu na vigingi vya kutosha ila hadi sasa ameviruka.

Kama kwa Miaka 2 alipokuwa nje ya siasa hakuna aliyeweza kumdhuru fikiria atakuwa amebarikiwa kiasi gani
 
Lakin saa inakuja,nayo sasa ipo,ambapo mtavuna mnachokipanda, kwa jicho la mbali mnamuona kama anakijenga chama, katika jicho la upeo wa roho anadhoofisha chama, bosi wake na Viongozi wakuu wengne na kujijenga yeye.

Anajisafisha na kujitanabaisha alikuwa ni mtu mwema, kiongozi shupavu na jasiri. Mpaka sasa anamuheshimu mwendazake na ndiye bosi wake wa moyo wa mda wote. Ndo mana anaishi falsafa zake na ndio anazohubiri, falsafa hizo zinalengo la kuwaibua wale walompenda na kufanya aonekane yeye ndo mrithi sahihi, Wale walompenda Mwendazake sasa watampenda huyu kwa heshima na kweli na watamuimba kama shujaa wao na hakuna atakae weza kuzuia.

Mama Falsafa yako ilitanabaisha watumishi wa serikali wasifanye kazi kwa woga, bali kwa weledi na nidhamu,ila falsafa inayohubiria majukwaani kwa sasa ni hofu na umaarufu wa mtu.kwa vile watumishi wengi wa serikali ni waoga, wamejengwa kuogopa wanasiasa,zile zama za woga zinarudi, na hakika watumishi na wateule wako wote wanamuogopa huyu kuliko kiongozi yeyote ktkt taifa hili, huku akijijenga kwa wale wananchi mnaowaita walalahoi na wanyonge wamuone ndiye kiongozi pekee mwenye udhubutu na kukemea maovu.

Hakika nakwambia ,watanzania wanataka kiongozi anayesema na kutenda, anayeonya na kukemea kweli kweli, anayewajibisha watumishi wa umma wazembe na wabadhirifu wa mali za umma na hii ndio beat anayotembea nayo Mwenezi.
Asipofundwa vizuri atakufarakanisha na wale uliokuwa umeanza kupatana nao,haki uliyoitengeneza na kuipigania itapotea. Mhe raisi binafsi naamini unafanya kazi nzuri sana na nakupenda kwa dhati kwa sababu unapenda haki na usawa kwa wote lakin nakuomba usiamni sana hawa wasaidizi wako,wengi wao wanaangalia vyeo na matumbo yao,usiwakumbatie sana kana kwamba bila wao nchi haitaenda,kuna wateule wako wanakuharbia halafu wanakusifia wakiamn utafurahishwa na hizo sifa.maagizo yako hawayatekelezi kabisa na wanafanya yao kwa mgongo wako.

Ole wenu msipotafta namna ya kumfunda, ipo siku yaja hamtaweza kuyazuia mafuriko, Kama lengo ni kumjenga kuwa kiongozi basi ni vema mkamjenga sawasawa kwa sababu kama atabadilika ni kiongozi mwenye udhubutu na huenda akaleta Mabadiliko katika nchi, anahulka ya kupenda Maisha ya kifahari lakini anachukia wengine wanaoyaishi, anapenda mamlka na kuamuru lkn hapendi anayemzidi mamlaka, anapenda kusaidia watu na anataka ajitanabaishe ni yeye pekee mwenye huruma na moyo wa kusidia watu, anapenda kuonekana ni mcha Mungu kuliko wanaosimama madhabahuni.

Maisha yameguwa magumu sana mtaani,Mama sekta bnafsi zinazofanya kazi na serikali hasa zinazolipwa na pesa kutoka HAZINA hazilipwi kwa wakati na kusababisha baadhi kuzorota au kufa hasa za wazawa,umeme umekuwa ni tatizo na kero kubwa sana kwa wananchi,watu wanategemea umeme kufanya shughuli zao zinazowaingizia kipato na kuendesha Maisha yao lkn umeme umekuwa ukikatika kila uchao jambo linalowafanya wananchi kuanza kuchukia serikali.zaidi Viongozi wa serikali wengi hasa wateule wako wanaishi Maisha ya kifahari na bila shaka kero ya umeme kwao haiwapati

Iwe jumapili njema kwenu,Maandiko yanasema ‘basi sasa msiwe watu wa kudharau,vifungo vyenu msije vikakazwa,maana nimeskia kwa Bwana,Bwana wa majeshi,Habari ya hukumu itakayotimizwa,nayo imekusudiwa.
Huyu ndiyo tunamtaka kwasasa na si kesho. Anayemchukia ni mjinga na mwenye ajenda zake za siri. Unamchukia vipi mtu, tena kiongozi wa chama tu aliyejitoa kutetea na kutatua kero za wananchi, tena wanyonge. Rais kashindwa, makamu kashindwa, waziri mkuu kashindwa, naibu waziri mkuu kashindwa, mawaziri wameshindwa, naibu waziri wameshindwa, wakuu wa mikoa wameshindwa, wakuu wa wilaya wameshindwa, RAS, DAS hovyo tu. Usidhani kama sisi ni wajinga kujaa kwenye mikutano yake. Ana kitu huyu kijana na anafaa kwasasa kwani amesaidia watu wengi mno. Vipi kama angekuwa na mamlaka ya kikatiba sasa? Go Makonda gooooo!
 
Mara ngapi? Sisi huku ni shangwe tuu muache azidi kuharibu

Sent using Jamii Forums mobile app
Anaharibu wapi, acheni kudanganya watu nyie... Msimtishe Mh Rais wetu bila sababu. Mnadhani wenyewe hamjui vizuri. Tatizo, bana, mafisadi yakishaona kuna hali ya hatari, yanaanza kujitengenezea barrier ya kutoguswa. Hata kama anatembelea nyota na Magufuli, kuna tatizo gani? Wakati katika nyota ile, hata mama yetu Dr SSH alikuwemo. Mmeshaona chama kinajirekebisha na kuwa kikali, mmeanza kulialia. Wacha watu wachape kazi, iwe lolote lakini wananchi wanahitaji matokeo: maji, umeme, bei nafuu, mfumuko wa bei chini, mafuta chini, sukari chini, n.k. Sijui unaelewa. Hayo mengine ni propaganda zako za kutunga.
 
Back
Top Bottom