lord atkin
Senior Member
- Sep 30, 2018
- 197
- 683
Tofauti na zamani nilivyokuwa nadhani nimekuja kugundua kuwa wanasiasa wa Tanzania nao wanakariri maisha kama vile mwanafunzi wa kidato cha kwanza anavyokariri masomo shuleni. Ni wazi kwamba katika awamu ya tano ili kiongozi ateuliwe au atoke kisiasa ilikuwa ni lazima ama ajipendekeze kwa Rais JPM, ajiunge na kundi la wanasiasa la kusifu na kuabudu. Ilikuwa ukijitokeza na kusifu vizuri utawala kwa ubunifu mkubwa basi baada ya muda utateuliwa.
Baada ya kuingia Mama Samia katika hii awamu ya sita cha kushangaza baadhi ya wanasiasa wameendelea kukariri mambo ya awamu ya tano bila kujali mambo yamebadilika Kuna Rais mpya mwenye maono na vision mpya. Watu hawa bado wanaendelea na kusifu na kuabudu, uchawa na kujipendekeza wakijua kuwa ndiyo njia sahihi ya kumpendeza Rais Samia kama ilivyokuwa kwa mwendazake.
Nilichogundua ni kwamba katika swala hili Rais Samia ni tofauti sana na Mwendazake, yeye si Rais anayependelea sana kupambwa na kusifiwa bila mpangilio. Rais Samia anapenda kiongozi ambaye anajisimamia, mwenye misingi na misimamo yake bila kujali misimamo hiyo inakinzana naye kiasi gani. Katika uteuzi huangalia zaidi uwezo na sifa za mtu zaidi kuliko kujipendekeza kwa mhusika.
Mfano watu kama Humphrey Polepole kwa jinsi alivyokuwa akiukosoa uongozi wa Rais Samia baada ya kuondolewa kwenye uenezi CCM basi ingekuwa ni awamu ya tano asingeliteuliwa kuwa balozi, lakini kwa Mama Samia ni tofauti hakuangalia huyu mtu ananipinga kiasi gani bali aliangalia uwezo na hoja za mhusika akamteua Polepole kuwa balozi.
Mfano mwingine ni Askofu Gwajima kwa Kasi ile aliyoanza nayo ya kupingana na Mama Samia kwenye swala la chanjo ingekuwa awamu ya tano pengine angekuwa ashafukuzwa hata chama. Lakini Mama Samia alihudhuria mkutano wake Jimbo la kawe na kuaddress issue ya chanjo.
Hii ni baadhi ya mifano inayoonesha Mama Samia ni mtu wa namna gani. Kwenu wanasiasa mliokariri siasa za kusifu na kuabudu kama nyenzo ya kufanikiwa kwa Mama Samia hamtatoboa badilikeni. Badala ya mbunge kukaa bungeni na kujipendekeza kwa Rais kutaka picha yake iweke kwenye noti isimamie serikali kwa bidii, wabane mawaziri kwa hoja wasipumue nakuhakikishia utateuliwa kuwa naibu waziri au waziri.
Kitu kingine Mama Samia anacho kipenda ni Demokrasia na uhuru, hivyo kwa wateule wanaotaka kumfurahisha ni vizuri wakacheza kwa madaha wimbo wa uhuru na Demokrasia watafika mbali sana.
Nihitimishe kwa kusema nimependa siasa za Mpina siyo muda mrefu anaula uwaziri.
Wakatabahu
Baada ya kuingia Mama Samia katika hii awamu ya sita cha kushangaza baadhi ya wanasiasa wameendelea kukariri mambo ya awamu ya tano bila kujali mambo yamebadilika Kuna Rais mpya mwenye maono na vision mpya. Watu hawa bado wanaendelea na kusifu na kuabudu, uchawa na kujipendekeza wakijua kuwa ndiyo njia sahihi ya kumpendeza Rais Samia kama ilivyokuwa kwa mwendazake.
Nilichogundua ni kwamba katika swala hili Rais Samia ni tofauti sana na Mwendazake, yeye si Rais anayependelea sana kupambwa na kusifiwa bila mpangilio. Rais Samia anapenda kiongozi ambaye anajisimamia, mwenye misingi na misimamo yake bila kujali misimamo hiyo inakinzana naye kiasi gani. Katika uteuzi huangalia zaidi uwezo na sifa za mtu zaidi kuliko kujipendekeza kwa mhusika.
Mfano watu kama Humphrey Polepole kwa jinsi alivyokuwa akiukosoa uongozi wa Rais Samia baada ya kuondolewa kwenye uenezi CCM basi ingekuwa ni awamu ya tano asingeliteuliwa kuwa balozi, lakini kwa Mama Samia ni tofauti hakuangalia huyu mtu ananipinga kiasi gani bali aliangalia uwezo na hoja za mhusika akamteua Polepole kuwa balozi.
Mfano mwingine ni Askofu Gwajima kwa Kasi ile aliyoanza nayo ya kupingana na Mama Samia kwenye swala la chanjo ingekuwa awamu ya tano pengine angekuwa ashafukuzwa hata chama. Lakini Mama Samia alihudhuria mkutano wake Jimbo la kawe na kuaddress issue ya chanjo.
Hii ni baadhi ya mifano inayoonesha Mama Samia ni mtu wa namna gani. Kwenu wanasiasa mliokariri siasa za kusifu na kuabudu kama nyenzo ya kufanikiwa kwa Mama Samia hamtatoboa badilikeni. Badala ya mbunge kukaa bungeni na kujipendekeza kwa Rais kutaka picha yake iweke kwenye noti isimamie serikali kwa bidii, wabane mawaziri kwa hoja wasipumue nakuhakikishia utateuliwa kuwa naibu waziri au waziri.
Kitu kingine Mama Samia anacho kipenda ni Demokrasia na uhuru, hivyo kwa wateule wanaotaka kumfurahisha ni vizuri wakacheza kwa madaha wimbo wa uhuru na Demokrasia watafika mbali sana.
Nihitimishe kwa kusema nimependa siasa za Mpina siyo muda mrefu anaula uwaziri.
Wakatabahu