Hivi mnajua mkubwa wa Interpool hapa TZ ni nani?
Tuambie ni nani?
Hivi mnajua mkubwa wa Interpool hapa TZ ni nani?
Huyu si ndio wakili wa AM?
Angalia usije ukawa unamuombea mabaya Mfadhili wenu mkuu...
Kama TISS na POLICE wako ICU acha tu interpol watusaidie japo kutuonyesha wabaya wetu ingawa sina hakika kama watachukuliwa hatua zozote za kisheria,tutaishia tu kuwafahamu kwa majina.
Naomba kuuliza hivi ukiwa na ndugu yako aweza kuwa kaka,mdogo wako au baba yako au shangazi yako mwizi unafanyaje kuonyesha kuwa upendii tabia yake hiyo ya wizi kwani kwako unaona inaleta jina baya kwa familia na kuwa ni jambo baya na jamii inawachukulia ninyi nyote wanafamilia na jamaa zenu wote kuwa ni wezi walewale.,ukizangatia baadhi ya Wanandugu na marafiki zenu wanamfurahia ndugu yenu mwizi jinsi anavyowapa na kuwatimizia mahitaji yao yote kwa pesa za wizi.
Naomba kujua utatumia njia gani kumshughulikia ndugu yako huyo mwizi ili usilete lawama na mtafaruku kwa ndugu zako na jamaa ambao daima wamekuwa wakifaidika na wizi wake huo?
Lakini si bora wamejulikana, ukimjua mwizi utajihadhali unapokutana naye kuliko kutomjua, angalia habari ya Shimbo ingawa bado ni tuhuma/tetesi lakini watu wanajiuliza inakuwaje kiongozi wa jeshi afanye hayo?, mbali na wananchi kujiuliza hata yeye anajiuliza watu wananifikiriaje, hali hiyo kwa pande zote inatosha sana kusaidia kujirekebisha kwa kiwango fulani.Mkuu, Interpol watawafichua, polisi na TISS watawalinda kwa gharama zoote! This Is Tanzania (TIT)
Hata wewe leo unajifanya kumkana mfadhili wenu mkuu ajabu.............Angalia usije ukawa unamuombea mabaya Mfadhili wenu mkuu...
pesa halali ni DOLAJe mtanzania unatakiwa kuwa na sh ngapi bank au mkono? Je pesa alali ni hipi ? MBONA RIZI ONE ajakamatwa Je wajua kwani anajiita Rizi one ?
Kumbe haya mamlaka tumeyakabidhi Interpol, poor Tanzania !
Subiri utayasikia mengi wamemfukuza mshika fuko wakati alikuwa anajua dili zote unayoyaona ni cha mtoto wakati ukifika mtabaki midomo wazi.Mbunge wa Arusha mjini muheshimiwa Lema na waziri wa mambo ya ndani kivuli kwenye kuwasilisha hotuba yake toka kambi ya upinzani aligusia mambo mengi ikiwepo rushwa ndani ya jeshi la polisi pamoja na mahakami lakini Lukuvi alipinga hoja zote za upinzani kuhusiana na hotuba ile akidai imejaa uchochezi, lakini leo hii tunaanza kuyaona kama haya kwa wakili wakujitegemea kukutwa na kiasi kikubwa cha fedha kama hiki ambacho hakilingani na kazi yake! je na huko mahakamani mawakili na makarani account zao ziko vipi?????...! Tafakari.